Hali ya Chid Benz Inasikitisha sana

Hali ya Chid Benz Inasikitisha sana

Daah Kuna Ngoma yake naangalia muda huu kaimba na P unit kutoka Kenya jamaa Yuko Bling bling hatar na ana afya njema tu nikisoma huu Uzi nasononeka sana
Kuna Ile Ngoma kaimba na Diamond kuna siku nilikua zangu Upanga kule hospital kuna Jamaa walikua wanarekebisha nguzo za Shule bwanawee walipomaliza usiku ule si wakaweka Goma lile linaitwa 'Tunaishi Nao' bwanawee huo mdundo nasema mdundo wa lile beat la Ile Ngoma utafikiri hautoki kwenye Gari acha niishie hapa
 
Kila mmoja anatupa lawama kwa mwengine kuhusu yanayoendelea maishani mwake.

Kutoa lawama ni tabia aliyoianzisha SHETANI ndani ya BABA yetu ADAM (Mwanzo 3). Unaulizwa uliko na MUNGU unajibu eti huyu MWANAMKE uliyeniletea ndiye . . .

Kingine ni LOW SELF ESTEEM iliyomjaa mtu mwenyewe. Anajiona vile alivyo haitoshi ila angekuwa kama fulani aliyetoboa pua na kuvaa HELENI, kuvuta ganja na kubwia unga, kuiga na kuishi maisha ya plastic surgery ndiye bora kukuliko.

Mara kwa mara hatumweki Mwenyezi MUNGU mbele yetu pale tunapofanikiwa katika maisha kutokana na KIBURI na UJINGA anaotujaza shetani na hatimaye tunaharibikiwa na kuharibu maisha ya wengine kwa kuwa tunao wanaotugemea na wale tulio wa inspire kwa mafanikio yetu.

Bado hatujachelewa kuwaokoa wenzetu kutoka katika changamoto na majanga ya kimaadili na kimaisha, kiafya. SWALI ni Je, wako tayari kuopolewa kutoka huko?
 
Chidi ni rapa mkali sana ila mfumo wa nchi kwenye mziki wa hip hop haujampa mafanikio kulinganisha na alichotoa(uwezo wake) imepelekea kupata msongo wa mawazo na kutumbukia kwenye uraibu wa madawa ya kulevya.

Mtu mwingine anayekuja kwa sifa ni Young dee soon kitaumana.
Haukumpa mafanikio wakati kipindi kile yupo kwenye peak 2008-2011 alikuwa kila shoo kubwa lazima aitwe, ndio alikuwa top kwa wasanii wa bongo. Lakini ghafla alikuja kutangaza kuwa anastaafu mziki. Kumbe nyuma ya pazia alishaanza uraibu wa madawa ya kulevya.

Watu wamejitikeza kumpeleka rehab center lakini yeye mwenyewe hayuko tayari kujikubali na kubadilika.

Kuvimba kwa miguu ni matokeo utumiaji wa madawa ya kulevya. Na kama anashinda maskani za mateja basi jua kuwa amesha relapse tena na kurudi kuvuta. Kuacha madawa ni mpaka uamue kutoka ndani ya nafsi...ni ngumu kama kuacha kubeti au punyeto.

Mungu tulinde sisi na vizazi vyetu na walippotea warudiahe kwenye mstari wa sawasawa ameen
 
Waja si wanasema kuwa uyu jamaa ni jiniazi japo ameshawehuka lakin bado watu wanamchukulia kichwa haitaji msaada wa kisaikolojia. Ila uyu mwamba ni jeuri na mjuaji sana hapaswi kusaidiwa
Hao ambao sio wajeuri na sio wajuaji,wewe umesha wasaidia wangapi mpaka sasa?
 
Umesema ukweli japo ni mchungu. Dunia na maisha kwa ujumla hayana huruma. Ndiyo, watu kama hawa wakishafika hiyo stage ya uteja wanahitaji msaada kwani wenyewe wanakuwa hawana uwezo wa kujisaidia tena, lakini kiuhalisia kwa maisha ya kitanzania hili ni gumu kutokea. BTW si ni watu wa CCM hawa? Au inawapenda wanapokuwa wazima tu?
Mkuu upo kisiasa sana, haupo kiuhalisia.

Unadhani wangetawala Chadema ChidiBenz asingekuwa kwenye hali hiyo?

Muda mwingine tuwe kwenye uhalisia.
 
Mkuu upo kisiasa sana, haupo kiuhalisia.

Unadhani wangetawala Chadema ChidiBenz asingekuwa kwenye hali hiyo?

Muda mwingine tuwe kwenye uhalisia.
Uhalisia wa kushirikiana na majambazi? Kama ni CHADEMA kinaongoza na kina tabia ya ufisadi na uzembe kama ya CCM unadhani nitaichekea kwa sababu tu ni CHADEMA. Kitu ambacho watu mnatakiwa mjuwe ni kuwa tunaipinga CCM siyo kwa sababu ya jina au rangi ila ni kwa sababu ya kung'ang'ania kwake madaraka huku wamefeli kila kitu. Unaleta uchawa hapa na kusema uchawa ni kawaida?
 
Uhalisia wa kushirikiana na majambazi? Kama ni CHADEMA kinaongoza na kina tabia ya ufisadi na uzembe kama ya CCM unadhani nitaichekea kwa sababu tu ni CHADEMA. Kitu ambacho watu mnatakiwa mjuwe ni kuwa tunaipinga CCM siyo kwa sababu ya jina au rangi ila ni kwa sababu ya kung'ang'ania kwake madaraka huku wamefeli kila kitu. Unaleta uchawa hapa na kusema uchawa ni kawaida?
You are a politician, Sir.

You try to view everything politically.

Ni sawa. Kama umeamua hivyo.
 
Hakuna atakaekusaidia kuishi maisha yako zaidi yako. Acha aishi maisha yake, mtu akishafikia hatua ya kujiona yupo sawa na wakati hayupo sawa sio jambo jepesi kumtoa huko alipo, unadhani familia yake imempotezea?
Mkuu Chidibenz angekua kaka ako ,sidhani kama ungemuacha aendelee kuishi maisha anayoishi sasa
 
Kama unaikumbua series ya Narcos, kuna afisa wa CIA alitoa kauli hii:

" Cocaine hijacks the pleasure centers in the brain. A rat will choose cocaine over food and water. It would choose cocaine over sleep, over sex over life itself".

Usijaribu hii kitu coz kutoka ni ngumu mno kwani mbadala wake ni ngumu kupatikana! Kaulize madaktari wa ubongo watakuambia kwa nini ni ngumu kutoka.

Mfano huo hapo juu kuhusu panya na cocaine kwenye maabara! Aliwekewa cocaine na hivyo vingine lakini bado akachagua cocaine!

Unaacha chakula, maji, mapenzi,usingizi na hata maisha yenyewe kisha unachagua cocaine!
Hio ni noma mzee😁 hadi mbususu unaiona sio kitu
 
teja ni teja tu hata angepewa bilions atabaki kuwa teja. Kinachomsumbua ni kile alicholisha ubongo wake. Nakumbuka miaka flani Ray C kabla na yeye hajawa teja aliwahi kusema Chd Benz anatumia Madawa ya kulevya kilichofuata alimkung'uta ngumi za kutosha. Hivo suala ni la kwakwe yeye mwenyewe si la jamii wala taifa. Kipindi anafanya mziki mdo kipindi na wanzake kina Sugu. AY, FA , Lady JD na wengine pia walikuwa wanafanya mziki, wao waliwezaje kusastain?
Nikurekebishe kidogo, kipindi Ray c anasema Chidibenz ni teja, Tayar Ray c alishakua amepitia uteja ila akapata bahati ya kusaidiwa ,alivyo recover ndo akasema bado wasanii wengi wanahitaji msaada wa kupelekwa rehab akamtaja Chidibenz
 
Sema vizuri anakaa maskani kwa Konde au maskani kwa nani?
Chidibenz kwa sasa yuko pale msasani maskani ya mateja, ukiiona hiyo sehemu wanapokaa utasikitika sana,
 
Back
Top Bottom