Hali ni tete Mtwara Leo, Sakata ya Gesi

baada ya kutoridhishwa na bajeti ya nishati na madini vurugu zimeshaanza mitaa ya Magomeni, Soko kuu na Coco beach Pande za mtwara ....
nimetulia ndani naskizia mabomu yanavurumishwa ...
for more updates stay tuned ....


Kwenye red hapo kama uko ndani tutapate updates????????????????????????????


kama sio za kutunga!:kev:
 
mbona naona wamejaa vina wetu wale wanaopewa 5000 ili wafanye fujo hii siyo ya mtwara nzima bali ni kundi la wahuni.
 

acha utoto, nguvu ya umma siku zote hailinganishwi na askari. Asikari wenyewe hawafiki hata laki mbili wa majeshi yote. Je utalinganisha na raia zaidi ya milion 30 wenye uwezo wa kupigana? nyie ndo mnawapa watu hasira na baadae watu wakiamua kufanya kweli mnabakia kuwayawaya Unafikiri misri, tunisia na kwingineko kulikuwa hakuna askari ? jifunze busara na si zarau za kitoto hizo zinazoweza kuleta madhara makubwa .
 
Mji mkongwe wa Mikindani hali ni ngumu. Vurugu zimetawala na ofisi za serikali ze mitaa karibia yote zimeteketezwa kwa moto ikiwemo ofisi ndogo ya Mbunge wa Mtwara mjini.

Polisi wameingia Mikindani kupitia bahari baada ya barabara zote zinazoingia na kutoka kufungwa na wananchi wenye hasira. Hali ni tete kwani kuna boti mbili zinapeleka askari kwa wingi huko.

Chanzo: Ndugu aliyeko huko.
 
Cvm wanayataka wenyewe .. Suala la kutumia diplomasia kulimaliza wao hawataki hawajali wanatumia nguvu.. No wonder hadi bungeni wanamwaga mitusi ya nguoni
 

tumia akili,kwani mtwara mpo watu m 30?
unadhani bunduki moja ya askari ina replace raia wangapi wenye mawe?MTU UMEJIFUNGIA NDANI HALAFU UNAPIGA KELELE ETI,HAITOKI,!Hizo c ndizo kelele zenyewe za chura?
 
Ni milio ya risasi na Mabomu kila kona Polisi wanapambana na Wananchi wenye hasira baada ya serikali kutangaza azma yao ya kusafirisha gesi kwa bomba kwenda Dar.kauri za wanasiasa zilizo jaa jazba wakiongelea mbali na eneo la tukio wamekwisha sababisha maafa.Nani wa kutunusuru na balaa hiliiiii
 
Hakuna haja ya kunusuliana,mambo mdundo kama syria,acha tuharibu vizazi vijavyo watarekebisha.
 
Serikali Mtwara haipo kwa sababu mkuu wa mkoa angejitokeza na wananchi wakakaa kwenye uwanja wa wazi wasikilize wote hotuba ya waziri wa nishati na madini ,ili kwa pamoja weka usalama wa mtwara sasa serikali mtwara imejificha imeacha jeshi la polisi wameteka mji wanadhani wananchi watakubali hawawezi kukubali
 

TBC Kuna watendaji wa ovyo sana wasiojua saikolojia. Ilipaswa sana leo hii wananchi hawa waachwe wasikilize hotuba yooooote bila kuingiliwa ili wasikie Waziri atasemaje kuhusu gesi ya Mtwara. Hata kama hotuba hii ingezungmza mazuri kwa wana Mtwara na gesi yao TBC kuzima matangazo ya TV kumeleta hisia mbaya kwamba kitakachosemwa kitakuwa hakina maslahi kwao. TBC huku wakidhani kuzima matangazo kungesaidia kuleta amani ikifananishwa na ndege aina ya kware ambaye huficha kichwa chake akiwa amefumba macho akidhani haonekani kisa kwasababu yeye mwenyewe haoni kumbe kwasababu kafumba macho, ndivyo TBC walichokifanya. TBC wamejaribu kuzima matangazo yao lakini siyo hisia za wana Mtwara na umoja wao.

Sasa kama kawaida CCM kupitia Nape watakuja na yao kwamba waliochoma ofisi hizo ni CUF au CHADEMA. La hasha si hao bali ni MAGAIDI
.
 
kwa jinsi wana mtwara walivyodanganyika, hata kama serikali itaamua kumjenge nyumba kila mtu na kumpa mtaji wa biashara, hawatakubali. wamedanganyika kweli. hivi kwa ile speech ya leo ya waziri wa nishati na madini kulikuwa na sababu kweli ya wana mtwara kuleta fujo? au kwa vile ndo hawajaisikia
 
kwa nini sasa jengo la ccm lichomwe moto? hawa watu wana malengo gani?
Unashangaa hilo mbona Masasi walichoma ofisi ya Halmashauri, magari yaliyokuwepo mpaka jengo walilokuwa wanatumia manesi wanafunzi kama hosteli. Haya na manesi wanahusika vipi hapo?
 
Tanzania nzima TBC 1 haionekani mpaka kwa satelite usije sema ni mtwara kwa 7bu ya badget unakosea ila kama umefanikiwa kuwa na king'amuzi umeona badgeti iko poa na wala sina tatizo nayo kama itafanikishwa kwa yaliyosemwa na waziri. Ila TBC kukatisha matangazo ni nchi nzima sio kusini pekee jarb kuwa mtafitiii

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…