Updates: Yanayojiri Mtwara - hali bado tete (Mei 23/24, 2013)

Updates: Yanayojiri Mtwara - hali bado tete (Mei 23/24, 2013)

AirTanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 17, 2011
Posts
1,139
Reaction score
1,040
  • Mabasi 5 ya Champion yamebeba Wanajeshi yako njiani yanakuja.
  • Serikali yatoa tamko yasema watu 91 wanashikiliwa.
  • Bunge laahirishwa tena. Kupisha uchunguzi na kuepusha uchochezi kutoka kwa baadhi ya wabunge. (Kwa mujibu wa Spika)
  • Maeneo ya Magomeni, Chikongola, Nkanaledi, Mikindani maaskari wanaingia majumbani mwa watu na kumsomba mtu yeyote ambaye ni mwanaume awe amehusika awe hajahusika na kumkamata. Pia inaripotiwa na uhalifu unafanywa na maaskari hao hao. Jambo linaloamsha hisia kwa wananchi.
  • RPC anaongea na vyombo vya habari na kuwasihi wananchi waende makazini. Lakini kiuhalisia hali sio shwari.
  • Mahakama ya mwanzo ya Mitengo imechomwa moto
  • Mpaka sasa ni vita baina ya wananchi na maaskari. Mabomu yamesikika pamoja na milio ya risasi masaa 24. Na milio ya Risasi na mabomu inaendelea kusikika.
  • Raia wapatao 7 wameripotiwa kufariki (wengine walipelekwa hospitali ya Ndanda Ndogo na mmoja ameripotiwa kupokelewa Ligula.

  • Nyumba za viongozi zinaendelea kuchomwa moto.

  • Majibizano baina ya Polisi na Raia yanaendelea maeneo ya Magomeni, Nkanaledi na Mikindani.

  • Maduka yamefungwa na hakuna huduma zozote

  • Barabara zimewekwa vizuizi magogo na matairi yamechomwa moto. Hakuna njia ya kupita.

Update: Mabomu yametulia. Hali ya ukimya imetawala.

Update:

  • Maduka maeneo ya Magomeni yamechomwa moto ikiwamo pia mali za Askari magereza na uhalifu ukifanyika vidole vinawaelekea Polisi.
  • Afisa Usalama wa Taifa ambaye anamiliki nyumba ya wageni naye amevamiwa na kuporwa mali ikiwamo fedha katika gesti yake. Haijajulikana ni kiasi gani cha mali kilichopotea.
  • Mwanafunzi wa CHUNO afikishwa hospitali Ligula na majeraha ya risasi mguuni.

Update:

  • Mwanamke anayekadiriwa miaka 25 mjamzito auawa kwa kupigwa risasi maiti ipo Ligula.

--Magomeni A hatuna amani, askari POLISI wanaingia nyumbani kwetu, wanatupiga na kutunyang'anya simu, yaani huku Magomeni hatuna amani kabisa, tumepotezana na watoto na hatujui hata wake/waume zetu wako wapi

--Mwanadada mjamzito alibakwa na askari Polisi kisha kupigwa risasi. Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Mohamedi Kodi alithibitisha kupokea mwili wa mjamzito ukiwa na tundu tumboni, linaloaminika kuwa linatokana na risasi.

--Umati wa watu wengi wao wakiwa kinamama na watoto umemiminika kwenye Hospitali ya Ligula kukimbia msako wa nyumba kwa nyumba unaofanywa na polisi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

--Wakazi wengi wamelalamikia kitendo cha POLISI kuingia katika makazi yao, kuwapiga na kuwapora mali zao. Magomeni A askari wanaingia nyumbani kwetu, wanatupiga na kutunyang'anya simu, yaani huku Magomeni hatuna amani kabisa, tumepotezana na watoto

--Hadi sasa huduma za kijamii zimesimama, hakuna maduka yaliyofunguliwa, hakuna usafiri wa daladala wala pikipiki, mji upo kimya huku sauti za milio ya mabomu na bunduki ikitawala, wanajeshi waliovalia sare wametapakaa sehemu mbalimbali za mji wakiwa katika magari na pikipiki.

--Pamoja na Nchimbi kufika, Pia ndege kubwa ya jeshi nayo ilitua huku na wanajeshi walikuwa wakipakua vitu mbalimbali vilivyoaminika kuwa vifaa.

--Polisi wamechomba nyumba nyingi sana za raia maeneo tofauti baada ya Waziri Nchimbi kuwasili

Kituo cha televisheni cha ITV kimerusha habari usiku huu kuhusu vurugu zilizojitokeza kwa takribani siku mbili huko Mtwara. Taarifa hiyo imelitaja waziwazi jeshi la Polisi kuhusika na uchomaji wa nyumba za raia na kufanya uharibifu wa mali katika kile kile kilichoelezwa kusaka wahalifu.

Mwandishi wa ITV aliyeripoti habari hiyo kutoka Mtwara amesema "...kwa upande mwingine askari Polisi wameonekana wakichoma nyumba katika kusaka wahalifu waliochochea vurugu hizo..."

Nimejaribu kuploud voice clip ya mwandishi huyo lakini naona network inasumbua. Naendelea kujaribu ikikubali nitaweka wakati mjadala unaendelea.

NB: Jeshi la Polisi limeshutumiwa kuendeleza ghasia za Mtwara badala ya kuzituliza. Imeripotiwa katika vyombo mbalimbali kuwa Polisi wameongeza maafa Mtwara. .
==========================
Matukio katika Picha
==========================


mtwara.jpg


attachment.php


mtwara.jpg



912692_525451360851524_254745933_n.jpg


975602_525452254184768_555502831_n.jpg
 
Wakuu leo Mtwara hali nI mbaya zaidi kuliko jana kwa vitendo viovu VINAVYOFANYWA na askari wa jeshi la polisi.
Iko hivi;
-Polisi wanafyatua risai za moto kwa raia
-wanavunja mabanda ya biashara ya raia na kupora mali, fedha na chochote kilichopo KISHA KUYACHOMA MOTO
-Wanasachi na kunyang'anya fedha, simu na chochote alichonacho mfukoni kisha wanamjeruhi vibaya yeyote wanayekutana naye bila kujuwa kuwa ni nani
-wanavunja nyumba za raia na kubeba wanachoona kinawafaa

NB: Vijana wengi hasa wa mitaa ya Majengo, Mdenga na Magomeni wameyakimbia makazi yao wako mafichoni nje kdogo ya mji
 
Kikwete asifikiri anaongoza familia yake, jeuri yake itamtokea puani, Busara inahitajika katika kuongoza nchi, viongozi waliokosa busara na wasio na heshima kwa wananchi hawana nafasi katika Jamii yetu. Wasifikiri hii nchi ni yao, wajue kuwa nchi hii ni ya Watanzania kama wameshindwa kuongoza waondoke hatuwalazimishi na hakuna aliyelazimishwa kuongoza hii nchi.
 
unapenda wenzako waendelee kufa mkuu? washauri wakaze buti kufanya kazi,serikali sikivu ishawapuuzia toka mwanzo mwa vurugu hizi mpaka sasa,usishangae jeshi likajenga kambi kabisa huko,

japo kuna mda unashindwa hata usimame upande upi kwa haya yanayotokea,ila historia inajieleza,hapa dar wamachinga walipingwa virungu toka enzi za makamba,leo neema imehamia kwao ili wasije dar ila serikali imegeuza kuwa laana kwao,kwani serikali ikijenga kiwanda pale itapoteza nini?
 
Kikwete awe mwangalifu hii nchi ni ya watanzania wote, yeye alichonacho ni dhamana ya uongozi ambayo ina hatima yake, sasa asijisahau akadhani aliinunua hii nchi kama mali yake,mamba yakizidi kuharibika huko mtwara ata ambao anadhani wako naya karibu watamruka maili mia...hapo ndio ataelewa busara inanguvu kuliko liburi na ubabe
 
Wakuu leo Mtwara hali nI mbaya zaidi kuliko jana kwa vitendo viovu VINAVYOFANYWA na askari wa jeshi la polisi.
Iko hivi;
-Polisi wanafyatua risai za moto kwa raia
-wanavunja mabanda ya biashara ya raia na kupora mali, fedha na chochote kilichopo KISHA KUYACHOMA MOTO
-Wanasachi na kunyang'anya fedha, simu na chochote alichonacho mfukoni kisha wanamjeruhi vibaya yeyote wanayekutana naye bila kujuwa kuwa ni nani
-wanavunja nyumba za raia na kubeba wanachoona kinawafaa

NB: Vijana wengi hasa wa mitaa ya Majengo, Mdenga na Magomeni wameyakimbia makazi yao wako mafichoni nje kdogo ya mji

Mkuu, kuna uwezekano wa kutupia picha mbili tatu?
 
Nadhani ni Wakati sasa Serikali itafakari upya mpango wake wa ujenzi wa bomba la gesi. Ni vyema iyo gesi ivunwe huko mtwara, plant ya kufua umeme ijengwe huko huko na kisha umeme usafirishwe kwa njia ya Nguzo.

Naamini gharama za kusafirisha gesi kwa bomba kuja Dar na kisha kujenga plant kwa ajili ya kufua umeme ni kubwa kuliko ujenzi wa Plant huko huko Mtwara. Wanamtwara wanataka kufaidi 'Multiplier effect' ya ujenzi wa plant ya kufua umeme huko Mtwara na sio kwamba hawataki Watanzania wengine wafaida matunda ya gesi.

After all, Annual maintanance ya Bomba ni kubwa kuliko Annual maintanance ya nguzo za Umeme. Tutafakari!
 
Wakuu leo Mtwara hali nI mbaya zaidi kuliko jana kwa vitendo viovu VINAVYOFANYWA na askari wa jeshi la polisi.
Iko hivi;
-Polisi wanafyatua risai za moto kwa raia
-wanavunja mabanda ya biashara ya raia na kupora mali, fedha na chochote kilichopo KISHA KUYACHOMA MOTO
-Wanasachi na kunyang'anya fedha, simu na chochote alichonacho mfukoni kisha wanamjeruhi vibaya yeyote wanayekutana naye bila kujuwa kuwa ni nani
-wanavunja nyumba za raia na kubeba wanachoona kinawafaa

NB: Vijana wengi hasa wa mitaa ya Majengo, Mdenga na Magomeni wameyakimbia makazi yao wako mafichoni nje kdogo ya mji

Jana si ulimsikia amiri jeshi mkuu wao akiwaambia wasiishie kung'oa meno na kucha tu bali wang'oe na mapembe pia.

Badala ya kutafuta ufumbuzi wa kudumu kwa tatizo lililo mbele yao wao wanaongeza chuki, hasira na uhasama ambao hautaisha leo wala kesho.
 
Nadhani ni Wakati sasa Serikali itafakari upya mpango wake wa ujenzi wa bomba la gesi. Ni vyema iyo gesi ivunwe huko mtwara, plant ya kufua umeme ijengwe huko huko na kisha umeme usafirishwe kwa njia ya Nguzo.

Naamini gharama za kusafirisha gesi kwa bomba kuja Dar na kisha kujenga plant kwa ajili ya kufua umeme ni kubwa kuliko ujenzi wa Plant huko huko Mtwara.

After all, Annual maintanance ya Bomba ni kubwa kuliko Annual maintanance ya nguzo za Umeme. Tutafakari!

Wewe unaona vyema lakini wale waliopewa dhamana siamini kama kweli akili zao zinafanya kazi sawasawa. Kila kukicha wanalaumu upinzani ; hivi kweli upinzani ndo umefanya maisha ya wanaMtwara kuwa magumu hadi kufikia hatua waliyo nayo?
 
Sasa kukamata wanaume wote na kuwasweka ndani manake nini si nikuzidisha mgogoro kama watu wako ndani ya nyumba zao kwa nini kuwavunjia nyumba zao
 
Back
Top Bottom