Hali ni mbaya sana, nazidi kudhoofika

Hali ni mbaya sana, nazidi kudhoofika

Naja naja

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2016
Posts
747
Reaction score
1,559
Hali ya sasa ya kimaisha hairidhishi hata kidogo. Kimbilio la vijana wengi lilikuwa ni viwandani ila kwa sasa hata huko viwandani kazi hakuna.

Viwanda vingi uzalishaji ni mdogo mno kiasi kwamba hata wale vibarua permanent nao hawapati nafasi ya kuingia kazini
Viwanda vingine navyo vimefungwa na haijulikani lini wataanza tena kufanya kazi.

Vile viwanda ambavyo miaka ya nyuma vilikuwa vikikimbiwa na watu kisa ugumu wa kazi navyo siku hizi hata ukienda hupati nafasi maana kumejaa

Mfano mzuri ni kiwanda cha nondo kilichopo Jeti siku hizi nafasi ni adimu mno. Viwanda vingine vibarua wazoefu hawataki kuachia nafasi wanaunga shift usiku na mchana hawataki kutoka.

Viwanda vingine hawakupokei mpaka uhonge au uwe na mtu anayekujua mf kiwanda cha Pepsi ,Jambo ,kiwanda cha kioo,serengeti nk

Viwanda vingi sana vimefungwa mf Kiwanda cha Jumbo,Murzah one.Murzah Two.

Vibarua wanakimbilia Murzah four napo kazi hakuna uzalishaji mdogo mno.

Kiwanda kingine ni kiwanda cha samaki ila napo wanachukua idadi ndogo mno haswa wale wazoefu na wanawake

Kiwanda cha rasta napo siku hizi pagumu mno.

Vijana tunakufa njaa
 
Mkuu ajira milioni 6 hukupata. Anyway usijali kuna ajira nyingine milioni 8 zinatengenezwa kwaajili ya wanyonge🤣

Vile vile Kuna miradi mingi ya Maendeleo kama Flyover, Stigler's gorge, SGR, bomba mafuta n.k huko kote ajira kibaooooo.

Anyway tuko UCHUMI WA KATI. Nchi inapaa kuzidi "URAYA" au ulikuwa mpiga deal.
 
Mkuu ajira milioni 6 hukupata [emoji1787]

Kuna miradi mingi ya Maendeleo kama Flyover, Stigler's gorge, SGR, bomba mafuta n.k huko kote ajira kibaooooo.

Anyway tuko UCHUMI WA KATI. Nchi inapaa kuzidi "URAYA" au ulikuwa mpiga deal.
Hizi tabia za kudhihaki wenye shida zinazidi sasa, muda mwngne kama huna Cha kusadia hata kimawazo ni bora upige kimya tu
 
Back
Top Bottom