Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,947
- 4,445
Kuna sehemu niliona Topic ya Maisha bora kwa kila Mtanzania nimeitafuta nimeikosa sijui imepotelea wapi. Haya ndo maisha yetu sisi wadanganyika hii ni moja kati ya Zahanati hapa hapa Tanzania tulipo aahidiwa maisha bora kwa kila Mtanzania matokeo yake huduma muhimu za msingi tunakosa,kama vitanda, madawa huyo mgonjwa hapo juu kapigwa dripu la maji baada ya kukosa dawa. Hali kama hii itakoma lini jamani?
Ndugu zetu vijijini wanateseka sana kweli mtu yupo hospitali analala kwenye kitanda cha kamba dah inasikitisha sana.