Half Mtanzania na Figure Skating kwenye Olympic

Half Mtanzania na Figure Skating kwenye Olympic

Meticulously speaking, hakuna mtu anayeitwa Abdulhalim. 'Abdulhalim' follows a social convention of naming in context of social oversimplification. In the same way, hakuna nchi inayoitwa Tanzania, na hakuna mtu anayeweza kunithibitishia kuwa ana asili ya Tanzania.

He kweli akili nyingi huondoa maarifa eti hakuna nchi inayoitwa Tanzania,hivi neno nchi lina maana gani?
 
Baba yake anaitwa nani ?mbona hamsemi,kwani jina la mwisha si la kitanzania
 
baba yake anaweza kuwa prominent doctor hapo Muhimbili au so,maana walionana na kijana huyu mara yua kwanza Vienna ,wakati baba mzazi alikuwa kwenye meeting huko Vienna
 
Akishinda we can claim him...kama hajashinda abaki na uraia wake wa Kijerumani
 
Alikuwa anapewa nafasi kubwa ya kupata Gold Medal kufuatia kufanya vizuri sana katika mashindano ya awali J'pili ambapo yeye na mwenzie walikuwa wanaongoza. Jana bahati mbaya yeye akaanguka na pair mbili za Wachina kuwapita na hivyo wao kuambulia Bronze medal. Alipomaliza alijua hataweza kupata gold alitia huruma sana kwa kuonyesha wazi frustration yake ya hali ya juu hasa ukitilia maanani yeye na mwenzie kama sikosei ni mabingwa wa dunia katika mchezo huo kwa miaka miwili mfululizo.
 
Naona huwafahamu Wazungu wewe.

Akifanya kitu cha aibu utashangaa watakavyompamba kuwa ni Mtanzania kafanya hivi au kile.

Freddy Mercury, mwimbaji wa kundi la Queen alipokufa UK, magazeti yakaandika "MTANZANIA AFA KWA UKIMWI". Kuna Utanzania wa damu na Utanzania wa makaratasi. Mie hapa leo nina makaratasi ya Botswana (hihiiii), ila kwa damu bado ni Mtanzania.

Mimi sijauliza wazungu wanamconsider nani. Mimi nimeuliza yeye mwenyewe anaji consider nani? Mjerumani au Mtanzania?
 
Tatizo letu kubwa ni kuzaa na kutelekeza we dont play role in raising those kids until when they become famous then we start point fingers on them oh you know he/she is a Tanzania or wherever any African country be it.

Na sik zote mtoto aliye telekezwa anayefuatwa baada ya kufanikiwa lazima ajiuliza mara mbili mbili. Je isingekua hiyo figure skating huyu jamaa tungemtaja leo hii?
 
He kweli akili nyingi huondoa maarifa eti hakuna nchi inayoitwa Tanzania,hivi neno nchi lina maana gani?

Inategemea unatumia scale gani ktk kutoa conclusion. Basi ni kama mfano wa sisimizi na kidimbwi cha maji, au mfano wa tembo na kidimbwi cha maji. Wewe waonaje?
 
Salam kwako mzee wa Saikong,

kumbe mzee wewe hii sheria ya dual citizenship inavyopigwa danadana hupati tabu kabisa manake uliyopenya penya hadi umekamata makaratasi ya Botswana!!

Btw: watu wengine huwa hawataki kukubali kukiri ukweli mdomoni,ingawa akilini anakusoma vizuri sana.Unajua kuna watu wasioweza kujitambulisha utanzania wao wakishavuka mipaka ya ubalozi wao wa nyumba kumi, kwahiyo achana nao ndivyo waliyo.

Hivi ule mpango wa kuingia kilingeni kupambana na Saidi Nkumba bado upo au umetupa kule!

Mkuu Mwita,

Umenifurahisha na hilo jina la SAIKONG. Sijui umelisikia wapi. Lakini naona utakuwa mwenyeji wa mitaa ya Tutuo vile kama siyo Sikonge kwenyewe. Maana wengine ndiyo tumetulia hapa Usupilo na nina kimeza changu pale kwenye Mizambarau (madukani kwa akina Sabena).

Makaratasi ya Botswana ilibidi niyatafute maana yule Mchina wa Botswana alinifurahisha sana na nikaamua kwenda kumtafuta. Kufika kule nikaona mambo ndiyo haya sasa. Watoto wa Kitswana poa kabisa nikavuta mmoja 🙂 Na wao wakanipa asante ya makaratasi.

Yule Said Nkumba naona safari hii sintawahi. Kuna vijana wanaenda shule na kuchukua pesa kuzipeleka wenye kampeni (kamari) itakuwa ni risk sana na hasa kwa maisha ya vijana hapo mbeleni. Nimeamuwa nivute muda kidogo. Ila ntaangalia mpinzani wake ni nani na kama ni mzuri basi ntamsaidia safari hii ila uchaguzi ujao, ntaingia mwenyewe Mjengoni. Watanzania wakiniuliza makaratasi, ntawaambia kwanza mimi ni Mwanangwa na pili ntavuta katoto ka Kinyamwezi na nipate tena makaratasi ya Tanzania. Nashangaa watu wanalilia uraia wa Tanzania, si unaowa/kuolewa tu na binamu yako na ngoma imekwisha?
 
Mimi sijauliza wazungu wanamconsider nani. Mimi nimeuliza yeye mwenyewe anaji consider nani? Mjerumani au Mtanzania?

Si unaona hata nguo alizovaa hapo? Angelikuwa hataki kujiona ni Mtanzania/Mwafrika basi wala hiyo kitu asingelivaa. Mwisho nimesema kuwa bila ya kujali yeye anajiona ni nani, kama ameishi kwenye miji midogo na hasa East German, basi huko atakuwa kashashambuliwa si mara moja. Kama alikutana na baba yake, sidhani kama ilikuwa kwa bahati mbaya. Mwisho wa siku inabidi sisi Watanzania tumwambie "welcome home son" na si kutegemea mwenyewe ajilete kichwakichwa kuwa mie ni mwanenu. Siyo wote ni kama Obama.

Na sik zote mtoto aliye telekezwa anayefuatwa baada ya kufanikiwa lazima ajiuliza mara mbili mbili. Je isingekua hiyo figure skating huyu jamaa tungemtaja leo hii?

Mkuu, nimeandika hapo nyuma kuwa sheria za German ni kali sana kwa watoto. Utake usitake, mtoto aliyezaliwa German, milele atabaki kuwa Mgeruman na hii itabadilika tu siku akiwa mtu mzima na yeye mwenyewe aende kuchukua gamba la nchi nyingine. Hii haijalishi mtoto ana baba au mama wa German. Hivyo unakuta mchezo rahisi sana unafanyika. Wewe unanyimwa VISA au unakataliwa kufanya kazi na hapo unakuwa huna ujanja ila kurudi kwenu. Mamaa akisema yeye hataki kwenda Africa utamfanyaje? Ukijifanya Mjanja basi POLIZEI wamekugongea mlangoni......
 
Back
Top Bottom