The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,186
- 4,939
"Lakini pia, Mheshimiwa Rais, kulikuwa na madai ya kuwepo makaburi ya halaiki. Kulikuwa na madai hayo kupitia vyombo vya habari vya kimataifa na mitandao ya kijamii kuhusu uwepo kwa makaburi ya halaiki eneo la makaburi ya Kondo, Kunduchi, Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam.Tume imefanya uchunguzi ikiwa ni pamoja na kutembelea na kukagua eneo la makaburi, kufanya mahojiano na kupata taarifa ya afisa msimamizi wa makaburi hayo kutoka Manispaa ya Kinondoni na kuchukua ushahidi wa wasimamizi wa makaburi ya Kondo.
Tume pia imeshirikisha wataalamu mbalimbali ili kufanya uchunguzi wa kisayansi kuhusu madai hayo ikiwa pamoja na picha za satellite zilizotumika kuleta madai hayo. Maoni ya wataalamu hao wakiwemo wachambuzi wa mbalimbali wa mifumo ya taarifa za kijiografia, Remote Sensing and Geographical Information System, ni kwamba madai hayo hayakuweza kudhibitishwa.
Soma Pia Uchunguzi wa CNN wasema huenda kaburi la halaiki lipo katika Makaburi ya Kondo, Dar es Salaam
Lakini Tume pia ilifanya ukaguzi na kubaini kuwa eneo la makaburi ya Kondo limezungukwa na makazi ya watu na ambayo bado linatumika kwa shughuli za kilimo cha msimu na lina ulinzi muda wote.
Kwa upande wa ushahidi na uchunguzi wa Tume wa uandani na kuzingatia hali ilivyoonekana katika eneo la makaburi hayo pamoja na taarifa za wataalamu wa uchunguzi wa kisayansi, Tume imebaini kuwa madai ya kuwepo kwa makaburi halaiki eneo la Kondo hayakuweza kuthibitishwa." - Jaji Chande