Samson Ngomboli
JF-Expert Member
- Oct 30, 2019
- 1,431
- 2,243
EPACopyright: EPA
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu pia ametoa taarifa baada ya kukutana na waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken mjini Tel Aviv hii leo.
Alitaja shambulio baya la Jerusalem leo asubuhi, ambalo Hamas ilidai kuwa lilitekelezwa na wanachama wake. Netanyahu alisema ni "Hamas hao hao ambao wanajaribu kutuua kila mahali". "Nilimwambia: Tumeapa, nimeapa, kuwaondoa Hamas. Hakuna kitakachotuzuia."
Netanyahu anasema alimwambia Blinken kwamba Israel itaendeleza vita hadi ifikie "malengo matatu", ambayo anasema ni: "Kuwaachilia mateka wetu wote, kuwaondoa kabisa Hamas na kuhakikisha kwamba hakuna tishio kama hili litakalotokea tena kutoka Gaza."
BBC Swahili
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu pia ametoa taarifa baada ya kukutana na waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken mjini Tel Aviv hii leo.
Alitaja shambulio baya la Jerusalem leo asubuhi, ambalo Hamas ilidai kuwa lilitekelezwa na wanachama wake. Netanyahu alisema ni "Hamas hao hao ambao wanajaribu kutuua kila mahali". "Nilimwambia: Tumeapa, nimeapa, kuwaondoa Hamas. Hakuna kitakachotuzuia."
Netanyahu anasema alimwambia Blinken kwamba Israel itaendeleza vita hadi ifikie "malengo matatu", ambayo anasema ni: "Kuwaachilia mateka wetu wote, kuwaondoa kabisa Hamas na kuhakikisha kwamba hakuna tishio kama hili litakalotokea tena kutoka Gaza."
BBC Swahili