Fall Army Worm
JF-Expert Member
- Jan 8, 2015
- 19,371
- 14,481
Waheshimiwa Sana Wana JF, Hbr za jioni? Kama kichwa kinavyosema katika mapito niliyopitia nimegundua kuwa hakuna Binadamu "ANAYEKUPENDA KWA DHATI',. Mwenye upendo wa dhati nawe ni Mwenyezi MUNGU aliyekuumba na kukupa Pumzi na riziki na Wazazi wako tu waliokuzaa na kukulea vema.
Fuatilia visa hivi.
Mimi Nilikuwa na rafiki yangu mkubwa ambaye tulikuwa tunasaidiana ktk shida na raha, Lakini kuna wakati nilikuja kuyumba Sana kimaisha jamaa alikuwa vizuri, Siku moja nikaomba anikopeshe 50,000/= (Elfu hamsini tu),jamaa alikataa kunikopesha kuwa hana Hela wakati huo Mimi najua jamaa ana pesa kwasababu yeye mwenyewe alikuwa anasema kuhusu mipango yake na baada ya hapo akaanza kupunguza mawasiliano na ukaribu.
Rafiki zangu wengine waliacha kabisa kuwasiliana na Mimi, wakati nilipokuwa na hali nzuri kiuchumi walikuwa ni watu safi sana wakionyesha kuwa Wana upendo wa dhati kwangu, Kumbe sivyo.
Kisa kingine ni Cha mdogo wangu,huyu alipatwa na matatizo makubwa hadi kufungwa jera,aisee marafiki zake aliokuwa akijidai nao kuwa oh!, Mimi Nina rafiki wengi tulioshibana, aisee walijiweka mbali sana na shida hiyo hata kwenda gerezani hawakwenda,hata kuulizia tu maendeleo yake hawakuthubutu kabisa.Alipotoka ndio wakawa wanakuja kwa aibu wanasema eti "Tuliogopa kuja gerezani", Wengine wakasema "Tulikuwa na mpango wa kuja baadaye", wakati mtu amekaa jera miezi minne.
Hitimisho
Ndugu yangu/zangu ukiwa vizuri kimaisha,kwa maana ya kazi nzuri, biashara nzuri,cheo kizuri,n.k.Usije ukalewa sifa kutoka kwa rafiki zako hao wanakupendea nafasi uliyonayo na si wewe, ukitaka kuthibitisha hilo hebu pata msukosuko kidogo uone jinsi jamaa zako watakavyotoka nduki.
Hivyo ushauri wangu ukiwa na nafasi nzuri jari kwanza Wazazi wako,Famili Yako,Bila kumsahau Mwenyezi MUNGU;Km unataka kumsaidia mtu msaidie tu km Ibada tu na si kutegemea kurudishiwa fadhila. Kuwa na Marafiki ni kitu kizuri lakini uwe mwangalifu,ishi nao huku ukijua wazi kuwa siku mambo yakikuendea mrama lazima hao marafiki zako wakukimbie au wakusaliti.Tujifunze pia kupitia kwa Yesu namna Wanafunzi wake walivyomkwepa wakati wa Mateso yake.
Fuatilia visa hivi.
Mimi Nilikuwa na rafiki yangu mkubwa ambaye tulikuwa tunasaidiana ktk shida na raha, Lakini kuna wakati nilikuja kuyumba Sana kimaisha jamaa alikuwa vizuri, Siku moja nikaomba anikopeshe 50,000/= (Elfu hamsini tu),jamaa alikataa kunikopesha kuwa hana Hela wakati huo Mimi najua jamaa ana pesa kwasababu yeye mwenyewe alikuwa anasema kuhusu mipango yake na baada ya hapo akaanza kupunguza mawasiliano na ukaribu.
Rafiki zangu wengine waliacha kabisa kuwasiliana na Mimi, wakati nilipokuwa na hali nzuri kiuchumi walikuwa ni watu safi sana wakionyesha kuwa Wana upendo wa dhati kwangu, Kumbe sivyo.
Kisa kingine ni Cha mdogo wangu,huyu alipatwa na matatizo makubwa hadi kufungwa jera,aisee marafiki zake aliokuwa akijidai nao kuwa oh!, Mimi Nina rafiki wengi tulioshibana, aisee walijiweka mbali sana na shida hiyo hata kwenda gerezani hawakwenda,hata kuulizia tu maendeleo yake hawakuthubutu kabisa.Alipotoka ndio wakawa wanakuja kwa aibu wanasema eti "Tuliogopa kuja gerezani", Wengine wakasema "Tulikuwa na mpango wa kuja baadaye", wakati mtu amekaa jera miezi minne.
Hitimisho
Ndugu yangu/zangu ukiwa vizuri kimaisha,kwa maana ya kazi nzuri, biashara nzuri,cheo kizuri,n.k.Usije ukalewa sifa kutoka kwa rafiki zako hao wanakupendea nafasi uliyonayo na si wewe, ukitaka kuthibitisha hilo hebu pata msukosuko kidogo uone jinsi jamaa zako watakavyotoka nduki.
Hivyo ushauri wangu ukiwa na nafasi nzuri jari kwanza Wazazi wako,Famili Yako,Bila kumsahau Mwenyezi MUNGU;Km unataka kumsaidia mtu msaidie tu km Ibada tu na si kutegemea kurudishiwa fadhila. Kuwa na Marafiki ni kitu kizuri lakini uwe mwangalifu,ishi nao huku ukijua wazi kuwa siku mambo yakikuendea mrama lazima hao marafiki zako wakukimbie au wakusaliti.Tujifunze pia kupitia kwa Yesu namna Wanafunzi wake walivyomkwepa wakati wa Mateso yake.

