Hakuna aliyeweza kujibu hoja ya Zitto Kabwe

Hakuna aliyeweza kujibu hoja ya Zitto Kabwe

Taarifa ya naibu wazir wa fedha haitoshelizi kujibu hoja ya CAG, kama hizo data zilikuwepo walishindwaje kuzitoa kwa CAG , someni report ya CAG mlinganishe na huu utetez wa sasa! Mpaka sasa hakuna aliyejibu hoja za CAG
Unajuaje juu ya utendaji kazi uliopo kati ya waziri na ofisi ya CAG?, kwa naibu waziri kujibu hadharani sio kigezo kwamba haupo utaratibu wa kikazi wa wizara kutoa majibu kwa CAG.

Punguzeni siasa za kukuza mambo ambayo kwa asilimia kubwa hamuyajui vizuri.
 
Mheshimiwa Zitto; kwa wakati tofauti umezungumzia Mawaziri hawana mamlaka ya kujibu hoja za mkaguzi mkuu wa serikali na kufanya hivyo wanaenda kinyume na sheria zilizompa mamlaka CAG. Hata hivyo unataka mawaziri wakujibu hoja mfu ya matumizi ya serikali ambayo unaamini hayakuwa accounted. Kama ulivyosema awali; makatibu wa kuu ambao ni accounting officers watajibu hiyo hoja na CAG akilizika na majibu ataifungwa hiyo hoja na CAG akiona majibu hayajiridhishi italetwa tena itaendelea kuletwa kwa taarifa zijazo. Cha pili chama chako ni moja ya chama ambacho hakikuleta mahesabu yake kukaguliwa kama sheria zinavyohitaji. Hapo unaonyesha ni namna gani chama chako hakitaki kukaguliwa na kuvunja sheria za taifa hili.
 
Mimi nipeni elfu 30 yangu niwaache maana naona mnataka kunidhulumu kama Noah!
 
Mkuu, fuatilia namna ya mfumo mpya wa kihasibu wa acrual basis unavyofanya kazi utaelewa mengi kuhusiana na hizi fedha.

Hayo mengine mengi uliyoyaandika ni siasa zilizozoeleka miongoni mwetu watanzania.
Bukililo mm siyo mtaalamu wa uhasibu hata ww huna huo utaalamu zaidi ya ofisi ya CAG yenye wataalamu waliobobea na wao ndiyo waliotoa hiyo ripoti kuwa kuna fedha hazieleweki zimetumikaje.

Mbona yy kaeleza vizuri wakati anahojiwa na Azam TV na ameliomba bunge lifuatilie ili lipewe maelekezo kutoka serikalini zimetumika vipi. Tafuta hiyo clip
 
Bukililo mm siyo mtaalamu wa uhasibu hata ww huna huo utaalamu zaidi ya ofisi ya CAG yenye wataalamu waliobobea na wao ndiyo waliotoa hiyo ripoti kuwa kuna fedha hazieleweki zimetumikaje.

Mbona yy kaeleza vizuri wakati anahojiwa na Azam TV na ameliomba bunge lifuatilie ili lipewe maelekezo kutoka serikalini zimetumika vipi. Tafuta hiyo clip
Naibu waziri Mama Kijaji akiwa ndani ya bunge ametoa maelezo marefu juu ya hizo fedha. Kama ambavyo CAG aliomba maelezo hayo yatolewe ndani ya bunge.

Mbele ya rais CAG kakanusha siasa za kipuuzi za mheshimiwa Zitto za kutaka kuichonganisha serikali na wananchi.

Huyu Zitto hajaanza leo, enzi za JK alikuwa na michezo hii hii ya kutafuta habari kutoka kwa watu wa serikali halafu anazitumia dhidi ya serikali hiyo hiyo lakini awamu ile iliweza kumvumilia kwa sababu JK alikuwa ni mtu wa kuyachukulia poa mambo mengi tu.

This time JPM ni tofauti sana, hatoi kiki nyepesi nyepesi.
 
Mwenye zile video za yule mwanamama mwenyekiti wa kamati akitolea ufafanuzi wa utetezi wa ripo ya si eijii awetuwekee hapa, naona kuna wengine hawajaiona
 
Lumumba FC kwenye ubora wao wanakataa report inayowahusu.
 
Naibu waziri Mama Kijaji akiwa ndani ya bunge ametoa maelezo marefu juu ya hizo fedha. Kama ambavyo CAG aliomba maelezo hayo yatolewe ndani ya bunge.

Mbele ya rais CAG kakanusha siasa za kipuuzi za mheshimiwa Zitto za kutaka kuichonganisha serikali na wananchi.

Huyu Zitto hajaanza leo, enzi za JK alikuwa na michezo hii hii ya kutafuta habari kutoka kwa watu wa serikali halafu anazitumia dhidi ya serikali hiyo hiyo lakini awamu ile iliweza kumvumilia kwa sababu JK alikuwa ni mtu wa kuyachukulia poa mambo mengi tu.

This time JPM ni tofauti sana, hatoi kiki nyepesi nyepesi.
Huyo zito unayesema enzi ya jk alikuwa anatoa vijimaneno ndiyo vilivyoibua scandal za escrow, epa, Richmond, meremeta mpaka baadhi ya mawaziri waliwajibika na msemo wa mafisadi ulipoanza au hivyo vitu havipo?

Endelea kutetea ila elewa ya kuwa tumeshapigwa. Kama unakumbuka issue ya escrow jk aliongea hadharani kuwa zile fedha siyo za umma leo akina rugemarila wapo wapi? Ila we endelea kutetea tumbo hapa mjini
 
Huyo zito unayesema enzi ya jk alikuwa anatoa vijimaneno ndiyo vilivyoibua scandal za escrow, epa, Richmond, meremeta mpaka baadhi ya mawaziri waliwajibika na msemo wa mafisadi ulipoanza au hivyo vitu havipo?

Endelea kutetea ila elewa ya kuwa tumeshapigwa. Kama unakumbuka issue ya escrow jk aliongea hadharani kuwa zile fedha siyo za umma leo akina rugemarila wapo wapi? Ila we endelea kutetea tumbo hapa mjini
Unahisi kwamba umepigwa na unayo haki yako ya kikatiba kuwa na mitazamo ya namna hiyo.

Umeshajiuliza Zitto ametajirika kiasi gani kupitia hizo kashfa ulizozitaja?.
 
Unahisi kwamba umepigwa na unayo haki yako ya kikatiba kuwa na mitazamo ya namna hiyo.

Umeshajiuliza Zitto ametajirika kiasi gani kupitia hizo kashfa ulizozitaja?.
Nashukuru umeanza kunielewa. Tatizo siyo zito kutajirika kwa vipi hizo scandals hazipo?. Kama zito ametajirishwa basi kwa scandal hii atakuwa tajiri mkubwa sana
 
Nashukuru umeanza kunielewa. Tatizo siyo zito kutajirika kwa vipi hizo scandals hazipo?. Kama zito ametajirishwa basi kwa scandal hii atakuwa tajiri mkubwa sana
Mkuu hii ya trilioni 1.5 sio scandal ni yeye kutoelewa mambo ambayo alitakiwa kueleweshwa kwanza.

Kiburi na ujuaji wake vikamfanya akimbilie kuongea vitu ambavyo vimekanushwa mpaka na mkuu wa nchi.

Malengo mengine ya wanasiasa yana madhara makubwa kwa nchi kama yetu ambayo inawategemea wahisani.
 
Unajuaje juu ya utendaji kazi uliopo kati ya waziri na ofisi ya CAG?, kwa naibu waziri kujibu hadharani sio kigezo kwamba haupo utaratibu wa kikazi wa wizara kutoa majibu kwa CAG.

Punguzeni siasa za kukuza mambo ambayo kwa asilimia kubwa hamuyajui vizuri.

Mkuu tunaelewa mambo , hii ni professional field yangu! Ninajua namna serikali inavyofanya na inavyotakiwa kufanya kazi,siyo lazima pia uwe proffessional uweze kudadavua mambo, ZZK ni mchumi lkn amedadavua hii teport kuliko hata wataalamu kwenye hii field, ndiyo maaana tunasema mpaka sasa hakuna aliyeweza kujibu hizi hoja za kitaalamu zaid ya kufanya personal attacks! Hakuna anaye weka siasa nyie msiofikiria au kujiongezq ndiyo mnaongea siasa.
 
Mkuu tunaelewa mambo , hii ni professional field yangu! Ninajua namna serikali inavyofanya na inavyotakiwa kufanya kazi,siyo lazima pia uwe proffessional uweze kudadavua mambo, ZZK ni mchumi lkn amedadavua hii teport kuliko hata wataalamu kwenye hii field, ndiyo maaana tunasema mpaka sasa hakuna aliyeweza kujibu hizi hoja za kitaalamu zaid ya kufanya personal attacks! Hakuna anaye weka siasa nyie msiofikiria au kujiongezq ndiyo mnaongea siasa.
Naibu waziri ni professional kama wewe kamjibu vizuri tu huyo mheshimiwa, ingia youtube au nunua magazeti uone jinsi Zitto alivyojibiwa.
 
TUNAWEZA KUWA NA HOJA YA MSINGI SANA KUHOJI JUU YA HIZI PESA ILA TUNAKOSEA KUMNYOOSHEA MAGUFULI YA KWAMBA HIZI PESA kaweka mfukoni mwake hapa tu ndipo tunapokosea.....And what if ikithibitika hizi pesa HAZIJAFANYIWA MCHEZO BWOWOTE MCHAFU kama WENZETU upinzani WANAVYOTUMIA NGUVU NYINGI kutuaminisha hivyo???
Mkuu ni kwanini mtu akihoji vitu vya msingi anaonekanza mpinzani?
 
Naibu waziri ni professional kama wewe kamjibu vizuri tu huyo mheshimiwa, ingia youtube au nunua magazeti uone jinsi Zitto alivyojibiwa.

Mkuu nasita ku argue na wewe kwa sababu nahisi huelewi,hoja yangu isome vizur! Huu uzi uliletwa hapa kabla ya majibu ya naibu wazir na rais kulisemea hili, pamoja na yote si rais wala naibu wazir ameweza kujibu hoja za CAG, wameshindwa kujibu kwa sababu hii ni taaluma na si siasa! Nakushauri uisome report ya CAG uchukue majibu ya Rais wetu, pole pole, naibu wazir fedha, kafulila na wengine huenda ukaelewa tunacho zungumza kuliko kudandia hoja na kuzifanya za kisiasa! Na siyo lazima uchangie hoja kama hujui,ama subiri hoja za siasa upate uwanja mpana wa kupambana kwa hoja
 
Back
Top Bottom