harakat
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 2,888
- 1,347
Tumeendeleza mifumo iliyowekwa na wakoloni enzi na enzi hatujafikiria wala kuthubutu kuibadili mifumo hiyo iendane na Sera za Nchi kwa kipindi Fulani.
Elimu yetu ninavyoiona inahitaji mabadiliko makubwa mno vinginevyo tutashindwa kuwashawishi vijana wetu waendelee kuwejeza kwenye Elimu na pia wazazi wataacha kuwekeza kwenye Elimu kama silaha ya kwanza ya kumpatia mtoto kwa ajili ya kupambana na umasikini.
Elimu ya mkoloni ililenga kumpatia cheap labourers kwenye maeneo yake ya kazi ila Elimu yetu ya sasa enatakiwa ilenge kwenye kumkomboa MTU mmoja mmoja kutoka kwenye maisha ya kutaka kuwa mtumwa au kutafuta ajira na kujiajiri yeye mwenyewe na pia kuajiri wengine .
Haiingii akilini tu kuwalaumu vijana wanaotafuta ajira kwenye taasisi mbalimbali kwa kuwaambia wanatakiwa wajiajiri wakati hatukuwaanda kwa hilo.
Ni hivi majuzi tu Waziri Wa Elimu alisema kwamba kwa sasa waalimu Wa masomo ya arts wanatosha .Tusisahau kwamba kuna tundo la waliomaliza masomo hayo na kuna kundi lingine la wanaosoma vyuoni na pia kuna wanafunzi wanooandaliwa kuja kusoma kozi hizo hizo kwenye baadhi ya vyuo tulivyonavyo. Katika muktadha huu ndio ninapoona uhitaji Wa Sera mpya ya Elimu na mabadiliko makubwa ya mitaala yetu kuelekea viwandani yaani kwenye kuzalisha Mali zaidi ya hii ya vitabuni ya kukaririshana mashairi na sayansi ya lugha .
Tunahitaji vijana wawe na Elimu inayoendana na mazingira yao kama ni wafugaji basi iwasaidie kufuga kisasa kama ni wakulima iwaongezee mbinu za kufuga kitaalamu na sio baada ya kumaliza chuo wazunguke na bahasha kutafuta ajira ambazo kimsingi ni chache sana au hazipo na tuendako hazitakuweoo kabisa pengine.
Mfumo huu Wa Elimu ninahisi una tatizo sehemu na Kubwa kwenye mitaala yetu vitu tunavyowafundisha vijana wetu not applicable in real life. Kijana tumuandae awe chachu ya kusisimua ukuaji Wa viwanda na wala sio awe mzigo kwenye suala la viwanda .
Jinsi tunavyofundisha hata madarasani ni muendelezo tu Wa kukaririshana mavitu mengi yasiyo na Tija kwa maisha ya mwanafunzi husika .Sasa hapa Vijana wetu wanakosa uelekeo na wanaanza kufikiria upya wafanye kitu gani katika maisha yao.
Baada ya kumaliza tu shahada ya sheria utahitaji kuifanyia kazi ili uweze kuishi ukiona imekua ngumu kua kwamba hiyo bidhaa haina soko na kama haina soko maana yake ni hasara lakini ni nani anatakiwa kuja na suluhisho la tatizo hili?
Ni nani afikirie jinsi ya kulitatua na kulipatia tiba ?
Luna viongozi wengi wamekua wakizungumzia ukosefu Wa ajira kama janga la kitaifa ila hawakutoa tiba ya tatizo hili badala tu ya kuzungumza na kuacha likining'inia hewani kama popo wafanyavyo.
Sasa si muda muafaka wakulijadili badi kulifanyia kazi ndio itakua muhimu kwa mustakabali wa taifa.
Je wewe unaona ni nini kifanyike?
Elimu yetu ninavyoiona inahitaji mabadiliko makubwa mno vinginevyo tutashindwa kuwashawishi vijana wetu waendelee kuwejeza kwenye Elimu na pia wazazi wataacha kuwekeza kwenye Elimu kama silaha ya kwanza ya kumpatia mtoto kwa ajili ya kupambana na umasikini.
Elimu ya mkoloni ililenga kumpatia cheap labourers kwenye maeneo yake ya kazi ila Elimu yetu ya sasa enatakiwa ilenge kwenye kumkomboa MTU mmoja mmoja kutoka kwenye maisha ya kutaka kuwa mtumwa au kutafuta ajira na kujiajiri yeye mwenyewe na pia kuajiri wengine .
Haiingii akilini tu kuwalaumu vijana wanaotafuta ajira kwenye taasisi mbalimbali kwa kuwaambia wanatakiwa wajiajiri wakati hatukuwaanda kwa hilo.
Ni hivi majuzi tu Waziri Wa Elimu alisema kwamba kwa sasa waalimu Wa masomo ya arts wanatosha .Tusisahau kwamba kuna tundo la waliomaliza masomo hayo na kuna kundi lingine la wanaosoma vyuoni na pia kuna wanafunzi wanooandaliwa kuja kusoma kozi hizo hizo kwenye baadhi ya vyuo tulivyonavyo. Katika muktadha huu ndio ninapoona uhitaji Wa Sera mpya ya Elimu na mabadiliko makubwa ya mitaala yetu kuelekea viwandani yaani kwenye kuzalisha Mali zaidi ya hii ya vitabuni ya kukaririshana mashairi na sayansi ya lugha .
Tunahitaji vijana wawe na Elimu inayoendana na mazingira yao kama ni wafugaji basi iwasaidie kufuga kisasa kama ni wakulima iwaongezee mbinu za kufuga kitaalamu na sio baada ya kumaliza chuo wazunguke na bahasha kutafuta ajira ambazo kimsingi ni chache sana au hazipo na tuendako hazitakuweoo kabisa pengine.
Mfumo huu Wa Elimu ninahisi una tatizo sehemu na Kubwa kwenye mitaala yetu vitu tunavyowafundisha vijana wetu not applicable in real life. Kijana tumuandae awe chachu ya kusisimua ukuaji Wa viwanda na wala sio awe mzigo kwenye suala la viwanda .
Jinsi tunavyofundisha hata madarasani ni muendelezo tu Wa kukaririshana mavitu mengi yasiyo na Tija kwa maisha ya mwanafunzi husika .Sasa hapa Vijana wetu wanakosa uelekeo na wanaanza kufikiria upya wafanye kitu gani katika maisha yao.
Baada ya kumaliza tu shahada ya sheria utahitaji kuifanyia kazi ili uweze kuishi ukiona imekua ngumu kua kwamba hiyo bidhaa haina soko na kama haina soko maana yake ni hasara lakini ni nani anatakiwa kuja na suluhisho la tatizo hili?
Ni nani afikirie jinsi ya kulitatua na kulipatia tiba ?
Luna viongozi wengi wamekua wakizungumzia ukosefu Wa ajira kama janga la kitaifa ila hawakutoa tiba ya tatizo hili badala tu ya kuzungumza na kuacha likining'inia hewani kama popo wafanyavyo.
Sasa si muda muafaka wakulijadili badi kulifanyia kazi ndio itakua muhimu kwa mustakabali wa taifa.
Je wewe unaona ni nini kifanyike?