Domhome
JF-Expert Member
- Jun 28, 2010
- 3,197
- 3,930
Tarehe 08 Desemba 2008 siku ya Jumatatu majira ya saa 4 usiku nilifiwa na shemeji yangu mdogo wake kabisa na wife. Shemeji yangu huyo aliugua kwa zaidi ya wiki mbili na siku alofariki ndo siku aliruhusiwa toka hospitali moja kubwa ya private akiwa na nafuu kabisa. Hata nami niliporudi job majira ya saa 11 jioni nilimkuta nyumbani na tulitaniana huku akiwa na furaha kubwa ya yeye kutoka hospitali.
Mnamo majira ya saa 4 za usiku hali ilibadilika ghafla na kupelekea Shemeji yangu huyo kuanza kutapika damu mbichi kabisa mfululizo na wakati tukimkimbiza hospitali ile ile alokuwa kalazwa kwa zaidi ya wiki 2 alifariki tukiwa njiani.
Ilibidi turudi nyumbani na mwili ili tujue nini tunafanya, niliwajulisha jamaa na marafiki usiku huo huo na baadhi walifika home na walilala na sisi pale nyumbani. Mimi na wife tuliamua ni lazima kesho tusafirishe mwili kwenda kuzika nyumbani hivyo, usiku ule ule tulifanya mchakato wa kupata gari kusafirishia mwili, sanduku (jeneza) na vyote vihusianavyo na msiba.
Mwili tuliamua ulale palepale home kwavile safari tulipanga iwe kesho yake asubuhi na tulipanga twende hospitali mapema ili tumpate daktari aje na dawa autibu mwili kabla ya kuanza safari kuelekea mkoani, Kilichonikuta hapa ndo chanzo cha habari yangu hii ya kweli kabisa ilonitokea nikiwa moja ya mikoa ya Magharibi mwa nchi yetu.
Mapema asubuhi nilienda kwanza job nikachukua Compasionate leave siku 14 ndipo nikaamua kwenda hospitali kumpata daktari wa kuja kuutibu mwili kabla ya kuanza safari ya mkoani. Wanasema, ukistaajabu ya Ndugai utayaona ya Tulia na kweli niliyaona. Tukiwa mimi na Mchungaji wangu tulipofika hospital ndo tukakutana na maajabu ya Rajabu kumuoa Mwajabu binti wa Mzee Rajabu.
Kwanza, tuliambiwa dawa hakuna baada ya vuta nikuvute ndpo jamaa akatuambiwa dawa zimeisha na kuwa kwasasa hospitali hiyo ya wilaya (jina kapuni) imebaki na dozi ya kutibu miili 2 tu na hivyo hawaruhusiwi kutibu mwili wowote ule nje ya miili hiyo miwili wanayopaswa kuitibu. Mchungaji akamuuliza miili hiyo ni ipi?
Jamaa, akajibu siruhusiwi kuitaja miili hiyo ila kifupi dawa hamna... Mimi Nikaingiza mkono mfukoni nikatoa elfu 30 nikamshikisha jamaa. Shaaabashiiii, jamaa akasems kwa sauti ya juu, nanukuu.." akifa Mbunge au Mkuu wa wilaya shauri yao mimi siwezi kufa njaa kwaajili ya kusubiri miili yao" Tulipigwa na bumbuwazi mimi pamoja na Mchungaji wangu ila tulishukuru kwani elfu 30 ilitufanya tujue mengi. Yaani Mtumishi wa Serikali anaamua kubuni uongo ili tu kuhalalisha mazingira ya yeye kupata fedha.
Mwili ulitibiwa na tukasafirisha kwenda kuzika Kanda ya Kati salama salimini. Leo nimekumbuka tukio hili lilotokea miaka 15 ilopita tena nilkiwa mkoani. Nawatakia Jumatano Njema na Mungu awabariki sana.
Vipi wewe uliwahi kutwa na tukio gani lilohusisha rushwa/ hongo ndipo ukapewa huduma?
Mnamo majira ya saa 4 za usiku hali ilibadilika ghafla na kupelekea Shemeji yangu huyo kuanza kutapika damu mbichi kabisa mfululizo na wakati tukimkimbiza hospitali ile ile alokuwa kalazwa kwa zaidi ya wiki 2 alifariki tukiwa njiani.
Ilibidi turudi nyumbani na mwili ili tujue nini tunafanya, niliwajulisha jamaa na marafiki usiku huo huo na baadhi walifika home na walilala na sisi pale nyumbani. Mimi na wife tuliamua ni lazima kesho tusafirishe mwili kwenda kuzika nyumbani hivyo, usiku ule ule tulifanya mchakato wa kupata gari kusafirishia mwili, sanduku (jeneza) na vyote vihusianavyo na msiba.
Mwili tuliamua ulale palepale home kwavile safari tulipanga iwe kesho yake asubuhi na tulipanga twende hospitali mapema ili tumpate daktari aje na dawa autibu mwili kabla ya kuanza safari kuelekea mkoani, Kilichonikuta hapa ndo chanzo cha habari yangu hii ya kweli kabisa ilonitokea nikiwa moja ya mikoa ya Magharibi mwa nchi yetu.
Mapema asubuhi nilienda kwanza job nikachukua Compasionate leave siku 14 ndipo nikaamua kwenda hospitali kumpata daktari wa kuja kuutibu mwili kabla ya kuanza safari ya mkoani. Wanasema, ukistaajabu ya Ndugai utayaona ya Tulia na kweli niliyaona. Tukiwa mimi na Mchungaji wangu tulipofika hospital ndo tukakutana na maajabu ya Rajabu kumuoa Mwajabu binti wa Mzee Rajabu.
Kwanza, tuliambiwa dawa hakuna baada ya vuta nikuvute ndpo jamaa akatuambiwa dawa zimeisha na kuwa kwasasa hospitali hiyo ya wilaya (jina kapuni) imebaki na dozi ya kutibu miili 2 tu na hivyo hawaruhusiwi kutibu mwili wowote ule nje ya miili hiyo miwili wanayopaswa kuitibu. Mchungaji akamuuliza miili hiyo ni ipi?
Jamaa, akajibu siruhusiwi kuitaja miili hiyo ila kifupi dawa hamna... Mimi Nikaingiza mkono mfukoni nikatoa elfu 30 nikamshikisha jamaa. Shaaabashiiii, jamaa akasems kwa sauti ya juu, nanukuu.." akifa Mbunge au Mkuu wa wilaya shauri yao mimi siwezi kufa njaa kwaajili ya kusubiri miili yao" Tulipigwa na bumbuwazi mimi pamoja na Mchungaji wangu ila tulishukuru kwani elfu 30 ilitufanya tujue mengi. Yaani Mtumishi wa Serikali anaamua kubuni uongo ili tu kuhalalisha mazingira ya yeye kupata fedha.
Mwili ulitibiwa na tukasafirisha kwenda kuzika Kanda ya Kati salama salimini. Leo nimekumbuka tukio hili lilotokea miaka 15 ilopita tena nilkiwa mkoani. Nawatakia Jumatano Njema na Mungu awabariki sana.
Vipi wewe uliwahi kutwa na tukio gani lilohusisha rushwa/ hongo ndipo ukapewa huduma?