Haki na maendeleo havichangamani

Haki na maendeleo havichangamani

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,252
Reaction score
16,171
Wazungu waliendelea na kukusanya mitaji kwa kuvunja haki za watu wengi sana, na wanaendelea kuvunja haki za watu ili kuendeleza maendeleo yao na mitaji.

Wachina, Warusi, Israel, Mzee Kagame na baadae JPM waliligundua hilo pia. Huwezi kujali haki za walipa kodi, watumishi, wanasiasa na wafanyabiashara halafu upate maendeleo. Utakusanya kidogo sana na kukigawana chote.

Kama unataka kujenga nyumba ya familia lazima watoto watoto watapoteza haki zao za pizza, chips kuku, nguo mpya, nk ili nyumba yao ikamilike, hasa kama kipato chako ni kidogo. Lakini baada ya nyumba kukamilika watoto watapata furaha zaidi kwa kulala kwenye nyumba yao bila bugudha ya kodi wala mama mwenyenyumba.

Tanzania kama hatutaikumbatia hii falsafa basi tutakuwa kama wengine tu Afrika. Tatizo letu kubwa ni kukosekana kwa dira na mkakati wa pamoja wa kitaifa juu ya taifa letu na hatima yake. Yaani tunaelekea wapi na namna ya kwenda kwa miaka 100 ijayo.
 
Huyo Magufuli hakuwa na sifa hizo. Angekuwa ni mpenda maendeleo ya kweli, asinge ubariki ule uhuni wa baadhi ya wabunge na madiwani wa upinzani wa kuchezea hela za walipa kodi, kwa kuunfa mkono juhudi zake feki!

Angekuwa ni mpenda maendeleo ya kweli, angepunguza pia matumizi kwenye serikali yake na yale ya wabunge! Badala ya kuwaonea watumishi wa umma pekee! Alimsifia hadharani DED aliyenunua gari la kutembelea kwa milioni 400! Yeye mwenyewe alijiimarishia ulinzi na msululu wa magari ya kifahari kwenye misafara yake!

Wakati mwingine jaribu kutofautisha kati UZALENDO kwa nchi na UBINAFSI wa mtu. Rangi nyeusi kamwe haiwezi kulinganishwa na rangi nyeupe!
 
Ingekuwa kukandamiza haki kunafanya taifa liwe liwe na maendeleo, bara la Afrika si ndo lingekuwa ndilo bara lenye maendeleo zaidi kuliko yote duniani? Asia na kwenyewe ni bara linaloongoza kukandamiza haki, lakini ukiondoa China, mataifa yaliyo maskini Asia ndiyo hayo hayo yanayokandamiza haki, tofauti na mataifa kama South Korea au Japan! Ukirudi Americas, nako hivyo hivyo! Mataifa yanayoongoza kukandamiza haki ndo hayo hayo mataifa maskini! Venezuela ina utajiri wa asili maradufu ukilinganisha na Mexico lakini Mexico ndiyo ina maendeleo maradufu kulinganisha na Venezuela!

Mkiona tunawa-support zile mada zenu za kijinga za Kenya vs Tanzania mnashindwa kufahamu kwamba tunfanya vile kwa ajili ya uzalendo tu akini uhalisia, alichofanya Magufuli ni ujinga mtupu ukilinganisha na aliyofanya Kenyatta ambae yupo juu kwenye kuangalia haki compared to JPM! Nenda Ghana nchi inayojali demokrasia na haki halafu linganisha na utawala wa kidikteta wa JPM kisha rudi hapa tuambie ni wapi yamefanyika makubwa
 
Aristotle aliwahi kusema 'A good monarch is better than a democracy'
 
Umeongea ukweli mtupu..!!

Kuna watu huwa nawasikia walalamika eti miaka ya 1940+ tulikuwa sawa kiuchumi na China, au karne ya 19 huko tulikuwa sawa kiuchumi na Ulaya..!! Mi huwa nawaulizaga mnajua China na Ulaya walifanya nini mpaka sasa mnatamani kuwa kama wao? Tukisema tufanye kama walicyofanya wao mtakuwa tayar?

Wenzetu walijenga nchi zao kwa mijeredi, hakuna kudai ata mishahara wala marupurupu..!! Leo hii mna haki kibao mnataka mjenge nchi muwe kama UK..!! Imposible
 
South Korea wamevunja haki ya nani? Sweden, Norway, Finland wamevunja haki ya nani? Uholanzi wamevunja haki ya nani??

Hizo roho zenu za kiburundi tumeshawaambia hazina nafasi hapa kwetu Tanzania. Na tumewagundua wote, zoezi linalofuata ni kuwarudisha wote Burundi
 
Mada ya kijinga kabisa kutoka kwa mmoja wa wanaoweweseka baada ya kuondoka duniani Dikteta la Kwanza la Kitanzania! Ingekuwa kukandamiza haki kunafanya taifa liwe liwe na maendeleo, bara la Afrika si ndo lingekuwa ndilo bara lenye maendeleo zaidi kuliko yote duniani? Asia na kwenyewe ni bara linaloongoza kukandamiza haki, lakini ukiondoa China, mataifa yaliyo maskini Asia ndiyo hayo hayo yanayokandamiza haki, tofauti na mataifa kama South Korea au Japan! Ukirudi Americas, nako hivyo hivyo! Mataifa yanayoongoza kukandamiza haki ndo hayo hayo mataifa maskini! Venezuela ina utajiri wa asili maradufu ukilinganisha na Mexico lakini Mexico ndiyo ina maendeleo maradufu kulinganisha na Venezuela!

Mkiona tunawa-support zile mada zenu za kijinga za Kenya vs Tanzania mnashindwa kufahamu kwamba tunfanya vile kwa ajili ya uzalendo tu akini uhalisia, alichofanya Magufuli ni ujinga mtupu ukilinganisha na aliyofanya Kenyatta ambae yupo juu kwenye kuangalia haki compared to JPM! Nenda Ghana nchi inayojali demokrasia na haki halafu linganisha na utawala wa kidikteta wa JPM kisha rudi hapa tuambie ni wapi yamefanyika makubwa
Hata Bibi yangu anafahamu kuwa kama unataka kulima eneo kubwa toka asubuhi sana na usipoteze muda kujiandalia chakula kizuri, huwa wanakula ngararumu, yaani mahindi makavu yanachemshwa tu basi na kuletwa shambani na maji tu ya kunywa.

Tanzania ni nchi ndogo sana na maskani, huwezi kujenga miundombinu ya usafiri, umeme, maji, afya, elimu, mahakama nchi nzima kwa muda mfupi huku unaongeza mishahara, unaajiri, magereza wanakula nyama, wanajeshi wanapewa kila kitu kama wenzao wa ulaya na marekani, nk.

JPM alikuwa sahihi sana na ndio maana dunia ilimtambua kwa kuingiza Tz katika uchumi wa kati. Nikisema yuko sahihi namaanisha style yake ya leadership. Hata kukosea kwake kulikuwa kwa kibinadamu tu. Ni kweli JPM aliikuta Tanzania ikijengwa upande mmoja tu wa Kaskazini. Mikoa ya kaskazini ilikuwa na nafuu kwenye upatikanaji wa huduma za kijamii kuliko kusini na magharibi. Hivyo kama binadamu lazima angetafuta uwiano.

Huwezi kuwa na ulinzi legelege wakati unapambana na wauza madawa ya kulenvya na kuvuruga mikataba ya kinyonyaji ya madini na vinu vya kufua umeme vya wazungu.

Hata akina Hitler wameijenga ujerumani lakini wana shida zao za pembeni pia. Kagame tunamsifu lakini ana mabaya yake pia. Wazungu, wachina, Asia fisadi anachinjwa hafharani, jee sisi tunaweza hivyo? Hapa kwetu Rais anashindwa kunyonga hata wale walioua wengine
 
Tanzania ni nchi ndogo sana na maskani, huwezi kujenga miundombinu ya usafiri, umeme, maji, afya, elimu, mahakama nchi nzima kwa muda mfupi huku unaongeza mishahara, unaajiri, magereza wanakula nyama, wanajeshi wanapewa kila kitu kama wenzao wa ulaya na marekani, nk.
Utawala wa JK haukuwa wa Kidikteta kama wa Magufuli lakini bado aliweza kujenga chuo kikuu kabisa nchini kama sio Afrika Mashariki. Aliweza kujenga mashule! Aliweza kujenga barabara zilizompa umaarufu Magufuli! Alitoa ajira kila mwaka! Alipandisha mishahara kila mwaka! Alibadilisha madaraja ya mishahara! alijenga madaraja! Aliongeza idadi kubwa ya wanafunzi walioenda kusomea ualimu ili waweze kufundisha kwenye mashule yaliyokuwa yametapakaa kila mahali! Na ukweli uchungu ni kwamba, asilimia kubwa ya miradi ya JPM ameirithi kutoka kwa JK.

Kwahiyo hoja yako haina msingi!
JPM alikuwa sahihi sana na ndio maana dunia ilimtambua kwa kuingiza Tz katika uchumi wa kati. Nikisema yuko sahihi namaanisha style yake ya leadership. Hata kukosea kwake kulikuwa kwa kibinadamu tu. Ni kweli JPM aliikuta Tanzania ikijengwa upande mmoja tu wa Kaskazini. Mikoa ya kaskazini ilikuwa na nafuu kwenye upatikanaji wa huduma za kijamii kuliko kusini na magharibi. Hivyo kama binadamu lazima angetafuta uwiano.
Unaposema habari za uchumi wa kati tu ndipo unapoonesha hujui lolote! JF hapa hapa zilitolewa takwimu ambazo zilionesha JK aliacha nchi ikiwa na GNI per capita $980. Aidha, takwimu hizo zilionesha katika awamu ya kwanza ya JK na Mkapa, kila mmoja alipandisha GNI per capita kwa $220. Lakini kwa miaka 4, JPM aliweza kupandisha GNI per capita kutoka $980 hadi $1080; yaani kwa $100 TU! Labda utokee muujiza ndipo kwa 2020/2021 peke yake angewez kupandisha kwa $100 ili angalau afikishe $220 za wenzake. ISINGEWEZEKANA!!

Kwa takwimu hizo, kama JPM angekuwa mzuri kiasi hicho basi alitakiwa kuifikisha nchi kwenye uchumi wa kati back 2017 kwa kuzingatia speed ya wenzake; lakini alishindwa!
Huwezi kuwa na ulinzi legelege wakati unapambana na wauza madawa ya kulenvya na kuvuruga mikataba ya kinyonyaji ya madini na vinu vya kufua umeme vya wazungu.
Kuna kupambana na uhalifu na kupambana na uhalifu kwa njia ya stunt! Nikukumbushe tu kwamba hata China ambako wauza unga wananyongwa, bado watu wanapeleka unga! Seuze Tanzania?!
Hata akina Hitler wameijenga ujerumani lakini wana shida zao za pembeni pia. Kagame tunamsifu lakini ana mabaya yake pia. Wazungu, wachina, Asia fisadi anachinjwa hafharani, jee sisi tunaweza hivyo? Hapa kwetu Rais anashindwa kunyonga hata wale walioua wengine
Anayemsifu Kagame ni watu aina yako kwa sababu ni mjinga tu ndie anaweza kuiacha nchi yake na kwenda kutafuta maisha Rwanda licha ya PK kukaa madarakani kwa miaka kadhaa! Watu wa aina yako mnachoshindwa kufahamu ni kwamba, watu walikuwa hawampendi JK, na kwahiyo PK akawa ndie anatolewa mfano kwamba anatushinda! Uhalisia ni kwamba, Rwanda haijawahi kuwa mbele ya Tanzania kwa maendeleo!!! Ukitoa pale Kigali ambapo PK kapafanya iwe ndiyo sura ya Rwanda, ukienda huko kwingine ni taabu tupu!
 
Haki na demokrasia haikai chumba kimoja njaa, umaskini, maradhi na ukosefu mkubwa wa huduma. Idadi ya waChina ni robo ya dunia, kama kila mchina angepewa haki na demokrasia ya kusema na kutenda wachina wangekuwa ombaomba duniani, wangekufa njaa, wangeshindwa kujivisha, wangeshindwa kujilaza.

Hata wazazi wetu kama wangetupa demokrasia na haki zetu za kulala na kuamka asubuhi huenda tusingekwenda shule.

Hata ulaya usipolipa kodi adhabu yake ni kubwa sana.

Lazima tuburuzane wenyewe kwa wenyewe ili tuzalishe kwa wingi ndipo tuje tukae kitako tugawane ziada (surplus) kwa haki (equitably). Masikini hana haki wala demokrasia atakunywa maji pamoja na mifugo kwenye dimbwi moja kama hakuna maji safi kwaajili ya binadamu, sisi ni masiki bila hata ya kupepesa macho, hatuwezi kuwaza kugawana ambacho hatuna badala ya kuwaza kwenye kuzalisha kwanza. Hata wazungu hawakuanza na demoakrasia, na mataifa walioanza na haki na demokrasia yalifeli, kama vile USSR, North Korea, Venezuella, Tanzania, Cuba.

Wazungu walituletea demokrasia na haki mapema kwakuwa wanajuwa kuwa vitatudumaza kiuchumi. Tutatumia muda mwingi kubishana, barabarani kuomba kuomba kura, kuomba wanachama ma kiandamana kudai haki na demokrasia, tutapigana risasi wenyewe kwa wenyewe na kuuana na kusahau muda wa kuzalisha.

Mbaya zaidi hata hao watetezi wa haki na demokrasia wanafanya hivyo kama ajira yao na sio hasa kutoka mioyoni mwao. Primary goal yao ni kipato sio kile kile kilichoandikwa kwenye makablasha yao.

Lazima watu wote bila kujali jinsia, dini, vyama vya siasa, kabila au rangi tukae kitako tutengeneze agenda yetu ya miaka 100 ijayo inayoonyesha tunakotaka kuwa na namna ya kuwa tunachotaka. Falsafa yetu ni nini?

Rais Samia sina mashaka anaifahamu falsafa hii, wanzungu watatupenda sana kama tukihubiri haki na demokrasia kwenye mataifa yetu kwakuwa wanafahamu madhara yake kiuchumi. Wao bado wanapora hadi leo kutoka mataifa mengine resources za kwenda kutekelezea haki na demokrasia kwenye mataifa yao, sisi tutakwenda kupora wapi?

Kwakuwa kanuni ya maendeleo ni kupora haki demokrasia resources (personnel, money, materials and Time) za wengine bila kuwalipa kabisa au kuwapa kidogo sana ndio maana labda JPM hakuongeza mishahara watumishi, alipora wafanyabiashara, hakuajiri sana, alipunhuza wenye vyeti feki bila kuwalipa, hakuna dawa kwenye zahanati, hakuna pesa kwenye mawizara na ofisi, hakuna kusafiri nje, hats yeye alitumia magari kusafiri, nk ili spate fedha za maendeleo na ndiyo maana Leo tunaona hayo tunayoyaona kwenye awamu ya tano.

Kama unataka maendeleo lazima upore haki, demokrasia na resources za watu wako au za watu wengine, nothing less nothing more. Hiyo ndiyo maana sasa hivi Wachina wanapora, wamarekani wanapora , Rwanda inapora kutoka DRC, na ulaya wanapora hiki na kile kutoka kwa wengine kwa njia mabalimbali zikiwemo, mikataba, kibiashara, kivita, na mikopo.

Kwakuwa sisi hakuna kwa kupora nje ya nchi kilichobaki ni kupora kifogo haki, demokrasia na nguvu za watu wetu wenyewe kwenye kuzalisha. Mfano, wafungwa wapewe zana za kisasa za kilimo, kuchimba na kuvua wakalime sana, wakachimbe sana na kuvua sana kwa ujira mdogo kabisa wa chakula na mavazi na matibabu tu, wanajeshi wazalishe mahitaji yao na ziada badala ya kusubiri vita ambayo haipo, watu wooote walipe kodi wakiwemo wabunge na kila mtu nchini, hakuna msamaha wa kodi kwa mtu wala taasisi yoyote ile, demokrasia ipewe nafasi kidogo sana ili watu watumie muda wao kufanyakazi, wakulima lazima walime kwa lazima mazao yanayotakiwa, sio hiari. Kama tukisema mkoa huu umlime alizeti kuondoa uhaba ya mafuta ya kula lazima watu walime sio kwa hiari. Mfugaji lazima afuge kwa tija kwa lazima sio hiari yake, alazimishwe afuge mbegu fulani inayotoa nyama ya uzito fulani na ngozi yenye ubora fulani, na maziwa kiasi fulani.
 
Niliwaambia kuwa Rais Samia yuko makini sana. Hakina na maendeleo havichangamani. Kuna covid, kuna SGR, Bwawa la umeme, kuhamia dodoma, kujenga barabara, kusambaza maji na kuongeza mishahara kwa watumishi, aache kipi?
 
Niliwaambia kuwa Rais Samia yuko makini sana. Hakina na maendeleo havichangamani. Kuna covid, kuna SGR, Bwawa la umeme, kuhamia dodoma, kujenga barabara, kusambaza maji na kuongeza mishahara kwa watumishi, aache kipi?
Wapuuzi watakupuuza!
 
Wapuuzi watakupuuza!
Wacha wanipuuze lakini hiyo ndiyo kanuni ya maendeleo. Labda tuamue tuachane na miradi ipi ili tupate za kugawana. Kama tunataka kuwa na gawio kubwa kwa watu wetu lazima sera yetu ya mambo ya nje tuubalishe ili tuunde jeshi na kushiriki migogoro ya nje kwa faida. Tuwe na jeahi la uporaji mataifa mengine. Hatuwezi kuwa na jeshi kubwa hivi lisilozalisha linalosubiri vita. Majeshi ya wazungu ni majeshi ya kiuchumi, yanapora na kurudisha nyumbani, hayapigani vita kwwnye nchi isiyokuwa na mali ya kupora tofauti na majeshi ambayo ni ya ukombozi tu na kukinda amani.
 
Pole pamoja na maigizo yote ya kumlilia, huyo mungu wa Burigi alizikwa CHATO
 
Ila mimi sikuelewa awamu ya jiwe,kulikuwepo na uhusiano gani kati ya kuvunja haki kidemkrasia na maendeleo. Yaani wakiwepo wapinzani wanakwamishaje maendeleo
 
Haki na demokrasia haikai chumba kimoja njaa, umaskini, maradhi na ukosefu mkubwa wa huduma. Idadi ya waChina ni robo ya dunia, kama kila mchina angepewa haki na demokrasia ya kusema na kutenda wachina wangekuwa ombaomba duniani, wangekufa njaa, wangeshindwa kujivisha, wangeshindwa kujilaza.

Hata wazazi wetu kama wangetupa demokrasia na haki zetu za kulala na kuamka asubuhi huenda tusingekwenda shule.

Hata ulaya usipolipa kodi adhabu yake ni kubwa sana.

Lazima tuburuzane wenyewe kwa wenyewe ili tuzalishe kwa wingi ndipo tuje tukae kitako tugawane ziada (surplus) kwa haki (equitably). Masikini hana haki wala demokrasia atakunywa maji pamoja na mifugo kwenye dimbwi moja kama hakuna maji safi kwaajili ya binadamu, sisi ni masiki bila hata ya kupepesa macho, hatuwezi kuwaza kugawana ambacho hatuna badala ya kuwaza kwenye kuzalisha kwanza. Hata wazungu hawakuanza na demoakrasia, na mataifa walioanza na haki na demokrasia yalifeli, kama vile USSR, North Korea, Venezuella, Tanzania, Cuba.

Wazungu walituletea demokrasia na haki mapema kwakuwa wanajuwa kuwa vitatudumaza kiuchumi. Tutatumia muda mwingi kubishana, barabarani kuomba kuomba kura, kuomba wanachama ma kiandamana kudai haki na demokrasia, tutapigana risasi wenyewe kwa wenyewe na kuuana na kusahau muda wa kuzalisha.

Mbaya zaidi hata hao watetezi wa haki na demokrasia wanafanya hivyo kama ajira yao na sio hasa kutoka mioyoni mwao. Primary goal yao ni kipato sio kile kile kilichoandikwa kwenye makablasha yao.

Lazima watu wote bila kujali jinsia, dini, vyama vya siasa, kabila au rangi tukae kitako tutengeneze agenda yetu ya miaka 100 ijayo inayoonyesha tunakotaka kuwa na namna ya kuwa tunachotaka. Falsafa yetu ni nini?

Rais Samia sina mashaka anaifahamu falsafa hii, wanzungu watatupenda sana kama tukihubiri haki na demokrasia kwenye mataifa yetu kwakuwa wanafahamu madhara yake kiuchumi. Wao bado wanapora hadi leo kutoka mataifa mengine resources za kwenda kutekelezea haki na demokrasia kwenye mataifa yao, sisi tutakwenda kupora wapi?

Kwakuwa kanuni ya maendeleo ni kupora haki demokrasia resources (personnel, money, materials and Time) za wengine bila kuwalipa kabisa au kuwapa kidogo sana ndio maana labda JPM hakuongeza mishahara watumishi, alipora wafanyabiashara, hakuajiri sana, alipunhuza wenye vyeti feki bila kuwalipa, hakuna dawa kwenye zahanati, hakuna pesa kwenye mawizara na ofisi, hakuna kusafiri nje, hats yeye alitumia magari kusafiri, nk ili spate fedha za maendeleo na ndiyo maana Leo tunaona hayo tunayoyaona kwenye awamu ya tano.

Kama unataka maendeleo lazima upore haki, demokrasia na resources za watu wako au za watu wengine, nothing less nothing more. Hiyo ndiyo maana sasa hivi Wachina wanapora, wamarekani wanapora , Rwanda inapora kutoka DRC, na ulaya wanapora hiki na kile kutoka kwa wengine kwa njia mabalimbali zikiwemo, mikataba, kibiashara, kivita, na mikopo.

Kwakuwa sisi hakuna kwa kupora nje ya nchi kilichobaki ni kupora kifogo haki, demokrasia na nguvu za watu wetu wenyewe kwenye kuzalisha. Mfano, wafungwa wapewe zana za kisasa za kilimo, kuchimba na kuvua wakalime sana, wakachimbe sana na kuvua sana kwa ujira mdogo kabisa wa chakula na mavazi na matibabu tu, wanajeshi wazalishe mahitaji yao na ziada badala ya kusubiri vita ambayo haipo, watu wooote walipe kodi wakiwemo wabunge na kila mtu nchini, hakuna msamaha wa kodi kwa mtu wala taasisi yoyote ile, demokrasia ipewe nafasi kidogo sana ili watu watumie muda wao kufanyakazi, wakulima lazima walime kwa lazima mazao yanayotakiwa, sio hiari. Kama tukisema mkoa huu umlime alizeti kuondoa uhaba ya mafuta ya kula lazima watu walime sio kwa hiari. Mfugaji lazima afuge kwa tija kwa lazima sio hiari yake, alazimishwe afuge mbegu fulani inayotoa nyama ya uzito fulani na ngozi yenye ubora fulani, na maziwa kiasi fulani.
🙏Jamii ingelipata watu kama Nyinyi nchi hii ngelifika mbali sana, Sasahivi tuna kizazi Cha kulalamika tu, Watanzania hatujui tunaitaji nini,ukiuliza wanao lalamika utasikia tunataka democlasia,mala tunataka uhuru wa kuongea.Kipindi Jk walipewa Uhuru,hao hao wakambeza,basi tuliitaji watu kama kariba ya Magufuri zaidi ya miaka kama 20 hivi,nchi ingepiga hatua kubwa.
 
Ila mimi sikuelewa awamu ya jiwe,kulikuwepo na uhusiano gani kati ya kuvunja haki kidemkrasia na maendeleo. Yaani wakiwepo wapinzani wanakwamishaje maendeleo
Hujui kitu gani hapo? JPM alikuwa na uchungu mwingi uliopitiliza juu ya Tanganyika. Alichukia na namna CCM na serikali yake inavyogeuka kuwa ombaomba kutoka kwa matajiri na nchi hisani wakati Tanganyika inazo mali nyingi sana zinazoporwa na wajanja.

Aliamini kuwa Tanzania ni nchi tajiri lakini tunakinga bakuri kwa wahisani na wafanyabiashara akina Rostam na wenzake. Hivyo aliichukia CCM na serikali zilizopita.

JPM alijua pia kuwa wazungu walituletea habari za haki za binadamu na demokrasia ili vitupotezee muda mwingi kubishana wakati wao wakipita katikati yetu kupora mali zetu kwa kuunga mkono kundi moja kwa mwamvuli wa demokrasia na haki za binadamu.

Kumbuka wazungu hawakuanza kwa haki za binadamu na demokrasia kwenye mataifa yao. Hata leo wanahubiri demokrasia kwa raia wao lakini sera zao za nje ni zakiporaji.
 
🙏Jamii ingelipata watu kama Nyinyi nchi hii ngelifika mbali sana, Sasahivi tuna kizazi Cha kulalamika tu, Watanzania hatujui tunaitaji nini,ukiuliza wanao lalamika utasikia tunataka democlasia,mala tunataka uhuru wa kuongea.Kipindi Jk walipewa Uhuru,hao hao wakambeza,basi tuliitaji watu kama kariba ya Magufuri zaidi ya miaka kama 20 hivi,nchi ingepiga hatua kubwa.
Tanzania ina fursa nyingi sana, ina ardhi kubwa ya kulima, kufuga na kujenga, kuna mito, bahari na maziwa, kuna madini, miti, wanyama na amani telee, lakini cha ajabu hata profesa anadai nyongeza ya mshahara kutoka kwa mwajili wake, hawezi kujiajili na hata akistaafu anaomba tena kuajiliwa kwa mkataba, hawezi kujiajili.

Tulipaswa kulima, kufuga, kuvua na kuchuuza pia kama sehemu ya kujiongezea kipato chetu wakati serikali kuu ikiandaa miundo mbinu ya umeme, maji, hospitali, barabara, reli, masoko, elimu, ndege na mawasiliano ya simu na internet.
 
Hatuitaki hiyo falsafa ya kishenzi
 
Hatuitaki hiyo falsafa ya kishenzi
Inatumika duniani kote labda kwenu tu. Waliopewa haki ya kulala hawakwenda shule kabisa, waliopewa haki ya kufanya chochote hawakumaliza shule.

Baba alipokuwa anatujengea nyumba yetu tulinyimwa haki yetu ya kwenda kutembelea mbugu za wanyama akasema hana hela amelipa mafundi, alipunguza baadhi ya vitu tulivyovozea. Labda asingefanya hivyo huenda mpaka sasa tungekuwa tuko kwenye nyumba za kupanga.

Bro, huwezi kutafuna na kupiga mluzi muda huohuo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom