Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

HADITHI YA KUSISIMUWA MIMBA YA JINI-45-

ILIPOISHIA:
Mustafa kila alipokuwa kazini alikuwa na maswali mengi juu ya tumbo la Shehna kuwa kubwa kama puto lililojazwa hewa lakini lilikuwa laini na kupenda kulishika muda wote hata kumfanya kila siku alale kwa muda mchache.
SASA ENDELEA...


Kilichomuumiza akili kilikuwa ukubwa wa tumbo kila wakizima taa lakini akiwa na nguo zake za kulalila ilikuwa mimba ya kawaida.

Alijiuliza kwa nini wakizima taa linakuwa kubwa na kingine kwa nini hataki kumruhusu kulichezea tumbo lile kwenye mwanga! Alipanga siku ile usiku amtegee Shehna amelala awashe taa ili kutaka kujua kwa nini usiku tumbo lake linakuwa kubwa sana. Aliendelea na kazi kama kawaida huku taarifa za Sara zikizidi kumchanganya kutokana na kuelezwa hajulikani halipo wala hakuaga.
Mazingira ya kutoweka yalikuwa yakilingana na ya mara ya kwanza kitu kilichomfanya ajiulize Sara ana matatizo gani yanayosababisha kutoweka bila taarifa. Alikumbuka maelezo aliyopewa na Sara siku aliyorudi kazini baada ya kupotea kimiujiza alitoka kwenda kununua chakula cha usiku na kujikuta akiwa katika pori la kutisha na baada ya kutembea bila kujua na kutokea Dodoma.
Kingine kilichomshtua kuambiwa kuna mbwa alikutwa chumbani kwa Sara baada ya kumfukuza alirudi tena usiku na kusimama kwenye mlango uleule. Alijiuliza kipi hasa kimempata Sara na ana siri gani ambayo yeye na majirani zake hawaijui. Alipanga akienda kwa Shehna kumueleza tatizo lile labda angeweza kumsaidia.
Usiku ulipoingia kama kawaida aliposhtuka usingizini alijikuta yupo pembeni ya mpenzi wake Shehna. Kama kawaida tumbo lilikuwa la kawaida lililokuwa katika nguo nyepesi ya kulalia. Baada ya kuliwazana wote walipitiwa usingizi, Mustafa hakulala sana alishtuka mapema na kutulia kitandani alilichezea tumbo la Shehna ambalo lilikuwa haliishi hamu kwa vile lilimpa raha ya ajabu kila alipolipapasa.
Alitulia kwa muda kusubiri Shehna usingizi umkolee, baada ya muda alimsikia akikoroma. Alijua usingizi umemkolea. Aliteremka kitandani taratibu na kuelekea kwenye kandili ya dhahabu, aliiwasha huku akitetemeka aliipandisha mwanga ili aone vizuri.
Baada ya kuwasha taa na kumulika kitandani, alishtuka kuona kiumbe cha ajabu juu ya kitanda. Sura ilikuwa ya mpenzi wake Shehna lakini tumbo lake lilikuwa la ajabu lililokuwa kubwa na pembeni lilikuwa na rangi kama magamba ya nyoka na chini alikuwa na mkia mnene unaoungana na tumbo.
Mustafa alishtuka sana na kuanza kutetemeka, kingine kilichomshtua kuona kitanda walichokuwa wamelalia kilikuwa juu ya maji katika ya bahari. Mshtuko uliompata ulimfannya aanguke chini na kupoteza fahamu.
Baridi kali lilimuamsha Shehna usingizini, alipofumbua macho alishtuka kukuta amelala juu ya bahari. Haraka alijirudisha katika umbile la kawaida, palepale usiku mwili wake ulirudi kama kawaida na kuwa chumbani kwake lakini kandili ilikuwa ikiwaka. Alijiuliza nani aliyeiwasha taa ile, alishangaa kujikuta peke yake na kujiuliza Mustafa alikuwa wapi!
Alipoteremka kitandani alishtuka kumkanyaga mtu, alipoangalia alimuona Mustafa akiwa amelala chini amepoteza fahamu. Alijua tayari siri yake ilikuwa hadharani, alijiuliza atamwambia nini Mustafa amuelewe kuwa yeye ni jini pia alijiuliza akimueleza ukweli atakuwa tayari kuendelea kuwa naye!
Shehna alianza kulia kitu kilichomshtua mama yake baada ya kudondokewa na machozi. Malkia Bi Zaldau mke wa mfalme wa bahari ya dhahabu alikwenda katika chumba cha mwanaye. Alipofika alimkuta jasho likimtoka japokuwa kulikuwa na hali ya baridi, alishangaa kumuona Mustafa amelala chini.
"Vipi?"

Shehna ilibidi amweleze mama yake kilichotokea aliposhtuka usingizini.

Itaendelea wiki ijayo Msikonde wapenzi.......
 
Navuta pumzi nahema Efyuu!!! Itaendelea lini tena

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
IILIPOISHIA:
Muda wote John alikuwa ametulia
akimuangalia bosi wake aliyekuwa
ameinama.
“John,” Mustafa alimwita huku akinyanyua
kichwa kumtazama.
“Naam.”
“Kuna kitu kinanichanganya sana.”
“Kitu gani bosi?”
“Kuna baadhi ya mambo siyaelewi ni ya
ndotoni au kweli?”
“Mambo gani?”
“Unamjua yule mwanamke mzuri anayekuja
hapa?”
“Ndiyo.”
“Unamuonaje?”
“Kivipi?”
SASA ENDELEA...
“Unamuona yupo kama wanawake wengine?”
“Ndiyo, kwani vipi?”
“Ushawahi kuona mwanamke mzuri kama
yule?”
“Mmh! Sijawahi wewe umemtoa wapi, kwa
kweli ni mzuri sana tena sana ajabu kila
nikimuona mwili unanisisimka na mapigo ya
moyo hunienda mbio.”
“Unajua kwa nini?”
“Hata sijui.”
“Mimi nawasiwasi na yule mwanamke ni ji....”
Mustafa alinyamaza ghafla baada ya
kumuona aliyekaa mbele yake hakuwa mlinzi
John bali Shehna akiwa anamtazama uso
wake umejaa machozi ya damu. Alishtuka
sana mpaka akaanguka chini ya kiti, John
aliyekuwa amekaa kwenye kiti alishtuka
kumuona Mustafa akishtuka na kuanguka vile.
Alimuokota na kumkalisha chini kisha
alimnyanyua kumrudisha kwenye kiti, lakini
ajabu kila alivyoongea sauti haikutoka. John
alishtuka na kujitahidi kumwita Mustafa
ambaye alinyanyua mdomo kuzungumza kakini
sauti haikutoka. Alimpigia simu mkewe
ambaye naye alifika mara moja. Alishtuka
kumkuta mumewe kwenye hali.
“Vipi ilikuwaje?” alimuuliza mlinzi.
“Tulikuwa tukizungumza ghafla nilimuona
mwenzangu akishtuka na kuanguka chini.
Nilipomuinua kila alipotaka kusema sauti
ilipotea.”
“Sasa kipi kimempata jamani mume wangu?”
Husna aliuliza.
“Hata mi nashangaa, kwa kweli siku ya leo
simuelewielewi kabisa bosi.”
“Inawezekana ni malaria tumuwahishe
hospitali.”
Mustafa kila alipojaribu kuzungumza sauti
haikutoka, alikwishajua makosa yake kwa
kutaka kutoa siri ya Shehna ambaye
alifahamu kuwa si kiumbe cha kawaida
kutokana na matukio yaliyokuwa ya kimtokea
japo awali hakutaka kukubaliana na akili yake
kuwa Shehna si kiumbe cha kawaida.
Aliamini yote yaliyotokea haikuwa ndoto bali
kweli baada ya kuupata ukweli wa wasiwasi
wake wa tumbo la Shehna. Vyote alivyoviona
na kujikuta amelala katika ya bahari aliamini
moja kwa moja mpenzi wake si mtu wa
kawaida bali jini japokuwa hakuwahi kumuona.
Alijiuliza nini hatima yake baada ya kutaka
kuitoa siri ya Shehna ambayo hakutaka
kiumbe chochote akijue. Aliwasikia
aliyopanga jinsi ya kumpeleka hospitali,
aliwakatalia kwa kutikisa kichwa na kuomba
kurudishwa nyumbani kwa kuwaandikia
kwenye kalatasi.
“Sasa mume wangu utaponaje?”
“Nirudisheni nyumbani,” aliwaandikia
kuwasisitiza wasimpeleke hospitali. Lakini
alipoulizwa anaumwa nini aliwambia hajui ila
wamrudishe nyumbani. Mkewe alikubaliana na
mumewe na kumrudisha nyumbani.
Mustafa alitegemea kupata simu kutokwa
kwa Shehna naye apate nafasi ya kuomba
msamaha. Lakini wiki ilikatika bila dalili
zozote za simu kutoka kwa Shehna, kazini
hakuweza kwenda kwa wiki nzima ilibidi
apewe mtu mwingine nafasi ile huku kampuni
ikijitolea kumtafutia matibabu.
Hospitali zote alizokwenda halikuonekana na
tatizo lolote, Mustafa aliogopa kuwaeleza
sababu ya yeye kuwa vile kwa kuhofia adhabu
zaidi toka kwa Shehna. Baada ya tiba ya
hospitali kushindwa, watu walimshauri Husna
kuangalia upande wa pili labda mumewe
kachezewa. Mustafa pia hakutaka kwenda
kwa mganga kwa kuhofia kukatazwa kwa
mkewe kwenda kwa mganga na Shehna wakati
wa matatizo. Lakini ilibidi akubali kwa vile
ndugu zake wasinge muelewa.
Ilipelekwa kwa mganga mmoja Vingunguti,
alipofika walisubiri kwa muda ndipo
walipopata nafasi ya kuonana na mganga.
Alikuwa mganga kijana lakini alikuwa mtu
aliyejijengea sifa kutokana na kuwasaidia
watu matatizo yao. Baada ya kukaa mganga
alitaka kujua wateja wake wana tatizo gani.
Husna mkewe alimuhadithia mganga toka siku
ya kwanza kutokewa na tatizo lile kutokana
na maelezo ya mlinzi na hatua walizochukua
mpaka siku ile waliyompeleka mbele yake.
Baada ya kuwasikiliza alishika mkono wa kulia
kwenye paji la uso, baada ya muda akitikisa
kichwa kama amesisimka na kuanza kutua
mbwewe mfurulizo kisha aliweka mkono
sikioni kama anasikiliza simu na kuwa kama
anakubaliana alichokisikia kupitia kiganja
chake cha mkono na yeye alijibu kwa kusema:
“Eeh... ndiyo... ndiyo...ndiyo...
sawasawa...sawasawa... hapana...eeh...ndiyo...
hapana...sawa..sawa nimekuelewa.”
Baada ya kuzungumza vile kwa zaidi ya robo
saa alitoa mkono sikioni na kuwatazama
wateja wake kwa kutembeza macho kwa kila
mmoja huku macho yake yakionekana
kumeremeta kama ya simba na kuwatisha
wateja wake. Wote walikuwa kimya
wakimsikiliza kwa sauti kama mtu anayevuta
moshi wa kitu ndani alisema:
“Tatizo nimeliona, lakini linaonesha mwenyewe
analijua tatizo.”
“Kwa hiyo unatusaidia vipi?”
“Dawa yake hakuna ila naomba wote mtoke
abakie mgonjwa,” mganga aliomba kuachwa
peke yake na mgonjwa.
“Mmh! Kwa hiyo ndiyo atapona?” Husna
aliuliza.
“Naomba kwanza mtoke.”
Walitoka nje na kumuacha Mustafa na
mganga, baada ya kutoka mganga alitulia kwa
muda kisha alimwita Mustafa kwa jina lake.
“Mustafa.”
“Naam,” sauti ilitoka.
“Unajua tatizo lako?”
“Ndiyo.”
“Kwa nini ulifanya vile?”
“Nilikuwa na wasiwasi na mpenzi wangu
kutokana na mimba yake, ndiyo maana
nilikiuka masharti yake ili nione gizani kuna
nini.”
“Unajua kilichompata msaidizi wako?”
“Sijui.”
“Ubishi kama wako, sasa hivi ni mbwa.”
“Mungu wangu!” Mustafa alishtuka na kushika
mdomo.
“Baada ya kufanya kosa la kwanza bado
umeendelea kufanya kosa lingine la kutaka
kutoa siri ambayo ni yako peke yako hatakiwi
mtu kujua. Ni kweli mpenzi wako ni jini hilo
ulitakiwa kulijua mapema na si kwa kuitoa siri
nje.”
“Jini?” Mustafa alishtuka.
“Unashtuka nini wakati matukio yote yalikuwa
si ya kawaida, kwa vile bado ilibakia siri,
mpenzi wako kila alipozima taa aligeuka kuwa
jini kamili na tumbo lile kubwa ni mimba
yake.”
“Sasa nitafanyaje?”
“Kitendo cha Shehna kuja mbele yako wakati
unataka kutoa siri nje, amesababisha
maumivu makali ya tumbo sasa hivi yupo hoi.
Msaada wako ni kuendelea kuwa hivyohivyo ili
ibakie siri mpaka ajifungue, kama atakufa
lazima na wewe utakufa kwa vile tayari kuvuli
chako kimo ndani ya damu yako ambayo wale
wanao walio tumboni katika ujauzito ile.
“Hukutakiwa kuuona tumbo akiwa katika
umbile la kijini, ungeweza kufa muda uleule,
lakini mapenzi ya jini yule ni makubwa sana.
Kwa vile bado hukutaka kuelewa ukutaka
kutoa siri ile hapo ndipo ulipopewa adhabu
ambayo itaisha mpaka ajifungue.”
“Lini?”
“Baada ya miaka miwili.”
“Miaka miwili niwe hivihivi?” Mustafa
alishtuka.
Nn kitaendelea sijui let's wait and see.................................mzizi mkavu usinimaindi ni ktk kukusaidia kazi tuu!!maana najua una majukumu mengi...

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Ubunifu wako nimeupenda .
Keep it up.
Ukituanzishia hadithi nyingine ukapiga moja kwa moja bila kupumzika itakuwa poa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom