Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

Hadithi ya kusisimua- Mimba ya Jini

Nimetumia masaa 4 kuisoma hii hadithi mpaka hapa ilipofika. Kweli ni yenye kusisimua na nilitarajia iwe imekamilika yote. Sina budi kusubiri.

Asante MziziMkavu kwa hii burudani.
 
Last edited by a moderator:
Nimetumia masaa 4 kuisoma hii hadithi mpaka hapa ilipofika. Kweli ni yenye kusisimua na nilitarajia iwe imekamilika yote. Sina budi kusubiri.

Asante MziziMkavu kwa hii burudani.

Ohoo nawewe pia unapataga muda na hizi maneno? Its good by the way
 
Last edited by a moderator:
HADITHI YA KUSISIMUWA MIMBA YA JINI -42

ILIPOISHIA:
“Kweli labda kichaa anaweza kutuuma pia hata watoto wetu.”
Jirani mmoja alishika fimbo na kuingia chumbani kwa Sara na kushtuka kumuona mbwa juu ya kitanda.


SASA ENDELEA..

Alimtishia kumpiga ili atoke nje lakini Sara alitaka kujitetea kwa kuwaeleza kuwa yeye si mbwa ni mtu kama watu wengine lakini aliishia kumfokea kitu kilichoonesha anataka kumuuma.
Ilibidi jirani amtandike fimbo iliyomfanya Sara apige kelele kwa maumivu na kutoka nje ili kujiokoa na kipigo kile na kutokomea mitaani.
Kila mtaa alipopita watoto walimpiga mawe kitu kilichozidi kumweka kwenye wakati mgumu, yeye alijifahamu ni mwanadamu na si mbwa lakini kila kona alipopita aliitwa mbwa.
Alitafuta jumba bovu na kuingia humo kujificha japokuwa kulikuwa na kinyesi ambacho kilikuwa na harufu mbaya, lakini aliamini ile ni sehemu salama kwake kuliko kuzurura mitaani na kupigwa mawe na watoto.
***
Shehna baada kumtia adabu Sara japokuwa moyo wake haukupenda kutoa adhabu yoyote, alirudi nyumbani kwao na kuingia chumbani kwake na kuanza kulia sana, kitu kilichomshtua mama yake Bi Zaldau, mke wa mfalme wa bahari ya dhahabu aliyempenda sana mwanaye Shehna kama mboni ya jicho lake, hakupenda hata siku moja kumuona akiumizwa na kitu.
Akiwa amejipumzisha chumbani kwake, alishtuka kuona machozi yamemdondokea kifuani, ile ilimjulisha mwanaye ana tatizo na muda ule alikuwa akilia.
Alijiuliza kipenzi chake Shehna kipi kimempata mpaka kulia machozi mengi yaliyomfikia yeye, alikwenda moja kwa moja chumbani kwa mwanaye na kumkuta akiendelea kulia.
“Shehna,” alimwita na kumfanya mwanaye ashtuke na kujifuta machozi haraka kisha alimgeukia mama yake.
“Shehna mwanangu una tatizo gani mama?”
“Hapana mama sina tatizo bali nimemkumbuka mpenzi wangu Mustafa.”
“Shehna nilikueleza mapema kuwa kama unamtaka mwanadamu, mtafute asiye na mke ungeweza kuja naye huku.”
“Mama, Mustafa nilimpenda muda mrefu sana lakini ninyi ndiye mliyenichelewesha kuonana naye mpaka akaoa mwanamke mwingine.”
“Ulikuwa bado hujatimiza umri wa kukutana na mwanaume.”
“Hata kama bado, nilitakiwa nionane naye mapema ili asioe mwanamke mwingine anisubiri mimi.”
“Hilo kweli tulifanya kosa, lakini mbona linawezekana kurekebishika.”
“Utalirekebisha vipi wakati ana mke tayari?”
“Si tunampoteza mkewe.”
“Hapana mama siwezi kufanya hivyo, kosa la mkewe lipi mpaka apotezwe?” Shehna alimkatalia mama yake kumuua mke wa Mustafa.
“Basi tumfanye asiwe na hamu na mumewe.”
“Vilevile sioni kosa lake.”
“Halafu mbona inaonesha kinachokuliza sicho unachonieleza, ulitoka na Kubash, mlikwenda wapi halafu juzi nilimuona Shush akiwa na damu mikononi, kuna nini ambacho sikijui?” mama Shehna mke wa mfalme wa bahari ya dhahabu Malkia Bi Zaldau alihoji.
“Mama ndicho kinachoniliza, kuna msaidizi wa Mustafa ananifuatilia sana, nimejaribu kumtisha lakini hasikii. Jana usiku alikwenda kwa waganga wawili, mmoja alikataa kumtaka kumfanyia kazi yake lakini wa pili alikubali na kutaka kuniua. Wakati nimejilaza, nilianza kupoteza nguvu na kumwita Shush haraka awahi kumzima yule mganga kwani angechelewa ningekufa mimi.”
“Sasa umempa adhabu gani?”
“Nimemgeuza mbwa.”
“Shehna mtu anataka kukuua, unamgeuza mbwa adhabu gani hiyo isiyolingana na dhamira yake mbaya?” mama yake alikasirika.
“Mama hata kumgeuza mbwa kwangu nimeona ni adhabu kubwa sana, nilitaka kumuacha lakini imebidi nifanye hivyo.”
“Mwanangu huruma gani hiyo ya kujiumiza?”
“Mama, kosa lake kwenda kwa mganga bila hivyo wala asingenisumbua, nimemuua mganga kwa vile alitaka kuniua, zaidi ya hapo nisingesumbuka naye.”
“Mmh! Sasa kinakuliza nini?”
“Sipendi kuingia katika dhambi ya kulazimishwa.”
“Basi kama umempa hiyo adhabu inatosha, usilie mwanangu.”
“Sawa mama nimekuelewa.”
Shehna alijilaza kifuani kwa mama yake kuonesha amekubaliana naye.”
***
Mustafa alishtuka, siku ya pili alishtuka kufika kazini na kukuta ofisi bado imefungwa, alifungua na kuingia ndani. Ofisi ilikuwa chafu, hata hali ya hewa ilikuwa mbaya. Alijiuliza Sara atakuwa wapi mpaka muda ule, kitendo cha kuchelewa kazini kilizidi kumfanya amchukie Sara na kupanga akifika lazima amfukuze kazi.
Alishindwa kukaa ndani kutokana na hali aliyokuwemo na kutoka nje, alikwenda hadi kwa mlinzi ili akamwambie afanye usafi. Kabla hajafika kwa mlinzi, simu yake iliita. Alipoangalia ilikuwa inatoka kwa mpenzi wake Shehna.
Aliipokea na kuzungumza.
“Haloo mpenzi.”
“Haloo laaziz, vipi mpenzi wangu?”
“Safi tu.”

Itaendelea kwenye Jumamosi
 
HADITHI YA KUSISIMUWA MIMBA YA JINI -43-

ILIPOISHIA:
Kabla hajafika kwa mlinzi simu yake iliita alipoangalia ilikuwa inatoka kwa npenzi wake Shehna.
Aliipokea na kuzungumza.

"Haloo mpenzi." SASA ENDELEA...


"Haloo laaziz, vipi mpenzi wangu?"
"Safi tu."
"Mbona kama mnyonge?"
"Bwana huyu msichana ananichanganya sana."
"Kafanya nini?" Shehna alijifanya kuuliza.
"Hajafika mpaka saa hizi yaani ofisi chafu."
"Basi usikonde mpenzi wangu baada ya dakika mbili watakuja wasichana wangu kuja kufanya usafi uwape nafasi tu."
"Hakuna tabu."
Baada ya muda kidogo wasichana wawili warembo walibisha hodi kwenye geti, Mustafa alipowatazama alijua ndiyo waliotumwa na mpenzi wake Shehna.
"Asalaam aleykum," wale wasichana waliwasalimia kwa bashasha na sauti tamu.
"Waleykum salaam, nina imani ninyi ni wageni wangu?" Mustafa aliuliza.
"Swadakta, hatuna muda tuoneshe hiyo kazi."
Mustafa aliongozana nao hadi ofisini, baada ya kuwaonesha mmoja alisema:
"Haya tupishe tufanye usafi."
"Hakuna tatizo," Mustafa alijibu huku akitoka nje na kuwaacha wale wasichana.
Baada ya kutoka walipiga makofi, haikuchukua muda waliongezeka wengine ambao walifanya kazi ya usafi kwa muda mfupi. Baada ya usafi wenzao walitoweka na kuwaacha wale wawili. Nao walitoka hadi alipokuwa amekaa Mustafa getini na mlinzi walipokuwa wakizungumza tabia za Sara zilivyobadilika tofauti na zamani.
Walipofika walimweleza kwa sauti tamu yenye lafudhi ya kimwambao.
"Bwana sisi tunakukimbia tuna imani utafurahia usafi wetu."
"Nina waamini, nashukuru sana."
"Haya si tukukimbie."
"Haya, msalimieni sana Shehna."
"Salamu zimefika."
Wasichana wale walitoka nje ya geti na kutembea kufuata barabara, baada ya kuwa sehemu ambayo walijua Mustafa hawaoni walitoweka ghafla kurudi chini ya bahari.
Mustafa alirudi ofisini na kuikuta ofisi inapendeza kila kitu kilikuwa kimesafishwa ndani kulikuwa na hewa na harufu nzuri ya manukato. Alikaa kitini na kuanza kazi huku akiamini kama atamuoa Shehna basi ataishi maisha sawa na peponi.
***
Kila usiku Mustafa alifuatwa akiwa ndotoni na kujikuta yupo sehemu nzuri akiwa amelala pembeni ya Shehna aliyekuwa amelala huku tumbo lake likizidi kukua. Lakini alikuwa amevaa gauni jepesi lililoziba tumbo lake. Usiku sana Shehna alizima taa na kuondoa nguo zake na kumruhusu Mustafa alichezee tumbo lake lakini ikiwa gizani.
Siku zote Mustafa alifurahi kuwa karibu na mpenzi wake na kutamani siku zote awe karibu yake. Tumbo la Shehna halikuwa likimsisimua lakini hakupata nafasi ya kuliona, siku zote alimbembeleza kuliona Shehna alimwambia avute subira. Mustafa alikubaliana na mpenzi wake.
Katika siku alizolala alishangaa tumbo la Shehna kuwa kubwa akilala akiwa hana nguo tofauti na akimkuta amevaa nguo. Ile ilimfanya apange kumvizia wakati amelala ili awashe taa aone sababu ya tumbo lile kuwa kubwa tofauti na matumbo ya kawaida ya wanawake wenye mimba.
Wakati huo Sara aliendelea kuteseka na baridi na njaa hakutoka kwenye nyumba ile mbovu mpaka kiza kilipoingia, aliogopa kutoka muda ule kwa kuhofia kupigwa na kuumizwa. Kiza kilipoingia ndipo alipotoka na kurudi nyumbani, lakini alipofika sehemu ya chumba chake ambacho kilikuwa kimefungwa alisikia mtu akisema:
"Jamani yule mbwa wa asubuhi amerudi tena."
"Jamani huyu mbwa atakuwa ametumwa tu, tena amesimama kwenye chumba cha Sara."
"Jamani lazima kutakuwa na tatizo, Sara jana si alilala chumbani kwake ajabu asubuhi tukumuona na kukuta mlango upo wazi na mbwa huyu alitoka ndani. Ajabu tulimfukuza asubuhi usiku amerudi," shoga yake Happy alisema.
"Sasa na Sara atakuwa wapi?"
"Hapa ndipo tunachanganyikiwa maana hajaaga kama amepata dharura usiku."
Sara yote aliyasikia akiwa bado amesimama kwenye mlango wake, lakini alishindwa kuzungumza kwa kuhofia kubweka na kuwatisha kitu kitakachowafanya wamfukuze kwa kumpiga.



Itaendelea Jumanne ijayo
 
Khaaa wewe mimi ndio nilipewa mimba na mstaafa ukiendelea kusimulia nitakupa adhabu ya sara uwe paka kabisa wewe
 
HADITHI YA KUSISIMUWA MIMBA YA JINI -44-

ILIPOISHIA:
"Jamani lazima kutakuwa na tatizo, Sara jana si alilala chumbani kwake, ajabu asubuhi hatukumuona na kukuta mlango upo wazi na mbwa huyu alitoka ndani. Ajabu tulimfukuza asubuhi, usiku akarudi," shoga yake Happy alisema.
"Sasa Sara atakuwa wapi?"

SASA ENDELEA...

"Hapa ndipo tunachanganyikiwa maana hajaaga kama amepata dharura usiku."
Sara yote aliyasikia akiwa bado amesimama kwenye mlango wake, lakini alishindwa kuzungumza kwa kuhofia kubweka na kuwatisha, jambo ambalo lingewafanya wamfukuze kwa kumpiga. Akiwa bado amesimama mlangoni alisikia akiitwa jirani yake kwa sauti aje amfukuze.
"Baba John, yule mbwa wa asubuhi amerudi tena," mama John alimwita mumewe.
Sara alijua majanga bado yanamuandama, alilia kilio cha kimyakimya kwa kuogopa kutoa sauti kuwatisha. Alijiuliza atajitetea vipi ikiwa hawezi kuzungumza sauti ya kibinadamu. Alimuona jirani yake baba John akitoka ndani na kuuliza:
"Yupo wapi?"
"Yule pale kwenye mlango wa Sara."
"Huyu mbwa anatafuta kufa hapa subiri," alisema kwa sauti ya hasira aliyoisikia Sara.
Baba John alisogea pembeni na kuchukua gongo ili ampige, Sara alishangaa kusikia sauti iliyokuwa ikimtokea bila kumuona anayezungumza ikisema:
"Sara ondoka haraka watakuumiza."
Sara hakuchelewa alitimua mbio, alipoondoa mguu tu gongo lilitua kwenye mlango na kutoa sauti, alisikia sauti ya baba John akisema:
"Bahati yake lingempata angekufa, ------- kafie mbele kama umetumwa."
"Jamani huyu ni mchawi, huyu mbwa si bure, iweje ang'ang'anie hapa tena kwenye chumba kimoja cha Sara?" alisema Happy kwa uchungu.
Sara alitimua mbio mpaka nyumba ya jirani na kutweta huku akijiuliza nini hatima ya maisha yale?Alijiuliza atalala wapi usiku ule wenye baridi, kama angekuwa na uwezo wa kibinadamu basi angechukua kamba na kujinyonga. Njaa na kiu vilimshika, asingeweza kula jalalani au maji machafu. Kwake kilichobadilika kilikuwa umbile tu lakini akili ilikuwa ileile ya kibinadamu.
Wingu la mvua lilitanda na baridi ilizidi kuwa kali na kumfanya atetemeke, ilionesha mvua kubwa inaweza kuteremka wakati wowote. Aliona sehemu anayoweza kujistiri usiku ule ni mule kwenye jumba bovu lenye harufu kali ya kinyesi.
Alijiuliza nini hatima yake hata kama usiku ule utapita na atawezaje kulala na njaa na kesho yake aamke?
Hakuwa na jinsi kwani wingu lilikuwa zito, alikimbilia kwenye jumba lile na kuingia ndani ili mvua isimkute. Alisogea kwa ndani na kutafuta sehemu kavu kisha alijilaza chini, moyoni alijuta kutosikiliza maneno ya Shehna. Kiherehere chake kilimponza na kujiuliza hata kama Shehna ni jini, bado hakumuhusu kwa vile Mustafa hakuwa mumewe, wala ndugu yake na ujio wake pale hakumuathiri chochote.
Sara alilia sana lakini hakuna aliyesikiliza kilio chake kwa vile kilikuwa cha kujitakia, hakikuwa na pole. Njaa nayo ilizidi kumchonyota kwa vile toka asubuhi hakuwa ameweka kitu chochote tumboni wala kunywa maji. Hakuwa na jinsi, alikubaliana na yaliyokuwa mbele yake na kumuachia Mungu aamue maisha yake.
Majira ya saa saba usiku, mwanga mkali ulimpiga machoni, alipoangalia vizuri aliwaona wanawake wawili wazuri waliokuwa wamesimama mbele yake na kumwita jina lake.
"Sara."
Alishindwa kuitikia kwa kuhofia kubweka, aliwaangalia tu huku akijiuliza wale ni akina nani na wamejuaje yupo pale. Wale wasichana warembo walimwambia atoke ndani, alinyanyuka na kuwafuata. Alishangaa kuwasogelea bila kushtuka, alipowasogelea walimshika kichwani, ghafla Sara alirudi katika umbile la kibinadamu.
"Sara tumetumwa na Shehna tukuletee chakula."
"A..asa..sante," Sara alishukuru huku akipiga magoti.
Alijua baada ya chakula atabakia katika umbile lake la kibinadamu, alitoka nje ya jumba lile na kurudishwa kwenye chumba chake kisha akala chakula kile kitamu na kunywa maji.
Baada ya kula na kushiba alielezwa maneno yaliyomnyong'onyesha na kutamani ardhi ipasuke na kummeza.
"Sara, samahani tutakurudisha katika umbile la adhabu kisha tutakurudisha tulipokutoa."
"Jamani nisameheni, sirudii tena, nikirudia nifanyeni vyovyote," Sara alipiga magoti kuwaomba msamaha.
"Sara sisi hatujui sababu ya wewe kugeuzwa mbwa, tumetumwa tukuletee chakula tu, zaidi ya hapo hatuna mamlaka yoyote."
"Na..naomba unikutanishe na Shehna nimweleze haya."
"Sara unatuchelewesha," walimshika kichwani mara moja Sara akarudi katika umbile la mbwa. Wale wasichana warembo walitoweka ghafla na kumuacha Sara nje ya jumba bovu walipomtoa na kumrudisha.
****
Mustafa kila alipokuwa kazini, alikuwa na maswali mengi juu ya tumbo la Shehna kuwa kubwa kama puto lililojazwa hewa lakini lilikuwa laini na kupenda kulishika muda wote hata kumfanya kila siku alale kwa muda mchache.

Itaendelea wiki ijayo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom