Hadithi ya Kongamano la Iringa

Hadithi ya Kongamano la Iringa

umbwa mzee

Member
Joined
Sep 16, 2016
Posts
11
Reaction score
2
TAMU NA CHUNGU YA KONGAMANO LA IRINGA.







Naitwa Vailet, wengi hupenda kuniita vai, Ni mkazi wa Dar es laam, ilala msimbazi center, huko ndiko ninakoishi na mume wangu mpenzi anaeitwa Ray, ambae tumeona miaka mitau iliyopita, mume wangu anafanya kazi ofisi za TRA Dar.
Katika maisha yetu tulikuwa tukiishi kwa furaha siku zote, mume wangu alinipenda sana na mimi pia nilimpenda Sanaaa, alikuwa akinijali na kunithamini sana,
Tangu tumeoana sikuwahi kumsaliti mume wangu hata Siku moja na yeye hakuwahi kunisaliti nikajua.
Mimi ni mhadhiri wa chuo kikuu cha dar es salaam. Ambapo nafundisha fasihi.pia ni mwanachama wa chalufakita.
wakati kongamano la chalufakita likiwa linatangazwa kwenye makundi ya what's up, kuwa litafanyika Iringa, yaani nilifurahi sana nikamshirikisha mume wangu, nikamwambia kongamano la chalufakita litaenda kufanyika iringa lazima twende wote. Mume wangu aliniangalia tu bila ya kunijibu chochote, kitu ambacho sio cha kawaida kabisa, kwani tulikuwa na tabia ya kwenda wo wote kwenye sherehe yoyote ile, hata ikiwa nje ya mkoa. Baadae akanijibu..." nitaangalia ratiba za kazi".
Ulipofika mwezi mmoja kabla nikamuuliza tena mume wangu kuhusu safari ya kwenda kwenye kongamano la chalufakita iringa, ndipo mume wangu akaniambia, " nakupenda sana malikia wangu, natamani tuwepo wote siku hio ya kongamano, lakini nisamehe sana, sitaweza kuhudhuria kongamano hilo kutokana na majukumu ya kikazi yalivyonibana, lakini wewe nakuruhusu uende, ila nakuusia usiache mbachao kwa msala upitao, ukajichunge sana huko uendakona pia fahamu ya kuwa sio kila king'aacho ni dhahabu, nakuomba sana mke wangu kamwe usijeukavunja heshima ya ndoa yangu ambayo tumeiweka ndani ya miaka mitatu sasa".
Aliongea kwa hisia kali sanaa mpaka nikapata wasiwasi.
Lakini nikamuitikia, nimekuelewa mume wangu kamwe siwezi kukusaliti.Siku zilizidi kwenda tukawa tunaishi maisha ya Furaha sana na mume wangu.
Zikiwa zimebaki wiki tatu kabla ya kongamano,
Siku moja nilipokuwa kazini akaja secretary akaniambia madam kuna barua yako, nikamuuliza inatoka wapi? Akaseama utasoma mwenyewe.
Ndipo nikapokea barua ambayo sikujua nani kaituma. Moyo ulinipasuka sana, lakini nikaifungua muda huohuo, kumbe barua hii alikuwa ameandika mpenzi wangu wa zamani ambaye nilikuwa naye kabla ya kuolewa na alijulikana kwa jina la Cheni.
Cheni alikuwa mpenzi wangu wa zamani kabla sijaolewa, na tulikuwa tunafanya nae kazi chuo kikuu cha dar es salaam yeye akifundisha isimu na mimi nikifundisha fasihi. Cheni alinipenda sana na tuliwekeana ahadi kedekede, ikiwemo ahadi ya kuja kuoana, lakini ahadi hio ilivunjika baada ya yeye kwenda kujiendeleza kimasomo nchini Uingereza. Hata hivyo baada ya kumaliza masomo yake alifanikiwa kupata kazi hukohuko na kukataa kurudi Tanzania kabisa.
Roho iliniuma sana kwa kumpoteza mpenzi wangu huyu ambae nilimpenda kwa dhati, kibaya zaidi hata simu zake zilikuwa hazipatikani. Nilimvumilia sana Mpenzi wangu cheni kwa muda wa miaka miwili lakini hakurudi wala sikuwa na mawasiliano naye yoyoyete, ndipo nikaamua kuolewa na kijana huyu aitwae Ray, ambae ndio mume wangu wa sasa. miaka mitano sasa imepita tangu tupotezane na mpenzi wangu cheni, ndipo nikapata barua hii iliokuwa imeandikwa hivi;
Kwako Mpenzi Vai,
Mimi ni mpenzi wako zamani wa cheni,
Natumaini umzima wa afya, nilishawahi kuja dar mwaka jana nikaambiwa kuwa demu wangu keshaolewa, nilihuzunika sana, nikakosa Furaha kabisa. Jiji la dar nikaliona kama jehanamu, nilikuwa kama kinda la ndege lililotelekezwa na mama yake, kwani nilikuwa mpweke sana, ukizingatia nilishajiwekea malengo ya kuja kukuoa. Bali mihangaiko ya maisha ndio iliyoniweka mbali na wewe malkia wangu, baada ya kukukosa ndipo nikaamua kurudi zangu Uingereza. Ambako kwa sasa nimebadilisha fani nafanya kazi katika kampuni binafsi.
kikubwa kilichonipelekea nikuandikie barua hii ni kwamba nimepata habari kuwa Kutakuwa na Kongamano la Chama cha Lunga na fasihi ya kiswahili ambalo litafanyika chuo kikui cha Iringa mwezi August, Hivyo Mimi kama mdau Wa Kiswahili nitahudhuria kongamano hilo kwa kuwa mwezi huo nitakuwa Tanzania, hivyo nakuomba Fanya uwezavyo tukutane katika kongamano hilo ili nikueleze kilichonipelekea kupoteza mawasiliano na binti mrembo kama wewe.
Ukipata barua hii naomba unijulishe kwa namba zangu za simu zilizopo hapo chini.
Wako akupendae,
. Cheni.
Nilipatwa na mshangao baada ya kusoma ile barua, ghafla nikajiuliza maswali huyu mtu anajua kuwa nimeolewa, sasa he mume wangu akijua itakuwaje? Na mume wangu akiiona hii barua je? Maswali yote hayo sikuyapatia majibu nikabaki kwenye dembwi la mawazo tele.
Niliporudi nyumbani mume wangu alinipokea kwa shamrashamra sanaa, akaniambia nimerudi mapema na nimekuandalia chakula mpenzi, nikamwambia sawa, lakini nikawa nababaika sana hasa alipotaka kunipokea mkoba. Nikamwambia hapana usinipokee. Hata wakati tunakula nilikuwa nababaika sanaa mpaka mume wangu akawa na wasiwasi na mimi. Akaniuliza "uko sawa mke wangu? Najua unawaza safari ya iringa tu, nitakugharamia kila kitu sipendi upate shida hata kidogo, nataka uwe na Furaha sana siku hiyo, wewe ndio mwanamke wa maisha yangu."
Alisema hivyo huku akinyanyuka na kunikumbatia, nikajikuta natabasamu na kuanza kusahau mawazo ya Cheni.
Baada ya kula nikaingia bafuni kuoga, nilipotoka tu nikachukuwa mkoba wangu ili niifiche barua ile nilioandikiwa na mpenzi wangu Cheni, lakini sikuiona. Nilimwaga vitu vyote kitandani lakini sikuiona, nikamuita mume wangu nikamuuliza, akasema hajawahi kusachi mkoba wangu hata siku Moja, na hana tabia hio, akaniuliza hio barua imetoka wapi? Mimi sikumjibu, niloendelea kutafuta mpaka nikachoka, sikuwa na raha hata kidogo, niliwaza sana nimeiacha wapi hio barua, nikampigia simu mtu aende ofisini kwangu akaitizame lakini akaniambia hakuiona. Kijasho chembamba kikawa kinanitiririka nisijue nini chakufanya. Siku hio nililala mzungu wa nne na mume wangu, huku kichwa kikiniuma sana.
Mume wangu hakufurahishwa na hali hio akanifokea sana, akasema, "wewe mwanamke hio barua imetoka wapi? Naomba usinifanye Fala mimi , nieleze ukweli.
Nikamdanganya imetoka kwa rafiki yangu wa kike, haikuwa rahisi kuniamini lakini aliniamini kiasi.
JE NINI KITAENDELEA?
 
KONGAMANO LA IRINGA-2



Toleo lililopita tulimuona Vai akitafuta sana barua yake bila mafanikio, huku akihofia mume wake kuichukua barua hio.
Vai anaendelea kusimulia..... Nililala nikiwa na mawazo mengi sanaa, hata usingizi sikupata vizuri, nilijiuliza maswali mengi sanaaa kwamba je kama hio barua ameichukuwa mume wangu Ray hivi ataniruhusu niende kwenye kongamano kweli?. Nilijikuta usiku mzima nageuka geuka mpaka mume wangu akaamka akawa ananiangalia tu.
Asubuhi kulipokucha nilidamka sana, ili kuwahi ofisini kwangu ili nikaangalie ile barua. Nilichukua usafiri wangu haraka nikaingia barabarani, wakati kukiwa na foleni ya magari katika Jiji la dar, nilishikwa na hasira sanaa, nilitamani niruke niwe tayari nimefika kazini kwangu. Taratiibu foleni ilipungua na mimi nikaendesha gari haraka kuwahi ofini. Niliposhuka nikaingia haraka ofisini nikapekua kila kona kwa umakini zaidi lakini barua ile sikuiona. nikachangua mafaili yangu yote pamoja na kufungua droo zote lakini barua sikuiona.
Akili ikanijia nitoke nje kwani inawezekana niliiangusha, nje nikakuta kumeshafanyiwa usafi, loooh wasiwasi ulizidi kunitawala, ikanibidi nimuulize mfanya usafi kama ameona barua yoyote ile, akasema ameokota makaratasi mengi na ameshaenda kuyachoma moto.
Nilirudi ofisini nikiwa sina raha kabisa, lakini baadae nikajiuliza kwani hii barua naitafuta ya nini? Mbona kama ni namba ya mawasiliano ya Cheni nilikuwa nimesha ihifadhi kwenye simu yangu?, hapohapo nikapiga simu ya Cheni ikawa inaita na alipopokea alifurahi sana kusikia sauti yangu, akaniuliza " Vai uwa la moyo wangu kwa nini umetupa jongoo na mti wake? Hujui kuwa nakupenda sana?" Nilijikuta nacheka tu nikamwambia Mimi nimeshaolewa tayari ila tutaendelea kuwa marafiki, yeye akanijibu " awali ni awali Vai kumbuka mimi ndio niliokuingiza mjini" . Tuliongea mengi sana mengine yakawa ni ya utani lakini kikubwa alinisisitiza lazima tukutane Iringa kwenye kongamano la CHALUFAKITA, pia akaniambia tuwe tunawasilina kwa njia ya what's up, nikamwambia sawa na maongezi yetu yaliishia hapo.
Niliishi kwa Mashaka sanaaa, huku nikitafakari mahali ilipo ile barua, lakini mume wangu hakuthubutu kuniuliza chochote, kitu kilichonipelekea niamini kuwa hakuichukuwa ile barua. Mimi binafsi nilikuwa nababaika sana muda wote sina raha, pia nikawa mkali sana na simu yangu kitu kilichopelekea mume wangu kuhisi kitu kibaya.
Niliendelea kuchati na mpenzi wangu wa zamani Cheni na akaniambia ameshaingia Dar tayari kwa kujiandaa na kongamano, pia akaniambia ameshaweka booking ya Chumba Royal hotel iliopo Iringa mjini, halaf akanitaka nimjulishe kila hatua niliyofikia.

Ikiwa kesho yake ndio safari safari, mume wangu siku hio hakwenda kazini, aliniandalia kila kitu, alinipigia pasi nguo zangu, akanisaidia kupika vyakula vyepesi ambavyo ningekula njiani kama chipsi, nyama, na mayai, yaani kwa kifupi mume wangu alikuwa na heka heka kuliko hata mm mwenye safari, kitu ambacho kilinifanya niamini asilimia mia moja kuwa mume wangu hakuichukuwa ile barua.
Niliendelea kuchati na Mpenzi Cheni akaniambia, ili mume wangu asifahamu kitu yeye atatangulia Iringa
halafu mimi nitamkuta stendi. Nilikubaliana nae na nikawa naificha sana simu yangu ili mume wangu asione zile Meseji.
Usiku ulipoingia tukiwa kitandani na mume wangu akaniambia maneno haya yafuatayo; "Vai narudia tena na tena nakupenda sana mke wangu, Angalia hilo kongamano la CHALUFAKITA, Lisije likawa CHAFUA NDOA, nakuomba fata kilichokupeleka huko, kwani Siku moja tu inaweza kubadilisha maisha yako yote, Mimi nitakupa hela za kutosha mpaka za kuishi hoteli ili mradi tu usipatwe na tamaa ya aina yoyote." Aliongea kwa msisitizo sana maneno hayo namimi nikamhakikishia kamwe siwezi kumsaliti mume wangu.
Asubuhi kulipokucha Nilidamka nikajiandaa na mume wangu akanipeleka stendi, akanilipia nauli na kisha akaniaga kwa busu zito huku machozi yakimtiririka mashavuni kwake. Kisha akaondoka.
Wakati gari inaondoka niliwaza mengi sana, nikajiuliza kwa nini mume wangu alitokwa na machozi aliponiaga? Lakini baadae nikapuuzia.
Nilianza kuwasiliana na Cheni, alifurahi sana kusikia kuwa mambo yetu hayajagundulika, akanihidi kuwa nitaenjoy sana tutakapoonana.
Gari ilienda kwa kasi sana njiani nikaanza kumuwaza sana mume wangu jinsi alivyonipenda kwa dhati, halaf nikawaza jinsi nitakavyokuwa na Cheni usiku ule kisha nikasema kutenda kosa si kosa bali kurudia kosa ndio kosa, ngoja nikajaribu kumsaliti mume wangu kwa mara ya kwanza.
Meseji zilizokuwa zikirushwa kwenye kundi la what's up jinsi watu wanavyowasili na baridi iliyopo huko iringa, zilizidi kunitia hamasa zaidi na nikatamani kufika haraka Iringa.
Gari iliingia Iringa mjini na kuanza kushusha abiria, Mimi niliposhuka tu macho yangu yaligongana uso kwa uso na cheni, ambae kwa kweli Cheni alikuwa Cheni kweli, kwani alizidi kuwa mtanashati, alivaa flana nzuri na jinzi ya blue, halaf alivaa cheni kubwa ya dhahabu, alivaa raba za blue zenye madoa meupe, kichwani alinyoa staili flani hivi kama wasanii wa nchi za nje, kwa kifupi alionekana mtanashati sanaa.
Alisogea na kunikumbatia huku akinishangaa na kusema Vai kwanini unaishi na kabwela? Angalia ulivyochujuka, urembo wote umeisha, ziwapi zile dimpozi zilizokuwa zikiupendezesha uso wako? Uwapi ule weupe uliokuwa unakufanya ung'ae kama mbalamwezi? Iwapi ile ngozi yako laini iliyokuwa inakufanya uonekane kama mtoto mchanga? Mbona mume wako amekukondesha hivi?" Mrembo kama wewe inabidi uishi na watu wenye ukwasi kama sisi, sio hao mafakiri wasiojua thamani ya mke.
Cheni aliongea maneno mengi sana hadi ikafika kipindi nikawa namuangalia tu. Alipomaliza kunishangaa akaniambia njoo kwenye gari. Akanipakiza kwenye gari aina ya Toyota Mark X, gari lake ambalo lilikuwa ni zuri sana na la thamani kubwa, tukaondoka mpaka hotelini.
Tulifika akaniandalia maji nikaoga halaf tukatoka kwenda kula, huko ndio akanihadithia mambo mengi sana kuhusu maisha yake. akasema yeye kwa sasa ni tajiri sana anamiliki kampuni ya kuuza magari hapa Tanzania ambayo anaisimamia mdogo wake, pia ana nyumba tano dar es salaam, akasema aliachana na kazi ya ualimu sababu alikuwa anaona anachelewa kupata mafanikio.
Aliniomba niachane na mume wangu ili anichukuwe tukaishi uingereza.
Tuliongea mengi na kunywa pombe nyingi sana mpaka ikafika saa tano usiku ndio akasema turudi chumbani tulikofikia. Cheni alinipania sana alisema "usiku wa Leo Maji utayaita mma kwa jinsi nitakavyo kupeleka puta kitandani, nikamwambi sawa twende ndani.
Kwa kuwa Cheni alikunywa pombe nyingi sana na alikunywa pombe Kali kama kilevi aina ya dompo, yaani alipoingia chumbani tu alijibwaga kitandani kama gogo hata Viatu hakukumbuka kuvivua, nilijaribu kumuamsha lakini wapi, nikaamua nimuache alale nikajisemea kimoyomoyo ama kweli mpania maji hayanywi. Mimi nikaoga halafu nikalala.
Ilipotimu saa nane wakati ndio usingizi unaanza kunoga, nikasikia kwa mbaaali mlango ukigongwa, nikajiuliza huyu anaegonga mlango ni mchawi au ? Nikakaa kimya ili nisikilize vizuri, nikasikia sauti ya kiume iliyobanwa ikisema " Mimi mhudumu naomba ufungue," mmmh nikajiuliza tena huyu mhudumu ametokea wapi muda huu na anataka nini?. Kila Nikimuangalia mpenzi Cheni yeye ndio kwaanza anakoroma, yaani. Nikaanza kuchanganyikiwa, lakini nikajipa moyo nikajifunga kanga yangu Moja nikaenda kufungu mlango, lahaula.....! Nilijikuta nashika kichwa kwa mikono miwili, Alikuwa ni mume wangu Ray akiwa amefura hasira Kali, mwili ukimtetemeka, na machozi yakimtiririka kwa kasi kama bomba la mvua. Kilichoniogopesaha zaidi ni jambia alilolishika mkononi likiwa linawakawaka kama limetoka kwenye mashine ya cherehe. Ray akasema AMA ZAKO AMA ZANGU, NA UKIPIGA KELELE TU...........
JE NINI KITAENDELEEEA....?
USIKOSE KESHO
 
mkuu kama utaiendeleza iendeleze hapa hapa usifungue uzi mwingine,unganisha hapa hapa
 
KONGAMANO LA IRINGA-3


Naomba niendelee na simulizi hii tam na ya kusisimua. sehemu iliyopita tuilimuona Ray akivamia chumbani alimolala mke wake Vai pamoja na Cheni, huku akiwa ameshika jambia mkononi mwake.
Vai anaendelea kusimulia.....
Nilitetemeka sanaa, meno yakawa yanagongana na midomo ikawa inacheza cheza, kijasho chembambaaa kikanitiririka, mapigo ya moyo yakabadilika na kwenda kwa kasi sanaaaa, sikujua nifanye nini, nikabaki najiuliza maswali moyoni mwangu je Rai amekujaje Iringa? Na amejuaje kuwa tumepangisha chumba hiki?
Pia nikajiuliza watu huwa wanasema siku za mwizi ni arobaini, mbona mimi leo ndio Siku yangu ya kwanza na nimekamatwa? Wakati nikiendelea kuwaza hayo ghafla nikashtushwa na sauti ya Ray ikisema, "Wewe kicheche nenda kamuamshe huyo hawala wako, maana nataka niwacharange mapanga mkiwa pamoja"

Nilijikuta napiga magoti na kuangua kilio kikubwa kilichomfanya Cheni ashtuke na kusimama, Cheni alisimama akiwa amevaa nguo zake zilezile alizokuja Nazo kwani alishindwa kuzivua na kulala hivyohivyo.
Ray alizidi kukasirika na kumsogelea Cheni na lile jambia huku akimwambia" sali sala zako za mwisho wewe fala, usione vyaelea vimeundwa hivi, "
mimi nilikimbilia pembeni ya ukuta nikilia na kuomba msamaha.

Hamadi mungu si athumani Cheni aliingiza mkono kwenye bukta yake na kutoa bastola, huku akimuelekezea Ray na kumwambia "naomba uweke jambia lako chini na usipoweka nakupasua kichwa sasahivi,"
looh sikuwahi kushuhudia ugomvi mkali kama huu, Mume wangu Ray alisalimu amri na kuamua kuweka jambia lake chini huku akitetemeka.
Mambo hayo yote yaliyokuwa yakitokea niliwahi kuyashudia tu kwenye luninga hasa nilipokuwa nikiangalia filamu za ngumi, lakini siku ile mambo hayo niliyshuhudia yakitokea mbele ya macho yangu yaani niliogopa sana, hata hivyo nikajikaza tu ili nisije nikageuziwa kibao.
Cheni aliniambia kwa sauti " Vai naomba chukuwa funguo ufungue hiyo brifkesi yangu kuna kamba yangu ndefu ya kufanyia mazoezi naomba uitoe nikufundishe cha kufanya, kweli nikitoa ile kamba huku nikitetemeka sana akanielekeza nimfunge mume wangu mikono na miguu kama mzigo wa kuni, huku akiwa amemuelekezea ile bastola ili asipige kelele,
mume wangu alipoleta vurugu alimpiga na Kitako cha bastola usoni, hali iliyompelekea mume wangu kuchanika kidogo usoni na kutoka damu, Ray akasema, "mke wangu unaniuwa sababu ya kongamano la chalufakita"? Alipoongea tu maneno hayo Cheni alimpiga tena, hali iliyompelekea mume wangu Ray kuzimia.
Nilizidi kuogopa sana maana nilijua nikileta ubishi tu au nikimtetea mume wangu na mimi naweza nikauliwa.
Cheni aliweka bastola yake chini na kuanza kumfunga vizuri Ray mikono na miguu, halafu akachukuwa shuka la hotelini akamfunga mdomoni ili asiweze kupiga kelele hata atakapoinuka. Alipomaliza Cheni akaniambia "umeona eee, dawa ya moto ni moto, Njoo sasa tule bata shori wangu, huyu jamaa ameingia choo cha kike na atajuta kuzaliwa."
Roho iliniuma sanaa hasa nilipomuangalia mume wangu pele chini alipolala, damu zinazomtiririka, na kamba alizofungwa, taratiibu machozi yakaanza kunitiririka na huruma ikanijia nikaanza kumpigia Cheni magoti ili amfungue mume wangu na asimtese kiasi kile, Cheni akanikaripia kwa sauti Kali, Weeeeeeeee weeeee, koma kabisa wewe kichenchede, nitakugeuzia kibao sasa hivi, ungekuwa unampenda mume wako mda huu ungekuwepo hapa? Si ungekuwa na mume wako huko?
Nilijikuta nanyamaza kimya huku nikitetemeka, nilipoangalia nguo yangu niliyovaa ilikuwa imetota, na nilipoikagua vizuri ilikuwa imejaaa mikojo, kumbe nilijikojolea bila ya kujijua.
Usiku huo hatukulala kabisa, Furaha tuliokuwa tunaitarajia ilitoweka ghafla, chumba kilitawaliwa na kimya kikubwa na majonzi humo ndani.
Ilipofika saa 12 asubuhi mume wangu Ray alikuwa bado hajazinduka, Cheni akaniambia nijiandae niende kwenye kongamano, nilipojaribu kukataa alinifokea sanaaa, akaniambia watu wote wanajua umeshaingia Iringa na umepangwa katika kuwasilisha mada yaani ni lazima uwende, mimi nitakupeleka halafu nitarudi.
Kwa hofu kubwa ya kuhofia kupigwa nilijiandaa haraka haraka na kumwambia tayari nimeshajiandaa twende akasema sawa.
Alinipakiza kwenye gari lake ambalo kwa wakati huo sikuona kama linathamani tena, nilipofika viunga vya chuo kikuu cha Iringa nikatelemka, na yeye akageuza gari kurudi Yaani huwezi amini nilijiona mwepesiii majengo ya Chuo kikuu cha Iringa nikayaona kama yanazunguuka, nikahisi kama akili yangu haifanyi kazi vizuri, nilizunguuka majengo ya chuo hicho kwa muda Wa saa moja bila hata ya kujua kama ukumbi CHALUFAKITA uko wapi? Mpaka akaja mlinzi akaniuliza Dada mbona unazunguuka sana ? Nikamwambia natafuta ukumbi ambapo Kongamani la Kiswahili linafanyika, akasema sawa mbona ndio huo hapo mbele yako? .
Hapo ndio nikaona kidogo akili zangu zinaanza kurudi taratiiibu, wakati naingia kwenye ukumbi nilihisi kila mtu ananishangaaa mimi , kwa aibu ilanibidi niiname chini, nikaenda kukaa kwenye kiti cha katikati.

Alipoingia Naibu waziri wa habari, tuliamka tukaanza kuimba wimbo Wa Taifa na baadae tukakaa kwenye viti, Ratiba iliendelea kama kawaida, Ukumbini kulikuwa na MC wawili waliobobea ambao niliwatambua kwa majina Sovu na Shadidu, yaaani walichangamsha ukumbi sana, lakini mwenyekiti wa CHALUFAKITA aliposimama na kuanza kuongea kuhusu chama, nikajikuta nasinzia, yaani nilisinzia mpaka nikapitiwa na usingizi kabisaa, wakati nipo kwenye usingizi nikaota mume wngu amechinjwa ukumbini hali iliyopelekea ukumbi wote kujaa damu, wakati huo maaskari washapigiwa simu na wako ndani ya ukumbi sasa akaja askari mmoja akanishika begani akinitaka nimfate.
Ghafla nikashtuliwa na kijana aliekuwa ananishika begani akiniamsha nikajikuta napiga kelele sio mimi jamani mnanioneaa
JE NINI KITAENDELEA.....?
USIKOSE TOLEO LIJALO.....
 
Back
Top Bottom