The Supreme Conqueror
JF-Expert Member
- Feb 13, 2017
- 609
- 1,574
Wapangaji 6 Wa nyumba moja walichanga changa na kununua bastola kujihami dhidi ya majambazi.
Makubaliano kuwa kwa kuwa bwana Ugoko yuko chumba cha karibu na mlango Wa kuingilia awe analala na bastola tayari kumkabili yeyote atakayejaribu kuwavamia
Siku bastola ilipowasili toka dukani na kutua kwa bwana Ugoko,
Ugoko aliwabadilikia wapangaji wenzake na kuwaamuru wote waweke mikono juu, akawaamuru wagaregare kwenye matope ya uwani,waruke kichurachura na vitimbi chungumzima
Waliowahi kukwaruzana naye huko nyuma na wale anaowadai waliipata "fresh".aliwasomea marufuku nyingi sana.
Hawakuruhusiwa kufungulia radio 📻 sauti ikasikika,
Kukaanga ni marufuku na sheria nyingine kibao.
Akawaapia kuwa yeye sio mtu Wa mchezo mchezo anayetaka ajaribu na aone!
Baadhi ya majirani walilalamika chini chini na wengine walimpongeza kuwa Ugoko ni kiboko.
Yamebaki na majuto na hawana namna tena cha kufanya wanasubiri labda risasi ziishe waweze kumkabili Ugoko,lakini je watawezaje kujua hilo wakati tayari Ugoko alikuwa mbele ya muda kwani amri zote alizishika yeye?
#Ugoko.
Makubaliano kuwa kwa kuwa bwana Ugoko yuko chumba cha karibu na mlango Wa kuingilia awe analala na bastola tayari kumkabili yeyote atakayejaribu kuwavamia
Siku bastola ilipowasili toka dukani na kutua kwa bwana Ugoko,
Ugoko aliwabadilikia wapangaji wenzake na kuwaamuru wote waweke mikono juu, akawaamuru wagaregare kwenye matope ya uwani,waruke kichurachura na vitimbi chungumzima
Waliowahi kukwaruzana naye huko nyuma na wale anaowadai waliipata "fresh".aliwasomea marufuku nyingi sana.
Hawakuruhusiwa kufungulia radio 📻 sauti ikasikika,
Kukaanga ni marufuku na sheria nyingine kibao.
Akawaapia kuwa yeye sio mtu Wa mchezo mchezo anayetaka ajaribu na aone!
Baadhi ya majirani walilalamika chini chini na wengine walimpongeza kuwa Ugoko ni kiboko.
Yamebaki na majuto na hawana namna tena cha kufanya wanasubiri labda risasi ziishe waweze kumkabili Ugoko,lakini je watawezaje kujua hilo wakati tayari Ugoko alikuwa mbele ya muda kwani amri zote alizishika yeye?
#Ugoko.