Hadithi: Nyuma Ya Machozi

Hadithi: Nyuma Ya Machozi

ILIPOISHIA:
Baada ya kutoka kwenye kikao na mkuu wake wa kazi, Fukwa aliwaita vijana wake wa kikosi maalumu na kutoa amri ya kijeshi.
“Nina imani mmemsikia mkuu, kwa hiyo sitaki kusikia tena muuaji bado anatamba, mpaka kesho jioni nataka tuwe tumemkamata. Sijui mtamkamata vipi, hiyo si juu yangu bali kusikia yupo mikononi mwa polisi, sawa?” Mkuu wa upelelezi Fukwa.
“Sawa mkuu,” vijana aliitikia kikakamavu.
SASA ENDELEA...

“Nina imani mmepata pa kuanzia?”
“Ndiyo mkuu.”
“Haya tawanyika mkimkosa na ninyi msirudi hapa.”
Ilikuwa kauli iliyowapa wakati mgumu kikosi cha kazi kinachodili na mtukio kama yale. Walikubaliana kutawanyika huku kila mmoja akijipa jukumu lake ili wakikutana wajue wamefika wapi.
***
Kachero Mzengwa alitembea taratibu maeneo ya Mirongo kwa kupita katika vijiwe vya Anko Jay Jay. Kwa vile alikuwa katika vazi la kawaida alifika kwenye uwanja wa mpira wa shule ya Mirongo na kuwakuta vijana wakicheza kamali huku wakivuta bangi hakufanya kitu na yeye alijichanganya.
Na yeye aligongea sigara ya kawaida na kuvuta huku akifuatilia kamari.
Mara alisikia jamaa mmoja akisema:
“Washikaji tumempoteza mwanetu Jay kama utani,” jamaa aliyekuwa akivuta bangi alisema.
“Mmh! Unajua naye alizidi kila kazi alifanya unakumbuka Tom nilimweleza Jay kwa kazi yake ya ukuwadi ipo siku atakufa. Jamani Jay kufa kwa risasi kama siyo kumkuwadia mume wa mtu ni nini?” mwingine aliongezea huku akilamba lizila unyonge bangi.
“Na kweli jamaa alizidi, mi nilijua mwisho wake mbaya.”
“Tena Side bahati yake alikwenda bushi la sivyo na yeye angekufa.”
Wakiwa katikati ya mazungumzo alitokea jamaa mmoja na wote waligeuka na aliyekuwa akinyonga alisema:
“Sideeee wapi Jay, jichanganye na wewe utamfuata mwenzako, fanya kazi zote lakini ya ukuwadi ni kifo.”
“Mwambie, hivi wewe mkeo akikuwadiwa utajisikiaje?”
“Jamani mbona umekosa ya kuzungumza, naona kijiwe hakinifai nikajichanganye na masela wa Lake sekondary,” Side alisema huku akiondoka taratibu na kuwaacha jamaa wakiendelea kumpaka mbovu.
“Side kuondoka siyo dawa, kama utafanya kazi ya rafiki yako nawe si muda mrefu utamfuata.”
“Ninyi mnajuaje kama kauawa na mke wa mtu?” Side alisimama na kuuliza.
“Side hata kama mimi siyo mpelelezi lakini ukiangalia mauaji yalivyotokea picha nzima inaonesha kauawa mwanamke aliyekuwa nyumba ya wageni. Hata siku mbili hazijapita kauawa Jay tena na mtu wa aina moja mwanamke anayevaa vazi refu la kumziba mwili na uso.
“Huyo mwanamke lazima amegundua yule mwanamke aliyemuua hotelini anatembea na mumewe na mtengeneza mipango ni Jay na yeye kumuua. Sasa nawe jipendekeze moto ukuwakie sisi siyo wajinga kukomaa na kazi za upusha, tunapenda maisha mazuri lakini mwisho wake kufa kama jambazi.” Jamaa mmoja aliyekuwa akisema kwa sauti nzito huku akinyonga ganja.
Machero Mzengwa alijikuta akipata kitu kipya ambacho hakuwahi kukiwaza, alichosema jamaa aliyekuwa akinyonga ganja. Japo alifurahi kumuona Side mtu muhimu kwake lakini pia alipata mwanga mwingine ambao aliamini utamsaidia atakapozungumza na Side. Alimpigia simu dereva wa defenda ili apate usafiri wa kuondoka na Side.
“Poa, lakini mnanionea bure,” Side alizidi kujitetea.
“Tukuonee vipi ikiwa wewe na Jay mlikuwa mnatutenga na kutuona sisi sio kwa vile mnakamata fedha ya ukuwadi.”
Mara ghafla kulizuka ugomvi baada kudhulumiana kwenye kamali, ile ilimpa nafasi kachero kumfuata Side aliyekuwa amesimama pembeni na kumsalimia.
“Side vipi?”
‘Poa mkubwa.”
“Sasa Side tuzungumze kidogo.”
Walisogea pembeni kidogo ili wazungumze, ghafla lilitokea defenda na kuwafanya waliokuwa wakicheza kamali na kuvuta bangi kukimbia. Side naye alitaka kukimbia lakini alishikwa na kachero Mzengwa na kushindwa kukimbia.
“Vipi Brother?” alilalamika ili aachiwe.
“Tulia,” Kachero Mzengwa alisema kwa sauti ya amri.
Baada ya gari kusimama Side alipakiwa na gari lililokwenda moja kwa moja hadi kituo cha makosa ya jinai. Waliteremka na kuingia naye kwenye chumba cha mahojiano. Kwa vile Side alikuwa na wasiwasi sana kachero Mzengwa alimuagizia soda ya baridi kwanza. Baada ya kutulia alianza kumuhoji.
“Side ondoa wasiwasi hutafanywa kosa lolote ila nahitaji msaada wako,” Mzengwa alianza kwa kumtoa wasiwasi.
“Msaada gani?”
“Anko Jay Jay alikuwa nani yako?”
“Rafiki yangu sana.”
“Kabla ya wewe kwenda shamba alikuwa na dili gani?”
“Mmh! Nakumbuka alipewa kazi na dada mmoja ya kumfuatilia mume wake.”
“Mume wake alikuwa na tatizo gani?”
“Alikuwa na wasiwasi anatembea na mwanamke mwingine.”
“Mmh! Baada ya hapo nini kiliendelea?”
“Aliniambia amegundua kweli yule mwanaume alikuwa na mwanamke kampangia hotelini.”
“Baada ya hapo?”
“Alipomaliza kazi yake alilipwa chake na mimi kesho yake nilisafiri, nikiwa bushi nilipopata taarifa za kushtusha kuwa mchizi wangu Jay ameuawa,” Side alisema kwa uchungu.
“Unakumbuka huyo mwanamke alikuwa amepangiwa hoteli gani?”
“Gorden Crest.”
“Na hiyo mwanamke unamjua?”
“Kwa kweli sikuwahi kumuona.”
“Sehemu anapokaa unapajua?”
“Ni Isamilo lakini nyumba siikumbuki vizuri kwa vile tulikwenda usiku ila nakumbuka nilimsubiri sehemu na kuingia kwenye nyumba yenye geti.”
“Hukumbuki hata kidogo?”
“Nikifika nitaijua japo sikuangalia vizuri siku tuliyokwenda.”
“Nafikiri twende muda huu ukatuoneshe hiyo nyumba.”
“Sawa.”
Walikubaliana kwenda kuitafuta nyumba ya mwanamke aliyempa kazi Anko Jay Jay ambayo waliamini anaweza kuhusika kwa asilimia kubwa katika mauaji yale.
*****
Majira ya saa kumi na mbili za jioni Land Cruser ilitembea taratibu katika mitaa ya Isamilo. Walilipaki sehemu na kuteremka kisha kutembea taratibu kufuata mtaa ambao Side alikuja siku moja na marehemu Anko Jay Jay kufuata malipo ya kazi aliyopewa ya kumchunguza mume wa mtu.
Sehemu aliposimama kumsubiri ilimchanganya kidogo kutokana na nyumba zile kufanana kidogo katika nyumba aliyoingia Jay.
“Vipi umeikumbuka?” kachero Mzengwa alimuuliza.
“Kati ya nyumba hizi mbali moja wapo, sikumbuki nilisimama wapi kwa vile ilikuwa usiku.”
“Joe unasemaje?” Mzegwa alimuuliza mwenzake.
Kabla hajamjibu lilikuja gari na kusimama kwenye nyumba moja kati ya zile mbili na kupiga honi. Baada ya muda alitoka mama mmoja mwenye mwili mkubwa kufungua geti huku akisema:
“Mume wangu leo nimekuwa mlinzi.”
“Mlinzi yupo wapi?”
“Nimemtuma mara moja.”
Baada ya kufungua geti gari lilingia ndani na kulifunga, baada ya kufungwa geti Side alisema:
“Itakuwa nyumba hii.” aliionesha nyumba jirani na gari lilipoingia gari.
“Kwa nini?”
“Jay alinieleza yule mwanamke anaishi na mume na mtoto mchanga hii inaonekana wenye nyumba ni watu wazima pia nyumba ile alinieleza haina mlinzi.”
“Una uhakika?”
“Ndiyo ni nyumba hii.”
“Basi tuondokeni tukajiandae kuja usiku nina imani kazi itakuwa si ngumu sana.”
“Na huyu?” Joe aliuliza kuhusu Side.
“Huyu tutakuwa naye mpaka zoezi la leo usiku liishe kisha atarudi kwake.”
Walirudi kwenye gari lao na kurudi ofisini kwa ajili ya operesheni ya kumtia mikono Kilole ambaye waliamini ndiye aliyekuwa akijua kila kitu juu ya kifo cha msichana aliyeuawa Gorden Crest na Anko Jay Jay japokuwa hawakujua muuaji ni nani, lakini waliamini kumtia mikononi yule mwanamke angewasaidia upelezi wao kwa kiasi kikubwa.
*****
Deus baada ya kuikagua siraha yake alisogea mpaka karibu ya dereva teksi Abdul aliyekuwa amezama kwenye penzi na mwanamke wa usiku.
“Mzee vipi?” Deus alimshtua Abdul.
“Poa mkuu.”
“Naona upo kazini?”
“Hapana nimemwita huyu baada ya kuona maboweka.”
“Njoo basi nje mara moja.”
Walitoka mpaka nje pamoja hadi ya cassino.
“Vipi mzee?” Abdul alimuuliza Deus akimtazama usoni.
“Mose unafahamiana naye sana?”
“Kiasi ila tunaelewana sana.”
“Kuna kazi nataka kukupa ukiifanya vizuri nitakupa fedha nzuri.”
“Kazi gani mkubwa?”
“Nina shida Mose ila nataka ukamtoe bila wapambe wake kuja nina mazungumzo naye.”
“Hilo mbona dogo.”
“Lakini usimwambie kama kuna mtu anamwita.”
“Hiyo kazi niachie mimi, akili yangu ukisikia fedha huwa haishindwi na kitu chochote hata kumfukua marehemu.”
“Basi nifanyie hiyo kazi mara moja, ila ukija hakikisha wewe unasimama huku na yeye huku.”
“Hakuna tatizo bosi wangu.”
Abdul aliingia ndani mara moja hadi kwenye meza za kamali na kumkuta Mose bado kashikilia bunda la dola akisubiri kuingia kucheza kamali.
“Mose,” Abdul alimwita alipomkaribia.
“Unasemaje Brother Abby?”
“Samahani nakuomba mara moja.”
“Una shiga gani brother? Zungumza nakusikiliza.”
“Naomba tutoke nje mara moja.”
“Si unajua muda wangu wa kuingia kwenye gemu umekaribia, jana walinila leo nina usongo nao,” Mose alijitetea ili asiende mbali.
“Dakika tano tu, waachie washikaji wakushikie unarudi sasa hivi.”
“Paul shika mkwanja huu narudi.”
“Poa mkubwa.”
Walitoka hadi sehemu ya kupakia magari, Deus alipomuona anakuja alizunguka nyuma ya gari. Walichomoa bastora tayari kwa tukio, walipofika walisimama Mose akiwa amempa mgongo Deus kama alivyomuelekeza Abdul. Aliiweka bastora yake tayari na kumsogelea taratibu hadi waliposimama na kumwekea bastora Mose kisogoni huku akisema kwa sauti ya chini yenye amri.
“Fungua mlango wa mbele wa gari na uingie ndani bila kuleta ujanja la sivyo nitakufumua ubongo.”
“Mheshimiwa vipi?” Abdul alishtuka kuona Deus ameshikilia bastora.
“Sitaki swali nawe ingia upande wako mara moja.”
Abdul hakutaka kubishana alizunguka upande wake na kuingia ndani na Mose naye alifanya kama alivyoelekezwa. Deus aliingia mlango wa nyuma na kusema kwa sauti ya amri.
“Elekea baharini mara moja.”
“Sawa,” Abdul alijibu huku akiwasha gari na kuondoka.
“Kaka mkubwa nimefanya nini?” Mose aliuliza kwa sauti ya upole.
“Utajua muda si mrefu.”
Gari lilitoka hoteli ya Piedimonte San Germano na kuingia barabara kubwa na kuelekea upande wa baharini.
“Abdul nataka gari likimbie kama linapaa,” Deus alitoa amri ya kijeshi.
“Hakuna tatizo mkubwa.”
Abdul alibadili gia na kukanyaga mafuta na kulifanya gari liondoke kwa mwendo wa kasi. Kabla ya kulivuka daraja refu gari la kina Mose lilikuja nyuma kwa kasi na kuwavuka na kusimama mbele yao kwa ghafla na kumfanya Abdul kufunga bleki kwa nguvu zote. Lakini gari lao liliseleleka na kwenda kuligonga gari la kina Mose wakati huo wapambe wa Mose walikuwa wametoka ndani ya gari na bastora mkononi tayari kumsaidia bosi wao.
Deus akili ilimchemka na kuona kafanya makosa ya kutoka naye mbali sana, lakini aliamini atapambana nao mpaka tone la mwisho la damu yake japokuwa alikuwa peke yake akipambana na kundi la zaidi ya watu sita wote wana siraha.
Deus naye kwa wepesi wake alitoka nje na kujificha nyuma ya teksi ya Abdul ambaye alikuwa hajui afanye nini. Wapambe walikuwa amekwisha ivamia gari na kumtoa bosi wao. Jamaa aliyetupwa juu ya gari na Abdul naye aliona ile ndiyo sehemu ya kulipa kisasi kwa Abdul.
Bila kuuliza alimjaza Abdul risasi za kichwa mpaka alipoamini amekata roho na kichwa hakitamaniki.
“Jamani mbaya wetu asikimbie,” Mose alisema kwa sauti ya juu.
“Hatoki lazima tumtie mikononi.”
“Nataka tusimuue tumshike akiwa hai,” Mose alitoa amri wa wapambe wake.
“Huyu hatoki hapa.” Ilikuwa kauli ya kumuunga mkono Mose ambaye alikuwa na hasira na Deus.
Deus aliinama kwa chini ili asionekane, wakati huo risasi zilikuwa zikirindima sehemu aliyojificha naye alijitahidi kujihami kwa kurudisha mashambulizi. Risasi ya bega iliyompata Deus ilimfanya adondoshe bastora chini. Alipotaka kuiokota kwa mkono cha kushoto alikuwa amechelewa teke zito lilitua usoni kwake na kumrudisha nyuma.

Itaendelea
 
SEHEMU: 41
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500
ILIPISHIA:
Deus aliinama kwa chini ili asionekane, wakati huo risasi zilikuwa zikirindima sehemu aliyojificha naye alijitahidi kujihami kwa kurudisha mashambulizi. Risasi ya bega iliyompata Deus ilimfanya adondoshe bastora chini. Alipotaka kuiokota kwa mkono cha kushoto alikuwa amechelewa teke zito lilitua usoni kwake na kumrudisha nyuma.
SASA ENDELEA...

Hakutaka kufa kikondoo alipambana kiume kwa kutumia mkono mmoja na mateke. Alijitahidi kuwadhibiti huku Mose akiendelea kuwakataza wenzake kutotumia siraha ili kumkamata akiwa hai.
“Jamani tusimuue lazima tujue nani kamtuma,” Mose alipaza sauti.
“Bosi usiwe na wasi atalegea muda si mrefu.”
Kauli ile ilimpa nguvu Deus ya kuendelea kupambana huku akishangaa ujasiri wa Mose wa kuwakataza wenzake wasitumie siraha na kuendelea kupambana kwa mikono. Kitu kizito kilichompiga Deus kisogoni kilimpoteza fahamu na kuanguka chini kama mzoga.
Mose na vijana wake kwa haraka alimchukua Deus na kumweka kwenye gari lao na kuelekea naye baharini.
“Mkuu wapi hii?” mmoja wa wapambe wake aliuliza.
“Huyu lazima tukamhoji bahari baada ya kupata ukweli tunamuua na kumtupia majini ili kuondoa ushahidi, pia inatakiwa usiku huu tuondoke Sicily twende Torino kwa muda ili sakata ili lipite lazima watatulitilia mashaka kwa vile gari letu linaweza kuonekana kwenye kamera zao.”
“Hakuna tatizo.”
Walimbeba Deus kuelekea ufukweni kwa ajili ya kumhoji na kumuulia mbali.
******
Kilole baada ya kufanikiwa kuwapata vijana waliomchimbia shimo nyuma ya nyumba. Aliwalipa ujira wao na kusubiri muda wa usiku auzike mwili wa mpenzi wake Kinape aliyemuua kwa bahati mbaya wakati wakigombea bastora.
Akiwa amesimama kwenye uzio kwa ndani aliona watu wakielekezana nyumba yake, ile ilimtisha sana na kuona bwawa linaweza kuingia luba.
Mapigo ya moyo wakiwa yana mwenda mbio alitulia akiwachungulia awaone wanataka kufanya nini.
Baada ya muda aliwaona wakiondoka, alijikuta akijiuliza watu wale walikuwa na shida gani. Baada ya kuondoka alirudi ndani na kutafuta pombe kali na kunywa ili kupunguza maumivu ya moyo baada ya kumuua mtu muhimu maishani mwake.
Majira ya saa tatu na nusu usiku Kilole alitoka mpaka nje ya geti kuangalia hali ya hewa ambayo ilikuwa tulivu. Aliamini hakukuwa na mtu aliyekuwa akimtilia mashaka alirudi hadi ndani na kwenda moja kwa moja chumbani na kuufunga vizuri mwili wa mpenzi wake katika shuka ambao ulikuwa amepoa na kuanza kukauka.
Aliuvilingisha shuka kisha aliuvuta mpaka chini na kuanza kuburuza kuupeleka nje kwenye shimo. Aliuburuza mwili hadi nje na kupumua kidogo kutokana na uzito wa mwili wa mpenzi wake. Alijifuta jasho kwa mkono kisha aliendelea kuuvuta mpaka karibu na shimo ili autumbukize na kuufukia.
“Hapo hapo... Upo chini ya ulinzi,” Sauti kali ya amri ilimshtua Kilole na kumfanya adondoke chini kwa hofu.
Alipoangalia aliwaona watu zaidi ya wanne wakiwa na silaha mkononi.
“Unafanya nini?” sauti kali ilimuuliza.
“Si.si..si..” Kilole aliingiwa kigugumizi huku haja ndogo ikimtoka kwa hofu.
“Unaburuza nini?”
“Jamani bahati mbaya sikukusudia.”
“Hukusudia nini?”
“Jose mbona kama mtu huyu?” Kachero Mzengwa aliuliza baada ya kuuona kilichokuwa kikiburuzwa kilikuwa kama mtu.
Wakitumia tochi kukichunguza kilichokuwa kikiburuzwa na Kilole, askari aliyeimana kuangalia alisema kwa sauti ya juu.
“Ha! Mtu?”
“Eti?” walishtuka.
“Bwana we, mwili wa mtu huu.”
“We mwanamke unaupeleka wapi huu mwili?”
“Samahanini jamani...ba..ba..ha..”
“Huyu nani?”
“Mu.mu..mu..me ..wa..wa..ng...”
Presha ya Kilole alikuwa kubwa sana kiasi cha kumfanya aishiwe nguvu na kupoteza fahamu. Walimpatia huduma ya kwanza lakini haikusaidia waliteuliwa askari wawili kumuwahisha Kilole hospitali ya Seko Toure katika ulinzi mkali.
Kabla ya kuupeleka mwili wa marehemu hospitali walifanya upekuzi kila kona ya nyumba ile. Ndani ya nyumba waligundua vitu vingi vikiwemo vifaa vya Kilole vya kufanyia mauaji. Pia bastora na risasi vyote vilivyokutwa ndani. Baada ya kukamilisha upekuzi walimchukua mtoto wa Kilole aliyekuwa amelala hajui lolote ili kumpeleka kwa mama yake.
Mwili wa marehemu waliupeleka hospitali ya Seko Toure kwa ajili ya uchungu kabla ya kufanya taratibu zote za kuwatafuta ndugu wa marehemu. Baada ya taratibu zote walimpeleka mtoto kwa mama yake wadini, walimkuta Kilole ameamka akiwa amejilaza mkono wake mmoja ukiwa na pingu iliyofungwa kwenye kitanda alicholala.
Aligeuka na kuwangalia askari na mtoto wake na kujikuta akiangua kilio, mtoto wake naye aliamka na kuanza kulia ilibidi anyanyuke na kunyonyesha ili anyamaze.
****
Deus alipepesa macho kuangalia sehemu aliyokuwepo alishtuka na kujiuliza pale alikuwa akiota au kweli. Alirudisha kumbukumbu kilimtokea mara ya mwisho ni kweli huku akijipapasa, mkono wake ulitua kwenye bega la mkono wa kulia na kukutana bandeji.
Alizidi kushtuka aligeuza shingo taratibu na kukutana na tabasamu pana.
“Pole mpenzi,” sauti tamu ya Teddy ilitua kwenye ngoma za masikio ya Deus.
“Teddy!” Deus alimwita akiwa bado anajipapasa.
“Abee mpenzi.”
“Ninachokiona mbele yangu ni kweli au naota?”
“Huoti mpenzi ni kweli mpenzi.”
“Hapana hii ni ndoto tu,” alisema huku akirudisha mkono kwenye bandeji na kuanza kukandamiza kwa nguvu. Lakini Teddy aliwahi kumshika mkono.
“Deus unataka kufanya nini?”
“Teddy hii ni ndoto tu.”
Alipoangalia pembeni alimuona mwanaye kipenzi Rose akiwa amelala usingizi, alizidi kujishangaa.
“Hapa ni wapi?”
“Ndani ya ndege,” Teddy alimjibu huku akimshika mkono aliouondoa kwenye jereha na kuanza kuupapasa taratibu.
“Ndani ya ndege! Tunatoka wapi na tunakwenda wapi?”
“Tunatoka Italia na tunarudi Tanzania.”
“Hapana...Hapana hii ni ndoto si kweli,” Deus alizidi kukataa.
“Kwa nini mpenzi?”
“Teddy nimekuacha Tanzania umefikaje Italia na umewezaje kuniokoa kwenye kinywa cha mauti?”
“Ni historia ndefu naomba kwanza tufike nyumbani, la muhimu mshukuru bwana Mungu wako kwa kukuwezesha kuendelea kuvuta pumzi yake mpaka muda huu.”
Pamoja na kuelezwa yote bado Deus aliamini ile ni ndoto kutokana na hali aliyokutananayo ya kuwa ndani ya kinywa cha mauti. Pamoja na kuamini ile ni ndoto lakini bado hakujua yupo wapi japokuwa ndoto ilimuonesha yupo sehemu salama.
Teddy aliamini kabisa Deus yupo katika wakati mgumu kuamini kilichomkuta na sehemu aliyokuwepo ilibidi amrudishe katika hali ya kawaida.
“Deus,” alimwita kwa sauti ya chini huku akitembeza mkono yake kichwani kwa Deus aliyekutana na joto la kumsisimua.
Deus hakuitika japo alisikia akiitwa aligeuza shingo na kumtazama Teddy aliyekuwa amekaa pembeni yake akitembeza mikono yake taratibu.
“Deus, najua ni vigumu kuamini hali iliyokutokea na sehemu uliyopo sasa ndiyo inakuchanganya sana.”
“Hapana Teddy si hicho.”
“Nini sasa kinachokufanya usiamini kama ni kweli?”
“Mimi na wewe tumeachana lini?”
“Juzi usiku.”
“Wapi?”
“Dar.”
“Ukijiandaa kwenda wapi?”
“Mwanza.”
“Huoni kuwa mbele yangu ni ndoto usiyokubalika?” Deus alisema akiwa amemkazia macho.
“Deus mpenzi wangu, najua hicho ndicho kinacho kutatiza, ni kweli uliniacha Dar lakini sikwenda Mwanza kama nilivyo kuahidi bali nilikufuata Italy.”
“Muongo!”
“Kweli mpenzi wangu, sema tu tumeomdoka ndege tofauti ya Italy mimi ndiye niliyewahi saa moja kabla yako niliondoka na ndege ya Fly Emirates.”
“Teddy mi si mtoto mdogo wa kudanganywa namna hiyo, Italy si sawa na kutoka Ubungo kwenda Kariakoo, kuna maandalizi yake hasa kutoka nje ya nchi kuna taratibu zake si za saa zaidi siku nzima hata siku mbili.”
“Ndiyo maana nikakueleza ni historia ndefu, moyo wangu haukukubali kukuamini moja kwa moja uende peke yako. Nilichowaza ndicho kilichotokea bila kufanya hivyo lazima ungekufa na mimi kusakwa mpaka kukamatwa kisha kuuawa kifo kibaya sana namjua vizuri sana Mose ana roho mbaya sana.”
“Mmh! Bado siamini.”
“Kweli Deus moyo wangu ulikataa kukuacha peke yako kwa vile namjua vizuri Mose. Nilijua kama ningekueleza tuongozane ungekataa hivyo nilifanya mipango yangu kwa siri bila wewe kujua ulipofika Italy nilikufuatilia kila hatua.”
“Uliwezaje kuniokoa katika kundi la vijana hatari kama wale?” Deus alikubaliana na hali halisi ilibidi awe mpole.
“Kwa vile niliwahi kufika Italy nilisubiri wageni watakaoingia na ndege uliyopanda na kuweza kukuona. Kabla sijaja niliwasiliana na mtu mmoja katika kampuni ya magari ya kukodi aniandalie gari atakalo liweka uwanja wa ndege na kunieleza lipo sehemu gani.
“Nilipofika nililikuta aliponielekeza likiwa katika hali nzuri, nililikagua na kukuta lipo kama nilivyoitaka. Huwezi kuamini nilikuwa tayari kwa lolote niliamini kama sikufa mimi basi Mose.”
“Na Rose?”
“Rose nilimuacha Hotelini.”
“Hoteli gani?”
“Liola Hotel (Aquino.”
“Muongo si ndiyo hoteli niliyopanga mimi?”
“Nilibahatisha kati ya hoteli mbili, niliamini utapumzika lakini sikukuamini bado nilikufuatilia kwa kukaa mapokezi. Ulipotoka nilikufuatilia mpaka
Piedimonte San Germano bila wewe kujua. Hata uliporudi bado nikuwa na wewe mpaka mlipokutana na Mose na kundi lake bila wewe kumjua Mose haraka .
“Ilionekana ulimtambua na baada ya kashikashi ndogo mliachana nao kisha niliona mkiwafuata hapo ndipo nilipojua shughuli imeanza. Mpaka unamteka Mose na kuondoka naye niliamini umefanikiwa lakini kuna mpambe mmoja aliona mchezo ule na kuwafuata wenzake ndani.
“Hapo ndipo nilipojua kazi imeiva, niliwaacha watangulie nami niliwafuata nyuma huku moyoni nikijiapia ama zao ama zangu. Nikiwa kwa mbali niliona mchezo mzima. Lazima nikusifu wewe ni mwanaume wa shoka mpaka kukushinda walitumia nguvu ya ziada.
“Sikuweza kuingilia mapigano yenu baada ya kuanguka moyo uliniuma sana mpaka machozi ya uchungu yalinitoka nikajua wamekumaliza. Walipo kuchukua na kuondoka na wewe sikujua wanakupeleka wapi, niliwafuatilia na kuwaona wanakupeleka ufukweni.
“ Kwa vile sehemu ilikuwa ya uwazi niliwaacha niwaone wanaenda wapi. Nilipowaona wamesimama niliamua kuwafuata kwa kuingia ndani ya maji.
“Namshukuru Mungu nilikuwa mtundu toka nilipoingia kwenye kazi hii ya hatari. Niliogelea hadi karibu yao na kutokeza kwa taratibu na kuwaona wanakumwagia maji uamke. Nilitumia nafasi ile kuwaua wote kwa risasi kisha nilitoka na kukuta hujafa ila una jeraha la risasi begani.
“Nilitumia gari lao kukubeba mpaka nilipopaki langu na kukuhamishia kwenye gari langu. Nilikupeleka kwa daktari wangu ambaye alikushughulikia na kusema huna tatizo kubwa zaidi ya jeraha tu. Nilitaka nisafiri naye mpaka Tanzania lakini alisema hakuna sababu ya yeye kusafiri na sisi kwa vile huna tatizo kubwa sana.
“Kwa vile nilijua kimenuka sikuwa na jinsi ilibidi nikodi ndege kwa gharama kubwa sana ili kuhakikisha usiku uleule tunaondoka Italy. Nilimfuata Rose hotelini na kuondoka mpaka uwanja wa ndege kisha tukaondoka. Hivi ninavyozungumza tuna saa sita tupo angani toka tutoke Italy.”
“Kwa hiyo Mose umemuua?”
“Yeye ndiye wa kwanza nilimpiga risasi tatu za kichwa kisha wenzake. Yaani hakuna siku niliyofurahi kama leo,” Teddy alisema kwa furaha huku akiubusu mkono wa Deus aliyekuwa bado amegandisha macho kwake.
Imauhakika gani kama Moses amekufa?”
“Baada ya kutoka ndani ya maji nilichukua bastora yake iliyokuwa na risasi kumi na kukisambaratisha kichwa chake kama atakuwa mazima tena basi nitajua ni mzimu.”
“Kwa hiyo kazi yangu imekuwa ya kitoto?” Deus aliuliza kiunyonge.
“Hapana mpenzi, kazi uliyofanya wewe ilikuwa kubwa sana mimi nimemalizia tu, nisingeweza kupambana na mijitu kama ile ambayo umeitoa jasho.”
“Unafikiri kwa nini Mose hakutaka kuniua?”
“Nina imani alitaka kujua umetoka wapi na nani kakutuma, anaamini mtu wa pale hawezi kumfanyia kitendo kama kile.”
“Baada ya kunihoji nini kingefuata?”
“Baada ya kupata ukweli wangekuua na kukutupia baharini.”
“Nashukuru sana Teddy kuyaokoa maisha yangu.”
“Nikushukuru wewe mpenzi kwa kuyatoa maisha yako kwa ajili yangu, Deus sijawahi kuona mwanaume mwenye mapenzi mazito na mimi kama wewe umekubali kuyatoa maisha yako kwa ajili yangu, umekubali kupoteza kazi yako kwa ajili yangu. Sina cha kukulipa zaidi ya kukuahidi upendo wa dhati na maisha mazuri mpaka kufa kwako, nife unizike ufe nikuzike.”
“Nashukuru kwa kulitambua hilo, ila nami nina kazi yangu.”
“Ipi?”
“Ya kumsaka Kilole na Kinape.”
“Nitakusaidia mpenzi wangu mpaka tuwatie mkononi na hakuna hukumu nyingine zaidi ya kifo.”
Ndege iliingia Dar es salaam Tanzania majira ya saa tano usiku, Deus alichukuliwa na kupelekwa kwenye moja ya jumba lililokuwa likitumiwa na kikundi cha wauza dawa za kulevya ambalo lilikuwa lipo mikononi mwa Teddy ambalo alilikimbia kumkimbia Mose lakini baada ya kumuua hakuwa na wasiwasi tena na lilikuwa kwenye hali nzuri.
Alimpigia simu daktari wao ambaye alifika kumhudumia Deus aliyekuwa na jeraha ambalo lililonekana lipo katika hali nzuri hakutakiwa kupewa huduma zaidi alitakiwa kupumzika.

Itaendelea
 
SEHEMU: 42
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500

ILIPISHIA:
Alimpigia simu daktari wao ambaye alifika kumhudumia Deus aliyekuwa na jeraha ambalo lililonekana lipo katika hali nzuri hakutakiwa kupewa huduma zaidi alitakiwa kupumzika.
SASA ENDELEA...
***
Siku ya pili Deus wakiwa sebuleni amejilaza kwenye sofa akiangalia tivii taarifa ya habari ya saa sita mchana. Deus alishtuka kumuona Kilole akiwa anatoka mahakamani chini ya ulinzi. Macho yalimtoka kumuona mbaya wake akiwa mikononi mwa chombo cha dola.
Alijikuta akinyanyuka na kukaa kitako huku macho yakemtoka pima, mtangazaji alisema kesi ile itaendelea tarehe iliyopangwa kufikishwa tena mahakamani kusikizwa kesi yake ya mauaji ya watu wa tatu. Mwanamke mmoja aliyekuwa akifanya kazi katika kampuni za kitalii mkoani Arusha aliyefahamika kwa jina la Happy pia mvulana mmoja aliyekuwa akifanya kazi za misheni tauni aliyefahamika kwa jina maarufu Anko JayJay pia mwanaume mwingine aliyefahamika kwa jina la Kinape ambaye inasadikiwa alikuwa mumewe wote aliwaua kwa risasi.
“Vipi mbona unaoneka umeshtuka na kukaa kitako wakati nimekueleza hutakiwi kuimana kwa mbele?” Teddy alimuuliza Deus baada ya kutoka chumbani na kumkuta amekaa kitako tofauti na alivyomuacha akiwa amejilaza.
“Aisee Kilole,” Deus alijibu kama anatoka usingizini.
“Kafanya nini?”
“Kumbe alikimbilia Mwanza, ameua.”
“Ameua?”
“Ndiyo, yupo mikononi mwa polisi ana kesi ya mauaji ya watu watatu.”
“Mauaji?”
“Ndiyo, ha..ha..rafu kuna jina sijaelewa vizuri sijui nimesikia vibaya.”
“Jina gani?”
“La Kinape.”
“Limefanya nini?”
“Ameuawa na Kilole.”
“Utani huo, si ndiye aliyeondoka naye kamuua kwa kosa gani?”
“Kwa kweli sijui kitu ila katika majina ya watu aliyowaua nimesikia jina kama hilo lazima atakuwa yeye kwa vile wamesema ni mume wake.”
“Kesi ipo wapi?”
“Mwanza.”
“Umesema imeahirishwa mpaka lini?” wakati huo Teddy alikuwa akimlaza Deus kwenye sofa taratibu asimtoneshe jeraha.
“Hata najua baada ya kuiona picha ya Kilole nimechanganyikiwa.”
“Kwa vile umejua yupo Mwanza kazi hiyo niachie mimi.”
“Hapana tusimuue nzi kwa nyundo wakati kajifia mwenyewe.”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Yule yupo chini ya mikono ya dola pia kesi yake ni nzito lazima atanyongwa kwa nini tutumie nguvu tukikosea mahesabu tuanze kukimbia upya.”
“Deus watu wale hawaaminiki anaweza kupona kimaajabu na kuanza kutusumbua. Nitamuua kwa mahesabu makali sana hakuna mtu atakayejua. Japokuwa najua kakuumiza lakini ndiye chanzo cha matatizo yote yako na yangu.”
“Mpenzi hebu kwanza tuiache mahakama ifanye kazi yake kisha tutajua tufanye nini?”
“Kwa hiyo tarehe ya kufikishwa mahakamani huijui?”
“Itabidi uulizie Mwanza.”
“Hakuna tatizo,” Teddy alisema huku akichukua simu na kupiga sehemu aliyokuwa amepanga.
“Haloo.”
“Haloo Juma mambo vipi?”
“Poa sister.”
“Eti Juma kuna mwanamke anashtakiwa kwa makosa ya mauaji hapo jijini?”
“Ndiyo dada, leo alipandishwa kuzimbani kwa mara ya kwanza.”
“Tarehe ya kurudi unaijua?”
“Mmh! Hebu subiri nikuulizie usikate simu.”
“Hakuta natatizo,” Teddy alisubiri baada ya muda sauti upande wa pili ilisema.
“Mpaka tarehe 22 ya mwezi ujao.”
“Asante.”
“Upo wapi dada?”
“Nipo Dar.”
“Utarudi lini?”
“Nitakujulisha.”
Teddy alikata simu na kumueleza Deus tarehe ya Kilole kupandishwa tena kizimbani.
“Nina imani mpaka siku hiyo nitakuwa nimepona.”
“Kwa hiyo tutakuwa mahakamani siku hiyo?”
“Itakuwa vizuri.”
***
Siku ya kupandishwa tena kizimbani Kilole ilifika, mahakama ilikuwa imejaa kusikiliza kesi ya mauaji yaliyotikisa jiji la Mwanza mwanamke mwenye vazi refu jeusi. Deus, Teddy na mtoto wao Rose walikuwa miongoni mwa watu waliokuwepo mahakamani pale.
Baada ya hakimu kuingia na kukaa kwenye kiti chake na watu wote waliokuwa wamesimama kuelezwa wakae chini mahakama ilianza. Kesi ilianza mara moja kwa kuitwa kesi ya kwanza ilikuwa ya uchomaji wa nyumba na kusababisha mauaji ya mtu mmoja na uhalibifu wa mali.
Mtuhumiwa alisomewa shtaka na kurudishwa rumande bila kujibu kitu. Kesi ya pili kutajwa ilikuwa ya Kilole. Kama kawaida alitoka rumande na kupandishwa kizimbani. Alipanda taratibu akiwa ameinama huku moyoni akijutia kitendo cha kuua mpenzi wake Kinape bila kukusudia.
Baada ya kupanda alisimama na kutulia kusubiri kusomewa mashtaka. Akiwa ameangalia chini kusubiri kusomewa mashtaka yake kwa mara ya pili, kwa vile hakutakiwa kujibu lolote mpaka upelelezi utakapokamilika alitulia kusubiri kusomewa ili arudishwe rumande.
Akiwa ameangalia chini alinyanyua macho yake taratibu na kuwaangalia watu waliokuwa mahakamani. Macho yake yalipogongana na Deus, alishtuka na kuyarudisha tena sura ilikuwa ileile ya Deus mtu anayejua amekwisha kufa.
Aliyatuliza macho yake huku mapigo ya moyo wakienda kwa kasi, alijiuliza anaota au ni kweli.
Akili yake anajua Deus aliisha kufa yule aliyesimama mbele yake ni mzimu wake au nani. Kingine kilichomchanganya zaidi kilikuwa mwanamke aliyekuwa amekaa naye ambaye alikuwa akimkisia ni mpenzi wa Deus, alikuwa pembeni yake na mtoto wake Rose.
Pale ndipo alipoamini yule ni Deus ambaye alidanganywa amekufa kumbe alikuwa hai. Hata alipoanza kusomewa mashtaka akili haikuwa pale yote ilikuwa kwa Deus na kujiuliza ni kweli au yupo ndotoni. Alijaribu kujifinya alihisi maumivu na kugundua si ndoto ni kitu cha kweli.
Moyoni alijiapiza kwa vile alijua kesi ile hawezi kupona lazima atanyongwa kutokana na ushahidi wote aliamini ile ndiyo nafasi ya pekee ya kutimiza azima yake ya kumuua Deus. Alimuangalia askari aliyekuwa pembeni yake ametulia akiangalia watu.
Alipoangalia kiunoni kwake aliiona bastora amekaa kihasarahasara. Alipiga hesabu zake na kuamini ataipata na kufanya mauaji ya mwisho mulemule mahakamani kabla ya hukumu yake ya kunyongwa. Baada hesabu zake kukamilika alichomoka kama mshale na kumpiga kikumbo askari mpaka chini na kuipokonya bastora iliyokuwa kiunoni.
Kwa wepesi wa ajabu aligeukia upande alipokuwa amekaa watu waliokuwa wamekaa watu sehemu yaliyokuwepo wabaya wake. Deus na Teddy kwa pamoja waliliona tukio lile na wote kulala chini, watu wengine nao wamelala chini kuhofia kupigwa risasi. Kuchanganyikana na watu ilimpa Kilole wakati mgumu kuwapiga risasi wabaya wake.
Kwa hasira alipiga risasi mfululiza eneo waliokuwepo na kuua watu ovyo na wengine kuwajeruhi. Askari aliyepigwa kikumbo na kunyang’wa bastora, alinyanyuka kishujaa baada ya Kilole kumpa mgongo. Alimvaa na kuanguka naye chini.
Kwa wepesi wake aligeuza batora na kumpiga yule askari kifuani.
Hali ya mahakamani ikawa tafrani kila mmoja alishikilia roho yake kutokana na milio ya risasi.
Teddy akiwa amejilaza alitoa bastora kwa siri na kumlenga Kilole sehemu ya kichwa ili ammalize kabisa. Wakati huo Deus alikuwa ameisha muona Teddy anataka kufanya nini, kabla hajafyatua alimsukuma kwa miguu na risasi aliyopiga Teddy ilimkosa Kilole na kwenda kupiga ukutani.
Wakati huo askari wa kikosi maalumu walikuwa amefika kwa vile Kilole alikuwa amepagawa askari mwenye shabaha alimpiga risasi ya bega aliloshika bastora na kuidondosha na kuwapa nafasi ya kumvamie. Kilole aliyekuwa akitokwa na damu begani huku akipiga kelele wamuue kabisa aliwekwa chini ya ulinzi mkali.
Askari walisaidia kuondoa maiti za watu watatu na askari mmoja na majeruhi zaidi ya ishirini. Mahakama haikuweza kuendelea ilibidi iahilishwe kutokana na tukio lile zito. Wakiwa nje ya mahakama baada ya kukamatwa Kilole na kuwekwa chini ya ulinzi mkali.
Teddy alimlaumu Deus kumkanyaga wakati alijua ile ndiyo ilikuwa nafasi ya kumuua mbaya wao bila tatizo.
“Deus umefanya nini?”
“Hapana, haikuwa na haja kulipa baya kwa baya.”
“Deusiiii! Angetuua huoni kama alitukusudia?”
“Ni kweli lakini bado siamini natakiwa kumhukumu kifo.”
“Kwa nini Deus?”
“Kesi aliyonayo bado ni hukumu nzito kumbuka kaua watu wengi na leo ameongeza kosa lingine la kuua watu wengine mahakamani.”
“Deus hayo hayaniingii akilini, tulikubaliana tumfanye nini?” Teddy alimuuliza huku machozi yakimtoka.
“Teddy unanipenda?” Deus alimuuliza akiwa akimkazia macho.
“Tena sana mpenzi wangu wewe kwangu ni kila kitu.”
“Basi nakuomba nisikilize mimi, tuachane na Kilole nina imani nisingefurahi kumuona anakufa mbele yangu. Sitakiwi kuwa na roho ya kisasi kwa vile Rose ni mwanangu mtoto wa Kilole.”
“Lakini si alikusudia kuua?”
“Ni kweli, tushukuru Mungu tumepona.”
*****
Kilole alipelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu ya jeraha la bega kisha hospitali ya wagonjwa wa akili ili kupimwa akili. Baada ya matibabu na vipimo vyote Kilole alikutwa akili yake ipo timamu hivyo alipandishwa tena kizimbani baada ya kupona jeraha katika ulinzi mkali. Kesi yake haikuchelewa alihukumiwa jela maisha na kazi ngumu.
Teddy alioana na Deus na kuwa mke na mume Rose alilelewa na Teddy ambaye tayari aliishajua ndiye mama yake wa kumzaa huku akisubiri wa kwake kuongeza familia. Waliamua kuhamishia maisha yao Mwanza na kufungua miradi na Teddy kuachana na biashara ya dawa za kulevya.
MWISHO
 
SEHEMU: 42
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500

ILIPISHIA:
Alimpigia simu daktari wao ambaye alifika kumhudumia Deus aliyekuwa na jeraha ambalo lililonekana lipo katika hali nzuri hakutakiwa kupewa huduma zaidi alitakiwa kupumzika.
SASA ENDELEA...
***
Siku ya pili Deus wakiwa sebuleni amejilaza kwenye sofa akiangalia tivii taarifa ya habari ya saa sita mchana. Deus alishtuka kumuona Kilole akiwa anatoka mahakamani chini ya ulinzi. Macho yalimtoka kumuona mbaya wake akiwa mikononi mwa chombo cha dola.
Alijikuta akinyanyuka na kukaa kitako huku macho yakemtoka pima, mtangazaji alisema kesi ile itaendelea tarehe iliyopangwa kufikishwa tena mahakamani kusikizwa kesi yake ya mauaji ya watu wa tatu. Mwanamke mmoja aliyekuwa akifanya kazi katika kampuni za kitalii mkoani Arusha aliyefahamika kwa jina la Happy pia mvulana mmoja aliyekuwa akifanya kazi za misheni tauni aliyefahamika kwa jina maarufu Anko JayJay pia mwanaume mwingine aliyefahamika kwa jina la Kinape ambaye inasadikiwa alikuwa mumewe wote aliwaua kwa risasi.
“Vipi mbona unaoneka umeshtuka na kukaa kitako wakati nimekueleza hutakiwi kuimana kwa mbele?” Teddy alimuuliza Deus baada ya kutoka chumbani na kumkuta amekaa kitako tofauti na alivyomuacha akiwa amejilaza.
“Aisee Kilole,” Deus alijibu kama anatoka usingizini.
“Kafanya nini?”
“Kumbe alikimbilia Mwanza, ameua.”
“Ameua?”
“Ndiyo, yupo mikononi mwa polisi ana kesi ya mauaji ya watu watatu.”
“Mauaji?”
“Ndiyo, ha..ha..rafu kuna jina sijaelewa vizuri sijui nimesikia vibaya.”
“Jina gani?”
“La Kinape.”
“Limefanya nini?”
“Ameuawa na Kilole.”
“Utani huo, si ndiye aliyeondoka naye kamuua kwa kosa gani?”
“Kwa kweli sijui kitu ila katika majina ya watu aliyowaua nimesikia jina kama hilo lazima atakuwa yeye kwa vile wamesema ni mume wake.”
“Kesi ipo wapi?”
“Mwanza.”
“Umesema imeahirishwa mpaka lini?” wakati huo Teddy alikuwa akimlaza Deus kwenye sofa taratibu asimtoneshe jeraha.
“Hata najua baada ya kuiona picha ya Kilole nimechanganyikiwa.”
“Kwa vile umejua yupo Mwanza kazi hiyo niachie mimi.”
“Hapana tusimuue nzi kwa nyundo wakati kajifia mwenyewe.”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Yule yupo chini ya mikono ya dola pia kesi yake ni nzito lazima atanyongwa kwa nini tutumie nguvu tukikosea mahesabu tuanze kukimbia upya.”
“Deus watu wale hawaaminiki anaweza kupona kimaajabu na kuanza kutusumbua. Nitamuua kwa mahesabu makali sana hakuna mtu atakayejua. Japokuwa najua kakuumiza lakini ndiye chanzo cha matatizo yote yako na yangu.”
“Mpenzi hebu kwanza tuiache mahakama ifanye kazi yake kisha tutajua tufanye nini?”
“Kwa hiyo tarehe ya kufikishwa mahakamani huijui?”
“Itabidi uulizie Mwanza.”
“Hakuna tatizo,” Teddy alisema huku akichukua simu na kupiga sehemu aliyokuwa amepanga.
“Haloo.”
“Haloo Juma mambo vipi?”
“Poa sister.”
“Eti Juma kuna mwanamke anashtakiwa kwa makosa ya mauaji hapo jijini?”
“Ndiyo dada, leo alipandishwa kuzimbani kwa mara ya kwanza.”
“Tarehe ya kurudi unaijua?”
“Mmh! Hebu subiri nikuulizie usikate simu.”
“Hakuta natatizo,” Teddy alisubiri baada ya muda sauti upande wa pili ilisema.
“Mpaka tarehe 22 ya mwezi ujao.”
“Asante.”
“Upo wapi dada?”
“Nipo Dar.”
“Utarudi lini?”
“Nitakujulisha.”
Teddy alikata simu na kumueleza Deus tarehe ya Kilole kupandishwa tena kizimbani.
“Nina imani mpaka siku hiyo nitakuwa nimepona.”
“Kwa hiyo tutakuwa mahakamani siku hiyo?”
“Itakuwa vizuri.”
***
Siku ya kupandishwa tena kizimbani Kilole ilifika, mahakama ilikuwa imejaa kusikiliza kesi ya mauaji yaliyotikisa jiji la Mwanza mwanamke mwenye vazi refu jeusi. Deus, Teddy na mtoto wao Rose walikuwa miongoni mwa watu waliokuwepo mahakamani pale.
Baada ya hakimu kuingia na kukaa kwenye kiti chake na watu wote waliokuwa wamesimama kuelezwa wakae chini mahakama ilianza. Kesi ilianza mara moja kwa kuitwa kesi ya kwanza ilikuwa ya uchomaji wa nyumba na kusababisha mauaji ya mtu mmoja na uhalibifu wa mali.
Mtuhumiwa alisomewa shtaka na kurudishwa rumande bila kujibu kitu. Kesi ya pili kutajwa ilikuwa ya Kilole. Kama kawaida alitoka rumande na kupandishwa kizimbani. Alipanda taratibu akiwa ameinama huku moyoni akijutia kitendo cha kuua mpenzi wake Kinape bila kukusudia.
Baada ya kupanda alisimama na kutulia kusubiri kusomewa mashtaka. Akiwa ameangalia chini kusubiri kusomewa mashtaka yake kwa mara ya pili, kwa vile hakutakiwa kujibu lolote mpaka upelelezi utakapokamilika alitulia kusubiri kusomewa ili arudishwe rumande.
Akiwa ameangalia chini alinyanyua macho yake taratibu na kuwaangalia watu waliokuwa mahakamani. Macho yake yalipogongana na Deus, alishtuka na kuyarudisha tena sura ilikuwa ileile ya Deus mtu anayejua amekwisha kufa.
Aliyatuliza macho yake huku mapigo ya moyo wakienda kwa kasi, alijiuliza anaota au ni kweli.
Akili yake anajua Deus aliisha kufa yule aliyesimama mbele yake ni mzimu wake au nani. Kingine kilichomchanganya zaidi kilikuwa mwanamke aliyekuwa amekaa naye ambaye alikuwa akimkisia ni mpenzi wa Deus, alikuwa pembeni yake na mtoto wake Rose.
Pale ndipo alipoamini yule ni Deus ambaye alidanganywa amekufa kumbe alikuwa hai. Hata alipoanza kusomewa mashtaka akili haikuwa pale yote ilikuwa kwa Deus na kujiuliza ni kweli au yupo ndotoni. Alijaribu kujifinya alihisi maumivu na kugundua si ndoto ni kitu cha kweli.
Moyoni alijiapiza kwa vile alijua kesi ile hawezi kupona lazima atanyongwa kutokana na ushahidi wote aliamini ile ndiyo nafasi ya pekee ya kutimiza azima yake ya kumuua Deus. Alimuangalia askari aliyekuwa pembeni yake ametulia akiangalia watu.
Alipoangalia kiunoni kwake aliiona bastora amekaa kihasarahasara. Alipiga hesabu zake na kuamini ataipata na kufanya mauaji ya mwisho mulemule mahakamani kabla ya hukumu yake ya kunyongwa. Baada hesabu zake kukamilika alichomoka kama mshale na kumpiga kikumbo askari mpaka chini na kuipokonya bastora iliyokuwa kiunoni.
Kwa wepesi wa ajabu aligeukia upande alipokuwa amekaa watu waliokuwa wamekaa watu sehemu yaliyokuwepo wabaya wake. Deus na Teddy kwa pamoja waliliona tukio lile na wote kulala chini, watu wengine nao wamelala chini kuhofia kupigwa risasi. Kuchanganyikana na watu ilimpa Kilole wakati mgumu kuwapiga risasi wabaya wake.
Kwa hasira alipiga risasi mfululiza eneo waliokuwepo na kuua watu ovyo na wengine kuwajeruhi. Askari aliyepigwa kikumbo na kunyang’wa bastora, alinyanyuka kishujaa baada ya Kilole kumpa mgongo. Alimvaa na kuanguka naye chini.
Kwa wepesi wake aligeuza batora na kumpiga yule askari kifuani.
Hali ya mahakamani ikawa tafrani kila mmoja alishikilia roho yake kutokana na milio ya risasi.
Teddy akiwa amejilaza alitoa bastora kwa siri na kumlenga Kilole sehemu ya kichwa ili ammalize kabisa. Wakati huo Deus alikuwa ameisha muona Teddy anataka kufanya nini, kabla hajafyatua alimsukuma kwa miguu na risasi aliyopiga Teddy ilimkosa Kilole na kwenda kupiga ukutani.
Wakati huo askari wa kikosi maalumu walikuwa amefika kwa vile Kilole alikuwa amepagawa askari mwenye shabaha alimpiga risasi ya bega aliloshika bastora na kuidondosha na kuwapa nafasi ya kumvamie. Kilole aliyekuwa akitokwa na damu begani huku akipiga kelele wamuue kabisa aliwekwa chini ya ulinzi mkali.
Askari walisaidia kuondoa maiti za watu watatu na askari mmoja na majeruhi zaidi ya ishirini. Mahakama haikuweza kuendelea ilibidi iahilishwe kutokana na tukio lile zito. Wakiwa nje ya mahakama baada ya kukamatwa Kilole na kuwekwa chini ya ulinzi mkali.
Teddy alimlaumu Deus kumkanyaga wakati alijua ile ndiyo ilikuwa nafasi ya kumuua mbaya wao bila tatizo.
“Deus umefanya nini?”
“Hapana, haikuwa na haja kulipa baya kwa baya.”
“Deusiiii! Angetuua huoni kama alitukusudia?”
“Ni kweli lakini bado siamini natakiwa kumhukumu kifo.”
“Kwa nini Deus?”
“Kesi aliyonayo bado ni hukumu nzito kumbuka kaua watu wengi na leo ameongeza kosa lingine la kuua watu wengine mahakamani.”
“Deus hayo hayaniingii akilini, tulikubaliana tumfanye nini?” Teddy alimuuliza huku machozi yakimtoka.
“Teddy unanipenda?” Deus alimuuliza akiwa akimkazia macho.
“Tena sana mpenzi wangu wewe kwangu ni kila kitu.”
“Basi nakuomba nisikilize mimi, tuachane na Kilole nina imani nisingefurahi kumuona anakufa mbele yangu. Sitakiwi kuwa na roho ya kisasi kwa vile Rose ni mwanangu mtoto wa Kilole.”
“Lakini si alikusudia kuua?”
“Ni kweli, tushukuru Mungu tumepona.”
*****
Kilole alipelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu ya jeraha la bega kisha hospitali ya wagonjwa wa akili ili kupimwa akili. Baada ya matibabu na vipimo vyote Kilole alikutwa akili yake ipo timamu hivyo alipandishwa tena kizimbani baada ya kupona jeraha katika ulinzi mkali. Kesi yake haikuchelewa alihukumiwa jela maisha na kazi ngumu.
Teddy alioana na Deus na kuwa mke na mume Rose alilelewa na Teddy ambaye tayari aliishajua ndiye mama yake wa kumzaa huku akisubiri wa kwake kuongeza familia. Waliamua kuhamishia maisha yao Mwanza na kufungua miradi na Teddy kuachana na biashara ya dawa za kulevya.
MWISHO

Safi sana...

Tamaa mbele umautu nyuma...

Kilole kapata kile anachastahilli, mtaka viwili vyote humponyoka... kinape nae kachezea maisha yake mwenyewe kwa kumuendekeza mwanamke... Happy kauliwa bila ya kua na hatia yoyote...

Deus nae alitakiwa afungiliwe mbali kwa kula rushwa za wauza madawa ya kulevya ila Mungu kawa upande wake...

Teddy nae ni vizuri sana alivyoamuma kuacha na biashara ya madawa ya kulvya...

Chapter Closed...


Cc: mahondaw
 
Back
Top Bottom