Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,662
- Thread starter
- #41
ILIPOISHIA:
Baada ya kutoka kwenye kikao na mkuu wake wa kazi, Fukwa aliwaita vijana wake wa kikosi maalumu na kutoa amri ya kijeshi.
“Nina imani mmemsikia mkuu, kwa hiyo sitaki kusikia tena muuaji bado anatamba, mpaka kesho jioni nataka tuwe tumemkamata. Sijui mtamkamata vipi, hiyo si juu yangu bali kusikia yupo mikononi mwa polisi, sawa?” Mkuu wa upelelezi Fukwa.
“Sawa mkuu,” vijana aliitikia kikakamavu.
SASA ENDELEA...
“Nina imani mmepata pa kuanzia?”
“Ndiyo mkuu.”
“Haya tawanyika mkimkosa na ninyi msirudi hapa.”
Ilikuwa kauli iliyowapa wakati mgumu kikosi cha kazi kinachodili na mtukio kama yale. Walikubaliana kutawanyika huku kila mmoja akijipa jukumu lake ili wakikutana wajue wamefika wapi.
***
Kachero Mzengwa alitembea taratibu maeneo ya Mirongo kwa kupita katika vijiwe vya Anko Jay Jay. Kwa vile alikuwa katika vazi la kawaida alifika kwenye uwanja wa mpira wa shule ya Mirongo na kuwakuta vijana wakicheza kamali huku wakivuta bangi hakufanya kitu na yeye alijichanganya.
Na yeye aligongea sigara ya kawaida na kuvuta huku akifuatilia kamari.
Mara alisikia jamaa mmoja akisema:
“Washikaji tumempoteza mwanetu Jay kama utani,” jamaa aliyekuwa akivuta bangi alisema.
“Mmh! Unajua naye alizidi kila kazi alifanya unakumbuka Tom nilimweleza Jay kwa kazi yake ya ukuwadi ipo siku atakufa. Jamani Jay kufa kwa risasi kama siyo kumkuwadia mume wa mtu ni nini?” mwingine aliongezea huku akilamba lizila unyonge bangi.
“Na kweli jamaa alizidi, mi nilijua mwisho wake mbaya.”
“Tena Side bahati yake alikwenda bushi la sivyo na yeye angekufa.”
Wakiwa katikati ya mazungumzo alitokea jamaa mmoja na wote waligeuka na aliyekuwa akinyonga alisema:
“Sideeee wapi Jay, jichanganye na wewe utamfuata mwenzako, fanya kazi zote lakini ya ukuwadi ni kifo.”
“Mwambie, hivi wewe mkeo akikuwadiwa utajisikiaje?”
“Jamani mbona umekosa ya kuzungumza, naona kijiwe hakinifai nikajichanganye na masela wa Lake sekondary,” Side alisema huku akiondoka taratibu na kuwaacha jamaa wakiendelea kumpaka mbovu.
“Side kuondoka siyo dawa, kama utafanya kazi ya rafiki yako nawe si muda mrefu utamfuata.”
“Ninyi mnajuaje kama kauawa na mke wa mtu?” Side alisimama na kuuliza.
“Side hata kama mimi siyo mpelelezi lakini ukiangalia mauaji yalivyotokea picha nzima inaonesha kauawa mwanamke aliyekuwa nyumba ya wageni. Hata siku mbili hazijapita kauawa Jay tena na mtu wa aina moja mwanamke anayevaa vazi refu la kumziba mwili na uso.
“Huyo mwanamke lazima amegundua yule mwanamke aliyemuua hotelini anatembea na mumewe na mtengeneza mipango ni Jay na yeye kumuua. Sasa nawe jipendekeze moto ukuwakie sisi siyo wajinga kukomaa na kazi za upusha, tunapenda maisha mazuri lakini mwisho wake kufa kama jambazi.” Jamaa mmoja aliyekuwa akisema kwa sauti nzito huku akinyonga ganja.
Machero Mzengwa alijikuta akipata kitu kipya ambacho hakuwahi kukiwaza, alichosema jamaa aliyekuwa akinyonga ganja. Japo alifurahi kumuona Side mtu muhimu kwake lakini pia alipata mwanga mwingine ambao aliamini utamsaidia atakapozungumza na Side. Alimpigia simu dereva wa defenda ili apate usafiri wa kuondoka na Side.
“Poa, lakini mnanionea bure,” Side alizidi kujitetea.
“Tukuonee vipi ikiwa wewe na Jay mlikuwa mnatutenga na kutuona sisi sio kwa vile mnakamata fedha ya ukuwadi.”
Mara ghafla kulizuka ugomvi baada kudhulumiana kwenye kamali, ile ilimpa nafasi kachero kumfuata Side aliyekuwa amesimama pembeni na kumsalimia.
“Side vipi?”
‘Poa mkubwa.”
“Sasa Side tuzungumze kidogo.”
Walisogea pembeni kidogo ili wazungumze, ghafla lilitokea defenda na kuwafanya waliokuwa wakicheza kamali na kuvuta bangi kukimbia. Side naye alitaka kukimbia lakini alishikwa na kachero Mzengwa na kushindwa kukimbia.
“Vipi Brother?” alilalamika ili aachiwe.
“Tulia,” Kachero Mzengwa alisema kwa sauti ya amri.
Baada ya gari kusimama Side alipakiwa na gari lililokwenda moja kwa moja hadi kituo cha makosa ya jinai. Waliteremka na kuingia naye kwenye chumba cha mahojiano. Kwa vile Side alikuwa na wasiwasi sana kachero Mzengwa alimuagizia soda ya baridi kwanza. Baada ya kutulia alianza kumuhoji.
“Side ondoa wasiwasi hutafanywa kosa lolote ila nahitaji msaada wako,” Mzengwa alianza kwa kumtoa wasiwasi.
“Msaada gani?”
“Anko Jay Jay alikuwa nani yako?”
“Rafiki yangu sana.”
“Kabla ya wewe kwenda shamba alikuwa na dili gani?”
“Mmh! Nakumbuka alipewa kazi na dada mmoja ya kumfuatilia mume wake.”
“Mume wake alikuwa na tatizo gani?”
“Alikuwa na wasiwasi anatembea na mwanamke mwingine.”
“Mmh! Baada ya hapo nini kiliendelea?”
“Aliniambia amegundua kweli yule mwanaume alikuwa na mwanamke kampangia hotelini.”
“Baada ya hapo?”
“Alipomaliza kazi yake alilipwa chake na mimi kesho yake nilisafiri, nikiwa bushi nilipopata taarifa za kushtusha kuwa mchizi wangu Jay ameuawa,” Side alisema kwa uchungu.
“Unakumbuka huyo mwanamke alikuwa amepangiwa hoteli gani?”
“Gorden Crest.”
“Na hiyo mwanamke unamjua?”
“Kwa kweli sikuwahi kumuona.”
“Sehemu anapokaa unapajua?”
“Ni Isamilo lakini nyumba siikumbuki vizuri kwa vile tulikwenda usiku ila nakumbuka nilimsubiri sehemu na kuingia kwenye nyumba yenye geti.”
“Hukumbuki hata kidogo?”
“Nikifika nitaijua japo sikuangalia vizuri siku tuliyokwenda.”
“Nafikiri twende muda huu ukatuoneshe hiyo nyumba.”
“Sawa.”
Walikubaliana kwenda kuitafuta nyumba ya mwanamke aliyempa kazi Anko Jay Jay ambayo waliamini anaweza kuhusika kwa asilimia kubwa katika mauaji yale.
*****
Majira ya saa kumi na mbili za jioni Land Cruser ilitembea taratibu katika mitaa ya Isamilo. Walilipaki sehemu na kuteremka kisha kutembea taratibu kufuata mtaa ambao Side alikuja siku moja na marehemu Anko Jay Jay kufuata malipo ya kazi aliyopewa ya kumchunguza mume wa mtu.
Sehemu aliposimama kumsubiri ilimchanganya kidogo kutokana na nyumba zile kufanana kidogo katika nyumba aliyoingia Jay.
“Vipi umeikumbuka?” kachero Mzengwa alimuuliza.
“Kati ya nyumba hizi mbali moja wapo, sikumbuki nilisimama wapi kwa vile ilikuwa usiku.”
“Joe unasemaje?” Mzegwa alimuuliza mwenzake.
Kabla hajamjibu lilikuja gari na kusimama kwenye nyumba moja kati ya zile mbili na kupiga honi. Baada ya muda alitoka mama mmoja mwenye mwili mkubwa kufungua geti huku akisema:
“Mume wangu leo nimekuwa mlinzi.”
“Mlinzi yupo wapi?”
“Nimemtuma mara moja.”
Baada ya kufungua geti gari lilingia ndani na kulifunga, baada ya kufungwa geti Side alisema:
“Itakuwa nyumba hii.” aliionesha nyumba jirani na gari lilipoingia gari.
“Kwa nini?”
“Jay alinieleza yule mwanamke anaishi na mume na mtoto mchanga hii inaonekana wenye nyumba ni watu wazima pia nyumba ile alinieleza haina mlinzi.”
“Una uhakika?”
“Ndiyo ni nyumba hii.”
“Basi tuondokeni tukajiandae kuja usiku nina imani kazi itakuwa si ngumu sana.”
“Na huyu?” Joe aliuliza kuhusu Side.
“Huyu tutakuwa naye mpaka zoezi la leo usiku liishe kisha atarudi kwake.”
Walirudi kwenye gari lao na kurudi ofisini kwa ajili ya operesheni ya kumtia mikono Kilole ambaye waliamini ndiye aliyekuwa akijua kila kitu juu ya kifo cha msichana aliyeuawa Gorden Crest na Anko Jay Jay japokuwa hawakujua muuaji ni nani, lakini waliamini kumtia mikononi yule mwanamke angewasaidia upelezi wao kwa kiasi kikubwa.
*****
Deus baada ya kuikagua siraha yake alisogea mpaka karibu ya dereva teksi Abdul aliyekuwa amezama kwenye penzi na mwanamke wa usiku.
“Mzee vipi?” Deus alimshtua Abdul.
“Poa mkuu.”
“Naona upo kazini?”
“Hapana nimemwita huyu baada ya kuona maboweka.”
“Njoo basi nje mara moja.”
Walitoka mpaka nje pamoja hadi ya cassino.
“Vipi mzee?” Abdul alimuuliza Deus akimtazama usoni.
“Mose unafahamiana naye sana?”
“Kiasi ila tunaelewana sana.”
“Kuna kazi nataka kukupa ukiifanya vizuri nitakupa fedha nzuri.”
“Kazi gani mkubwa?”
“Nina shida Mose ila nataka ukamtoe bila wapambe wake kuja nina mazungumzo naye.”
“Hilo mbona dogo.”
“Lakini usimwambie kama kuna mtu anamwita.”
“Hiyo kazi niachie mimi, akili yangu ukisikia fedha huwa haishindwi na kitu chochote hata kumfukua marehemu.”
“Basi nifanyie hiyo kazi mara moja, ila ukija hakikisha wewe unasimama huku na yeye huku.”
“Hakuna tatizo bosi wangu.”
Abdul aliingia ndani mara moja hadi kwenye meza za kamali na kumkuta Mose bado kashikilia bunda la dola akisubiri kuingia kucheza kamali.
“Mose,” Abdul alimwita alipomkaribia.
“Unasemaje Brother Abby?”
“Samahani nakuomba mara moja.”
“Una shiga gani brother? Zungumza nakusikiliza.”
“Naomba tutoke nje mara moja.”
“Si unajua muda wangu wa kuingia kwenye gemu umekaribia, jana walinila leo nina usongo nao,” Mose alijitetea ili asiende mbali.
“Dakika tano tu, waachie washikaji wakushikie unarudi sasa hivi.”
“Paul shika mkwanja huu narudi.”
“Poa mkubwa.”
Walitoka hadi sehemu ya kupakia magari, Deus alipomuona anakuja alizunguka nyuma ya gari. Walichomoa bastora tayari kwa tukio, walipofika walisimama Mose akiwa amempa mgongo Deus kama alivyomuelekeza Abdul. Aliiweka bastora yake tayari na kumsogelea taratibu hadi waliposimama na kumwekea bastora Mose kisogoni huku akisema kwa sauti ya chini yenye amri.
“Fungua mlango wa mbele wa gari na uingie ndani bila kuleta ujanja la sivyo nitakufumua ubongo.”
“Mheshimiwa vipi?” Abdul alishtuka kuona Deus ameshikilia bastora.
“Sitaki swali nawe ingia upande wako mara moja.”
Abdul hakutaka kubishana alizunguka upande wake na kuingia ndani na Mose naye alifanya kama alivyoelekezwa. Deus aliingia mlango wa nyuma na kusema kwa sauti ya amri.
“Elekea baharini mara moja.”
“Sawa,” Abdul alijibu huku akiwasha gari na kuondoka.
“Kaka mkubwa nimefanya nini?” Mose aliuliza kwa sauti ya upole.
“Utajua muda si mrefu.”
Gari lilitoka hoteli ya Piedimonte San Germano na kuingia barabara kubwa na kuelekea upande wa baharini.
“Abdul nataka gari likimbie kama linapaa,” Deus alitoa amri ya kijeshi.
“Hakuna tatizo mkubwa.”
Abdul alibadili gia na kukanyaga mafuta na kulifanya gari liondoke kwa mwendo wa kasi. Kabla ya kulivuka daraja refu gari la kina Mose lilikuja nyuma kwa kasi na kuwavuka na kusimama mbele yao kwa ghafla na kumfanya Abdul kufunga bleki kwa nguvu zote. Lakini gari lao liliseleleka na kwenda kuligonga gari la kina Mose wakati huo wapambe wa Mose walikuwa wametoka ndani ya gari na bastora mkononi tayari kumsaidia bosi wao.
Deus akili ilimchemka na kuona kafanya makosa ya kutoka naye mbali sana, lakini aliamini atapambana nao mpaka tone la mwisho la damu yake japokuwa alikuwa peke yake akipambana na kundi la zaidi ya watu sita wote wana siraha.
Deus naye kwa wepesi wake alitoka nje na kujificha nyuma ya teksi ya Abdul ambaye alikuwa hajui afanye nini. Wapambe walikuwa amekwisha ivamia gari na kumtoa bosi wao. Jamaa aliyetupwa juu ya gari na Abdul naye aliona ile ndiyo sehemu ya kulipa kisasi kwa Abdul.
Bila kuuliza alimjaza Abdul risasi za kichwa mpaka alipoamini amekata roho na kichwa hakitamaniki.
“Jamani mbaya wetu asikimbie,” Mose alisema kwa sauti ya juu.
“Hatoki lazima tumtie mikononi.”
“Nataka tusimuue tumshike akiwa hai,” Mose alitoa amri wa wapambe wake.
“Huyu hatoki hapa.” Ilikuwa kauli ya kumuunga mkono Mose ambaye alikuwa na hasira na Deus.
Deus aliinama kwa chini ili asionekane, wakati huo risasi zilikuwa zikirindima sehemu aliyojificha naye alijitahidi kujihami kwa kurudisha mashambulizi. Risasi ya bega iliyompata Deus ilimfanya adondoshe bastora chini. Alipotaka kuiokota kwa mkono cha kushoto alikuwa amechelewa teke zito lilitua usoni kwake na kumrudisha nyuma.
Itaendelea
Baada ya kutoka kwenye kikao na mkuu wake wa kazi, Fukwa aliwaita vijana wake wa kikosi maalumu na kutoa amri ya kijeshi.
“Nina imani mmemsikia mkuu, kwa hiyo sitaki kusikia tena muuaji bado anatamba, mpaka kesho jioni nataka tuwe tumemkamata. Sijui mtamkamata vipi, hiyo si juu yangu bali kusikia yupo mikononi mwa polisi, sawa?” Mkuu wa upelelezi Fukwa.
“Sawa mkuu,” vijana aliitikia kikakamavu.
SASA ENDELEA...
“Nina imani mmepata pa kuanzia?”
“Ndiyo mkuu.”
“Haya tawanyika mkimkosa na ninyi msirudi hapa.”
Ilikuwa kauli iliyowapa wakati mgumu kikosi cha kazi kinachodili na mtukio kama yale. Walikubaliana kutawanyika huku kila mmoja akijipa jukumu lake ili wakikutana wajue wamefika wapi.
***
Kachero Mzengwa alitembea taratibu maeneo ya Mirongo kwa kupita katika vijiwe vya Anko Jay Jay. Kwa vile alikuwa katika vazi la kawaida alifika kwenye uwanja wa mpira wa shule ya Mirongo na kuwakuta vijana wakicheza kamali huku wakivuta bangi hakufanya kitu na yeye alijichanganya.
Na yeye aligongea sigara ya kawaida na kuvuta huku akifuatilia kamari.
Mara alisikia jamaa mmoja akisema:
“Washikaji tumempoteza mwanetu Jay kama utani,” jamaa aliyekuwa akivuta bangi alisema.
“Mmh! Unajua naye alizidi kila kazi alifanya unakumbuka Tom nilimweleza Jay kwa kazi yake ya ukuwadi ipo siku atakufa. Jamani Jay kufa kwa risasi kama siyo kumkuwadia mume wa mtu ni nini?” mwingine aliongezea huku akilamba lizila unyonge bangi.
“Na kweli jamaa alizidi, mi nilijua mwisho wake mbaya.”
“Tena Side bahati yake alikwenda bushi la sivyo na yeye angekufa.”
Wakiwa katikati ya mazungumzo alitokea jamaa mmoja na wote waligeuka na aliyekuwa akinyonga alisema:
“Sideeee wapi Jay, jichanganye na wewe utamfuata mwenzako, fanya kazi zote lakini ya ukuwadi ni kifo.”
“Mwambie, hivi wewe mkeo akikuwadiwa utajisikiaje?”
“Jamani mbona umekosa ya kuzungumza, naona kijiwe hakinifai nikajichanganye na masela wa Lake sekondary,” Side alisema huku akiondoka taratibu na kuwaacha jamaa wakiendelea kumpaka mbovu.
“Side kuondoka siyo dawa, kama utafanya kazi ya rafiki yako nawe si muda mrefu utamfuata.”
“Ninyi mnajuaje kama kauawa na mke wa mtu?” Side alisimama na kuuliza.
“Side hata kama mimi siyo mpelelezi lakini ukiangalia mauaji yalivyotokea picha nzima inaonesha kauawa mwanamke aliyekuwa nyumba ya wageni. Hata siku mbili hazijapita kauawa Jay tena na mtu wa aina moja mwanamke anayevaa vazi refu la kumziba mwili na uso.
“Huyo mwanamke lazima amegundua yule mwanamke aliyemuua hotelini anatembea na mumewe na mtengeneza mipango ni Jay na yeye kumuua. Sasa nawe jipendekeze moto ukuwakie sisi siyo wajinga kukomaa na kazi za upusha, tunapenda maisha mazuri lakini mwisho wake kufa kama jambazi.” Jamaa mmoja aliyekuwa akisema kwa sauti nzito huku akinyonga ganja.
Machero Mzengwa alijikuta akipata kitu kipya ambacho hakuwahi kukiwaza, alichosema jamaa aliyekuwa akinyonga ganja. Japo alifurahi kumuona Side mtu muhimu kwake lakini pia alipata mwanga mwingine ambao aliamini utamsaidia atakapozungumza na Side. Alimpigia simu dereva wa defenda ili apate usafiri wa kuondoka na Side.
“Poa, lakini mnanionea bure,” Side alizidi kujitetea.
“Tukuonee vipi ikiwa wewe na Jay mlikuwa mnatutenga na kutuona sisi sio kwa vile mnakamata fedha ya ukuwadi.”
Mara ghafla kulizuka ugomvi baada kudhulumiana kwenye kamali, ile ilimpa nafasi kachero kumfuata Side aliyekuwa amesimama pembeni na kumsalimia.
“Side vipi?”
‘Poa mkubwa.”
“Sasa Side tuzungumze kidogo.”
Walisogea pembeni kidogo ili wazungumze, ghafla lilitokea defenda na kuwafanya waliokuwa wakicheza kamali na kuvuta bangi kukimbia. Side naye alitaka kukimbia lakini alishikwa na kachero Mzengwa na kushindwa kukimbia.
“Vipi Brother?” alilalamika ili aachiwe.
“Tulia,” Kachero Mzengwa alisema kwa sauti ya amri.
Baada ya gari kusimama Side alipakiwa na gari lililokwenda moja kwa moja hadi kituo cha makosa ya jinai. Waliteremka na kuingia naye kwenye chumba cha mahojiano. Kwa vile Side alikuwa na wasiwasi sana kachero Mzengwa alimuagizia soda ya baridi kwanza. Baada ya kutulia alianza kumuhoji.
“Side ondoa wasiwasi hutafanywa kosa lolote ila nahitaji msaada wako,” Mzengwa alianza kwa kumtoa wasiwasi.
“Msaada gani?”
“Anko Jay Jay alikuwa nani yako?”
“Rafiki yangu sana.”
“Kabla ya wewe kwenda shamba alikuwa na dili gani?”
“Mmh! Nakumbuka alipewa kazi na dada mmoja ya kumfuatilia mume wake.”
“Mume wake alikuwa na tatizo gani?”
“Alikuwa na wasiwasi anatembea na mwanamke mwingine.”
“Mmh! Baada ya hapo nini kiliendelea?”
“Aliniambia amegundua kweli yule mwanaume alikuwa na mwanamke kampangia hotelini.”
“Baada ya hapo?”
“Alipomaliza kazi yake alilipwa chake na mimi kesho yake nilisafiri, nikiwa bushi nilipopata taarifa za kushtusha kuwa mchizi wangu Jay ameuawa,” Side alisema kwa uchungu.
“Unakumbuka huyo mwanamke alikuwa amepangiwa hoteli gani?”
“Gorden Crest.”
“Na hiyo mwanamke unamjua?”
“Kwa kweli sikuwahi kumuona.”
“Sehemu anapokaa unapajua?”
“Ni Isamilo lakini nyumba siikumbuki vizuri kwa vile tulikwenda usiku ila nakumbuka nilimsubiri sehemu na kuingia kwenye nyumba yenye geti.”
“Hukumbuki hata kidogo?”
“Nikifika nitaijua japo sikuangalia vizuri siku tuliyokwenda.”
“Nafikiri twende muda huu ukatuoneshe hiyo nyumba.”
“Sawa.”
Walikubaliana kwenda kuitafuta nyumba ya mwanamke aliyempa kazi Anko Jay Jay ambayo waliamini anaweza kuhusika kwa asilimia kubwa katika mauaji yale.
*****
Majira ya saa kumi na mbili za jioni Land Cruser ilitembea taratibu katika mitaa ya Isamilo. Walilipaki sehemu na kuteremka kisha kutembea taratibu kufuata mtaa ambao Side alikuja siku moja na marehemu Anko Jay Jay kufuata malipo ya kazi aliyopewa ya kumchunguza mume wa mtu.
Sehemu aliposimama kumsubiri ilimchanganya kidogo kutokana na nyumba zile kufanana kidogo katika nyumba aliyoingia Jay.
“Vipi umeikumbuka?” kachero Mzengwa alimuuliza.
“Kati ya nyumba hizi mbali moja wapo, sikumbuki nilisimama wapi kwa vile ilikuwa usiku.”
“Joe unasemaje?” Mzegwa alimuuliza mwenzake.
Kabla hajamjibu lilikuja gari na kusimama kwenye nyumba moja kati ya zile mbili na kupiga honi. Baada ya muda alitoka mama mmoja mwenye mwili mkubwa kufungua geti huku akisema:
“Mume wangu leo nimekuwa mlinzi.”
“Mlinzi yupo wapi?”
“Nimemtuma mara moja.”
Baada ya kufungua geti gari lilingia ndani na kulifunga, baada ya kufungwa geti Side alisema:
“Itakuwa nyumba hii.” aliionesha nyumba jirani na gari lilipoingia gari.
“Kwa nini?”
“Jay alinieleza yule mwanamke anaishi na mume na mtoto mchanga hii inaonekana wenye nyumba ni watu wazima pia nyumba ile alinieleza haina mlinzi.”
“Una uhakika?”
“Ndiyo ni nyumba hii.”
“Basi tuondokeni tukajiandae kuja usiku nina imani kazi itakuwa si ngumu sana.”
“Na huyu?” Joe aliuliza kuhusu Side.
“Huyu tutakuwa naye mpaka zoezi la leo usiku liishe kisha atarudi kwake.”
Walirudi kwenye gari lao na kurudi ofisini kwa ajili ya operesheni ya kumtia mikono Kilole ambaye waliamini ndiye aliyekuwa akijua kila kitu juu ya kifo cha msichana aliyeuawa Gorden Crest na Anko Jay Jay japokuwa hawakujua muuaji ni nani, lakini waliamini kumtia mikononi yule mwanamke angewasaidia upelezi wao kwa kiasi kikubwa.
*****
Deus baada ya kuikagua siraha yake alisogea mpaka karibu ya dereva teksi Abdul aliyekuwa amezama kwenye penzi na mwanamke wa usiku.
“Mzee vipi?” Deus alimshtua Abdul.
“Poa mkuu.”
“Naona upo kazini?”
“Hapana nimemwita huyu baada ya kuona maboweka.”
“Njoo basi nje mara moja.”
Walitoka mpaka nje pamoja hadi ya cassino.
“Vipi mzee?” Abdul alimuuliza Deus akimtazama usoni.
“Mose unafahamiana naye sana?”
“Kiasi ila tunaelewana sana.”
“Kuna kazi nataka kukupa ukiifanya vizuri nitakupa fedha nzuri.”
“Kazi gani mkubwa?”
“Nina shida Mose ila nataka ukamtoe bila wapambe wake kuja nina mazungumzo naye.”
“Hilo mbona dogo.”
“Lakini usimwambie kama kuna mtu anamwita.”
“Hiyo kazi niachie mimi, akili yangu ukisikia fedha huwa haishindwi na kitu chochote hata kumfukua marehemu.”
“Basi nifanyie hiyo kazi mara moja, ila ukija hakikisha wewe unasimama huku na yeye huku.”
“Hakuna tatizo bosi wangu.”
Abdul aliingia ndani mara moja hadi kwenye meza za kamali na kumkuta Mose bado kashikilia bunda la dola akisubiri kuingia kucheza kamali.
“Mose,” Abdul alimwita alipomkaribia.
“Unasemaje Brother Abby?”
“Samahani nakuomba mara moja.”
“Una shiga gani brother? Zungumza nakusikiliza.”
“Naomba tutoke nje mara moja.”
“Si unajua muda wangu wa kuingia kwenye gemu umekaribia, jana walinila leo nina usongo nao,” Mose alijitetea ili asiende mbali.
“Dakika tano tu, waachie washikaji wakushikie unarudi sasa hivi.”
“Paul shika mkwanja huu narudi.”
“Poa mkubwa.”
Walitoka hadi sehemu ya kupakia magari, Deus alipomuona anakuja alizunguka nyuma ya gari. Walichomoa bastora tayari kwa tukio, walipofika walisimama Mose akiwa amempa mgongo Deus kama alivyomuelekeza Abdul. Aliiweka bastora yake tayari na kumsogelea taratibu hadi waliposimama na kumwekea bastora Mose kisogoni huku akisema kwa sauti ya chini yenye amri.
“Fungua mlango wa mbele wa gari na uingie ndani bila kuleta ujanja la sivyo nitakufumua ubongo.”
“Mheshimiwa vipi?” Abdul alishtuka kuona Deus ameshikilia bastora.
“Sitaki swali nawe ingia upande wako mara moja.”
Abdul hakutaka kubishana alizunguka upande wake na kuingia ndani na Mose naye alifanya kama alivyoelekezwa. Deus aliingia mlango wa nyuma na kusema kwa sauti ya amri.
“Elekea baharini mara moja.”
“Sawa,” Abdul alijibu huku akiwasha gari na kuondoka.
“Kaka mkubwa nimefanya nini?” Mose aliuliza kwa sauti ya upole.
“Utajua muda si mrefu.”
Gari lilitoka hoteli ya Piedimonte San Germano na kuingia barabara kubwa na kuelekea upande wa baharini.
“Abdul nataka gari likimbie kama linapaa,” Deus alitoa amri ya kijeshi.
“Hakuna tatizo mkubwa.”
Abdul alibadili gia na kukanyaga mafuta na kulifanya gari liondoke kwa mwendo wa kasi. Kabla ya kulivuka daraja refu gari la kina Mose lilikuja nyuma kwa kasi na kuwavuka na kusimama mbele yao kwa ghafla na kumfanya Abdul kufunga bleki kwa nguvu zote. Lakini gari lao liliseleleka na kwenda kuligonga gari la kina Mose wakati huo wapambe wa Mose walikuwa wametoka ndani ya gari na bastora mkononi tayari kumsaidia bosi wao.
Deus akili ilimchemka na kuona kafanya makosa ya kutoka naye mbali sana, lakini aliamini atapambana nao mpaka tone la mwisho la damu yake japokuwa alikuwa peke yake akipambana na kundi la zaidi ya watu sita wote wana siraha.
Deus naye kwa wepesi wake alitoka nje na kujificha nyuma ya teksi ya Abdul ambaye alikuwa hajui afanye nini. Wapambe walikuwa amekwisha ivamia gari na kumtoa bosi wao. Jamaa aliyetupwa juu ya gari na Abdul naye aliona ile ndiyo sehemu ya kulipa kisasi kwa Abdul.
Bila kuuliza alimjaza Abdul risasi za kichwa mpaka alipoamini amekata roho na kichwa hakitamaniki.
“Jamani mbaya wetu asikimbie,” Mose alisema kwa sauti ya juu.
“Hatoki lazima tumtie mikononi.”
“Nataka tusimuue tumshike akiwa hai,” Mose alitoa amri wa wapambe wake.
“Huyu hatoki hapa.” Ilikuwa kauli ya kumuunga mkono Mose ambaye alikuwa na hasira na Deus.
Deus aliinama kwa chini ili asionekane, wakati huo risasi zilikuwa zikirindima sehemu aliyojificha naye alijitahidi kujihami kwa kurudisha mashambulizi. Risasi ya bega iliyompata Deus ilimfanya adondoshe bastora chini. Alipotaka kuiokota kwa mkono cha kushoto alikuwa amechelewa teke zito lilitua usoni kwake na kumrudisha nyuma.
Itaendelea