Hadithi: Nyuma Ya Machozi

Hadithi: Nyuma Ya Machozi

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,746
Reaction score
25,646
Image may contain: 2 people

HADITHI : NYUMA YA MACHOZI
SEHEMU: 01
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500



SI KILA CHOZI LIDONDOKALO, hudondoka kwa huruma au maumivu, mengine nyuma yake yamebeba siri nzito. Siku zote siraha ya mnafiki huwa machozi, unaweza kuona anakuonea huruma kumbe kikulacho kinguoni mwako, anakutafuna taratibu ukishtuka amekumaliza. Deusi aliamini wote waliomlilia siku ya hukumu yake hasa mkewe na rafiki yake kipenzi walikuwa na uchungu wa kweli, lakini kumbe ilikuwa siri nyuma ya machozi. Ukitaka kujua yote naomba twende pamoja katika hadithi hii tamu. TWENDE SASA….

Gari aina ya Toyota Land cruser GX lilionekana likitembea taratibu mbele ya lango kuu la gereza la Segerea. Askari magereza wa zamu alilifuatilia lile gari huku moyoni akiamini kazi anayofanya na mshahara anaopata kununua gari lile ingebaki ndoto ya mchana.
Aliliona gari lile likisimama na kutulia kwa muda bila kufunguliwa mlango, kutokana na uzuri wake aliendelea kulitazama kwa matanio huku akijisemea moyoni’ Wenye fedha wanafaidi.” Baada ya dakika kumi mlango wa gari ulifunguliwa na kuteremka mwanamke mmoja aliyeonekana mjamzito, maisha yake mazuri, akiwa na kitoto kidogo cha kike cha miaka mitatu. Baada ya kutoka nje ya gari, yule mama alichuchumaa kuzungumza na kile kitoto. Baada ya muda yule mwanamke aliingia kwenye gari na kuondoka akimuacha mtoto amesimama peke yake. Alikuwa na boksi la biskuti ameshikilia sambamba na bahasha iliyofungwa kwa uzi mkononi. Kitendo kile kiliacha maswali mengi kwa askari , mbona kitoto kidogo kimeachwa pale. Wazo la haraka lilimjia huenda amekwenda sehemu mara moja atarudi kumchukua mwanaye. Lakini muda uliendelea kukatika bila kuonekana, na kitoto kile kiliendelea kusimama palepale kilipoachwa bila kujitikisa. Wakati huo wingu zito lilitanda na mvua ilianza kunyesha kitoto kile kikiwa pale pale huku kikiangua kilio cha kutaka msaada. Askari magereza alitoka kwenye lindo lake na kukifuata ili kukiondoa kwenye mvua. Alikibeba mpaka kwenye kibanda chake na kukiketisha kwenye benchi, ilibidi aingie kazi ya ziada kukimbembeleza kutokana na kumlilia mama yake. Jicho la askari lilitua kwenye bahasha aliyofungiwa mkononi yenye maandishi makubwa, MKUU WA GEREZA. Alishtuka na kujawa na mawazo mengi juu ya barua ile, alijiuliza kwa nini haikupelekwa moja kwa moja kwa mhusika au kulikuwa na ajenda gani kuachiwa mtoto mdogo barua ya mkuu wa gereza. Wasiwasi wake mkubwa alifikiria labda yule ni mtoto wa pembeni wa mkuu wa gereza hivyo aliletwa pale ili kumsusia. Hakutaka kumpeleka moja kwa moja kwa mkuu wa gereza, kuhofia kuleta mtafaruku ndani ya ndoa yake. Alimuita askari mwenzake aliyekuwa akipita. “John hebu njoo.” “Okote umeamua kuingia lindo na mwanao?” “Kaka wee acha, kuna gari moja la kifahari limesimama mbele ya lango kuu na kumuacha mtoto huyu.” “Halafu waliomuacha walikueleza nini?” “ Lilisimama kule, nilijua labda wamemwacha watamrudia, lakini mpaka mvua inateremka sikuona gari wala mtu. Ilibidi nikamchukue na kumuhifadhi hapa, kilichonichanganya na kutaka msaada wako ni barua aliyokuwa amefungwa mkononi , imeandikwa mkuu wa gereza.” “Eti?” “Imeandikwa mkuu wa gereza,” Okote alirudia kusema. “Sasa mkuu wa gereza na mtoto huyu wanahusiana nini?” “Kuna kitu kimenitisha.” “Kipi hicho?” “Huenda mkuu alimpa mimba mwanamke, leo ameamua kumletea mtoto hapa.” “Mmh! Inawezekana, kwani si yupo ofisini kwake?” “Sijui, nilikuwa naomba msaada niangalizie kama yupo tumpeleke mtoto na barua” “Gari lake sijaliona kupita atakuwa yupo.” “Basi naomba unipelekee na kumpa maelezo haya.” Alikubali kumpeleka, alimbeba na kuelekea naye kwenye ofisi ya mkuu wa gereza, mlango ulikuwa umefungwa, mlinzi wake alimuuliza. “Vipi John mbona na mtoto ofisini?” “Nina shida na mkuu.” “Shida gani?” “Sefu, shida ya mkuu nikueleze wewe?” “Ok, ingia.” John aliingia hadi mapokezi, sekretari naye alishtuka kumuona John amembeba mtoto. “John, vipi mtoto anaumwa mbona hivyo?” “Hapana nina shida na mkuu.” “Sasa hivi amesema hataki kuonana na mtu ana kazi nyingi.” “Najua lakini kuna mzigo wake.” “Huyo mtoto?” “Ndiyo na barua,” alimkabidhi barua ambayo aliisoma na kukutana na jina la Mkuu wa gereza. “Umemtoa wapi?” “Kuna mwanamke kamtelekeza hapo nje na kuondoka.” “Mmh, isiwe nyumba ndogo?” Suzy alisema kwa sauti ya chini. “Hata mimi ndiyo wasiwasi wangu.” “Hebu ngoja nimpigie simu nimsikie anasemaje, unajua John hii kashfa.” “Tena inabidi tusijichanganye tutakimbia kazi.” Suzy alimpigia bosi wake simu. “Halo Afande kuna ugeni wako mzito.” “Nani?” “Kuna mtoto katelekezwa nje ya gereza mkononi ana barua yako.” “Barua yangu! Inasemaje?’
”Hatujaisoma afande ila kuna jina la mkuu wa gereza.” “Mmh! Hebu mlete ofisini haraka.” John alimbeba mtoto na kuingia naye ofisi kwa mkuu wake, baada ya kupiga saruti alimtua mtoto . Mkuu wa gereza alimuangalia yule mtoto lakini hakugundua kitu chochote katika uso wa mtoto. “Nipe hiyo barua,” John alimkabidhi na kusubiri maelekezo. Mkuu wa Gereza Mzee Sikamtu aliifungua ile barua na kuisoma kwa muda kisha alishusha pumzi na kusema: “John.” “Naam afande.” “Nenda gerezani kaniletee mfungwa Deusi Ndonga njoo naye mara moja,” alisema huku akiweka barua juu ya meza. Baada ya maelekezo John alipiga saruti na kugeuka kisha aliondoka kwa mwendo wa ukakamavu.
********
Ndani ya gereza Deusi Ndonga alikuwa amejiegemeza kwenye ukuta huku maumivu ya moyo wake yalikuwa makubwa zaidi ya yale ya kufungwa gerezani miaka saba. Lakini kitendo cha usaliti wa mkewe Mwaka mmoja toka aingie gerezani kwa kosa la kukamatwa na dawa za kulevya ambazo aliamini kabisa ule ulikuwa mtego alitegewa na bosi wake. Kila dakika aliiona kama njozi ya mchana isiyo na ukweli wa kumuona mkewe akiwa mjamzito, mimba ambayo haikuwa yake. Akiwa katikati ya mawazo jina lake liliitwa. Alinyanyuka na kusogea mlangoni. “Deus unaitwa na mkuu wa gereza.” Deusi alitoka chumba cha gereza na kufuatana askari aliyetumwa na mkuu wa gereza. Akiwa nyuma yake, alijawa na mawazo na kujiuliza mkuu wa gereza anamuitia nini. Na kwa nini amuite ofisini kwake. Alipofika nje ya ofisi John alimweleza Deusi asubiri na yeye kuingia ofisini kwa mkuu wa gereza. Baada ya muda alitoka na kumweleza aingie, alipoingia moyo wake ulishtuka kumuona mtoto pale ofisini. Lakini hakutaka kuhoji kitu kwa vile aliitikia wito si kuuliza swali. “Deusi,” mkuu wa gereza alimuita baada ya kuketi kwenye kiti. “Naam mkuu.”
”Unamfahamu huyu?” alimuuliza huku akinyoosha mkono kwa mtoto mdogo aliyekuwa ameketi kwenye kochi. “Ndiyo mkuu.” “Unamfahamu vipi?” “Ni mwanangu,” Deusi alijibu kwa utulivu. “Shika barua hii usome,” aliipokea na kuanza kusoma taratibu. Alitembeza macho taratibu kusoma herufi moja baada ya nyingine, kila alichosoma kilikuwa sawa na kuupasua moyo wake kwa kisu butu bila ganzi. Mkuu wa gereza alimfuatilia Deusi alipokuwa akisoma barua huku akishuhudia michirizi ya machozi ikiteremka kwenye mashavu yake. Mishipa ya kichwa ilimsimama na macho kuzidi kuwa mekundu ikifuatiwa na kamasi nyepesi, baada ya kuimaliza kuisoma barua alimwangalia mwanaye aliyekuwa amekaa kwenye kochi akishangaa picha ya mkuu wa nchi iliyokuwa ofisini huku akiendelea kutafuna biskuti zake. Baada ya kumwangalia mwanaye aliyemuonea huruma huku moyo wake ukiongezeka maumivu mara dufu. Katika maisha yake kitendo cha yeye kufungwa gerezani hakikumuumiza moyo wake kwa kuamini ile ni mitihani ya maisha, mwanadamu anatakiwa kupambana nayo. Lakini pigo zito la kwanza lilikuwa kumuona mkewe akiwa na ujauzito usio wake, akiwa bado katika maumivu ya mkewe kukosa uaminifu mwaka mmoja baada ya kifungo chake. Pigo zito zaidi ya bomu la kilo 1000 lililousambalatisha moyo wake lilikuwa kwenye ile barua. Barua ilikuwa imeandikwa hivi: Dear zilipendwa, mume wangu wa zamani, najua kidonda cha kuona mwanaume mwenzako kunijaza tumbo bado hakijapona, lakini sina jinsi, siku zote punda unaweza kumlazimisha kumpeleka mtoni, lakini huwezi kumlazimisha kunywa maji. Hii ilikuwa sawa na tamaa ya wazazi wangu kunilazimisha niolewe na wewe, mwanaume asiye chaguo langu. Walijua kabisa chaguo la moyo wangu ni Kinape. Kuolewa nawe ilikuwa sawa na punda kumlazimisha kuingia mtoni lakini ilikuwa vigumu kuendelea kuwa na wewe kwa vile si chaguo langu. Baada ya kufungwa kwako ilikuwa ni nafasi yetu ya kujinafasi kufanya mapenzi kwa uhuru mkubwa. Kwa muda mrefu tulikuwa tukifanya kwa wizi, najua itakuuma sana na kuupasua moyo wako kwa kisu butu bila ganzi. Lakini ukweli unabaki palepale nilikuwa sikupendi na sitakupenda milele. Kama Kinape angekuja mapema hata huu uchafu wako usingeingia tumboni mwangu, nilipanga kukinyongea mbali. Lakini moyo wa huruma ulinijia wa kuidhuru damu yangu ilinishika. Nimeamua kukuletea mtoto wako ili ukae naye gerezani. Siwezi kumtunza mtoto wa mwanaume nisiye mpenda, siwezi kuchanganya mtoto wa njiwa na bundi. Mimi kuolewa na Kinape sawa na mshare umerudi porini haukupotea, sasa hivi mimi ni mke mtarajiwawa Kinape. Nakutakia maisha marefu yenye furaha na mwanao gerezani. Ni mimi dear zilipendwa Kilole. Mkuu wa gereza alimshuhudia Deusi akiwa naye kimwili lakini kiakili alikuwa mbali sana, alimuita. “Deusi...Deusi.” “Haiwezekani... haiwezekani, kwa nini lakini, kwa nini mke wangu unanitendea unyama kama huu. Nimekukosea nini? Kwa nini unamtesa mtoto asiye na hatia, kwa nini unanisaliti na rafiki yangu. Eee Mungu kosa langu nini, haya huyu mtoto mdogo nitamweka wapi, anajua nimefungwa anakuja kuniterekezea mtoto. ” Deusi alishindwa kujizuia aliangua kilio cha sauti ya chini. “Deusi pole,” Afande John alimtuliza. “John,” Mkuu wa gereza alimuita. “Naam afande.” “Nipe nafasi nizungumze machache na Deusi.” Baada ya John kutoka, alitulia kwa muda akimwangalia Deusi aliyekuwa akitoa kamasi kwa mkono na kufuta kwenye shati lake. Alinyanyuka na kwenda kwenye friji ndogo ya ofisini na kutoa chupa kubwa ya maji yaliyokuwa nusu na kummiminia kwenye glasi kisha alimpa Deusi. “Pole sana Deusi, naomba unywe maji haya kwanza.” Deusi aliipokea glasi na kuyanywa maji yote kwa mkupuo kisha aliiweka glasi juu ya meza. “Deusi.” “Naam mkuu.” “Kwanza pole sana.” “Sijapoa mkuu.” “Kuna siri gani kati yako na mkeo?”

Itaendelea kesho kutwa
 
HADITHI : NYUMA YA MACHOZI
SEHEMU: 02
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
Deusi aliipokea glasi na kuyanywa maji yote kwa mkupuo kisha aliiweka glasi juu ya meza. “Deusi.”
“Naam mkuu.”
“Kwanza pole sana.”
“Sijapoa mkuu.” “Kuna siri gani kati yako na mkeo?”
SASA ENDELEA...

“Kwa kweli sijui hata kitu kimoja, ni mwezi wa pili sasa, mke wangu ameujeruhi moyo wangu kwa kukosa uaminifu wa kubeba ujauzito usio kuwa wangu.”
“Mkeo ulimuoa kwa mapenzi yake au kwa kulazimishwa?” “Kwa kweli mke wangu nilichaguliwa na wazazi wangu nilipokwenda kijijini kuwatembelea. Mwanzo wa ndoa yetu alionesha mapenzi ya dhati kumbe nilikuwa nafuga nyoka, amekua sasa amenimeza. ” “Na Kinape ni nani?”
“Kinape alikuwa zaidi ya rafiki, tumesoma na kucheza pamoja kabla ya mimi kuendelea na masomo mpaka kupata kazi katika kitengo cha kuzuia dawa za kulevya.” “Na alifikaje kwako?”
“Ni historia ndefu”
******
Miaka minane iliyopita Deusi King’ole baada ya kuanza kazi kama mkuu wa kitengo cha kuzuia madawa ya kulevya. Miaka mitatu katika kazi yake alipata likizo iliyomfanya aende kijijini kwa wazazi wake. Katika watu wa karibu baada ya wazazi wake, walikuwa wazazi wa Kinape ambaye toka wakiwa shule ya msingi waliitwa pacha kutokana na ukaribu wao. Deus baada ya kufika kijijini na kupokewa na ndugu na jamaa ambao walimshangaa kumuona amerudi katika gari la kifahari, wengi walizoea kuliona gari kama lile kwa mbunge wao tu, alipokwenda kujijini kuwatembelea wapiga kura wake. Ilikuwa ni furaha hasa kwa wazazi wake ambao waliamini kazi ya kumsomesha mtoto wao ilikuwa imezaa matunda. Kitu kikubwa alichowaahidi wazazi wake kuhakikisha anayabadili maisha ya familia yake ikiwa pamoja na kuwajengea nyumba ya kisasa na kuwachimbia kisima cha maji. Baada ya kutulia alitaka kujua habari za rafiki yake Kinape.
“Jamani Kinape yupo?”
“Mmh! Nina siku sijamtia machoni,” mama Deusi alijibu.
“Nasikia sijui alikwenda mjini kutafuta kazi,” mdogo wake alisema.
“Sasa wewe mjini huko hukumuona?” Mzee King’ole aliuliza. “Baba mji ni mkubwa, mnaweza kukaa miaka kumi bila kuonana na mtu pengine mnakaa kitongoji kimoja.”
“Labda siku hizi, siku za nyuma watu tulikuwa tunajuana hata wageni walipoingia tuliwatambua.”
“Ni wakati huo baba, sasa hivi mji umepanuka.”
“Basi atakuwa hukohuko mjini.”
“Na yeye atarudi na gari?” Mdogo wake aliuliza.
“Siwezi kujua,” Deus alijibu kwa mkato.
“Lakini mzee Solomoni na mkewe si wapo?” Deus aliuliza.
“Wapo, waende wapi,” mzee King’ole alijibu.
“Basi ngoja nikawaone kabla ya kujipumzisha.”
“Haya baba,” mama Deus alijibu. Deus alinyanyuka ili aelekee kwa mzee Solomoni. “Kaka twende wote,” mdogo wake wa kike aliyekuwa anasoma kidato cha kwanza aliomba kuongozana na kaka yake.
“Hakuna tatizo,” alijibu huku akimshika mkono. Walikwenda hadi kwa mzee Solomoni, alimkuta mama Kinape akisuka ukiri. “Hodi hapa.”
“Karibu,” alijibu huku akiacha kusuka na kumtazama mgeni aliyekuwa amesimama mbele yake. “Shikamoo mama.” “Marahaba, karibu.”
“Asante.”
“Ndiyo baba,” ilionesha mama Kinape kamsahau Deus. “Mama unamjua huyu?” Salome mdogo wa Deus alimuuliza mama Kinape.
“Hata,” alijibu huku akijitahidi kumkazia macho.
“Si kaka Deusi huyu.”
“Deusi wa mjini?”
“Ndiyo.”
“Jamani, mwanangu mwenyewe nimemsahau, karibu baba tusameheane, macho ya uzee haya.”
“Kawaida, mama za hapa?”
“Hebu ngoja kwanza, Salome kamletee kiti kaka yako.” Salome alikwenda ndani na kurudi na kiti cha kukunja, alikiweka pembeni ya mama Kinape.
“Wee, Salome kiweke mbele nimuone vizuri,” Salome alifanya kama alivyo agizwa. Baada ya kukaa alianza kuzungumza: “Ndiyo, mama za siku?”
“Mmh! Hivyo hivyo tu baba, kila kukicha afadhari ya jana.”
“Ni kweli sasa hivi nasikia hata mvua zimegoma.”
“Kama unavyoona.”
“Baba yupo wapi?”
“Ametoka kidogo, ila achelewi, unavyomtaja pengine yupo njiani anarudi.”
“Na ndugu yangu?”
“Kinape?”
“Eeeh.”
“Mmh! Kakimbilia mjini.”
“Kufanya nini?”
“Mwanangu kwani wewe mjini unafanya nini?”
“Mimi nafanya kazi serikalini kutokana na elimu yangu.”
“Kwa kweli hatujui mjini anafanya kazi gani.”
“Anakaa wapi ili nikifika nimtafute?”
“Hatujajua ila yeye kasema atalala popote hata sokoni.”
“Mmh! Haya.”
“Vipi umeoa?”
“Bado.”
“Unasubiri nini?”
“Nilikuwa najipanga.”
“Deus wazazi wenu lini tutacheza na wajukuu?”
“Nina imani sasa hivi nitafuta machozi yenu.”
“Fanya hivyo, usiwe kama mwenzako kila siku kesi za watoto wa watu.”
“Sasa mama, wacha nikapumzike ndiyo nimefika nahitaji kupumzika.” “Hakuna tatizo, tuachie basi hata fedha ya unga.” Deus aliingiza mkono mfukoni na kutoa noti moja ya shilingi elfu kumi na kumkabidhi. Kabla hajaipokea alitokea mzee Solomoni na kusema: “Mheshimiwa nami usinisahau.”
“Aah, baba.” Deus alisema huku akimgeukia mzee Solomoni, Mzee Solomoni alishtuka kumuona Deus.
“Ha! Ni wewe Deus?”
“Ni mimi baba.”
“Umefika lini?”
“Leo.”
“Na lile gari la mbunge lililopaki kwenu?”
“Si gari la mbunge ni gari langu mwenyewe.”
“Ha! Ina maama na wewe siku hizi mbunge?”
“Hapana kuwa na gari kama lile halimaanishi mbunge, mtu yoyote anaweza kumiliki.”
“Kwa hiyo ni la kwako?”
“Ndiyo baba.”
“Hata hali yako inajionesha.”
“Kidogo kidogo.”
“Una habari gani?” Mzee Solomoni alisema huku akimtazama kwa makini Deus. “Nilikuja kuwajulia hali mara moja, ila nimesikitika kumkosa rafiki yangu kipenzi Kinape.”
“Yule rafiki yako mpumbavu, tena hana akili, amekimbia kilimo, ona jinsi tulivyochoka wazazi wake yeye anakimbilia mjini. Kibaya anapokwenda hana ndugu wala sehemu ya kufikia,” mzee Solomoni alisema kwa hasira.
“Lakini baba si kulalamika, ni kumuombea ili milango ya riziki ifunguke na kupata shughuli yoyote ya kumpatia kipato.”
“Kweli kabisa usemayo, kila siku baba yenu analalamika hajui kama ni laana kwa mtoto,” mama Kinape aliunga mkono.
“Wazazi wangu nakuahidini kitu kimoja, kwa vile mmesema yupo mjini nitamtafuta kila kona ili kuhakikisha nampata.”
“Litakuwa jambo la zuri.” Deus aliagana na wazazi wa Kinape ili arudi nyumbani, mzee Solomoni alikumbusha.
“Mwanangu na mimi mbona umenisahau?” Deus aliingiza mkono mfukoni na kutoa noti nyingine ya elfu kumi na kumkabidhi. “Asante sana mwanangu Mungu akizidishie.”
“Asante wazazi wangu, atuzidishie wote.” Deusi aliwaaga na kurudi nyumbani, njiani wakati wa kurudi walikutana na binti mmoja aliyekuwa amebeba chupa ya mafuta ya kula. “Shikamoo,” yule binti alimsabahi Deus.
“Marahaba.”
“Salome, mambo?”
“Poa, umemuona kaka yangu anayeishi mjini?”
“Kumbe ndiye huyu, shikamoo.”
“Jamani Kilole, mbona unataka kumchosha kaka yangu, shikamoo mara ngapi?”
“Jamani ya kwanza ya kutomjua, ya pili ya kumfahamu, kuna ubaya?”
“Hakuna ubaya, marahaba,” Deus aliitikia huku akitabasamu. “Karibu kwetu kaka.”
“Asante.”
“Haya nawahi nyumbani, Salome baadaye.”
“Haya.” Waliagana na Kilole kila mmoja aliendelea na safari yake, wakiwa wanarudi nyumbani Deus alijikuta akivutiwa na mchangamfu wa Kilole.
“Salome, Kilome mtoto wa nani?”
“Wa mzee Sikwera.”
“Mmh! Mbona huyu msichana simfahamu?”
“Kwani ulikuwa unapenda kutembea kijijini, mbona alikuwepo.” “Kumbe, rafiki yako?”
“Kiasi, vipi umemependa?”
“Basi tu kanivutia kwa uchangafu wake.”
“Hata mimi nampenda.”
“Ameolewa?”
“Mtu yupo kwao, atakuwa ameolewa vipi?”
“Kwa hiyo hajaolewa?”
“Hajaolewa.”
“Kama hajaolewa atakuwa na rafiki wa kiume?”
“Kaka swali hilo gumu.” Salome alificha siri ya Kilole kutokana na siku za nyuma kuwa na urafiki wa kimapenzi na Kinape rafiki kipenzi cha kaka yake. Kwa vile Kinape alikuwa na miezi sita toka aende mjini. Hakukuwa na haja ya kumzibia riziki kama kweli kaka yake anampenda.

Itaendelea kesho
 
HADITHI : NYUMA YA MACHOZI
SEHEMU: 03
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.
ILIPOISHIA:
Salome alificha siri ya Kilole kutokana na siku za nyuma kuwa na urafiki wa kimapenzi na Kinape rafiki kipenzi cha kaka yake. Kwa vile Kinape alikuwa na miezi sita toka aende mjini. Hakukuwa na haja ya kumzibia riziki kama kweli kaka yake anampenda. SASA ENDELEA...

“Basi tuachane na hayo,” Deus alibadili mada. “Vipi umempenda, kama umempenda nitafurahi siku moja akiwa wifi yangu.” “Ni haraka sana, kila kitu kizuri kinataka subira.” Kutokana na mazungumzo kupamba moto walijikuta wakifika kwao bila kujua, Deus hakutaka tena mazungumzo aliingia chumbani kwake na kujilaza. Kabla ya kulala mawazo yote yalikuwa kwa Kilole. Aliamini kabisa kama hana mtu basi nafasi ile aitumie vyema mpaka anarudi mjini awe amepata jibu la uhakika. wake kuhamishwa na wazazi wake kwa ajili ya tofauti ya dini. Deus alikuwa na Alikumbuka moyoni mwake kuna chumba hakina mpangaji baada ya mpangaji mpenzi wake anayefanya kazi katika shirika la vifaa vya Electonic kama Series Officer. Uhusiano wao ulianza taratibu, mpaka ulipofikia hatua ya kutambulishwa Deus kwa wazazi wa mpenzi wake Halima. Tatizo lilikuwa dini Halima muislamu na Deus mkiristo, wazazi wa Halima hawakuwa na pingamizi kama Deus atabadili dini kumfuata Halima.
Deus hakuwa tayari wazazi wake walisema kama ni hivyo hakuna ndoa. Deus alibembeleza wafunge ndoa ya serikali, pia hiyo waliikataa. Hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali kubwaga manyanga kutokana na kushindwa masharti. Miezi sita ilikatika huku ukaribu wake na Halima ukipungua na mwisho kabisa ulivunjika. Wazo la kutafuta mpenzi mwingine aliliweka kando na kujikita katika kuyatengeneza maisha yake na ya wazazi wake kijijini. Baada ya kukaa kwa muda alijikuta turufu yake ya upendo anaitupa kwa Kilole, baada ya kuwaza sana usingizi ulimpitia. ********** Alishtuka jioni, baada ya kuoga na kupata chakula alikaa na mama yake, katika mazungumzo alimgusia mama yake msichana aliyekutana naye wakati akitoka kwa mzee Solomoni. “Mama wakati narudi toka kwa mzee Solomoni, nimekutana na msichana mtoto wa m.. mmm..ze..ee.ee, eti Salome yule msichana tuliyekutana naye ni mtoto wa mzee nani?” Alimuuliza mdogo wake aliyekuwa amekaa mbali kidogo. “Mmh! Kaka bado unaye, kweli kakugusa.” “Salome hebu tuambie mtoto wa nani?” Mama yao alikuja juu. “Mama si Kilole?” “Kilole huyu mtoto wa mzee Sikwera?” “Ndiye huyo huyo.” “Eeh, amefanya nini?” Mama Deus alishusha sauti na kuzungumza kwa sauti ya chini na mwanaye. “Unamuonaje?” “Kivipi?” “Hata sijui, nimempenda alivyo pia ni mchangafu akiwa ndani nyumba haizubai.” “Kwa hiyo unataka awe mkeo?” “Mama mbona kila kitu kinajieleza.” “Kwa kweli ni mmoja wa wasichana wenye heshima hapa kijijini, mengine siwezi kujua lakini ametulia.” “Mmh! Sawa.” “Vipi? Tufanye mpango?” “Kwa sasa ni maandalizi kama atakuwa tayari, basi tujipange kwa harusi baada ya miezi mitatu tufunge ndoa, vipi kuhusu elimu?” “Mi sijui labda umuulize Salome.” “Eti Salome, shoga amesoma mpaka darasa la ngapi?” “Kidato cha nne.” “Kinatosha ataendelezwa kwa vile elimu haina mwisho.” “Basi kazi hii nitaifanya na baba yako leo usiku tutakwenda kwa wazazi wa Kilole.” ******** Usiku ulipoingia wazazi wa Deus walikwenda kwa wazazi wa Kilole kupeleka ujumbe wa Deus. Walipokelewa vizuri, bila kupoteza muda waliwaeleza kilichowapeleka. “Utani huo mzee mwenzangu, Deus aache wanawake wote mjini aje atafute kijijini?” Baba Kilole alisema baada ya kusikia ombi la mzee mwenzake. “Najua utasema hivyo, kila kitu ni uamuzi wa mtu.” “Wala hatujamshinikiza, sijui kamuona leo,” mama Deus aliongezea. “Jamani kampenda au kamtamani?” “Mzee mwenzangu mpaka kuja hapa tumelijadili jambo hili kwa kina.” “Mmh! Haya, umesikia mke wangu?” Baba Kilole alimuuliza mkewe. “Mimi nafikiri hili ni jambo jema, sifikiri tunatakiwa kuhoji sana,” mama Kilole alijibu. “Mke wangu kuuliza si vibaya japo sisi wenyewe tunajua.” “Ni kweli, lakini mpaka kufunga safari basi hawakuja kufanya utani.” “Wazee wenzetu tumekusikieni tupeni muda tuzungumze naye, majibu mtayapata kesho.” “Hakuna tatizo, jambo lolote zuri linahitaji subira.” “Na kama akikubali harusi mnatazamia iwe lini?” “Amesema baada ya jibu zuri kuna miezi mitatu ya maandalizi.” “Kama ni hivyo itatusaidia nasi kujipanga.” Waliagana na kurudi nyumbani, Deus alikuwa na shauku ya kujua wazazi wake wamerudi na jibu gani. Lakini baba yake alimtuliza kwa kumweleza ujumbe umefika jibu watalipata kesho yake. ******* Baada ya kuondoka wazazi wa Deus, mama Kilole alimwita mwanaye aliyekuwa ndio kwanza ametoka kuoga. “Kilole mwanangu.” “Abee mama.” “Unajijua wewe sasa hivi umeisha vunja ungo?” “Najua mama.” “Unajua huu ni mwaka wa ngapi?” “Mmh! Wa tano sasa.” “Kwa hiyo nina imani upo tayari kwa ndoa.” “Mmh! Nitaweza?” “Kilole kila siku ulikuwa unatoroka usiku kwenda kulala kwa Kinape, bado unajiona mtoto?” “Nani anataka kunioa? Kinape! Vipi amerudi?” Kilole aliuliza kwa mshtuko. “Siyo Kinape.” “Nani?” “Mtoto wa mzee King’ole.” “Yupi?” “Deus” “Yule anayekaa mjini?” “Huyo huyo, nasikia mlionana leo.” “Mmh!” Kilole aliguna. “Mbona unaguna?”
”Lakini mama si unajua kila kitu.” “Kuhusu Kinape?” “Ndiyo.” “Wee mtoto hebu acha ujinga, Kinape atakusaidia nini?” “Mama, siwezi kuvunja ahadi yangu na Kinape, ameniahidi anakwenda mjini kutafuta maisha na akirudi anakuja kunichukua.” “Mwanangu haya si ya kuyasema kwa baba yako, ile ilikuwa siri yetu. Baba yako akijua atatuua.” “Mama mimi siwezi kuolewa na mume nisiyempenda.” “Haya maneno yaishie hapa, chonde mwanangu usiangushe, nakuomba ukubali.” “Mama kama nitaolewa nitakuwa sikuolewa kwa hiyari yangu.” “Najua mwanangu, ila nakuomba unifichie aibu hii.” “Mama Kinape nitamueleza nini? Kumbuka nilimuahidi, kuendelea kumsubiri mpaka atakapo rudi na ahadi ni deni.” “Mwanangu, sivyo vyote vinavyo ahidiwa hutimia, kumbuka Deus ni mtu mwenye uwezo mkubwa kimaisha, huoni itatusaidia hata sisi wazazi wako? Hebu ona Mariamu mumewe ana uwezo mdogo, lakini wazazi wake wanaishi maisha mazuri. Deusi amejenga nasikia mshahara wake mkubwa ana gari zaidi ya matatu tofauti na hili alilokuja nalo kama la mbunge, tena ni mtu tunayemfahamu.” “Mama nakubali kwa shingo upande, bado nampenda Kinape,” Kilole alisema huku akibubujikwa na machozi. “Najua mwanangu, lakini inaonesha Deus naye mtu mzuri, si unaona familia yetu, hebu tutoe kwenye dimbwi la umaskini nafasi hii asije pata mwingine tukaijutia.” mama yake alisema huku akiwa amemkumbatia na kumpigapiga mgongoni taratibu. “Sawa mama, sina jinsi lazima nikubali.” “Asante mwanangu.” Mama Kilole aliagana na mwanaye aliyeingia chumbani kwake kulala, alishukuru Mungu mwanaye kukubali kuolewa na Deus. Alipoingia ndani alikutana na mumewe akimsubiri. “Vipi imekuwaje?” “Hakuna tatizo.” “Amekubali?” “Ndiyo.” “Lakini kuna kitu nina wasiwasi nacho,” kauli ile ilimshtua mama Kilole. “Kitu gani?” “Kuhusu uhusiano wa Kilole na Kinape.” “Uhusiano upi?” Mama Kilole alijifanya hajui kitu.
”Wewe ndiye ulitakiwa kunifafanulia na sio kuniuliza.” “Mume wangu, ungeweka wazi ili nielewe unalenga nini.” “Ukaribu waliokuwa nao.” “Ni wa kawaida, Kinape si alikuwa kama mtoto wa familia.” “Mbona nilisikia wana uhusiano wa kimapenzi, sio tumuoze aje atutie aibu.” “Kwa kweli hilo mwenzangu nilikuwa silijui, mbona hukunieleza mapema ili nilifanyie kazi.” “Nikueleze nini wakati siku zote siri za watoto wa kike wanajua mama zao.” “Mume wangu kumbukeni mmekuwa mkitutia lawama wazazi wa kike, kuna mzazi anayetaka mtoto wake wa kike aharibike?” “Mbona mama yako ndiye aliyekuwa akinipa wepesi wa kuzungumza na wewe?” “Kwa vile alijua una nia nzuri, lakini kama ungetaka kunichezea na kuniacha asingekubali.” “Tuachane na hayo, kwa hiyo amekubali?” “Amekubali.” “Na una uhakika bado msichana?” “Mume wangu hilo swali siwezi kulijibu labda umuulize mwenyewe.” “Si swali la baba kumuuliza mtoto wa kike bali mama yake.” “Basi nitamuuliza, kama hana itakuwaje?” “Tujiandae na aibu au kupimwa kukutwa na wadudu.” “Mungu apishe mbali.” “Basi tulale ili kesho tuwape jibu lao.”

Itaendelea Jumatatu
 
HADITHI : NYUMA YA MACHOZI
SEHEMU: 04
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
“Kwa vile alijua una nia nzuri, lakini kama ungetaka kunichezea na kuniacha asingekubali.” “Tuachane na hayo, kwa hiyo amekubali?” “Amekubali.” “Na una uhakika bado msichana?” “Mume wangu hilo swali siwezi kulijibu labda umuulize mwenyewe.” “Si swali la baba kumuuliza mtoto wa kike bali mama yake.” “Basi nitamuuliza, kama hana itakuwaje?” “Tujiandae na aibu au kupimwa kukutwa na wadudu.” “Mungu apishe mbali.” “Basi tulale ili kesho tuwape jibu lao.”
SASA ENDELEA...
*****
Lakini upande wa pili wa Kilole alikosa usingizi kuwaza usaliti wake kwa Kinape mwanaume aliyemuingiza katika katika dunia ya wapendanao. Katika maisha yake aliamini Kinape ndiye mwanaume pekee katika moyo, alijiuliza atamwambia nini akimkuta ameolewa. Akiwa amejilaza chali kalalia mikono kwa nyuma, alijikuta kwenye mtihani mzito wa kuingia katika maisha ya ndoa ya mwanaume asiyekuwepo moyoni mwake. Lakini alikumbuka shoga yake Mariamu mtoto za mzee Sadiki jinsi alivyo ibadili familia yake kimaisha baada ya kuolewa na mwanaume mwenye uwezo aliyekuwa akiishi mjini. Aliufananisha uwezo wa mume wa Mariamu haukuwa mkubwa kama wa Deusi mtoto wa mzee King’ole. Deus alikuwa akimzidi mara mia mume wa Mariamu. Mume wa mariamu pamoja na kuwa amejenga nyumba hakuwa na gari, Deus alikuwa na jumba la kifahari na magari ya kutembelea zaidi ya matatu. Japo moyoni bado alikuwa amemjaza Kinape alijikuta akijisemea moyoni: “Liwalo na liwe.” Alivuta shuka na kujilaza, lakini bado usingizi ulimkimbia na kujikuta akikumbuka ahadi aliyopeana na Kinape. “Kinape nakupenda sana, nakuomba usiniache kumbuka wewe ndiye unayeijua thamani ya usichana wangu, wewe ndiye uliyenionjesha tamu ya dunia. Nakupenda kulicho kitu chochote chini ya jua.” Kilole alikumbuka siku aliyomlilia Kinape baada ya kuzijua raha za dunia. “Kilole naheshimu zawadi uliyonipa, nakuhakikishia wewe pekee ndiye utakaye kuwa mke wangu. Nakuomba usinisaliti.” “Sitakusaliti, nakupenda sana Kinape.” Kilole alipoyakumbuka yale alijikuta akitokwa na machozi kwa kuamini kilichopo mbele yake ni maamuzi mazito kama kumeza mfupa.
********
Siku ya pili familia ya mzee Sikwera ilirudisha majibu kukubali Kilole kuolewa na Deus, taarifa ilipoifikia familia ya mzee King’ole walimfikishia Deus ambaye moyo wake ulijaa furaha baada ya ombi lake la kumuoa Kilole kufanikiwa. Alipata muda wa kuonana na mchumba wake kabla ya kuelekea mjini. Iliandaliwa siku maalumu ambayo ilikuwa kufahamiana na kukubaliana kuunganisha ukoo mbili. Sherehe ndogo ilifanyika nyumbani kwa mzee Sikwera baba yake Kilole. Deus na Kilole waliwekwa sehemu maalumu kwa ajili ya kufahamia kwa karibu. Wakiwa kimya kila mtu akitafakari lake Deus alikuwa wa kwanza kuvunja ukimya. “Kilole,” Deus alianza kwa kumuita jina lake. “Abee,” alijibu huku ameangalia chini. “Naomba unitazame basi.” “Sema tu ninakusikia,” Kilole alijibu huku akiwa ametawaliwa na aibu. Deus alitumia nafasi ile kumchunguza Kilole kwa karibu na kugundua vitu vingi sana, haiba na umbile lililojengeka kike hasa. Moyoni aliona muda aliopanga wa miezi mitatu ni mrefu sana. Mvuto wa Kilole ulikuwa mkubwa baada ya kumsogelea kwa karibu. “Asante sana.” “Asante ya nini?” “Ya kukubali ombi langu.” “Mmh,” Kilole aliguna tu. “Kilole nakuahidi kukupenda kwa moyo wangu wote.” “Asante, nami pia nitakuwa mke mwema.” “Pia nakuahidi kukuendeleza kimasomo.” “Nitashukuru kwa vile kiu yangu ya kutafuta elimu haijaisha.” “Nitakuacha kwa muda kwa vile nawahi kazini, ila kila kitu nimewaachia wazazi. Baada ya miezi mitatu tutakuwa mke na mume.” “Hakuna tatizo nitakusubiri.” “Nashukuru kusikia hivyo.” Baada ya mazungumzo na sherehe iliyochukua saa sita familia mbili ziliagana, Deus aliamini kila kitu duniani hupangwa na Mungu, hakuamini kama kijijini kutakuwa na wanawake wazuri kushinda mjini. Aliapa kumlinda Kilole kwa nguvu zake zote. Upande wa pili Kilole bado mzimu wa Kinape ulimsumbua, ulijikuta akilaumu muda mrefu uliopangwa wa harusi. Wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kwa Kinape kutokea kijijini kabla ya ndoa ya kuharibu kila kitu. Moyoni aliomba kila alichokijua ili Kinape asionekane kabla ya ndoa yake ili akikutana naye apate cha kudanganya.
BAADA YA MIEZI MITATU

Muda ulipotimu Deus alirudi mjini huku akiacha maandalizi ya harusi yake yakianza taratibu ikiwemo kuwekwa ndani kwa ajili ya mafunzo kabla ya ndoa. Deus baada ya kufika mjini aliendelea na shuhuli zake huku watu wake wa karibu akiwapa majukumu ya kufanikisha harusi yake. Muda ulipotimu Deus alimuoa rasmi Kilole na kuwa mke wake wa kufa na kuzikana. Ndoa yao ilijaa kila aina ya furaha huku Kilole ajilaumu kwa uamuzi wake wa kutaka kuikataa ndoa yake na Deus kwa ajili ya Kinape. Maisha aliyoishi kwa Deus hakuyawaza kuishi siku moja. Kwake aliamini maisha yale ni ya ndotoni kumbe yapo kweli.

KINAPE MJINI

Kinape naye baada ya kuingia mjini akiwa na shauku ya kupata maisha mazuri, lakini haikuwa kama alivyodhani. Maisha yalikuwa magumu sana kiasi cha kujiuliza maisha mazuri watu wanayapata vipi. Alijikuta akifanya kazi ngumu mshahara mdogo uliomtosha kula siku moja tu na siku ya pili alipoamka alianza upya. Alijikuta akiingia katika makundi ya wahuni ili aweze kuihimili kasi ya ugumu wa maisha kwa kulala nje ya soko kuu. Kila siku asubuhi walipo amka na kugombea kushusha mazao yaliyoingia sokoni, wazo la kuendelea kuishi mjini aliliona alifai kutokana na mateso ya kukamatwa na askari kila kukicha. Siku aliyopanga kesho yake arudi kijijini ndiyo usiku uliyokuwa mbaya kwake baada ya msako wa wazurulaji kukamatwa na kufunguliwa mashitaka. Kinape alikosa dhamana na kujikuta akihukumiwa miezi mitatu jela. Maisha aliyoishi gerezani yalimfanya kuuchukia mji. Siku alipotoka hakuwa na hamu ya kukaa mjini alirudi moja kwa moja kijijini kwao, hakutaka kuingia mchana kuhofia kuonekana na watu jinsi alivyo konda na mwili kuwa na upele na ukurutu. Aliingia kwao usiku hakuna aliyemuona. Alipofika wazazi wake walishtuka kumuona mtoto wao amedhoofu mwili. Walitaka kujua nini kimemsibu aliwaeleza: “Wazazi wangu nimekoma, kweli kiburi si maungwana jiji limeninyoosha.” Aliwaeleza yote yaliyomsibu mpaka kuingia gerezani. Wazazi wake hawakuwa na neno zaidi ya kumpokea. “Pole mwenetu hayo ndiyo maisha, tumshukuru Mungu umerudi salama, basi tusaidiane kwenye kilimo.” Kinape baada ya kurudi nyumbani kwao hakutaka kuonekana na mtu, aliishi maisha ya kujificha mpaka atakapopona upele na ukurutu. Hakuwa na hamu tena ya kusikia neno mjini, aliapa kwenda mjini kwa kazi maalumu na si kwenda kubahatisha. Kutokana na hali yake ya kukonda na ukurutu hakutaka kuonana hata na mpenzi Kilole. Alipanga hali yake itakapo imalika afya yake ndipo angeweza kujitokeza hadharani, pamoja na kuwa ndani taarifa za kuolewa kwa Kilole zilimshtua sana. Ili kupata ukweli alimuuliza mdogo wake wa kike. “Eti Eliza Kilole ameolewa kweli?” “Ndiyo kaka.” “Nasikia na rafiki yangu Deus.” “Ndiyo kaka.” “Siamini mpaka niende kwa mama Kilole anieleze ukweli, itakuwaje amuoze Kilolo akiujua ni mchumba wangu.” Kinape alijikuta akitoka ndani japo hali yake ilikuwa haijatengemaa vizuri na kwenda moja kwa moja nyumbani kwao Kilelo kupata ukweli wa kuolewa mpenzi wake ambaye ndiye aliyepanga kuwa mkewe. Njiani alijawa na mawazo juu ya usaliti wa Kilole aliyemuhakikisha kumsubiri mpaka atakaporudi. Alipofika nyumbani kwao Kilole alimkuta mama Kilole akianika mpunga, alipomuona alishtuka kwa mambo mawili. Kwanza kumuona Kinape aliyepotea miezi zaidi ya saba iliyopita, pili hali yake iliyodhoofika. Badala ya kumkaribisha alimshangaa. “Shikamoo mama,” Kinape alianza kumsalimia baada ya kugundua mama Kilole alikuwa akimshangaa. “Kinape!” Badala ya kuitikia alizidi kumshangaa. “Naam mama.” “Ni wewe?” “Ndiyo mama.” “Ulikuwa unaumwa?” “Hapana.” “Nini kimekusibu mwanangu?” “Ni habari ndefu mama.” “Hebu karibu ndani,” aliacha kazi zake na kumkaribisha ndani. Baada ya kuingia ndani alimkaribisha kwenye kigoda. “Karibu.” “Asante mama.” “Haya niambie nini kimekufanya uwe hivi wakati unasema ulikuwa huumwi?” Kinape alimueleza yote yaliyomkuta na kumfanya aishie gerezani badala ya kupata kazi. “Ooh, pole sana mwanangu.” “Asante mama.” “Inaonekana ulipoondoka hukuaga, baba yako kila siku alikuwa akilalamika, safari kubwa kama hizo unatakiwa kupata baraka za wazazi.” “Mama tuachane na hayo, kuna kitu kimoja muhimu ndicho kilichonileta hapa.” “Kipi hicho?” “Kuhusu Kilole.” “Kilole kafanya nini?” “Nasikia ameolewa?” “Ndiyo.” “Nani aliyetoa idhini ya kuolewa?” “Kwa nini unaliza swali kama hilo?” “Mama si unafahamu Kilole ni mchumba wangu?” “Najua.” “Sasa kwa nini mmemuoza kwa Deus?” “Uchumba wako na Kilole tulikuwa tunajua sisi lakini baba yake alikuwa hajui lolote, na penzi lenu lilikuwa la wizi halikuwa wazi.” “Hata hivyo lakini si mnajua mimi na mwanao tulikuwa na marengo gani katika maisha yetu?” “Nimekueleza idhini ya kuolewa kaitoa baba yake siyo mimi.” “Kwa nini hukumwambia amechumbiwa?” “Ningeanzia wapi wakati hatukujua upo wapi, ulikuja kutuaga kuwa unasafiri?” “Sikufanya hivyo, kutokana na dharula iliyojitokeza kwa hilo naomba mnisamehe.” “Sasa kama hivyo hatujui ulikuwa wapi tungeweza vipi kukusubiri mtu tusiyejua upo wapi na utarudi lini. Kuolewa ni bahati tusingeipoteza bahati ile ambayo msichana yoyote kijijini asingekubali kuipoteza” “Sawa, lakini kumbukeni wewe na mwanao mmenifanyia ukatiri mkubwa.” “Utatulaumu bure makosa umeyafanya mwenyewe.” Kinape aliaga na kuondoka huku moyo ukiwa na majonzi ya kuolewa mpenzi wake Kilole mwanamke ambaye aliamini ndiye aliyemuonesha raha ya mapenzi. Lakini hakuwa na jinsi kwa kujua siku zote mwenye kisu kikali ndiye hula nyama.

Itaendelea Jumatano
 
HADITHI : NYUMA YA MACHOZI
SEHEMU: 05
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
“Sasa kama hivyo hatujui ulikuwa wapi tungeweza vipi kukusubiri mtu tusiyejua upo wapi na utarudi lini. Kuolewa ni bahati tusingeipoteza bahati ile ambayo msichana yoyote kijijini asingekubali kuipoteza” “Sawa, lakini kumbukeni wewe na mwanao mmenifanyia ukatiri mkubwa.” “Utatulaumu bure makosa umeyafanya mwenyewe.” Kinape aliaga na kuondoka huku moyo ukiwa na majonzi ya kuolewa mpenzi wake Kilole mwanamke ambaye aliamini ndiye aliyemuonesha raha ya mapenzi. Lakini hakuwa na jinsi kwa kujua siku zote mwenye kisu kikali ndiye hula nyama.
SASA ENDELEA... MIAKA MIWILI BAADAYE Maisha mjini yaliendelea vizuri kwa Kilole kuzidi kupendeza baada ya kupata mtoto wa kike kwenye ndoa yake. Kijijini kwao nako hakukusahau kwa kupeleka misaada ikiwemo kubadili paa la nyasi na kuweka bati. Mabadiliko yale yalifanya mama Kilole aamini kama mwanaye angeolewa na Kinape angempoteza. Maisha ya Kinape aliyajua mwenyewe kazi yake kubwa kijijini ilikuwa kulima shamba la wazazi wake na mashamba ya watu na kulipwa fedha kidogo. Ugumu wa maisha ulimfanya akate tamaa ya maisha na kuamua kuwa mvuta bangi na mlevi wa pombe za kienyeji. Matumizi yale yalimchakaza na kuoneka amechoka kama alirudishwa gerezani, wazazi wake walisikitika kwa hatua aliyofikia. Hata jina lake alilibadili na kujiita Marehemu mtalajiwa kwa vile aliamini kuwa maisha mazuri ni sawa na ngamia kupita katika tundu la sindano yeye ni wa kusubiri kufa. Kama ilivyokuwa kawaida ya Deus kila baada ya miezi sita alikwenda kijijini kuwatembelea wazazi wake, taarifa za kuwepo rafiki yake Kinape zilimfikia. Baada ya kufika kijijini alikwenda moja kwa moja nyumbani kwao na Kinape ili aonane naye, alipofika alimkuta mama Kinape aliyempokea kwa furaha na bashasha. “Karibu mwanangu.” “Asante mama, za hapa?” “Nzuri kiasi.” “Shikamoo.” “Marabaha.” “Unasema kiasi kivipi?” “Ukimuona Kinape utamtambua?” “Kivipi?” “Kinape anajiita Marehemu mtalajiwa.” “Kwa nini?”
”Amekwisha kata tamaa ya maisha.” “Kwa nini?” “Maisha ya kijijini yamekuwa magumu kwake hata huko mjini alikokutegemea anapaogopa kama kuzimu.” “Yupo wapi?” “Akitoka asubuhi kurudi jioni.” “Mmh, sasa sijajua hiyo jioni itakuwa saa ngapi? Maana nategemea kuondoka saa kumi na mbili jioni.” “Baba wala usisumbuke kumsubiri, hiyo jioni bahati lakini muda wake kabisa ni saa mbili usiku akiwa amelewa.” “Sasa mama, nataka kufufua matumaini yaliyopotea ya Kinape.” “Yapi tena hayo baba?” “Nitamchukua, nina imani kwa muda mfupi atakuwa tegemeo la familia.” “Tutashukuru, kwani tumekwisha kata tamaa na kumuachia Mungu.” “Basi mama mwambie jumapili nitamfuata au kama nitakuwa na kazi nyingi nitamtuma mtu amfuate.” “Sijui baba nikushukuru vipi.” “Wala hakuna cha kunishukuru, Kinape ni ndugu yangu wa damu siwezi kukubali kumuona akiadhirika wakati ndugu yake nina uwezo wa kumsaidia.” “Nitashukuru baba,” mama Kinape alisema huku akitaka kupigia magoti, Deus alimuwahi asifanye vile. Waliagana huku akimsisitiza asisahau kumweleza Kinape siku hiyo asitoke, jioni ilipofika Deus alirudi mjini bila kuonana na rafiki yake kipenzi. **** Kinape aliporudi alikuta salamu kwa mama yake. “Kinape, Deus alikuja.” “Shida yake nini?” “Swali gani hilo mwanangu, Deus si rafiki yako?” “Deus si rafiki yangu ni adui yangu namba moja.” “Kwa nini unasema hivyo?” “Atamuoaje Kilole akijua ni mchumba wangu.” “Kinape, maisha yako yanakushinda ungeweza vipi kukaa na mwanamke?” “Hii haikuwa juu yenu.” “Basi kwa taarifa yako huyo adui yako ndiye anayetaka kuyabadili maisha yako kwa kukurudisha mjini.” “Kufanya nini?” “Deus ni mtu mkubwa sana, siku hizi ana gari kama la mbunge, kweli duniani hakuna mtu mwembamba. Deus kanenepa huyo na kitambi juu, kaacha maagizo kuwa jumapili atakufuata uende mjini.” “Ni umaskini ndiyo utakaonifanya niende kwake, lakini niliapa sitamsamehe mpaka nakufa.” “Lakini unamlaumu bure, nina imani alikuwa hajui, kama angejua sidhani angekubali kumuoa Kilole.” “Kwa nini hakuuliza kabla ya kuoa?” “Ni wazi alifichwa.” “Kama ni hivyo familia ya kina Kilole kimenitendea unyama.” “Kwa hiyo mwanangu nakuomba usiipoteze nafasi hii, nina imani ndoto zako huenda zikatimia.” “Sawa mama nitajiandaa na safari.” “Basi acha kunywa mipombe yako ili kidogo mwili upendeze kwa siku mbili” “Nitafanya hivyo mama.” ******* Siku ya jumapili Kinape alijiandaa na safari ya kwenda mjini kwa ajili ya safari. Saa nne asubuhi gari aina ya Toyota land cruser Vx ilisimama mbele ya nyumba ya mzee Solomoni baba yake Kinape. Kinape alikuwa wa kwanza kutoka nje ili aonane na rafiki yake kipenzi Deusi. Baada ya mlango kufunguliwa, kwanza kuteremka alikuwa Salome mdogo wake Deus, alipomuona tu alipaza sauti: “Kaka Kinape mwenyewe huyo hapo,” alisema huku akigeuza shingo kumuangalia mtu aliyefuatana naye. Alikuwa kijana mmoja mtanashati alisogea hadi alipokuwa amesimama Kinape. “Habari ndugu?” “Nzuri tu, karibu.” “Nina imani wewe ndiye Kinape?” “Hujakosea ndiyo mimi.”
”Vipi wazazi wamo ndani?” “Yupo mama, baba ametoka kidogo.” “Naomba nionane naye.” “Karibu kwenye kigoda nimwite,” Kinape alimkaribisha mgeni kwenye kigoda kisha aliingia ndani kumwita mama yake. Baada ya muda mama Kinape alitoka alipomuona mgeni alimkaribisha. “Karibu baba.” “Asante, shikamoo mama. “ “Marahaba, karibu.” “Asante, mama mimi si mkaaji nimetumwa hapa na brother Deus nimfuate Kinape.” “Hakuna tatizo baba, ndugu yenu mwenyewe huyo hapo.” “Nashukuru nilipofika tu Salome kanionesha, kwa hiyo nilikuwa naomba ruhusa niwahi kuondoka.” “Hakuna tatizo hata yeye mwenyewe amekwisha jiandaa” “Basi tunaweza kwenda.” Kabla ya kuondoka mama Kinape alimwita ndani mwanaye na kumpa maneno ya mwisho. “Kinape mwanangu najua wazi ulikuwa na urafiki wa karibu na Kilole, nakuomba chondechonde achana naye, fuata kilichokupeleka. Kumbuka kosa lako moja linaweza kuwa majuto ya milele. Muogope Kilole kama ukoma muone ni shemeji yako.” “Sawa mama nimekuelewa.” Kinape na Dereva aliyetumwaamfuate aliongozana hadi kwenye gari na kuondoka pamoja. ****** Dereva aliyemfuata Kinape alimjulisha Deus kuwa wamekaribia nyumbani, Deus alimjulisha tayari yupo nyumbani kwa ajili ya kumsubiri mgeni. Sauti ya gari ilimfanya Deus asogee mlangoni kusubiri kumpokea rafiki yake kipenzi waliopotezana muda mrefu. Gari liliposimama dereva alimfungulia mlango Kinape ambaye aliteremka kwenye gari, Deus alipomuona akipaza sauti huku akitoka mbio kwenda kumpokea rafiki yake kwa kumwita jina alilolizoea. “Keiii Piii.” “Dewuuuu.” Wote walikutana na kukumbatiana kwa furaha. “Ooh, karibu sana rafiki yangu.” “Asante nimekaribia” Walishikana mikono na kuiingia ndani pamoja, wakati wanaingia Kilole alikuwa anatoka kwenye friji kuchukua juisi ya mtoto. Macho yake yalipatwa na mshtuko baada ya kumuona Kinape ndani ya nyumba yake mwanaume aliyemkimbia na hakutaka hata siku moja aonane naye na kujibu maswali ambayo aliaminbi kwake ni magumu. Kinape hakushtuka sana kwa vile alijua Kilole yupo wapi na ni mke wa mtu, Kilole glasi ya juisi ilimponyoka na kuanguka chini. “Mke wangu vipi mbona hivyo?” “Ha..ha..pana.” “Kinape, karibu sana hapa ndipo ninapoishi.” “Asante kupafahamu.” “Nina imani nilikueleza tutakuwa na ugeni, naomba basi apatiwe huduma zote muhimu kisha aoneshwe chumba chake,” Deusi alimwambia mkewe. “Ha..ha..kuna ta..ta..tizo.” Kilole alisahau kuokota glasi iliyoangukia juu ya zuria, aligeuka na kuelekea chumba cha mgeni kuangalia kama matayarisho ya mwisho kabla ya kumkaribisha chumba mgeni. Alijikuta akikosa raha kwa kitendo cha mumewe kumwingiza ndani ya nyumba yake mwanaume ambaye lazima atataka majibu ya usaliti wa ahadi yao. Alijikuta akimlaumu mumewe kwa kitendo cha kutomjulisha ni mgeni gani anayekuja. Kwa upande wa Kinape alibakia na siri moyoni hakutaka kumueleza rafiki yake uhusiano wake na Kilole. Pia alikumbuka wosia wa mama yake juu ya kuwa karibu na mke wa mtu japo alikuwa mpenzi wake. ******* Baada ya Kinape kuoga na kubadili nguo Deus alimtambulisha rasmi rafiki yake kwa mkewe Kilole. “Mke wangu, huyu ni rafiki yangu kipenzi Kinape nina imani si mgeni kwako.” “Ni kweli, lakini sikuwa na mazoea naye,” Kilole alimjibu mumewe akiwa ameangalia chini. “Kinape huyu ndiye mke wangu Kilole ambaye ni shemeji yako.” “Nashukuru kumfahamu shemeji.” “Mke wangu, Kinape atakuwepo hapa kwa muda mpaka nitakapomtafutia kazi na yeye kuanza maisha yake.” “Hakuna tatizo, karibu shemeji,” Kilole alimkaribisha Kinape kwa sauti ya chini. Baada ya utambulisho ule, Deus na Kinape walizungumza mengi wakikumbushia mambo ya miaka mingi. Deus alikuwa na furaha tofauti na Kinape aliyejifikiria atatazamana vipi na Kilole mwanamke aliyemsaliti. Usiku ulipoingia waliagana kuonana kesho asubuhi. Chumbani aliyelala usingizi uzuri alikuwa Deus peke yake lakini Kinape na Kilole kila mmoja aliwaza lake. Kilole aliamini kabisa kuolewa na Deus kumeweza kuyabadili maisha yake, alijiuliza kama Kinape ameletwa na mumewe ili amsaidie, angeweza vipi kumtimizia mahitaji yake muhimu. Aliamini Kinape pamoja na kuahidiana kuoana angempotezea muda tu na si kumtengenezea maisha yake. Alijikuta akiondoa hofu moyoni na kuwa tayari kukabiliana na maswali atakayo ulizwa na Kinape. Naye Kinape alijikuta akiumia kwa usaliti wa mpenzi wake wa kuolewa na mtu mwingine. Kilichomuuma sana kilikuwa kuolewa na mtu wa karibu na kibaya zaidi kukaa nyumba moja huku wote wakilishwa na mtu mmoja. Siku ya pili Deus baada ya kujiandaa kwenda kazini alimfuata rafiki yake Kinape chumbani kwake kumuaga. “Best mimi nawahi kazini tutaonana jioni.” “Hakuna tatizo.” “Kila kitu nimemuachia maagizo shemeji yako, nakuomba uwe huru au siyo Keiiii Piii,” Deus alikumbushia enzi zao. ‘Hakuna tatizo Dewuuuu.” Walicheka pamoja na kuagana Deus alitoka chumbani kwa Kinape na kumpitia mkewe aliyembusu kisha walisindikizana hadi kwenye gari. “Bai Bebi.” “Bai honey safari njema, kazi njema.” “Asante mke wangu.” Deus aliondoka na kumwacha mkewe akimsindikiza kwa macho mpaka alipopotea ndipo alipogeuka kurudi ndani. Alirudi taratibu huku akiwa na mawazo mengi juu ya kuwepo Kinape pale, hakutaka hata siku moja katika maisha yake baada ya kuolewa na mtu mwingine kwa kuvunja ahadi yao asikae karibu na Kinape.
Itaendelea Ijumaa
 
Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi @Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad @Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya Lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO @multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij adden@bwii ONTARIO Kobe The Vein mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya SITAKI ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo @shedede kamtu33 SteveMollel Ngushi DONALD stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 Ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny @Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush mossad 03 white wizard xtaper Mzigua90 Ollachuga Oc Gidbang Mateja M.G Yango jipu abaa4all DIBAJI Agenda1 Grahnman The MaskmaN Slim5 Xubzero agprogrammer JoJiPoJi @Architectus blance86 Mamtolo monde arabe Ngao Ya Imani stardust JK naiman64 Dharra seledunga ABB SHAMMA Richard Waziri wa Kaskazini Mwinjuma1 Kanungila Karim baracuda Mwamba028 besaro Pyepyepye Bilionea Asigwa ibn Kiti Chema Tugas Royal Warrior mederii mmangO manzi james LIKUD adrenaline Royal Son Mhadzabe salaniatz Natasha Ismail jiwe jeusi chibalangunamchezo
John Mloy conjuget Van Pauser great G Mtoto wa nzi Zeus1 hindustan Sci-Fi MAN OF PEACE kashata emnly danny baraka bb MTOTELA kbosho TEMLO DA VINCA Khantwe
 
HADITHI : NYUMA YA MACHOZI
SEHEMU: 06
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.
...ILIPOISHIA:
Deus aliondoka na kumwacha mkewe akimsindikiza kwa macho mpaka alipopotea ndipo alipogeuka kurudi ndani. Alirudi taratibu huku akiwa na mawazo mengi juu ya kuwepo Kinape pale, hakutaka hata siku moja katika maisha yake baada ya kuolewa na mtu mwingine kwa kuvunja ahadi yao asikae karibu na Kinape.
SASA ENDELEA...
Kilole hata alipokwenda kijijini baada ya ndoa hakutaka kuonana na Kinape, aliingia kimya kimya mpaka anaondoka Kinape hakujua. Alijiuliza akimtaka mumewe amuondoe Kinape na kumtafutia sehemu nyingine atamuelewa. Jambo lingine alilojifikiria lilikuwa kama hilo litashindikana basi atatafuta mbinu nyingine kuhakikisha anauvunja urafiki wa Deus na Kinape. Baada ya kuingia ndani alifanya usafi wote muhimu, akiwa jikoni akiandaa kifungua kinywa, Kinape aliamka na kwenda hadi sebuleni. Sebule ilikuwa tupu ila runinga ilikuwa wazi, alikaa kwenye sofa viti ambavyo toka azaliwe hakuwahi kukalia. Taratibu alitembeza macho kuangalia uzuri wa nyumba ambayo ilikuwa na kila kitu, akiwa bado anashangaa alisikia sauti ya vyombo. Aliamini Kilole anaosha vyombo, alinyanyuka na kuelekea jikoni. Alimkuta akikaanga mayai huku amempa mgongo, alimsogelea taratibu bila kumshtua alipomkaribia alimsalimia. “Za asubuhi shemeji,” sauti ile ilimshtua sana Kilole na kumfanya ashike mkono kifuani. “Kilole usishtuke maji yamekwisha mwagika jione huru,” Kinape alimtoa hofu. “Sio hivyo Kinape ni wazazi si mimi,” Kilole alijitetea. “Najua, ndiyo maana nikasema jisikie huru, tupo sehemu ya watu tusije kosa mwana na maji ya moto.” “Nisamehe Kinape bado nakupenda nipo hapa kwa shinikizo, lakini mimi nilikuwa radhi kukusubiri mpaka atakaporudi,” Kilole alijikuta akiomba msamaha huku akibubujikwa machozi ya aibu. “Si kweli Kilole, kwa nini hukuwaeleza ukweli, ina maana mama yako hajui uhusiano wetu. Au ndiyo sababu ya pesa?” “Mama alikuwa anajua lakini alimuogopa baba ambaye hakuujua uhusiano wetu.” “Kilole muongo, baba yake alitufuma mara ngapi asijue?” “Kama alikuona alijua ni mzowezi si muoaji.” “Si kweli kwa nini hukumwambia kuwa mimi ndiye mumeo mtarajiwa au kwa vile sina kitu. Kumbuka Kilole mateso yote niliyoyapata mjini ni kwa ajili yako, nimefungwa kwa ajili yako kutafuta maisha mazuri ili tuje tuishi maisha mazuri. Lakini mwisho wa siku umeamua kunisaliti.” “Niamini Kinape si mimi ni wazazi wangu.” “Kwa nini hukukataa?” “Nilik...,” Kilole alinyamaza baada ya kusikia sauti ya gari, kweli alikuwa mumewe amerudi mara moja. Aliingia ndani haraka na kukutana na Kinape anatoka jikoni, alishtuka kumuona Kinape akitokwa na machozi. Hakumuuliza kitu alikwenda moja kwa moja jikoni, alishtuka kumkuta mkewe anafuta machozi alishtuka sana na kuhoji. “Vipi mbona mnalia, kuna usalama?” Kilole alishtushwa na swali la mume wake na kujilaumu kusahau kufuta machozi. “Mke wangu kuna nini mbona wote mnalia?” Kilole alikosa jibu la kumjibu mumewe alibakia ameinama huku akijiuliza mumewe kama atajua kuwa alikuwa na mahusiano na Kinape ndoa yake itakuwa hatiani. Alitamani kuomba radhi na kumweleza ukweli juu ya uhusiano wake na Kinape na kumhakikishia hawezi tena kuwa na uhusiano naye. Deus bado alikuwa yupo kwenye kizungumkuti asijue nini kimetokea muda mfupi baada ya kuondoka kwenda kazini na kumuacha Kinape amelala na mkewe akirudi ndani. Lakini amerudi na kukuta mabadiliko na mkewe kushindwa kumjibu. “Mke wangu kuna habari za msiba?” “Hapana.” “Sasa kuna nini?” Kilole aliendelea kukosa jibu kwa mumewe, Deus alimwacha mkewe jikoni na kumfuata Kinape aliyekuwa amesimama sebuleni akifuatilia jibu la Kilole ambalo alijua linaweza kuharibu ndoto yake kwa mara ya pili. “Kinape.” “Naam.” “Kuna nini mbona mnaniacha njia panda kuna kitu gani kimetokea muda mfupi baada ya kuondoka?” “Ni jambo la kijijini.” “Jambo gani lililowatoeni machozi?” “Ni kweli, sikutegemea shemeji kuniuliza swali kama lile.” “Swali gani?” Kilole mapigo ya moyo yalimwenda mbio miguu ilianza kumwisha nguvu kwa kuamini kosa moja la Kinape litayagharimu maisha yake yote. Alitamani kumuomba Kinape asiseme ukweli ambao ungemgharimu maisha yake. Alipotaka kumuomba Kinape anyamaze ili akayazungumze na mumewe ndani mdomo ulikuwa mizito alibakia akimuomba Mungu amuepushe na balaa lile. “Shemeji aliniulizia habari za rafiki yake kijijini.” “Sasa habari za rafiki yake na machozi yenu yanahusiana vipi?” Swali lile lilizidi kumuweka katika hali mbaya Kilole kwa kujiuliza yeye alimuuliza swali gani kuhusu rafiki yake lililosababisha watokwe na machozi. “Aliniulizia shoga yake aliyesoma naye ambaye alikuwa rafiki yangu wa kike, mwezi jana tumemzika baada ya kufa kwa uzazi. Kwa kweli kwangu ilikuwa sawa na kutonesha kidonda kilichoanza kupona, nilipomweleza habari zile shemeji alianza kulia kitu kilichonikumbusha maumivu ya moyo ya kumpoteza kipenzi changu aliyekufa na kiumbe changu tumboni.” “Ooh! Poleni sana, sikujua rafiki yangu kama ulipata msiba mzito kiasi hicho, Mungu atakulipia hiyo yote ni mitihani ya maisha.” Deus alimvutia kifuani rafiki yake na kumpigapiga taratibu huku akiendelea kumfariji. “Pole sana rafiki yangu Mungu atakulipia mara mbili.” “Asante.” Alimwacha Kinape na kwenda kumkumbatia mkewe aliyekuwa bado akitokwa na machozi ya hofu. “Pole mke wangu kwa kuondokewa na rafiki yako kipenzi.” “Asante mume wangu.” “Nakuombeni msahau yaliyopita kwani kuendelea kuumia ni kuingilia kazi ya Mungu na kuona kama mmeonewa lakini kumbe hiyo ni njia yetu sote tatizo kutangulia.” “Tumekuelewa, kwangu ulikuwa mshtuko ambao sikuutegemea,” Kilole alijikuta akipata nguvu za kuongeza uongo baada ya Kinape kumuokoa kwenye swali lililokuwa kama kaa la moto mdomoni mwake. “Basi jamani mimi si mkaaji nimerudia flash disic yangu niliisahau juu ya droo ya kitanda.” Deus alielekea chumbani na kumuacha mkewe akiwa bado amesimama, Kilole naye aliamua kumfuata mumewe chumbani. Alipofika alimkumbatia kwa nyuma na kusema kwa sauti ya chini. “Samahani sweet.” “Samahani ya nini tena mpenzi?” “Kwa hali uliyonikuta nayo, sikupenda upatwe na mshtuko kama ule.” “Aah, kumbe hilo mbona la kawaida, si ujajua nakupenda kiasi gani, sipendi kukuona kwenye matatizo, heri niteseke mimi si wewe kipenzi changu.” “Najua, ndiyo maana nikakuomba samahani mpenzi wangu, hata mimi sitaki nikuone unaumia kwa ajili yangu.” “Nashukuru kwa kulifahamu hilo.” “Basi mpenzi nisikucheleweshe, mke mwema ni yule anayemhimiza mumewe katika kazi zake na si yule anayemuacha akiharibikiwa.” “Asante sana mke wangu, lazima nimshukuru Mungu kunipa mke mwema.” Baada ya kuchukua Flash disc Deus alimuaga tena mkewe na kuwahi ofisini. ******** Baada ya kuondoka Kilole alishindwa amshukuru vipi Kinape kwa kumuokoa kwa mumewe kwa kuamini kama angejibu yeye lazima angejichanganya. Wakiwa wanapata kifungua kinywa, Kilole alimshukuru Kinape. “Kinape sikuwezi wewe kiboko sikutegemea ungejibu vile.” “Hiyo mbona kazi ndogo hata kama angenifumania natoka chumbani kwako bado ningeweza kujitetea na yeye angekubali kwa kukiamini nitakacho mweleza.” “Basi nilikuwa na wasiwasi na kujua talaka ipo usoni mwangu.” “Kama nilivyokueleza maji yameisha mwagika hayawezi kuzoleka.” “Usiseme hivyo Kinape, sipendi uumie kiasi hicho.” “Nimeishaumia kinachotakiwa kutuliza maumivu.” “Nitakusaidia kuhakikisha maisha yako yanakuwa mazuri.” “Sawa, lakini naomba tuishi kama mtu na shemeji yake tuondoe mazoea ya karibu yatakayo muondoa wasiwasi mumeo.” “Nashukuru Kinape kuwa muelewa, nakuhakikishia kuyasahau mateso yote ya kijijini na kuyaanza maisha mapya.” MWAKA MMOJA BAADAYE Maisha ya Kinape yalibadilika kutokana na kazi aliyokuwa akifanya, hata hali ya mwili ilikuwa ya mvuto kutokana na maisha aliyokuwa akiishi. Kilole alijikuta akivutiwa na Kinape kila alipopita au alipokuwa amekaa alimwangalia sana. Tofauti ya Deus na Kinape ilikuwa katika mavazi, Deus siku zote alivaa nguo za heshima muda wote tofauti na Kinape alivaa nguo zinazokwenda na wakati kama jeans tisheti na raba za bei mbaya kutokana na pesa aliyokuwa akipata. Kinape alijipenda kwa kujipulizia manukato ya bei mbaya kifuani alikuwa na mkufu mkubwa wa dhahabu. Kila mwanamke alitaka awe wake, lakini alichagua msichana mmoja ambaye aliamini ndiye anayefaa kuwa mkewe baada ya kila kitu kwenda vizuri. Hakuisahau familia yake kitu ambacho siku zote alisisitizwa na rafiki yake ahakikishe kipato anachokipata aikumbuke familia yake kijijini pamoja na kufanya marekebisha ya makazi ya wazazi wake. Kinape alikuwa makini sana katika maisha yake hakutaka mchezo kabisa. Mvuto wake machoni kwa wanawake ulikuwa mateso mazito kwa Kilole na kujikuta akimuona Kinape kama mwanaume pekee mwenye mvuto na uwezo wa kitandani tofauti na Deus, ambaye hakuwa mtundu sana kitandani zaidi ya upendo wa dhati. Kilole alijiuliza atawezaje kumsogeza karibu Kinape ambaye tayari ameisha jitangaza kuwa ana rafiki wa kike ambaye wakati wowote atatambulishwa kwao. Kila alipokuwa Kinape peke yake alitamani kuzungumza naye ili kumweleza jinsi gani anavyoteseka juu yake. Japo hakutaka kuachana na mumewe lakini shida yake wawe karibu ili kukumbushia mapenzi yao ya zamani ambayo aliamini hakuna mwanaume mwingine wenye kumpa raha kama Kinape.
Itaendelea Jumatatu
 
HADITHI : NYUMA YA MACHOZI
SEHEMU: 07
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
Kilole alijiuliza atawezaje kumsogeza karibu Kinape ambaye tayari ameisha jitangaza kuwa ana rafiki wa kike ambaye wakati wowote atatambulishwa kwao. Kila alipokuwa Kinape peke yake alitamani kuzungumza naye ili kumweleza jinsi gani anavyoteseka juu yake. Japo hakutaka kuachana na mumewe lakini shida yake wawe karibu ili kukumbushia mapenzi yao ya zamani ambayo aliamini hakuna mwanaume mwingine wenye kumpa raha kama Kinape.
SASA ENDELEA...
Wakati huo Deus mambo yake yalizidi kuwa mazuri kutokana na kuingiza kipato kikubwa kutokana na takrima ya kazi yake. Aliweza kumpa siri nyingi rafiki yake kipenzi jinsi anavyoweza kupata pesa nyingi nje ya kipato chake cha kawaida. Deus alijikuta akimuamini sana Kinape kwa kumweleza mambo mengi kuhusu uwezo wake wa kipesa na madaraka yake kazini. “Kinape nipo kwenye kitengo cha hatari sana ukiwa mnoko huchelewi kufa, hivyo inabidi uume na kupuliza. Kitengo cha kudhibiti madawa ya kulevya ni kitengo hatari sana vigogo ndiyo wahusika wakuu kama utakamata mizigo yao huchelewi kuhamishwa au kutengenezewa zengwe litakalo kulaza pabaya hata kukumaliza kabisa.” “Kwa hiyo vigogo hawakamatwi?” Kinape alimuuliza Deus. “Utaanzia wapi, nyuma yako kuna wakubwa wanakula kupitia mgongo huo huo, sasa wewe jitie kiherehere.” “Kwa hiyo matumizi ya dawa ya kulevya kwisha ni vigumu?” “Ni vigumu lazima tuseme ukweli.” “Sasa kitengo hicho kazi yake nini?” “Kudhibiti dawa za kulevya.” “Lakini mbona wengine mnawakamata?” “Hao ukiona hivyo hawana mikono ya wakubwa.” “Kwa hiyo unapata posho nene toka kwa hao vigogo?” “Kweli rafiki yangu, nisingeweza kuwa vitu hivi kwa muda mfupi.” “Alafu unafahamika sana na watu wazito, huwezi kuamini siku ile uliponituma niende kwenye kampuni ile nilipokelewa kama mfalme. Nje niliacha watu wakisota kuomba kazi hata jioni baada ya kazi nilipewa gari la kunirudisha nyumbani, wote pale wanajua Paroko ni ndugu yangu wa damu.” “Hao ndio watu tunaokula nao mjini, waswahili wanasema sema na watu uvae viatu.” ******* Wakati Deus akiuweka wazi uwezo wake wa pesa na njia zinazoingilia, Kilole alikuwa katika wakati mgumu kuhakikisha Kinape kabla ya kuhama mule ndani basi awe ameisha mrudisha katika himaya yake. Siku moja Deus alisafiri kikazi na kuwaacha ndani ya nyumba mkewe, Kinape na mfanyakazi wa ndani. Kilole aliamini ile ni nafasi pekee ya kumsogeza Kinape karibu, Lakini siku hiyo jioni ilikuwa chungu kwa Kilole baada ya Kinape kuja na mpenzi wake nyumbani kumtambulisha. Roho ilimuuma kwa kuamini Kinape amefanya vile ili kumlingishia yeye, alipofika na rafiki yake wa kike Kinape alimtambulisha kwa Kilole. “Shemu huyu ndiye ubavu wangu kama nilivyowataarifu, nilipanga leo awakute wote, lakini kwa vile Swahibu amesafiri nimeonelea si vibaya hata wewe kuwa muwakilishi hata siku akija asionekane mgeni.” “Karibu sana mgeni,” alimkaribisha kinafiki lakini moyoni alikuwa na donge zito. “Asante nimekaribia,” mgeni alijibu huku akijilaza kwenye kifua cha Kinape kama katumwa. “Shemu usione Kinape natakata sababu ya mtoto huyu, kwao wamemlea akalelewa, sifa ziende kwa wazazi wake.” “Mmmh! Kama hivyo hongera.” Siku ile walishinda pale na jioni alimsindikiza nyumbani kwao, aliporudi alimkuta Kilole hayupo katika hali ya kawaida kitu kilichomshtua Kinape. “Vipi shemu mbona upo hivyo, maana naona ghafla umekosa raha au unamkumbuka mzee mbona ni leo tu?” “Kwanza Kinape jina hilo unaloniita silipendi sema hujui tu.” “Jina gani?” “La shemeji.” “Aah, sasa wewe ni nani kama siyo shemeji yangu.” “Niite mpenzi au jina langu.” “Eti?” Kinape alishtuka. “Umesikia sana napenda uniite mpenzi mahawala hawaachani.” “Lakini kwangu wanaachana.” “Kinape kumbuka bado nakupenda.” “Hata mimi nakupenda,” Kinape alimjibu Kilole. “Sasa kwa nini unanionesha mwanamke wako mbele yangu?” “Jamani kuna ubaya gani nami kuwa na wangu mbona mimi sijakuzuia kunionesha kuwa ni mke wa Deus?” “Kinape sikia, kama nilivyokueleza kuwa mimi nilikubali kuolewa kwa shinikizo, lakini nakuhakikishia bado nakupenda na upendo wangu hautakufa milele.” “Sawa, sikatai lakini sasa hivi nitaendelea kukuheshimu kama shemeji yangu na si mpenzi wangu.” “Hilo najua endelea kuniheshimu kama shemeji yako, lakini Deus akiwa mbali utabaki kuwa mpenzi wangu. Nitahakikisha kutokana na uwezo wa mume wangu kukuwezesha kipesa kisha nitaachana naye ili tuishi pamoja.” “Kilole hilo halitawezekana hata siku moja,” Kinape alimjibu huku akimkazia macho. “Litawezekana, kwa vile wewe ndiye mwanaume aliye moyoni mwangu, hakuna mwingine zaidi yako.” “Kilole siwezi kumtendea unyama rafiki yangu kwa ajili ya tamaa zako za mwili, pia siwezi kukorofishana na rafiki yangu kwa ajili yako, sitaki nionekane mwizi wa fadhira kukosa nuksani kwa ajili ya starehe za muda.” “Kama hutaki tumfanye hivyo basi tufanye penzi la siri.” “Kilole hakuna siri katika mapenzi.”
“Lipo kama wenyewe tukiitunza siri hiyo.” “Haitawezekana, Kilole mshukuru Mungu kwa kukupa mume wenye uwezo pia mwenye mapenzi ya dhati na wewe. Kwa nini unataka kuichezea shilingi kwenye tundu la choo?” “Kumbuka wewe ndiye uliyenionjesha tamu ya dunia.” “Ni kweli, lakini kisicho riziki hakiliki, haukuwa riziki yangu ndiyo maana ameolewa na mwingine.” “Kama ulijua hivyo mbona ulinilaumu?” “Nilikulaumu kwa haki kwa vile ulivunja ahadi yetu, lakini uliponieleza umeozwa kwa shinikizo la wazazi wako nilikuelewa.” “Kinape nimekubali, basi naomba kwa leo tu ili nipoze machungu ya moyo wangu, usiponipa nitateseka na nitakuwa radhi kuachika na kurudi nyumbani.” “Kilole kwa nini hukusema mapema mpaka umesikia nina mwanamke ndiyo yazuke haya?” “Nilikuwa natafuta nafasi ili nikueleze, kumtambulisha mpenzio ilikuwa kama kuniwahi kuzieleza hisia zangu.” “Nimekuelewa, lakini nakuomba chonde heshimu ndoa yako, kumbuka bomu unalotaka kulitega litatusambaratisha na kijiji tutashindwa kurudi.” “Kinape nakuhakikishia hata Deus akijua hawezi kufanya lolote kwa vile nina siri zake nyingi chafu.” “Lakini kipi unachokikosa kwa mumeo?” “Mapenzi yako, ilinionjesha sasa hivi siyapati.” “Kilole bora lawama kuliko fedheha, nakuhakikishia siwezi kushea mapenzi na rafiki yangu na ukizidi kunilazimisha nitahama hapa. Kuanzia leo nione kama mbingu na ardhi,” Kinape alisema kwa kujiamini bila mzaha. “Wapii? Kinape nakuhakikishia lazima utakuwa mpenzi wangu.” “Labda kwa nguvu za giza.” “Walaa, situmii mizizi wala hirizi wenye hila ni wanawake bwana.” “Tutaona, na sasa naomba unione kama kituo cha polisi kwa muuza unga, Kilole nimeteseka sana kutafuta maisha, mwanga unaonekana unataka kunipeleka wapi, nitawaeleza nini wazazi wangu.” “Wee, maliza yote lakini mwisho wa siku utabakia kuwa mpenzi wangu, kumbuka wewe ndiye uliyenirubuni na kupoteza sifa za usichana wangu, leo hii eti nikuone kama kituo cha polisi na mvuta bangi. Kwa taarifa yako mimi nakuona kama jalala na siku zote ndilo kimbilio la mimi nzi.” “Haya tutaona.” “Si upo, ipo siku utakubaliana na mimi ninachokisema, haiwezekani nitunze mimi wengine wafaidi utamu. Kumbuka Kinape nimekuwa na wewe katika mazingira magumu na uliniahidi ipo siku nitafaidi raha. Leo hii umepata unanikataa.” “Sijakukataa, sasa hivi wewe ni mke wa mtu kuwa muelewa.” “Kwa hili siwezi kukuelewa mpaka naingia kaburini nakuapia ukinikataa nitajiua.” “Umefika mbali, lakini mbona una maisha mazuri mumeo anakuhudumia kila kitu kwa nini unataka kulipiga teke fuko la pesa.” “Kama unataka suruhu tufanye penzi la siri, nakuhakikishia kumheshimu mume wangu wala sitamdharau.” “Kilole najua hutanielewa nakuomba umkemee shetani wa uzinzi.” “Kinape uniniambia hivyo? Leo hii unajua kukutamani ni kuwa na shetani wa uzinzi kama ungejua hivyo usingenihalibia usichana wangu kumbuka nilikueleza mpaka utakaponioa au zawadi kwa mwanaume yeyote atakayenioa. Lakini ulinidanganya kuwa utanioa mbona hukunioa?” Kilole alizugumza huku akilia kwa hasira. “Kilole naomba unisikilize tena unisikilize kwa makini, kabla ya kuja mama yangu alilijua hili na kunieleza nisiwe na wewe karibu hivi akisikia nimefukuzwa na Deus kwa sababu yako nitakuwa mgeni wa nani. Kumbuka sasa hivi wazazi wangu wanaishi maisha ya raha kwa ajili ya Deus huoni kujiingiza katika mapenzi na wewe itakuwa sawa kukata tawi nililokalia?” “Kinape usiwe mwingi wa nahau, Deus hajui lolote kuhusu uhusiano wetu kwa hiyo itatupa nafasi ya kufanya mambo yetu kwa siri bila kujua.” “Kilole narudia tena sitafanya na wala sitegemei kufanya tuheshimiane na kuanzia leo humu ndani nahama nitakuja akiwepo Deus tu.” “Na akikuuliza kwa nini umehama utamjibu nini?” “Nitajua nitakacho mjibu lakini hakitahusiana na wewe.” “Kinape naomba uje unizike, ukiondoka jiandae kusikia msiba wangu.” “Kwa hilo sitakutenga nitahudhuria mazishi yako.” “Yaani upo tayari nife unaniona?” “Kwa hili nipo radhi ufe, nina imani hata bila kuwa na mimi bado utaendelea kufurahia maisha. Kusema utajiua kwa ajili yangu ni uongo mkubwa, kama ungekuwa na mapenzi na mimi usingeolewa.” “Nikueleze mara ngapi nililazimishwa lakini mapenzi yangu yote kwako.” “Nimekuelewa, basi endelea na mumeo.” “Upo tayari nife?” “Kwa hili nipo tayari, sipo tayari kujigeuza nyoka mdogo nimekuwa nammeza mfugaji kwa ajili ya tamaa zako za mwili.” “Kinape nimekuelewa, ila nakuomba kitu kimoja endelea kuniita shemeji na mimi nitakuheshimu kama rafiki ya mume wangu. Nakuahidi sitakutamkia tena maneno ya mapenzi. Nakuomba unisamehe kwa yote yaliyojitokeza, nina imani ukiondoka lazima siri itavuja naweza kukosa Bara na Pwani. “Kinape nisamehe sana, ni mapenzi mazito kwako, lakini nakuhakikishia nitarudia tena nisamehe sana,” Kilole alisema kwa sauti iliyoambatana na kilio. “Nimekusamehe Kilole, tuiheshimu safina hii tunayosafiri pamoja, lolote baya tukilitenda itakuwa sawa na kuitoboa kwenye kina kirefu tutazama wote.” “Nimekuelewa Kinape, nakuomba unisamehe sana.” “Nimekusamehe, asante kwa kunielewa.” Walikubaliana kuendelea na taratibu zilizokuwepo za kuheshimiana kama mtu na shemeji yake na si wapenzi. Kilole baada ya kugonga mwamba alikuwa na mpango mzito moyoni mwake wa kikakikisha anampata Kinape bila mwenyewe kujua. Wakiwa katikati ya mazungumzo simu ya Kinape iliita, alipoangalia aliona ni ya mpenzi wake. “Haloo sweet.” “Haloo darling.” “Niambie mpenzi wangu.” “Vipi upo tayari?” “Ooh, sorry nilikuwa na mazungumzo na shemeji kidogo yamechukua muda ngoja nijimwagie maji.” “Fanya haraka nakuja sasa hivi.” Baada ya kusema vile alielekea chumbani kwake kubadili nguo akaoge ili atoke na mpenzi wake. Usiku wa siku ile walipanga kwenda kwenye kumbi za starehe, Kinape toka awe na mpenzi wake mpya amekuwa akionjeshwa raha za duniani ambazo hakuwahi kuziota. Alipokuwa akielekea chumbani kwake, Kilole alimsindikiza kwa macho huku moyoni akisema “nitakomesha jeuri yake.” Akiwa bado yupo katika hali ya uvivu kutokana na maneno ya Kinape yaliyomkata maini. Alishtushwa na sauti ya Happy mpenzi wa Kinape akiwa katika vazi la kutokea jioni. “Aah, dada kumbe upo sebuleni, ina maana husikii hodi yangu?” “Aah! Kumbe ni wewe nilikuwa mbali kimawazo.” “Dada, shemeji kuondoka asubuhi tu umekuwa hivyo, je, akimaliza wiki?” “Wee acha mdogo wangu, nawe utaolewa utayaona.” “Ahaa! Umeishafika?” Kinape alisema akiwa anatoka bafuni. “Niliona unachelewa nikaamua nikufuate, si unajua mtu chake.” “Na kweli mdogo wangu,” Kilole alijibu huku roho ikimuuma. “Hongera umependeza,” Kinape alimsifia Happy. “Nawe nataka upendeze kama mimi, vaa nguo nilizokununulia.” “Hakuna tatizo dear nipe nusu dakika.” “Aah, wapi nakuja huko huko.” Waliongozana wote hadi chumbani huku Happy akiwa amemkumbatia Kinape. Kilole alijua Kinape amefanya vile kumuumiza roho, lakini aliapa kumshikisha adabu huku akipanga mpango kabambe wa kusambaratisha penzi lile. Baada ya muda walitoka wakiwa wameongozana katika mtembeo wa mapenzi mazito. Kilole aliwasindikiza kwa macho huku roho ikizidi kumuuma jinsi walivyopendana. Alijua maisha yale hakuna sehemu ya kuyapata zaidi ya kuwa na Kinape. Toka aolewe na Deus hakuwahi kwenda sehemu za starehe zaidi ya kwenda kwenye dhifa ya kiserikali. Lakini mashoga zake walimweleza raha wanazozipata wanapokwenda kwenye kumbi za starehe hata kwenye vikundi vya taarabu. Moyoni alijisemea: Leo mjanja lakini ipo siku utanijua mimi na yeye nani zaidi.”

Itaendelea Jumatano
 
SEHEMU: 08
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.
ILIPOISHIA:
Toka aolewe na Deus hakuwahi kwenda sehemu za starehe zaidi ya kwenda kwenye dhifa ya kiserikali. Lakini mashoga zake walimweleza raha wanazozipata wanapokwenda kwenye kumbi za starehe hata kwenye vikundi vya taarabu. Moyoni alijisemea: Leo mjanja lakini ipo siku utanijua mimi na yeye nani zaidi.”
SASA ENDELEA...
Kilole akiwa na mpango mzito moyoni mwake ambao aliujua yeye na Mungu wake, ili kuufanikisha alionesha ukaribu na mpenzi wa Kinape kitu kilichomziba macho Kinape kwa kuamini Kilole amekubaliana na alichomueleza *****
Maisha yaliendelea kama kawaida kwa Kilole naye kumtembea mchumba wa Kinape kuonesha ukaribu. Hali ile iliongeza mapenzi kwa Kinape kuona hali ipo shwari bila kujua kuna bomu zito limepangwa dhidi yake ya kulisambaratisha penzi lake. Wakati huo Kinape alikuwa katika hatua za mwisho kumpeleka happy kijijini kutambulishwa kwa wazazi wake. Kilole alipanga kutekeleza mpango kabla ya Kinape hajampeleka Happy kijijini, aliamini kama atachelewa itakuwa vigumu kuutekeleza mpango wake. Matumaini ya kutekeleza mpango wake yalikuwa makubwa baada ya kupewa na taarifa na mumewe ana safari ya kikazi nje ya nchi kwa siku tano. Siku ilipofika ya mumewe kusafiri ilikuwa tofauti na siku zote, Kilole alionesha kumhitaji mumewe kuliko kipindi chochote kilichopita.
“Mke wangu siku tano si nyingi,” Deus alimtuliza mkewe aliyekuwa akilia.
“Kwako si nyingi lakini kwangu naona kama miaka mitano,” Kilole alidondosha machozi ya uongo.
“Najua basi nitajitahidi safari nyingine tusafiri pamoja.”
“Itakuwa afadhari.”
“Kinape kuwa karibu na shemeji yako hata ukiwa mbali na nyumbani mpigie simu ili asipate upweke.” Deus alimweleza rafiki yake.
“Deus si mpo kwenye Facebook twitter instagram usiku tumieni kuliwazana ili usijione mpo mbali mbali,” Kinape alitoa wazo ili ajiweke mbali na Kilole.
“Na kweli mke wangu, kila baada ya kazi nitakuwa pamoja na wewe katika kuchati.”
“Lakini si sawa na wewe kuwa pembeni ya ubavu wangu,” Kilole alilia wivu wa uongo.
“Basi mke wangu niombee niende salama nirudi salama, si unajua kazi zetu.”
“Na ukirudi utimize ahadi ya kuninunulia gari langu,” Kilole alisema kwa sauti ya kideka.
“Kila kitu kipo tayari, subiri nikufanyie Surprise.”
“Waawoo mpenzi wangu.” Kinape alijikuta akifurahi furaha ya kweli baada ya kuona ndoto yake ya siku moja kuendesha gari lake mwenyewe inatimia. Alimkumbatia mumewe na kumtakia safari njema.
“Dear usafiri salama na urudi salama, ukiwa mbali kumbuka umeniacha kama kinda la ndege linalomsubiri mama yake aliyekwenda kutafuta chakula.”
“Hilo nalijua, nataka mpenzi wangu na mwanangu muishi maisha nusu ya peponi.” “Asante mume wangu.
” Kilole aliagana na mumewe na kurudi nyumbani na Kinape katika gari moja, wakiwa njiani Kinape alimchokoza.
“Ona ulitaka kupoteza bahati yako bure, haya ndiyo mapenzi unayotakiwa kuyapigania.”
“Kinape yale yalikwishapita achana nayo.
” Walirudi wote mpaka nyumbani, walipofika Kinape hakukaa aliaga na kwenda kuonana na mpenzi wake kitu ambacho Kilole hakupenda kukisikia.
*****
Kilole akiwa peke yake aliamini mpango alioupanga Kinape hawezi kuruka, alichukua simu yake na mkononi na kutafuta jina la mtu, kisha alipiga na kuiweka sikioni kusikiliza. Baada ya kuita kwa muda ilipokelewa upande wa pili.
“Haloo Sisiter.”
“Haloo Jimmy.”
“Ndiyo Sister lete stori, naona leo umenikumbuka.”
“Mambo mengi mtu wangu, upo pande zipi?”
“Ndiyo nafika kijiweni, ulikuwa unasemaje? Najua wito wako lazima nidake vumba nene.”
“Unaweza kuja nyumbani mara moja?”
“Hakuna tatizo.” “Basi njoo mara moja.”
“Okay, nakuja.”
Kilole alikata simu na kutabasamu mwenyewe huku akijisemea moyoni: “Kinape hana ujanja japo mjini aliwahi lakini mimi ndiye mwisho wa matatizo lazima arudi mikononi mwangu na uchumba wake ubakie hadithi.”
Kengele ya mlangoni ilimuondoa kwenye mawazo na kumfanya ananyuke kwenda kufungua.
“Ooh! Jimmy, karibu.”
“Asante Sister.”
Baada ya Jimmy kuingia alikaa kwenye kochi la watu watatu, Kilole alikaa kwenye kochi la mtu mmoja. Kwa vile Jimmy alikuwa mbali na Kilole, alimuomba asogee kochi la karibu.
“Jimmy, njoo ukae kwenye kochi hili.”
Jimmy alinyanyuka na kwenda kukaa karibu yake, Jimmy alionekana mtu mwenye wasiwasi sana.
“Jimmy mbona hivyo?”
“Mmh! Jinsi tulivyokaa mumeo akitokea inaweza kuwa msala.” “Kwani hajui kama wewe mpiga picha?”
“Anajua, lakini naona kama tumekaa karibu sana.”
“Wasiwasi wako kwanza mume wangu kasafiri.”
“Na mdogo wake?”
“Ametoka na hawezi kurudi sasa hivi.”
“Haya sister nipe dili basi.”
“Kuna kazi nitakupa uifanye, ukiifanya vizuri nitakupa pesa nzuri sana ambayo hukuwahi kuipata toka ulipoanza kazi ya kupiga picha.” “Kazi gani hiyo dada?”
“Ya kupiga picha.”
“ Mmh! Ni kazi ipi, mbona kama naona kama si ya kawaida?”
“Ni kweli, hii itakuwa siri yako na malipo yatakuwa mazuri.”
“Kazi hiyo itakuwa lini?”
“Ikiwezekana leo hii.”
“Poa basi ikiwa tayari nishtue.”
“Jimmy, naomba usifanye kazi yoyote kuanzia sasa hivi, nitakulipa pesa ya usumbufu na kazi ikikamilika nitakupa fedha nzuri sana.”
“Hakuna tatizo sister, nakuamini dada yangu wa ukweli.” “Nisubiri,” Kilole alinyanyuka na kwenda chumbani, baada ya muda alirudi na elfu 50 na kumpa Jimmy.
“Hii ya usumbufu, ya kazi bado.”
“Asante Sister.” Jimmy alipokea na kutoka akimwacha Kilole akifurahia mpango wake, alichukua simu yake na kumpigia Kinape. Baada ya simu kuita kwa muda Kinape upande wa pili aliipokea.
“Haloo Shemu.”
“Kinape upo wapi?”
“Nipo na mke mwenzio hapa.”
“Waawoo! Nimeipenda hiyo,”
. “Kweli?” Kinape alimuuliza.
“Kweli, inafurahisha, mmeonesha jinsi gani mnavyo pendana.” “Ndiyo shemeji yangu, una lipi tena?”
“Nimesahau kukujulisha kuwa leo ni siku yangu ya kuzaliwa.” “Wawooo, mbona hukuniambia mapema nikuandalie zawadi?” “Nilipitiwa lakini jioni kutakuwa na sherehe fupi ya kifamilia.” “Hakuna tatizo nitakutafutia zawadi nzuriii shemeji yangu.” “Nitashukuru, uje na Happy.”
“Hakuna tatizo.”
Baada ya kuzungumza na Kinape, alimpigia simu mtengeneza keki ili amuandalie keki ya birthday, ambaye aliwahi kumtengenezea mwanaye alipotimiza mwaka mmoja.
“Sakina ninaweza kupata keki ya birthday?”
“Lini shoga?”
“Leo hii jioni.”
“Jamani! Mbona haraka, ya nani?”
“Yangu mwenyewe.”
“Jamani shoga! Mbona hukunialika?”
“Kwani mimi? Shemeji yako ndiye kasema akirudi jioni akute keki, mwenyewe nilikwisha sahau kama leo siku yangu ya kuzaliwa,” Kilole aliunda uongo unaofanana na kweli. “Kwa hiyo jina lako ni lilelile?”
“Lipi hilo?”
“La Kilole?”
“Hilohilo mpenzi.”
“Basi hakuna tatizo nipe saa mbili kila kitu kitakuwa tayari.” “Nitashukuru.” Baada ya kuachana na mtengeneza keki, alikumbuka kitu muhimu kilichotakiwa kiwepo pale ili kufanikisha mpango wake. Alimpigia simu mpiga picha, simu iliita kwa muda kisha ilipokelewa upande wa pili.
“Oya, sister mambo tayari?”
“No, kuna kitu nataka kukutuma kabla ya kazi yetu.”
“Kitu gani hicho?”
“Eti kete ya unga shilingi ngapi?”
“Unga upi?”
“Kokeni, sijui heloin.”
“Una maanisha madawa ya kulevya?”
“Ndiyo.”
“Mmh! Ya nini?”
“Jimmy, utajua baadaye.”
“Sijajua bei yake, lakini sidhani kama inazidi elfu tano kwa kete.” “Basi njoo uchukue fedha ukaninunulie kete mbili.”
“Sister unajidunga nini?”
“Jimmy, kazi itakushinda.”
“Basi Sister nakuja.”
Baada ya muda mfupi alifika na kupewa elfu ishirini akanunue kete mbili za unga. Alitoka na kumwacha Kilole akiendelea na maandalizi ya mipango yake ambayo ilikuwa siri yake na Mungu wake.
Alimtuma mlinzi kununua vinywaji ambavyo alivijaza kwenye friza, kila kitu kilikwenda kama kilivyopangwa. Kilole baada ya kuridhika na mipango yake kwenda vizuri alijiandaa kuisubiri keki ili akamilishe zoezi lake.
Baada ya saa mbili kama alivyoahidia alijulishwa kuwa keki tayari, kwa vile hakutaka kutoka alimuomba mpelekewe. Sakina alimletea keki baada ya nusu saa, wakati huo mpiga picha alikuwa amefika na kumpa kete mbili za unga.
“Asante Jimmy, kwa kazi hii nitakupa posho elfu kumi, ila kuna kazi nyingine unatakiwa kuifanya.”
“Ipi hiyo?”
“Nitakupa namba hii nikikubip ipige, akipokea mwambie anatakiwa kwao haraka sana kuna matatizo.”
“Sawa.”
“Hakikisha unakaa mkao wa kazi usicheze mbali nakutegemea wewe ndiye steling wa picha.”
“Hakuna tatizo sister.”
“Jimmy ukiifanya kazi kwa ufanisi nitakupa laki mbili.”
“Utani huo sister!”
“Sina utani kwa jambo nitakalo kuahidi.”
“Sawa, wacha nikuache uendelee na mambo mengine.”
Jimmy aliondoka na kumuacha Kilole akitengeneza nyumba kwa ajili ya sherehe ya kutengeneza ya birhtday yake. Sebule aliipamba na kupambika ikawa katika muonekana wa kupendeza.

Itaendelea Ijumaa
 
SEHEMU: 09
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.
ILIPOISHIA:
“Jimmy ukiifanya kazi kwa ufanisi nitakupa laki mbili.” “Utani huo sister!”
“Sina utani kwa jambo nitakalo kuahidi.”
“Sawa, wacha nikuache uendelee na mambo mengine.”
Jimmy aliondoka na kumuacha Kilole akitengeneza nyumba kwa ajili ya sherehe ya kutengeneza ya birhtday yake. Sebule aliipamba na kupambika ikawa katika muonekana wa kupendeza.
SASA ENDELEA...
*******
Majira ya saa mbili usiku kila kitu kilikuwa kimepangwa sehemu yake, Kinape na mpenzi wake nao walikuwepo kwenye sherehe ya kuzaliwa kwa Kilole.
Ilikuwa sherehe iliyozuka kama uyoga, ule ulikuwa mpango wake maalumu wa kuhakikisha nasambalatisha penzi la Kinape na Happy pia kumrudisha mikononi mwake. Kabla ya sherehe kuanza simu ya Happy mchumba wa Kinape iliita, aliipokea na kuzunguza.
“Haloo.. eeh .. Nipo kwa Kinape... Kuna sherehe ya kuzaliwa shemeji yake...Eeeh!... Nini? Acha utani.. Mungu wangu nakuja...Aah.. lazima nije?”
“Vipi?” Kinape na Kilole waliuliza kwa pamoja baada ya kumuona Happy akitokwa na machozi huku ameshikilia mikono kichwani. “Mama,” alijibu kwa mkato.
“Mama kafanya nini?”
“Kavamiwa na majambazi walitaka kumpora gari.”
“Wamemjeruhi?”
“Wanasema hawajamjeruhi, wanaomba niendelee na sherehe lakini lazima nikamuone mama kisha nitarudi.”
“Kinape mpeleke mwenzako,” Kilole alijifanya mwema.
“Hapana dada ninyi endeleeni tu, nitarudi muda si mrefu, inaonekana tatizo siyo kubwa, nitakwenda peke yangu.” Happy aliwatoa wasi.
“Hapana mpenzi lazima nikupeleke,” Kinape alisema.
“Lakini kama umesema mama hana tatizo basi wacha nianze sherehe na Kinape ukirudi tutaungana pamoja,” Kilole alitumia nafasi ile kumbakiza Kinape.
“Kweli kabisa dada, nisiharibu utaratibu wa sherehe kwa vile ilikuwa ndiyo inaanza.” “Ila shampeni utaifungua ukirudi.”
“Hakuna tatizo.”
Kinape alimsindikiza Happy mpaka nje, baada ya kuingia kwenye gari na kuondoka alirudi ndani kuendelea na sherehe ya mtego aliyoandaliwa yeye bila kujijua. Wakati Kinape akitoka nje kumsindikiza mpenzi wake, Kilole alitumia nafasi ile kumuwekea dawa ya kulevya kwenye juisi.
Kinape aliporudi alikaa kwenye kochi na kuchukua glasi ya juisi na kunywa kidogo huku akimtupia swali Kilole kuvuta muda labda Happy atawahi kurudi. Kilole alifurahia moyoni na kuona mpango wake umekuwa rahisi tofauti na alivyopanga wa kumtumia Jimmy kumtoa Happy kwa simu ya uongo ili kitendo kifanyike kwa haraka. Lakini simu kutoka kwao kidogo imfanye apige yowe la furaha.
“Shemu, Deus anajua kama leo ni tarehe yako ya kuzaliwa?”
“Anajua na muda si mrefu nitakufanyieni bonge la surprise na mchumba wako.” “La nini tena, mbona umenirusha roho.”
“Utaliona muda si mrefu.” “Nigusie kidogo.”
“Ukijua haitakushtua, nataka uamini nakupenda shemeji yangu.”
“Mmh! Haya.”
Kinape alisema huku akichukua glasi ya juisi na kupiga funda zingine tatu na kurudisha glasi chini. Mara alianza kuhisi kichwa kizito, alijitahidi kushindana na hali iliyomtokea kila macho yalizidi kufumba. Kilole alifurahi kuona kila kitu kinakwenda kama kilivyopangwa.
Taratibu Kinape alijilaza kwenye kochi, kwa hatua ile Kilole aliona tayari mpango wa awali umekamilika. Alikumbuka mlango upo wazi alikwenda kuufunga, kisha alimpigia simu Jimmy.
“Haloo Jimmy.”
“Vipi Sister, nipige ile simu?” “Hapana, njoo nyumbani haraka.”
“Nipe dakika sifuri.”
Alipokata simu mlango uligongwa, alijua Jimmy amefika, alitoka hadi mlangoni na kufungua. Alishtuka kumuona Happy mbele yake, alipotaka kuingia ndani alimshika kifuani na kumrudisha nyuma.
“Vipi dada!” Happy aliuliza kwa mshangao.
“Kinape kakufuata.”
“Kanifuata vipi wakati nimemwambia narudi?” “Amesema huenda mama yako kapata matatizo makubwa.” “Jamani! Sasa kapitia wapi mbona sikumuona?”
“Kwa kweli sijui kitu, nimembembeleza akusubiri kakataa.”
“Kwa nini asinipigie simu?”
“Mmh! Siwezi kujua.” Happy aliamua kumpigia simu Kinape mbele yake, baada ya muda simu iliita ndani.
“Mbona simu yake inaita ndani?”
“Aliisahau kutokana na papara zake.”
“Sasa nikimfuata si nitapotezana naye, bora nimsubiri ndani.” “Happy, kutokana na king’ang’anizi cha mpenzi wako nimeamua kuahisha sherehe mpaka jumamosi.”
“Hata hivyo siwezi kusumbuka kumfuata, wacha tu nimsubiri,” Happy alisema huku akitaka kuingia ndani. “Happy kuwa muelewa, Kinape baada ya kuondoka nimemweleza nimeamua kuahirisha sherehe na yeye alisema hatarudi mpaka kesho. Sasa ukimsubiri itakuwaje?” “Mmh! Wacha nimuwahi,” Happy alisema huku akigeuka na kuondoka. Kilole hakuingia ndani mpaka aliposikia sauti ya gari la Happy likiondoka, wakati huo Jimmy alikuwa amefika.
“Ooh! Jimmy karibu ndani.”
“Asante,” Jimmy alijibu huku akiingia ndani. Alipofika sebuleni alishangaa kukuta kuna kitu kama sherehe, mbele kulikuwa na keki kubwa iliyoandikwa Happy Birthday Kilole na pembeni yake kulikuwa na chupa kubwa ya shampeni. Sehemu nyingine kulikiwa na vinywaji ndani ya glasi. Alipoangalia kwenye kochi alimuona Kinape ameutwanga usingizi.
“Vipi Sister naona ulikuwa na sherehe ya kuzaliwa kwako?”
“Ndiyo, lakini sicho nilichokuitia.”
Jibu lilimfanya Jimmy asiulize kitu zaidi ya kusubiri alichoitiwa.
“Ndiyo sister lete maneno?”
“Kazi niliyokuitia sasa imekamilika nataka ufuate maagizo yangu, malipo yako nilikuambia kiasi gani?”
“Laki mbili.”
“Nitakuongezea hamsini, itakuwa laki mbili na nusu.”
“Hakuna tatizo,” Jimmy alikubali bila kujua ni kazi gani. Baada ya kuhakikisha mlango ameufunga vizuri alimuomba Jimmy amsaidie kumuingiza ndani Kinape.
Walisaidizana kumwingiza chumbani, Kilole alimpeleka katika chumba chao cha kulala kisha walimlaza kitandani. Baada ya kumlaza walitoka mpaka sebuleni kupanga mipango yao. “Sasa sikiliza kazi niliyokuitia ni hii.”
“Kazi gani?”
“Nataka unipige picha kwenye tukio lote nitakalokuwa nalifanya kisha utaenda kunisafishia na kuniletea picha zote, sawa?” “Picha za tukio gani?”
“Nitakalo lifanya muda mfupi usilishangae nina sababu zangu ila nakuomba unifichie siri hii.”
“Hakuna tatizo.”
“Basi subiri.” Kilole alisema huku alielekea chumbani kwake, Jimmy alibaki akijiuliza anataka kupewa kazi gani. Baada ya muda Kilole alirudi akiwa katika vazi la kanga moja iliyoonesha hakuwa na nguo nyingine ndani. “Jimmy,” alimwita kwa sauti ya chini. “Na..na..aam,” Jimmy alionekana kuchanganyikiwa na umbile la Kilole lililokuwa la utata kwa mwanaume shababi.
“Jimiiii, utaiweza kazi kweli?”
“Kwa nini?”
“Umeona negative umechanganyikiwa ukiona picha si utashindwa hata kuifanya hiyo kazi.”
“Niwaweza tu wala usihofu.” “Umeisha andaa kamera yako?”
“Ndiyo.”
“Basi njoo chumbani.”
Jimmy kabla ya kwenda chumbani alifikiria ameitwa na Kilole kufanya naye mapenzi kwa kisingizio cha kupiga picha. Japo alijua mke wa mtu sumu lakini kwa mwanamke aliyeumbwa akaumbika kama Kilole ilikuwa sawa na nzi kufia juu ya kidonda. Uchu wa ngono ulimjaa na kujiona kama mbwa anayejipeleka mwenyewe kwa chatu, alitembea huku mwili wake ukiongezeka joto la matanio. Alipoingia chumbani alishangaa kumuona Kinape amelala kitandani hajitambui akiwa mtupu. Hali ile ilimshtua na kujiuliza kulikoni kuwa vile. Kilole alikwisha msoma Jimmy, ilikumtoa hofu alimwambia:
“Jimmy utakachokiona humu ndani kiache kama ulivyokiona, nikisikia chochote tutaonana wabaya, Kabla ya mimi kulikimbia jiji nitaanza na wewe.
” Kilole alitoa onyo kali kwa Jimmy. “Siwezi kufanya hivyo.”
“Sawa, sasa naomba upige picha kila tendo nitalofanya na Kinape.”
“Tendo gani?”
“Usiulize andaa kamera yako,” Kilole alikuwa mkali kidogo. Jimmy hakuongeza swali zaidi ya kufuata maelekezo, muda wote bado alikuwa gizani kutokana na hali iliyokuwemo mule chumbani kwa Kinape kulazwa chali kitandani akiwa mtupu na sehemu zake za siri zilikuwa zimenyanyuka. Kabla hajapata jibu Kilole aliitoa kanga iliyostiri mwili wake na yeye kubakia mtupu.
“Jimmy,” alimwita huku akipanda kitandani.
“Aah...Eeeh...Na..naa..m.”
“Naona umepagawa, sasa kila hatua piga picha, sawa?”
“Sawa,” Jimmy alijibu macho yamemtoka pima.
Jimmy alimshangaa Kilole mambo ya aibu aliyokuwa akiyafanya mbele yake bila haya, alifanya mapenzi na Kinape aliyekuwa hajitambui kwa kumkalia juu yake. Ajabu Jimmy alijisahau kazi aliyopewa ya kupiga picha na kujikuta akipandwa na mzuka wa ngono. Alimshangaa Kilole mke wa mtu kufanya mpenzi na shemeji yake ambaye alionekana amelewa kupita kiasi.
Aliona heri kama amezidiwa angemweleza yeye kuliko kufanya mapenzi na mtu asiyejitambua. Kilole alipofumbua macho alimshangaa Jimmy aliyekuwa amesahau kazi aliyomtuma. “Jimmiiiii,” sauti kali ya Kilole ilimshtua Jimmy aliyekuwa akiangalia Blue print live bila chenga.
“Jimmy, umeisha piga picha?”
“Samahani Sister,” Jimmy alibabaika.
“Samahani nini Jimmy, kazi imekushinda?”
“Ha..ha..pana,” Jimmy alibabaika hata kamera alikuwa ameweka chini ili afaidi vizuri mambo ya wakubwa. Aliiokota na kujiandaa kupiga picha huku akitetemeka.
”Naomba upige picha kila hatua sawa?”
“Sawa.” Kilole alianza zoezi upya la kijidhalilisha mbele ya Jimmy, naye alipiga picha kila hatua.
Baada ya zoezi lake kukamilika, alimuomba Jimmy amuoneshe picha zote. Alichagua zinazofaa na zingine kuzifuta kisha alimuomba Jimmy atoke akamsubiri sebuleni. Jimmy alitoka akiwa katika hali mbaya baada ya kuzidiwa na ashki, kuna kipindi aliwaza hata ambake Kilole.
Lakini alikumbuka alikuwa kazini na kazi ile ya hatari aliahidiwa pesa nyingi, alikaa sebuleni kumsubiri Kilole ambaye alikuja baada ya robo saa akionesha ametoka kuoga na kuvalia nguo ya kulalia.
“Jimmy, mzigo wako huu hapa, hizi ni laki na nusu, hamsini za kusafishia na laki moja adivansi ukileta picha zangu nakumalizia laki na nusu. Ila kuna zawadi yako kubwa kama utakuwa msiri, kuna kazi nyingine ya milioni moja.”
“Wacha!” “Wewe tu kuonesha uaminifu.”
“Basi dada kesho saa nne nakuletea mzigo wako, andaa fedha yangu tu.”
“Hakuna tatizo, tutaonana kesho, lakini chonde chonde siri hii asijue mtu yeyote.”
“Nakuhakikishia siri hii itabakia kwa watu wawili mimi na wewe tu.”
“Haya, usiku mwema.”
Itaendelea Jumatatu
 
SEHEMU: 10
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
“Jimmy, mzigo wako huu hapa, hizi ni laki na nusu, hamsini za kusafishia na laki moja adivansi ukileta picha zangu nakumalizia laki na nusu. Ila kuna zawadi yako kubwa kama utakuwa msiri, kuna kazi nyingine ya milioni moja.”
“Wacha!”
“Wewe tu kuonesha uaminifu.”
“Basi dada kesho saa nne nakuletea mzigo wako, andaa fedha yangu tu.”
“Hakuna tatizo, tutaonana kesho, lakini chonde chonde siri hii asijue mtu yeyote.”
“Nakuhakikishia siri hii itabakia kwa watu wawili mimi na wewe tu.”
“Haya, usiku mwema.” SASA ENDELEA...

Kilole aliagana na Jimmy na kurudi ndani, alipofika kitandani alivua nguo zote na kujilaza pembeni ya Kinape. Alfajiri kilevi kilipomwisha Kinape alishtuka usingizini, akili yake alijua aliyelala pembeni yake ni mpenzi wake Happy, lakini alipoangalia vizuri aligundua ni Kilole, alishtuka na kunyanyuka kitandani. Alishangaa kujikuta amelala kitanda kimoja na shemeji yake na kwa hali waliyokuwa kuwa nayo, aliamini lazima walifanya mapenzi. Alijiuliza ilikuwaje mpaka akawa kwenye kitanda cha rafiki yake wakiwa watupu na mkewe.
Alinyanyuka haraka kitandani na kupitia nguo zake bila kuzivaa na kukimbilia chumbani kwake. Alipokuwa akipapatika kama kuku aliyekatwa kichwa na kuachiwa, Kilole alikuwa akimuangalia kwa chati huku akichekea moyoni huku akisema:
“Kiko wapi, mimi na wewe nani mjanja.”
Hakujisumbua aliendelea kulala huku akichelelea moyoni, wakati huo Kinape baada ya kuingia chumbani kwake na kukaa kitandani mikono aliweka kichwani na kujiuliza kilichotokea ni kweli.
Ili kupata ukweli alizishika sehemu zake za siri na kukutana na majimaji kumuonesha kabisa katumika. Kila alivyorudisha mawazo yake ilikuwaje mpaka akalala katika kitanda cha rafiki yake kipenzi Deus na mkewe, jibu lilikuwa mbali.
Alikumbuka siku ya jana yake kwenye sherehe baada ya kuondoka Happy alibakia na shemeji yake Kilole wakipiga stori huku wakivuta muda kumsubiri Happy ili wafungue sherehe rasmi.
Wazo lake la haraka lilikuwa huenda ule ulikuwa mpango wa Kilole kama alivyomuahidi atahakikisha anamrudisha mikononi mwake. Kinape alijiapia kuwa kamwe pamoja na kufanya ujanja ule hawezi kuendelea kuwa mpenzi wake zaidi ya kuhama nyumba.
Wakati anatoka kuoga aliona simu yake juu ya kochi, aliichukua na kukuta imezimwa, alielekea nayo chumbani kwake. Alipoingia aliiwasha, haikupita muda ziliingia meseji zaidi ya kumi zote zikuwa za Happy akimlalamikia kwa kitendo alichomfanyia cha kumzimia simu.
Wakati akiendelea kusoma ujumbe wa Happy simu yake iliita, alikuwa Happy, alijiuliza atamwambia nini ili amuelewe. Lakini alijikaza kiume na kuipokea kwa kuamini hawezi kukosa cha kumueleza.
“Haloo Kinape umenifanya nini?”
“Happy mbona huniulizi nimepatwa na nini unaanza kunilaumu.”
“Kinape, nilikuambia narudi, lakini nilipofika nyumbani nikakuta hali ya mama ipo sawa, nimerudi nikasikia umenifuata na kusema utarudi kesho.
Nilipopiga simu yako kumbe uliiacha ndani kwa kuchanganyikiwa. Kinape, tulikuwa na mpango gani wa kulala pamoja na kusababisha sherehe ya shemeji yako kuvurugika?” Maneno yale yalimpa picha na kujua atamjibu nini ili kumfanya asiendelee kuumia.
“Mpenzi nilipokuwa nakuja kwenu, nilipata na ajali na kupelekwa polisi hata simu niliisahau nyumbani.”
“Sasa mbona baadaye nilipokutafuta ilikuwa imezimwa?”
“Nilikuta haina chaji.”
“Kwani ulirudi saa ngapi?”
”Saa nane usiku.”
“Ooh, pole upo wapi sasa?”
“Nyumbani.”
“Nakuja sasa hivi?” “Usije nisubiri kwenu.”
“Hapana mpenzi usisumbuke nakusubiri nitakufuata hapo hapo.”
“Sipo nyumbani, ndiyo maana nimekueleza nisubiri.”
“Kinape si umeniambia upo nyumbani sasa hivi! Mbona sikuelewi?”
“Nimetoka nyumbani sasa hivi kuelekea polisi, hivyo namalizana nao nipitie kwenu.”
“Mmh! Sawa.”
“Usisikitike dia, sawa.”
“Sawa dia, nimeumia sana kusikia umelala polisi kwa ajili yangu.”
“Hawakukupiga?”
“Hawakunipiga nipo sawa dia.”
“Ooh! Afadhari nakusubiri, una usafiri au nikufuate na gari?”
“Hapana, kuna teksi nilikodi,” Kinape alijitahidi kumzuia mpenzi wake.
“Hakuna tatizo mpenzi wangu, angalia usije ukapata ajali tena.”
“Unafikiri niligonga walaa, alijigonga mwenyewe mwendesha boda boda wala hakuumia polisi hawana dogo.”
“Mbona unaongea hivyo si upo polisi?”
“Nipo mbali nao.” “Basi kuwa makini nakupenda sana Kinape, mmmmmmwa.” “Mmmwa,” Kinape naye alijibu na kukata simu. Mara mlango uligongwa, alikuwa Kilole, bila kuitikia alinyanyuka na kwenda mlangoni, alipofungua alikutana naye uso kwa uso. “Za asubuhi shemeji?” Kilole alimsabahi Kinape aliyekuwa akimshangaa. “Nzuri.”
“Shemeji chai tayari.”
“Asante, nimeshiba.” “Imeanza lini na leo iwe ya pili, kama ulijua hunywi chai kwa nini hukuja kunieleza mapema. Si umenipita jikoni unakwenda bafuni kuoga.” “Sikukuona.”
“Basi lazima chai uinywe ndipo uende huko kwa mwanamke wako unayejifanya unampenda kuliko wanawake wote.”
“Shemu yote yamefikaje huko, tunazungumzia chai Happy kaingiaje?” Kinape alimuuliza Kilole huku akitengeneza shati lake. “Kama hutaki yote hayo, njoo unywe chai tena kuna kitu nataka unieleze kwa kituo kiniingie. Wewe si ulinikataa iweje univizie usiku?” Kilole alizungumza sauti ya kuonesha hakutendewa haki. “Mimi?” Kinape alishtuka kusikia vile. “Kwani hapa nazungumza na jiwe?” “Mmh! Bado sielewi nini kilitokea jana,” Kinape alisema akiwa ameangalia chini kwa aibu.
“Ndiyo maana nikasema kunywa chai tuzungumze.”
“Happy ananisubiri.”
“Happy wa muhimu kuliko tukio ulilonifanyia jana usiku, ulishindwa kuniambia nikakukubalia kwa hiyari yangu, ukanivizia nimelala huo si ubakaji? Nilijua bado unanipenda ndiyo maana nilikueleza nikupe penzi la siri kwa vile bado naheshimu penzi lako ukakataa.
“Lakini asubuhi nashtuka nakuona unakimbia, kweli Kinape wewe wa kunifanyia hivyo?” Kilole alimuuliza kwa msisitizo.
“Kilole hili suala linatakiwa tulifanyie kazi si la kukurupuka kulaumiana.”
“Sijakulaumu ila nimekuuliza ulishindwa vipi kunieleza una hamu na mimi, siwezi kukunyima, kwa vile wewe ndiye uliyenionesha raha na tamu ya dunia. Hili kwangu si tatizo lakini na mimi nina ombi langu nakuomba nani unitekelezee ili tuwe sawa.”
“Mmh! Hata sielewi, basi niache niende kwa Happy ili nikirudi tupange vizuri.” “Kinape umenionjesha naomba unimalizie kabisa.”
“Sawa nimekubali, nikirudi nitatimiza haja zako.”
“Kinape kuna tatizo gani ukinipa muda huu ili ukitoka usiwe na wasiwasi wa kufikiria nyumbani?”
“Mmh! Sawa.”
Kauli ile ilimfanya Kilole amsukumie Kinape nyuma na kumuangushia kitandani kwake. Kama kipanga aliyeona kifaranga cha kuku alimsaula nguo zote na yeye kutoa zake chache zilizovaa.
Kinape alijikuta akiwa kama mbwa kwa chatu, moyoni alijiapiza atatafuta kila njia ahame pale ili kujiweka mbali naye. Upande wa Kilole aliamini mpango wake umekwenda vizuri tofauti na alivyofikiria na kuapa kumfanyia mambo makubwa Kinape.
Baada ya kuondoka chumbani Kinape alibakia ameinama mikono kichwani alijiuliza maswali yasiyo na majibu, ilikuwaje akawa katika kitanda cha Deus, alichokumbuka kuamka asubuhi na kujikuta amelala na Kilole bila nguo bila kujua alifikaje pale.
Aliwaza labda ulikuwa mpango wa Kilole aliomuahidi hapo awali, lakini shutuma alizozitoa zilizidi kumchanganya kuonesha amemlazimisha kufanya naye mapenzi bila ridhaa yake. Kitendo kilicho onekana kuwa ni sawa na kubaka.
Japo hakupenda kufanya mapenzi tena na Kilole lakini kwa upande mwingine alimshukuru kwa uamuzi wake wa kutomshitaki polisi. Aliamini kama angempeleka basi angeweza kuozea gerezani, kwani ushahidi wote ulikuwepo wa kuonesha amebakwa.
Simu yake iliita zaidi ya mara sita na kukatika, aliisikia lakini akili yake ilikuwa mbali sana. Alikumbuka alikuwa na mpango wa kuonana na Happy nyumbani kwao, alinyanyuka na kwenda bafuni kuoga.
Baada ya kumnaliza kuoga na kubadili nguo, alipoangalia simu yake alikuta aliyepiga ni Happy zaidi ya mara sita. Hakutaka kumpigia alijua yote atamalizia huko huko akifika, alitoka kuelekea nyumbani kwao Happy. Wakati anatoka sebule haikuwa na mtu alitoka haraka kumuwahi Happy, alipofika mlango wa kutokea nje aliitwa nyuma na Kilole. “Kinape.”
“Naam,” aliitika huku akisimama.
“Safari ya wapi?”
“Si nimekueleza nakwenda kwa Happy.”
“Nataka nikuambie kitu kimoja, sipendi kusikia jina la mwanamke wako, kila nikisikia linanitia kichefuchefu.”
“Lakini si mchumba wangu?” “Mmh! Sasa hii chai anywe nani?”
“Nilimuahidi nitakwenda kwao muda uliopita nikizidi kuchelewa atajisikia vibaya.”
“Kinape unachekesha, nisijisikie vibaya mimi niliyekutaka ukanikataa ukaishia kunibaka.”
“Yaani sijui hata ilikuwaje hiyo jana!”
“Iweje na wewe umeamua kunibaka.”
Kauli ile ilimmaliza nguvu Kinape na kubakia amesimama kimya kama amenaswa na sumaku.
“Kinape siwezi kukulazimisha mapenzi kwa vile upo na mchumba wako, lakini sipendi dharau.”
“Lakini si nimekueleza hali iliyopo?”
“Kinape huyo Happy angekujulia wapi kama mimi ningemgomea mume wangu wee kuja mjini?”
Kilole alimuuliza huku ameshika kiuno. “Lakini mbona yamekuwa hayo....,” Kinape alinyamaza kimya baada ya mlango kugongwa. Kilole aliamini muda ule Jimmy alikuwa akileta picha, alipofika mlangoni alikutana na Happy. Japo moyoni alichukia lakini alitengeneza tabasamu la uongo.”
“Ooh! Happy karibu.”
“Asante dada,” Happy alisema huku akimtaza Kinape aliyekuwa amesimama karibu na mlango.
“Kinape unanifanya nini, nimekukosea nini mpaka uamue kunitesa hivi?” Happy alisema kwa sauti ya kilio.
“Happy mbona umekuwa mtu wa kulaumu bila kuuliza?”
“Niulize nini hapa ndiyo polisi?” “Hilo swali gani?”
“Kinape ni wazi hunipendi najipendekeza kwako,” Happy alilalamika huku machozi yakimtoka. “Happy unaniamini, huniamini?”
“Nikuamini vipi mtu muongo.” Wakati huo Jimmy mpiga picha alikuwa akiingia, ili kupoteza ushahidi Kilole alimueleza Kinape:
“Shemu naomba ukazungumzie nje mambo yenu nina mgeni.”
“Sawa,” Kinape aliitikia huku akimshika mkono Happy aliyekuwa ameiva na kuwa mwekundu kwa hasira.
“Hebu ngoja,” Happy alijitoa mkononi mwa Kinape.
“Happy hebu msikilize mwenzako,” Kilole aliingilia kati baada ya kuona Happy akitafuta msaada kwake.
“Sikiliza dada, Kinape ananinyanyasa sana.”
“Mdogo wangu ngoja nizungumze na mgeni, tutalimaliza nina imani kabisa Kinape anakupenda sana.” Kinape na Happy walitoka nje na kuwaacha Kilole na Jimmy.

Itaendelea Jumatano
 
SEHEMU: 11
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.
ILIPOISHIA:
“Sawa,” Kinape aliitikia huku akimshika mkono Happy aliyekuwa ameiva na kuwa mwekundu kwa hasira. “Hebu ngoja,” Happy alijitoa mkononi mwa Kinape. “Happy hebu msikilize mwenzako,” Kilole aliingilia kati baada ya kuona Happy akitafuta msaada kwake. “Sikiliza dada, Kinape ananinyanyasa sana.” “Mdogo wangu ngoja nizungumze na mgeni, tutalimaliza nina imani kabisa Kinape anakupenda sana.” Kinape na Happy walitoka nje na kuwaacha Kilole na Jimmy.
SASA ENDELEA...
**** Usiku baada ya kutoka kumpiga picha za aibu Kilole, Jimmy alikuwa mtu mwenye mawazo mengi sana. Toka aanze kazi ile hakuwahi kukutana na tukio zito kama lile. Tokio kubwa lilikuwa kuwapiga picha za utupu wake za watu au mastaa wa kike. Lakini la kushuhudia mtu akifanya mapenzi lilikuwa ndilo tukio lake la kwanza lililompa wakati mgumu sana. Alitamani bora Kilole angempa penzi yeye kuliko kufanya mapenzi na mtu aliyekuwa sawa na maiti asiyejielewa. Alijikuta akipata maswali yasiyo na majibu juu ya kitendo cha Kilole kufanya mapenzi na mtu anayemfahamu ni shemeji yake. Alijiuliza kufanya tukio lile huku akipiga picha alikuwa na maana gani, alijikuta akiingiwa na tamaa ya mapenzi kwa kuamini kupitia picha zile lazima na yeye ataweza kumtia mikononi. Wazo lingine lilikuwa kutengeneza pesa zaidi kupitia picha zilezile. Baada ya kuwaza sana akiwa amejilaza kitandani alijikuta akitabasamu baada ya kugundua picha zile zitakuwa sawa jiwe moja kuua ndege wawili. Hakuamini kabisa mwanamke yule pamoja na kumtisha anaweza kumfanyia lolote baya. Kabla ya kulala alirudia kuangalia picha moja moja ili aone zipi zimetoka vizuri na zipi zimeharibika, alijikuta akiwa amepiga picha chache zenye ubora. Kutokana kupatwa na kigagaziko kilichomfanya aifanye kazi katika wakati mgumu. Picha zingine alipiga ukuta badala ya watu, zingine aliwapiga mgongo au kupiga sehemu isiyohusika. Zote ambazo zilikuwa hazifai alizifuta na kubakiza chache ambazo zilikuwa zinafaa. Baada ya kuwaza sana alipitiwa na usingizi mpaka siku ya pili, asubuhi alipoamka baada ya kuoga alikwenda studio kusafisha picha zake. Kama kawaida picha zake za magumashi zilikuwa zinawahishwa kusafishwa kabla hawajaanza kazi yoyote. “Beka kama kawaida piga mara mbili.” “Za nani mwana?” “Kaka aina haja ya kujua, nifanyie kazi haraka.” Beka alimsafishia Jimmy picha mara mbili na kumpatia, alizichukua na kurudi zake nyumbani kwanza kabla ya kuzipeleka kwa mwenyewe. Alipofika alipitia picha moja baada ya nyingine, alichukua za kwake na kuziweka kwenye kabati na zilizobaki alimpelekea Kilole. ******* Jimmy alipofika kwa Kilole alishtuka kumkuta Kinape nusra atimue mbio kwa mshtuko, lakini alificha hofu yake na kuingia ndani. Baada ya Kinape na mpenzi wake kutoka nje walibakia wawili ndani. “Karibu ukae,” Kilole alimkaribisha Jimmy baada ya kuonesha wasiwasi, alijua baada ya kumuona Kinape. “Asante,” alijibu huku akikaa, kutokana na wasiwasi walijikuta akikaa chini. “Jimmy mbona unanitia aibu kazi utaiweza kweli?” “Samahani, unajua nimeshtuka sana.” “Hajui lolote, wasiwasi wako tu.” “Mmh! Nilishtuka sikutegemea kumkuta.” “Tuachane na hayo mzigo wangu upo wapi?” Kilole aliuliza. Jimmy alimpa bahasha ya picha, baada ya kuipokea aliichukua na kwenda nayo chumbani. Hakutaka kuzipitia alichukua kiasi cha fedha alizobakia kwenye deni lao, alipofika sebuleni alipa fedha yake na kumwambia: “Nina imani kila kitu kimekwenda vizuri?” “Nashukuru.” “Jimmy kama kuna kitu chochote nitakueleza.” “Hakuna tatizo.” “Naomba siri hii usimwambie yeyote ikivuja nitajua ni wewe, kwa hiyo usinilaumu kwa lolote litakalokukuta.” “Kwangu shaka ondoa, hakuna kitu kama hicho.” “Nakuhakikishia baada ya muda tegemea zawadi kubwa.“ “Nitashukuru sister.” “Basi baadaye.” Jimmy aliagana na Kilole na kuondoka zake, baada ya kuondoka Kilole alitoka nje na kuwakuta Kinape na Happy wakiwa katika mazungumzo ya kawaida. “Vipi jamani?” “Yamekwisha,” alisema Kinape. “Basi niwaache mimi nipo ndani.” “Hakuna tatizo.” Kilole alirudi ndani na kuingia chumbani kuangalia picha alizoletewa na Jimmy. Baada ya kufungua bahasha alichukua alitoa picha zote na kuzimwaga kitandani na kuanza kupitia picha moja baada ya nyingine. Zilikuwa picha za aibu ambazo hazikuonesha uhalisia wa watu wawili waliokuwa wanafanya mapenzi kwa ushirikiano. Picha zile zingekuwa kwa upande wa pili kwa ajili ya kumdhalilisha zingekuwa nzuri sana. Lakini kama mtego wa kuonesha wanafanya mapenzi alikuwa amefeli. Alijiuliza kama Kinape angegoma kufanya naye mapenzi, picha zile zisingeweza kumshtua kwani ilionesha wazi hakukuwa na ushirikiano wowote wa Kinape kwake. Moyoni alishukuru mkwala wake uliweza kumlainisha lakini kama angetegemea picha zile zisingemsaidia. Alijikuta akipandwa na hasira na kuamua kuzichana zote kisha aliziweka kwenye chombo na kuzichoma moto. Baada ya kuzichoma moto aliamini pamoja na kumtega na kuweza kufanya naye mapenzi bado hawezi kumdhibiti Kinape kwa vile ana uwezo wa kukataa na asimfanye lolote. Wazo lingine lililomjia ni kufanya naye tena mapenzi huku Jimmy akipiga picha wote wakiwa na akili timamu. Aliamini kwa mpango ule ataweza kumdhibiti Kinape pia hata kuweza kuvunja penzi lake na Happy ambalo kila kukicha lilimnyima raha. Alijikuta akijilaumu kwa kupanga mpango mbovu, lakini kwa upande mwingine ulisaidia kuweza kumvuta karibu Kinape mpenzi wake wa zamani. Alitoka nje na kuwakuta Kinape na Happy sebuleni wakizungumza, walipomuona waliacha kuzungumza na kumwangalia.
Uso wa Kilole ulionesha kuna kitu kimemsibu. Kinape alijua ni kutokana na Happy kuwa pale. “Dada vipi, bado unamkumbuka shemeji?” “Aah, wapi mbona nimeishazoea.” “Shemu vipi?” Kinape aliuliza. “Nikuone mara moja.” “Hakuna tatizo,” Kinape alijibu huku akinyanyuka. Kilole na Kinape walisogea pembeni, Kinape alijua lazima atagombezwa kuhusu Happy. “Kinape, kwanza samahani kwa kukukatisha kazungumzo na mpenzio.” “Bila samahani.” “Nina ombi moja, leo naomba tulale pamoja, kesho endelea na mpenzi wako.” “Hakuna tatizo.” “Basi endeleeni ma mazungumzo yenu.” Kinape alishangazwa na ustaarabu alioonesha Kilole, lakini moyoni alipanga Deus akirudi lazima aondoke. ****** Kilole alifurahia kukubaliwa ombi lake bila masharti yoyote, alimpigia simu Jimmy kumjulisha kazi nyingine ya usiku ule. “Jimmy.” “Ooh! Sister lete mpya.”
”Ile kazi haikuwa nzuri nataka leo tuirudie.” “Kwa malipo yaleyale?” “Hapana, nitakupa laki na nusu.” “Poa, nije saa ngapi?” “Saa mbili usiku, ila ukifika usiingine ndani nipigie simu, ooh! Nimekumbuka hebu njoo mara moja,” Kilole alikumbuka kazi ile ilitakiwa ifanyiwe maandalizi ili isije kwenda kinyume kutokana na muda wa kurudi mumewe kuwa umekaribia. Wakati huo Kinape na Happy walikuwa wameondoka na kuahidi kurudi jioni. Baada ya muda Jimmy alifika, alimzungusha kwa nyuma sehemu ya dirishani ili kuandaa maandalizi ya kupiga picha za ndani. Baada ya kuandaa eneo vizuri waliagana na kukubaliana kukutana muda huo. Majira ya saa mbili usiku Kinape alikuwa nyumbani, baada ya chakula cha usiku walikwenda chumbani kulala. Kama kawaida Jimmy alikuwa amekwishafika eneo la tukio. Baada ya kupewa taarifa ya kuacha kwa mchezo mchafu, alisogea dirishani na kuchungulia ndani. Ili kupata uhakika kama Jimmy amefika alinyanyuka na kwenda dirishani kama anataka kusogeza pazia, alipoangalia nje alimuona. Alilidhika na kurudi kitandani kuendelea na zoezi lake. Naye Jimmy kama alivyoelekezwa alipiga picha kutokana na jinsi Kilole alivyokuwa akifanya bila Kinape kujua. Japo alikuwa kwenye wakati mgumu huku akijawa na mawazo mtu na shemeji yake kufanya mapenzi. Hakutaka kujua sana, lakini katika siku iliyokuwa ngumu kwake ilikuwa ile. Mpaka wanamaliza Jimmy alikuwa hoi na kujichafua kutokana na kwenda na muvu ya mchezo. Baada ya kumaliza mpango wake Kilole alimtanguliza Kinape bafuni na yeye kutoka nje kuonana na Jimmy. “Vipi umefanikiwa?” Kilole alimuuliza Jimmy baada ya kumuona. “Ndiyo.” “Hebu nione.” Jimmy alimuonesha picha alizopiga katika hatua zote, zilikuwa picha nzuri sana ambazo aliamini kama Jimmy akiziona hawezi kuruka. “Jimmy kazi nzuri.” “Lakini umenipa mateso makubwa.” “Pole nitakuongezea elfu hamsini kwa hiyo itakuwa lakini mbili. Shika laki mbili zingine kesho.” “Hakuna tatizo, kuna lingine?” “Hakuna.” “Basi kesho.” Waliagana kwa Kilole kurudi ndani huku moyo wake ukiwa na furaha, alijikuta akiingia chumbani huku akitabasamu. “Vipi mbona una furaha?” Kinape alimuuliza. “Leo umekumbusha mbali sana.” “Umekumbuka nini?” “Penzi letu lilivyokuwa tamu adhimu, hakika leo nitalala usingizi mtamu.” “Lakini kumbuka kitendo hiki ni sawa na kukata tawi tulilo kalia.” “Hii ni siri yetu.” “Hakuna siri katika mapenzi.” “Basi kwetu itakuwa siri.” “Nimefanya tu lakini si kwa moyo wangu.” “Kinape mbona unataka kutia mchanga kwenye chakula kitamu, kwa vile tumeamua kula nguruwe basi tumchague aliyenona.” “Kumbuka mwenyewe muda si mrefu atakuwa hapa.” “Tutakuwa kama hatujuani, ila siku tukipata nafasi kama kawaida.” Waliendelea kula raha zao mpaka siku ya pili, huku moyoni Kilole akiapa akifanikiwa kuzipata picha zile lazima Kinape arudi mikononi mwake na kuvunja uchumba wake Happy. ***** Jimmy baada ya kufika kwake alijikuta akizidi kuwa na maswali mazito juu ya kitendo cha Kilole na Kinape kumhujumu Deus. Lakini bado alikuwa wazo lake la kuhakikisha kupitia picha zake anampata kimapenzi. Aliamini kama angekuwa na kamera ya kuchukua video basi angepata mkanda ambao angeweza kuuza kwa fedha nyingi siku za mbele. Pia aliona kupitia picha zile angepata faida mara mbili, hakuwa na haja ya kuzichambua kwa vile alizipiga katika ustadi mkubwa. Aliweka kamera yake kwenye kabati na kutoka nje kwenda kutafuta mwanamke wa kulala naye kwani alikuwa kwenye hali ngumu. Jimmy aliposhtuka siku ya pili alijikuta peke yake kitandani, mwanamke aliyelala naye hakuwepo. Hakujishughulisha naye baada ya kuoga aliwahi kusafisha picha, alimkuta Beka na kumweleza amsafishie mara mbili kama kawaida. Baada ya kusafishiwa alizichukua na kuzipeleka nyumbani, alipofika alishangaa kukuta sehemu alipoweka picha alizompiga Kilole mara ya kwanza hazipo. Kilichomshangaza ufunguo wa chumba chake alikuwanao mwenyewe. Alijikuta akishtuka na kujiuliza nani aliyechukua. Alikumbuka changudoa aliyelala naye na kuondoka akiwa amelala ndiye aliyechukua zile picha, alijiuliza amezichukua ili iweje. Wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kama zikivunja lazima Kilole atamuona hana manaa hata kumfanyia kitu kibaya.
Alipanga usiku akamtafute ili amrudishie picha zake, alichukua picha alizosafisha na kumpelekea Kilole.

Itaendelea Ijumaa
 
SEHEMU: 12
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.

ILIPOISHIA:
Kilichomshangaza ufunguo wa chumba chake alikuwanao mwenyewe. Alijikuta akishtuka na kujiuliza nani aliyechukua. Alikumbuka changudoa aliyelala naye na kuondoka akiwa amelala ndiye aliyechukua zile picha, alijiuliza amezichukua ili iweje.
Wasiwasi wake mkubwa ulikuwa kama zikivunja lazima Kilole atamuona hana manaa hata kumfanyia kitu kibaya.
Alipanga usiku akamtafute ili amrudishie picha zake, alichukua picha alizosafisha na kumpelekea Kilole.

SASA ENDELEA...
******
Kama alivyoelekezwa akitaka kupeleka picha alitakiwa amjulishe kwa simu ili azifuate mwenyewe kuliko kuingia ndani, kuondoa wasiwasi kwa Kinape. Jimmy alipofika alimpiga simu Kilole aliyekuwa amekaa sebuleni na Kinape wakitazama runinga.
Kilole baada ya kuona namba ya Jimmy aliikata simu na kuelekea chumbani bila Kinape kujua kinachoendelea. Alipofika chumbani alimpigia na kumuuliza:
“Vipi Jimmy?”
“Nimekwishafika.”
“Poa nakuja.”
Kilole alichukua upande wa kanga na kujitanda ili akirudi asionekane amebeba kitu, alipofika sebuleni Kinape alimuuliza:
“Vipi shemu?”
“Natoka kidogo.”
“Wapi tena?” “Nafika dukani.”
“Vipi utachelewa? Maana Happy kanipigia simu nimfuate ili nimpeleke hospitali hajisikii vizuri.”
“Sichelewi nisubiri, nafika dukani mara moja.”
“Hakuna tatizo.” Kilole alitoka nje na kwenda alipokuwa Jimmy, alipofika Jimmy alijitoa sehemu alipokuwa amesimama.
“Vipi tayari?”
“Tayari.”
“Poa.”
Kilole alichukua bahasha na kumpa fedha iliyobakia huku akiendelea kumsisitiza: “Jimmy nimekuamini kukupa kazi ya hatari, kama ukivujisha ishu hii ujue sitaona hatari kunyongwa kwa ajili yako. Nimekupa malipo mazuri ili kuhakikisha ufanyi uzembe wowote, au kuna kitu kimekwenda kinyume na mpango wetu?”
“Hapana.”
Jimmy alijibu akiwa na wasiwasi wa picha zilizopotea katika mazingira ya kutatanisha. Akiwa katikati ya mawazo Kilole alimshtua:
“Vipi mbona kama kauli yangu imekushtua?”
“Ha..ha..pana,” Jimmy alibabaika.
“Jimmy usiwe umefanya makosa tusije tukalaumiana, japo unaniona mwanamke kwenye hili nitakuwa zaidi ya mwanaume,” Kilole alizidi kusisitiza.
“Kilole mbona unanitisha kama uliona siwezi au huniamini kwa nini ulinipa kazi hii?”
“Si kwamba nakutisha maelezo yangu naona kama yamekubadili muonekano wako.”
“Wasiwasi wako tu, lakini nipo makini kuliko unavyofikiria.”
“Mmh! Sawa lakini zingatia hilo picha zote kwenye kamera umefuta?”
“Ndiyo.”
“Hebu nipe kamera nione.”
Jimmy alimpa kamera na kuangalia picha zilizokuwa zimebaki kwenye kamera hakuona picha ya tukio hata moja.
“Jimmy nakuamini najua huwezi kuniangusha.”
“Usihofu.”
Waliagana ili kumpumbaza Kinape alikwenda hadi dukani na kununua vitu vya kutafuna na kurudi navyo ndani. Alipofika sebuleni alimtupia bazoka Kinape na kumweleza:
“Unaweza kwenda lakini usichelewe.”
“Hakuna tatizo.”
Kinape alijibu huku akinyanyuka kujiandaa kwenda kwa mpenzi wake Happy bila kujua Kilole alimtoa kijanja ili apate nafasi ya kuangalia picha zake na kujipanga kumrudisha Kinape mikononi kwake na kuvunja penzi lao. Baada ya kuingia chumbani hakujiamini alijifungia kwa ndani na kuanza kupitia picha moja baada ya nyingine.
Zilikuwa picha alizozitalajia zenye kuonesha penzi la ushirikiano, picha zile zilimfanya atabasamu na kujikuta akiruka juu na kujitupa kitandani kuonesha alichokitaka ndicho kilichofanyika. Alijisemea kwa sauti ya chini:
“Kinape kwisha habari yake.”
Aliziweka picha vizuri na kiendelea na shughuli zake moyoni akiwa na furaha tele.
****
Baada ya kumaliza semina ya kikazi Deus alirudi nyumbani Tanzania, uwanja wa ndege alipokewa na mkewe Kilole na mwanaye mpenzi Gift.
Pia alikuwepo rafiki yake kipenzi Kinape na mpenzi wake Happy. Baada ya kufika Kilole alijitupa kifuani kwa mume wake kuonesha kweli alikuwa amekosa mahaba yake.
“Jamani mume wangu baba Gift, karibu sana nyumbani, yaani siamini macho yangu,” alijiliza machozi ya uongo.
“Mke wangu mbona hata wiki haikufika?”
“Basi hunipendi mume wangu, yaani nilivyoteseka unasema hivyo.”
“Basi mke wangu, mengine tutakwenda kuzungumzia nyumbani.”
Jinsi alivyokuwa akideka kwa mumewe Kinape alichekea moyoni na kuona jinsi mwanamke alivyo nyoka kwa kumdanganya mumewe anampenda kumbe anamla kisogo. “Mmh! Kinape za siku mbili tatu?”
“Nzuri tu best, za huko?”
“Eeh bwana nzuri tu, nimefurahi kuwakuta wote wazima, hii imenipa faraja kuwa wewe si rafiki bali ni ndugu wa damu kwa kuweza kuitunza familia yangu kipindi chote nilipokuwa mbali nayo.”
“Ni wajibu wangu kuilinda familia yako,” Kinape alisema huku moyoni ukiumia kwa kitendo cha kutembea na Kilole.
“Shemu vipi?” Alimgeukia Happy mpenzi wa Kinape.
“Safi, pole na safari shemu.”
“Asante, nina imani baada ya kurudi nitafanya kila niwezavyo kuhakikisha mnafunga ndoa.”
“Nitashukuru shemeji maana ndugu yako amekuwa mzito.”
“Best, umekwisha kwenda kumtambulisha shemu nyumbani?” Deus alimuuliza Kinape. “Nilisubiri urudi baada ya kufika nina imani ni muda muafaka sasa kwenda kumtambulisha mpenzi wangu nyumbani.”
Kauli ile ilikuwa kichefuchefu moyoni mwa Kilole na kujisemea kimoyomoyo: “Tutaona mimi na huyu mjinga mwenzenu nani zaidi.”
Moyoni aliapa kulivunja penzi la Kinape na Happy kwa msaada wa zile picha.
********
Baada ya Deus kurudi, kutokana na makubaliano kati ya Kinape na Kilole heshima ilirudi na kuitana mtu na shemeji yake. Pamoja na makubaliano hayo Kilole alitamani siku moja moja amtoroke mumewe na kwenda chumba cha Kinape kupata penzi la hamu. Lakini mara zote Kinape alikuwa makini hasa usiku alijifungia kwa ndani na kuwasha muziki kama Kilole atamfuata atasingizia hakusikia. Ilikuwa kama alivyowaza usiku mmoja Kilole alimuacha mumewe amelala na kwenda kwa Kinape.
Lakini kikwazo kilikuwa mlango uliofungwa kwa ndani, alipojaribu kugonga kwa taratibu sauti ya mlango ilimezwa na sauti ya muziki uliokuwa ukilia chumbani. Kilole alikasirika na kujikuta akipandwa na hasira akiwa tayari kutumia turufu ya picha chafu ili kumtisha Kinape na kukubaliana na masharti yake.
“Kinape mbona jana ulifunga mlango kwa ndani?” Kilole alimuuliza kwa sauti ya chini baada ya kukutana kwenye korido la msalani.
“Lini ulikuta mlango upo wazi na ulikuwa na shida gani?”
“Hujui au ndiyo ushanichezea kisha uniache?”
“Lakini hii si sehemu ya mazungumzo haya, tulizungumza nini mumeo akirudi?”
”Kuzungumza nini, mbona ulifunga mlango?”
“Jamani, si chumbani kwangu?”
“Ilianza lini ina maana unaogopa kuibiwa.”
“Ni utaratibu wangu wa siku zote.”
”Kwa nini uliwasha muziki?”
“Sasa hayo ni maswali gani?”
“Najua ulifanya vile ili nikigonga usinisikie.”
“Lakini lawama za nini, ulinieleza utakuja nikakufanyia hivyo?”
“Basi baadaye..” Kilole alisema baada ya kusikia akiitwa na mumewe. Baada ya kuondoka Kilole kuitikia wito wa mumewe, Kinape alibakia amesimama na kuona aliyoyakataa ndiyo yameanza na siku zote penzi kikohozi huwa halina siri.
Aliamini njia ya kujiepusha na tatizo lile ni kuhama kisha kufanya mpango wa haraka kukaa na Happy. Alipanga siku ile ile azungumze na Deus kwenda kujitambulisha nyumbani kwao Happy ili siku inayofuata naye ampeleke kijijini kumtambulisha kwa wazazi wake kabla ya kupanga mipango ya ndoa.
Aliamua jambo lile kulifanya kwa siri kuepuka vikwazo vya Kilole. Baada ya kufungua kinywa Kinape na Deus walitoka pamoja, njiani alimweleza dhamira yake ya kwenda kujitambulisha kwa kina Happy siku ile. “Mbona haraka sana?” Deus alimuuliza. “Nilipanga leo niende ila nilisahau kukujulisha, nataka kesho niende na Happy kijijini, isingekuwa vizuri kuanzia kwetu kabla ya mimi kujulikana kwao.”
“Hakuna tatizo, ni saa ngapi?”
“Saa mbili usiku.”
“Hakuna tatizo tutakwenda.”
Waliagana kila mmoja aliendelea na shughuli zake, Kinape ilibidi asubuhi ile ile ampigie simu Happy kumjulisha kuwa usiku wana ugeni wa kujitambulisha. Japo ilimshtua kuona imekuwa ghafla, lakini ilikuwa habari njema aliyoisubiri kwa hamu kama tone la maji katika kiu kali.
Nafasi ile hakutaka kuipoteza kwa kufanya maandalizi ya kupokea ugeni wa mchumba wake. Maandalizi yalikwenda vizuri na kumsubiri ugeni wa usiku huku Happy akiona ndoto yake ya kuolewa na Kinape imeanza kuwa kweli.
*****

Deus kama kawaida yake alikuwa hawezi kufanya jambo lililo kuwa nje na ratiba zake za kila siku bila ya kumtaarifu mkewe. Kwa vile walikubaliana na Kinape wakutanie mjini na kwenda moja kwa moja nyumbani kwa mchumba wake. Aliamua kumjulisha mkewe baada ya kumaliza kazi zake majira ya saa moja na nusu usiku. Ujumbe ule ulimshtua Kilole kitu kilichomshangaza mumewe.
“Mbona umeshtuka hivyo?” Deus alimuuliza mkewe.
“Nimeshtuka kwa vile jambo hilo mmelifanya kwa siri.”
“Kuna siri gani kama nimekupigia simu kukujulisha?” “Mbona hamkuniambia toka asubuhi.”
“Hili suala nimeambiwa asubuhi njiani na Kinape wakati nakwenda kazini.”
“Mmh! Sawa, nawatakia utambulisho mwema.”
“Hayo ndiyo maneno, na kesho wanakwenda kijijini kwa utambulisho wa upande wa pili.”
“Atiii?” “Mbona umeshtuka tena?”
“Sasa mbona mambo mnafanya mambo kienyeji,” Kilole alikuja juu kwa hasira za kweli huku wivu ikimpanda.
“Mke wangu kwani tatizo nini, haya si maandalizi ya awali, mipango ya harusi ikianza wewe utakuwa na majukumu makubwa kuliko unavyodhani.”
“Mmh! Haya, basi endeleeni na maandalizi mema.”
Baada ya kukata simu Kilole alijikuta moyo ukimuuma kwa kusikia habari zile, Alijiapiza kupitia picha zile lazima atahakikisha Kinape hamuoi Happy, alijikuta akipoteza furaha ya siku nzima na kujuta kupokea simu ya mumewe.
Baada ya kukata simu alikwenda chumbani na kurudia kuziangalia picha upya huku akiamini picha zile ndiyo suruhu ya kuangaika kwa Kinape. Alizirudisha kwenye bahasha na kuzificha sehemu yake. Utambulisho wa Kinape ulikwenda vizuri huku familia ya Happy akionesha furaha ya mtoto wao kupata mume.
Happy akiwa ndiye mtoto wa kwanza kuchumbiwa, baba yake mzazi aliwaahidi nyumba na gari kama zawadi kwa mtoto wake wa kwanza. Kinape naye aliwaahidi kumpeleka mchumba wake nyumbani kwao siku ya kesho yake. Walipewa baraka zote za familia za wazazi wa Happy kwenda kutambulishwa kijijini kwao.

*****
Kilole alijikuta akikosa raha na kumfanya atangetange sebuleni kama kuku anayetaka kutaga, akitoka upande mmoja kwenda mwingine, nyumba aliiona chungu. Moyoni aliendelea kujiapiza juu ya kuhakikisha Kinape hamuoi Happy.
Alijikuta amesahau hata kupika chakula cha usiku kwa ajili ya kumfikiria Kinape. Honi ya gari ya mume wake ilimfanya akimbilie ndani na kujilaza kitandani kusingizia anaumwa ili asiulizwe chakula cha usiku. Mume wake aliingia ndani alimkuta amejifunika shuka gubigubi.
“Vipi mke wangu?”
“Sijisikii vizuri.”
“Hali hii imeanza saa ngapi?”
“Wakati najiandaa kupika.”
“Basi amka twende hospitali.”
“Nimemeza dawa kidogo kichwa kimeanza kutulia.”
“Kwa maana hiyo hujapika?” “Nipike saa ngapi mume wangu, ungeniona nilivyokuwa ungenikimbiza hospitali.”
Itaendelea Jumatatu
 
SEHEMU: 13
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500

ILIPOISHIA:
“Wakati najiandaa kupika.”
“Basi amka twende hospitali.”
“Nimemeza dawa kidogo kichwa kimeanza kutulia.”
“Kwa maana hiyo hujapika?”
“Nipike saa ngapi mume wangu, ungeniona nilivyokuwa ungenikimbiza hospitali.”
SASA ENDELEA...

“Lakini si umekunywa dawa ya kutuliza kwa nini tusiende hospitali?”
“Mume wangu huwezi kuamini kuja kwako kama umenipa dawa, sasa hivi sijambo kabisa.”
“Mmh! Basi kama ni hivyo, jiandae baadaye twende tukachukue take a way.”
Baada ya kutengeneza uongo wake na kufanikiwa bado moyo wake bado uliendelea ulimuuma kila alipomuwaza Kinape na kibaya zaidi habari za kujitambulisha kwao na Happy alimueleza mbele ya mumewe.
“Samahani shemeji.”
“Samahani ya nini?”
“Sikukueleza mapema kuwa naitakwenda kujitambulisha nyumbani kwao na Happy, pia kesho nakwenda kijijini kumtambulisha mwenzangu.”
“Mmh! Safari njema,” (moyoni alijisemea tutaona si muda mrefu jeuri yako itakwisha)
***
Siku ya pili Kilole alikuwa na wakati mgumu kufikisha ujumbe kwa Kinape ili kuzuia asiweze kwenda kijijini kumtambulisha mchumba wake. Lakini juhudi zake zilikuwa bure, baada ya kuondoka na katika gari moja na mumewe. Roho ilimuuma sana kwa hila za Kinape za kumkwepa kwa kuondoka na mumewe kwenye gari moja. Alijifikiria kupiga simu kumzuia Kinape na kumweleza ukweli juu ya picha zile, lakini alisita kwa kuhofia mabadiliko yoyote yatakayo tokea kwa Kinape lazima mumewe angemtilia wasiwasi na pengine siri kutoka nje kabla ya kutimiza lengo lake.
Aliamua kumsubiri akirudi na kuingia anga zake ndipo amlipue. Kinape bila kujua kuna mpango kabambe wa kuvunja mipango yake ya kumuoa Happy. Utambulisho ulikwenda vizuri, familia ya Kinape kumpokea kwa bashasha mchumba wa mtoto wake huku wakimuahidi kumpa ushirikiano mkubwa kufanikisha ndoa ya mtoto wao.
Baada ya utambulisho walirudi mjini kujipanga kwa ajili ya maandalizi ya harusi ambayo Deus alimuahidi Kinape kuyasimamia kwa asilimia mia. Kinape aliutumia muda mwingi kumkwepa Kilole kwa kurudi muda ambao atakuwa amewasiliana na Deus kama yupo nyumbani. Hata walipokutana kwa bahati mbaya hakutaka kuzungumza kwa muda mrefu kwa kisingizio cha Deus yupo.
Moyoni Kilole alijiapiza hata kumfuata Kinape ofisini na kumweleza uchafu ule kwa kuugeuza upande wa pili kana kwamba Kinape ndiye aliyefanya mchezo ule.
Alipanga kufanya vile kabla mipango ya harusi haijaanza, lakini aliamua kuonesha kama halikumuuma baada ya kutumia nguvu bila mafanikio. Siku moja akiwa anaendelea na kazi zake alishangaa kumuona Kinape akirudi mchana ghafla huku akionekana ana wasiwasi mwingi.
“Vipi Kinape mbona leo mchana?”
“Kuna vitu nilisahau kuondoka navyo asubuhi, hivyo nimerudi kuvichukua,” alisema huku akielekea chumbani kwake.
Kilole alimsindikiza kwa macho huku akijiuliza aitumieje nafasi adimu kama ile, wazo la haraka lilimjia aanza kujiliza ili kuonesha kuna kitu kimempata na Kinape akiuliza basi afumue mzinga wa nyuki. Kinape wakati anatoka alishangaa kumkuta Kilole akilia kilio cha kwikwi.
“Shemu vipi?” Alimuuliza huku akimsogelea.
“Siamini kama unaweza kunifanya uliyonifanyia, sawa hunitaki kwa nini unataka kunivunjia ndoa yangu?”
“Kilole mbona sikuelewi!” Kinape alishangaa kusikia habari zile.
“Kinape nimekufanya nini?”
“Subiri usiondoke uone unyama ulionifanyia, nikiachika utapata faida gani?” Kilole alisema kwa sauti ya kilio.
“Mbona sikuelewi nimekufanyia nini?” Kinape alizidi kushangaa.
“Nimekuambia subiri halafu uniambie kama ulichokifanya ni haki.”
“Fanya haraka nimeomba ruhusu mara moja nifuate kalatasi hizi.”
Kilole alikwenda chumbani na kuchukua picha chafu walizopiga wakifanya mapenzi na kumpelekea Kinape aliyekuwa amesimama wima akimsubiri huku akionesha wasiwasi.
Alipofika alimpa baadhi ya picha na zingine kuziacha ndani, Kinape alipokea bahasha ya picha na kuanza kutoa picha moja, alishtuka kuziona picha zilizoonesha wakifanya mapenzi na Kilole.
“Ha! Hizi nini?” Kinape alishtuka huku akiendelea kuchambua picha.
“Nikuulize wewe, kwa nini umeamua kunidhalilisha kiasi hiki, kumbe ulikuwa na lako jambo, hebu fikiria picha hizi zimfikie mume wangu mimi nitakuwa mgeni wa nani?” Kilole aliangua kilio cha uongo na kuzidi kumchanganya Kinape.
“Wewe hizi picha umezitoa wapi?” Kinape aliuliza huku jasho la hofu likimtoka.
“Kuna mtu kazileta anasema kaziiba kwa jamaa mmoja ambaye amekula naye njama ili kunidhalilisha,” Kilole alisisitiza kama kweli.
“Nioneshe huyo aliyeleta picha hizi aeleze kazitoa kwa nani na huyo mwenye picha aseme kama mimi ndiye nilifanya mpango huu. Haki ya nani, leo ndiyo naziona hizi picha, sijui lolote maskini wa Mungu,” Kinape alizidi kujitetea.
“Kinape umebadilika baada ya kunivua nguo, shukurani yako kunidhalilisha, kwa taarifa yako najua kabisa nipo uchi pengine si mmoja aliyeziona kuna wengi. Pia wasiwasi wangu huenda zingine zimebaki na hizi ni baadhi ya hizo picha.
“Kwa maana hiyo bora nimweleze ukweli mume wangu na kumuonesha hizi picha nijue moja, anisamehe kwa kumuomba msamaha au aamue atakacho amua kwa vile siwezi kumlilia mtu. Inawezekana kabisa ulifanya makusudi ili niachike baada ya kuona nilikusaliti.”
“Kilole sijui nikueleza kitu gani ili unielewe, haki ya nani sijui lolote kuhusiana na hizi picha, pia nakuomba usimuoneshe mumeo wala kumueleza tulivyo hujumu ndoa yake, ni hatari si unajua jamaa ana bastora anaweza kuniua.”
“Naweza nisimwambie na kukaa kimya, kumbuka nimetoa laki tano ili nipewe hizi picha, kama zipo zingine wanashindwa nini kumuuzia mume wangu. Akijua uchafu wetu sura zetu tutaziweka wapi?” “Yaani nichechanganyikiwa hata sijui nikwambie nini.”
“Kinape hii ni hatari.”
“Kweli ni hatari tena kubwa, hivi Deus anavyoniamini nitamwambia nini akiona hizi picha?”
“Ndiyo maana nikaona bora nijisalimishe kwa mume wangu sina jinsi, kama picha hizi zikimfikia tumekwisha.”
“Mmh! Yaani hata sijui nani kafanya mchazo mchafu kama huu?”
“Unajua kila kitu lakini unanizunguka, kwani Kinape hapa jiji wapo wangapi?”
“Siwezi kujua labda wapo wengi.”
“Ina maana hiyo Kinape pia ni ndugu yake Deus.”
“Mmh! Yaani aliyeleta kasema hivyo?”
“Tena inasemekana umempa laki tatu, ndio maana kataka laki tano ili anipe picha.”
“Yaani, nimechanganyikiwa hata nguvu zimeniisha,” Kinape alisema huku akiketi kwenye kochi baada ya nguvu kumwisha ghafla.
“Kinape nilikuwa na maamuzi mawili?”
”Yapi hayo?”
“Moja la kujisalimisha kwa mume wangu, la pili kumuwahi Deus kabla picha hazijamfikia.”
“Utamuwahi vipi?”
”Ikiwezekana hata kumuua huoni hili likifika kwa wazazi litakuwa baya zaidi.”
“Mmh! Tumefika mbali sana huo si mpango mzuri.” Kinape alipinga mpango ule.
“Basi kama hatuwezi tumwambie.” “Bado huo si uamuzi sahihi.”
“Sasa tufanye nini?” “Tutafute njia nyingine zaidi ya hii.”
“Mimi nina siri za mume wangu kama tutazifikisha Takuru lazima atafungwa.”
“Sasa wewe utabaki na nani?”
“Na wewe.”
”Na Happy?”
“Kwa ulichokifanya heri niwe na wewe kwa vile siwezi tena kurudi kijijini.”
“Hapana, basi tutafute njia nyingine.”
”Hiyo nyingine nipe wewe.”
“Sina.”
“Basi wacha ninywe sumu ili ufurahi siwezi kuona nahukumiwa kwa kosa la kwako.
” Kilole alimtishia Kinape.
“Usinywe sumu bado tunaweza kujipanga kuhakikisha tunamdhibiti.”
“Nakupa siku moja kuhakikisha unapata ufumbuzi bila hivyo nitakacho amua tusilaumiane.” “Lakini naomba usimwambie kwanza Deus,” Kinape alijikuta akichanganyikiwa baada ya kukosa jibu la tatizo lililokuwa mbele yake.
“Ni wewe wa kunifanya nisimwambie, nataka kabla habari hizi hazimfikia tuwe tumekwishajua tumefanya nini.” “Nimekuelewa, yaani hata kazini sirudi nguvu zimeniisha,” Kinape alichanganyikiwa. “Kinape wewe mwanaume unatakiwa kuonesha unaweza kukabiliana na chochote kinachotokea mbele yako. Mbona mimi niliyetendewa sijachanganyikiwa zaidi ya kupanga mikakati ya kujiokoa na janga hili.”
“Najua huwezi kunielewa sijui lolote kuhusiana na hizi picha, kwa kweli zimenichanganya sana.” “Kwa kusema hivyo ina maana nimezipiga mimi?”
“Hapana sina maana hivyo, ila nimechanganyikiwa sijui hata nani aliyefanya mchezo mchafu kama huu.”
“Ndiyo tunatakiwa tutafute njia ya kujiepusha, kumbuka hili ni bomu likipasuka hakuna atakayepona.”
“Basi inawezekana alipoondoka aliweka mpelelezi ili atufuatilie.”
“Atufuatilie kwani anajua chochote kuhusiana na penzi letu la zamani?”
“Inawezekana kuna mtu anayetujua alipotuona tupo pamoja alimweleza na kuamua kufanya upalelezi.”
“Aweke asiweke lazima tutumie njia ya kumdhibiti kabla hajafanya lolote.”
“Sasa tutamdhibiti vipi?” “Kwa nini tusimuwekee sumu afe,” Kilole alisema bila wasiwasi. “Kilole mbona mpango huo ni mbaya!”
“Unafikiri tukimchelewesha akigundua lazima atatuua kwa risasi.”
“Tukimuua tutakosa fadhira hata Mungu atatulaani, tutafute njia nyingine ya kumdhibiti, ngoja nitoke nikirudi nitakupa jibu ila nakuomba chonde usimueleze Deus chochote kuhusiana na habari hii.”
“Siwezi hata mimi natamani kuishi maisha marefu.”
Baada ya kukubaliana Kinape aliondoka na kumwacha Kilole akifurahia mpango wake umekwenda kama alivyopanga. Aliamini jioni akirudi cha kwanza kitakuwa kuvunja uchumba wake na Happy kisha mengine yangefuata ya kumdhibiti Deus ili abaki na Kinape.

Itaendelea Jumatano
 
SEHEMU: 14
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500

ILIPOISHIA:
Baada ya kukubaliana Kinape aliondoka na kumwacha Kilole akifurahia mpango wake umekwenda kama alivyopanga. Aliamini jioni akirudi cha kwanza kitakuwa kuvunja uchumba wake na Happy kisha mengine yangefuata ya kumdhibiti Deus ili abaki na Kinape.
SASA ENDELEA...
****
Deus akiwa ofisini kwake akipitia ripoti ya uchunguzi wa wauzaji sugu wa madawa ya kulevya, simu toka kwa sekretari wake iliita. Alipokea mkono mmoja, mwingine ukiwa bado umeshikilia kwenye kalatasi ya ripoti.
“Haloo, ofisi ya kuzuia madaya ya kulevya hapa, nazungumza na nani?”
“Msamalia mwema.”
“Ndiyo Msamalia mwema, nikusaidie nini?”
“Mkuu, ndege ya shirika la Swiss air, inayoingia saa kumi na moja jijini Dar kuna dada mmoja mwenye umbile la kati maji ya kunde nywele za kipilipili, amevalia gauni fupi jekundu chini viatu virefu na kwapani atabeba mkoba wa rangi sawa na nguo zake.
”Pia anaweza kuwa miwani ya rangi hiyo hiyo kama atakuwa ameivaa kama ataivua basi chukueni vigezo nilivyo waeleza. Dada huyu ana dawa za kulevya mkamateni na kumpekua.”
“Samahani unazungumza toka wapi?” “Si muhimu kujua zaidi ya kufuatilia taarifa niliyokupa, asante.” “Haloo...haloo...”
Deus alichelewa simu ilikuwa imekatwa. Alinyanyuka na kutoka hadi kwa sekretari kuulizia simu inatoka wapi.
“Haloo Happy, simu inatoka wapi?”
“Namba zinaonesha inatoka Itary.”
“Asante,” Deus alijibu na kurudi ofisini kwake. Alijikuta akijiuliza aliyetuma taarifa na kujiita msamalia mwema alichokisema kina ukweli au ndiyo kutaka kuwasumbua. Lakini hakutaka kuipuuza taarifa ile, aliwaita vijana wake na kuwapa habari zile na kuwaeleza wafuatilie ndege ile kama kweli yupo huyo mwanamke basi akamatwe na kupekuliwa.
Kwa vile ilikuwa imebakia saa moja kabla ya ndege kuingia, aliwahimiza vijana wake kufika eneo husika kabla ndege haijafika. Baada ya kuwapa majukumu vijana wake aliendelea kupitia ripoti ya wauza dawa za kulevya sugu.
*****
Majira ya saa kumi ndege ya shirika la ndege la Swiss air iliwasiri uwanja wa ndege wa mwalimu JK Nyerere. Vijana wa Deus alikuwa katika kona yao kama kawaida. Baada ya ndege kusimama na mlango kufunguliwa waliteremka abiria mmoja mmoja waliokuwa katika mistari.
Dada mmoja maji ya kunde mwenye nywele fupi gauni jekundu fupi lililoishia juu kidogo ya magoti na viatu virefu alikuwa mmoja ya abiria katika ile ndege. Baada ya kutoka kwenye mlango wa ndege hakuteremka haraka aliangalia mandhali ya Tanzania kisha alivaa miwani yake nyekundu na kuteremka taratibu kwenye ngazi za ndege na kuelekea kwenye ukaguzi.
Vijana wa Deus hawakupata shida ya kumuona yule binti aliyeonekana mrembo tena bado mbichi. Walitegemea kusikia chochote kutoka sehemu aliyopitia, lakini alipita salama. Hawakuwa na haraka ya kumkamata walisubiri kuona yupo na nani pia mizigo yake.
Baada ya kutoka chumba cha usafiri alielekea kwenye gari aina ya Ranger Rover ‘Vogue’ ya rangi nyeusi iliyokuwa umepaki pembeni. Alipokaribia mlango ulifunguliwa, kabla hajaingia kikosi cha kuzuia dawa za kulevya kilifika na kujitambulisha kisha walimweka chini ya ulinzi msichana yule ambaye hakuonesha wasiwasi.
“Jamani vipi?” aliuliza huku akitoa miwani usoni. “Sisi ni askari wa kikosi cha kuzuia dawa za kulevya, tuna wasiwasi na wewe.”
“Mna wasiwasi gani?” “Tunaomba ufike kituoni kwa ajili ya upekuzi.” “Mbona mnanishangaza, ina maana wakaguzi wa kiwanjani hawafai?” Aliuliza kwa kuwashangaa askari wale.
“Samahani tunaomba ufuate maelekezo yetu.”
Wakati huo gari lao lilisimama pembeni yao na kumuomba aingine ndani ya gari. Kabla ya kuondoka yule msichana aliwaomba vitu vyake vitangulie nyumbani.
“Jamani vitu vyangu si hivi ngoja nivifungue hapahapa ili muone nimeweka wapi hayo madawa ya kulevya,” Alisema yule msichana huku akifungua pochi yake na kuvimwaga vyote vilivyokuwa ndani ya pochi kisha alitaka kufungua brif case ili vitu vilivyomo ndani avimwage chini waone kuna nini. Lakini walimkataza asifanye vile kwa vile kuna sehemu zake.
“Dada kwani tatizo lako nini, wewe twende ofisini, sisi tumetumwa tukukamate mengine anajua mkuu wetu, ingekuwa hatukutumwa wala tusingekusumbua,” askari mmoja alisema.
“Lakini kumbukeni nimechoka natakiwa kupumzika.”
“Tunajua, lakini sisi tumetumwa, hatuwezi kurudi mikono mitupu wakati mtu tuliyetumwa tumemuona.”
“Nani anayenifahamu na kuwatuma mje mnikamate, kumbukeni nitashitaki kwa kunidhalilisha,” binti yule alitishia. “Hatujakudhalilisha kwa vile hakuna mtu anayejua kinachoendelea hapa, zaidi ya wewe kumwaga vitu vyako bila kukuambia.”
“Basi turudini chumba cha ukaguzi uwanja wa ndege ili mnikague, ili niwahi nyumbani kuna mtu nimeahidiana kukutana naye.”
“Dada kuwa mwelewa, si wewe umevaa gauni jekundu?” Askari mmoja alimuuliza akisoma karatasi bila kumtazama. “Ndiyo.”
“Pochi yako nyekundu?”
“Ndiyo.”
“Miwani nyekundu?” “Ndiyo,”
“Na viatu vyako virefu?”
“Ndiyo.”
“Nywele zako za kipilipili?”
“Ndiyo.”
“Rangi maji ya kunde?”
“Ndiyo.”
“Sasa dada haya tumeyajulia wapi sisi?”
“Hata mimi nashangaa sijui nani anataka kunichafua?”
“Ungekuwa na tofauti na hii iliyoandikwa kwenye karatasi tusinge kugusa lakini kila kilichoandikwa kwenye karatasi unacho kwa asilimia mia,” walimweleza huku akimpa karatasi iliyokuwa na maelezo yote.
Askari walikuwa na uhakika kwa pale hakukuwa na ushahidi wowote kuwa yule dada kaingia na dawa za kulevya. Hata kama ilikuwa biashara yake siku ile walikuwa wamechemsha.
“Mmh! Sina jinsi twendeni lakini mnanipotezea muda bure,” alijitetea yule msichana aliyeonekana kujiamini katika mazungumzo yake.
Kama isingekuwa amri toka kwa mkubwa, waliona hakuna haja ya kumpoteza muda wake bure wangemuachia. Lakini vigezo vyote walivyoelezwa na mkuu wao Mr Deus ndivyo alivyokuwa navyo kwa asilimia mia. Hivyo hawakuwa na budi kumpeleka kwa mkuu wao. Walimuingiza kwenye gari na kumpeleka makao makuu kwa ajili ya upekuzi. Kabla ya kuondoka aliomba mkoba wake ambao hauna kitu utangulie nyumbani.
“Sasa kaka zangu kwa vile mkoba wangu hauna kitu naomba basi utangulie nyumbani.”
“Dada yetu haturuhusiwi kupoteza ushahidi wowote uliokuja nao, vyote vinatakiwa ili kukamilisha ushahidi.”
“Hakuna tatizo,” alijibu kwa kujiamini kitu kilichowafanya askari waamini hana kosa.
“Sasa Teddy itabidi nikufuate?” Dereva wa Ranger Rover alimuuliza mgeni wake.
“Noo Danny, tangulia nyumbani nitakuja sasa hivi kwa vile nakwenda kukamilisha walichotumwa na mkuu wao. Lakini kwa upande wangu sina tatizo lolote.”
Maneno ya kujiamini ya msichana yule yalikuwa na nguvu kubwa ya askari kumuachia lakini kwa vile walikuwa wakitimiza agizo la mkubwa wao hawakuwa na budi kumpeleka.
Walimuingiza kwenye gari na kumpeleka makao makuu kwa ajili ya kutimiza wajibu wa kazi. Walipofika walimpitisha chumba cha upekezi na kufanya upekuzi wote wa awali ambao haukuonesha dawa za kulevya. Taarifa alipelekewa mkuu wao Mr Deus.
“Mkuu hana kitu chochote.” “Mmempekuwa vizuri?”
“Ndiyo mkuu.”
“Mmetumia vifaa vya kisasa?”
“Vyote mkuu.”
“Mmempa chakula kigumu?”
“Kila kitu ujuacho tumekifanya lakini hatukumkuta na dawa.”
“Sasa aliyenipigia simu alikuwa na maana gani?”
“Kwani taarifa zimetoka wapi?” “Kwa msamalia mwema mmoja toka Itaria.”
“Ni kweli dada huyu anatoka Itaria.”
“Ina maana alikuwa anatudanganya?”
“Mkuu, huenda kweli anashughulika na biashara hii, lakini huenda njia aliyotumia si ile ambayo mtu aliyetutumia taarifa anaijua.”
“Inawezekana.”
“Lakini mmemuonaje?”
“Kwa kweli haoneshi wasiwasi zaidi ya kulalamikia muda wake.”
“Sasa fanyeni hivi mfuatilie mpaka atakapofikia fanyeni dolia usiku kucha ili tupate kujua kama kasingiziwa au ndiyo kazi yake.”
“Tutafanya hivyo mkuu.”
“Basi kamwachieni aende.” Kabla kijana wake hajaondoka alikumbuka kitu kimoja na kumwita.
“John hebu rudi kwanza.”
“Ndiyo mkuu.”
“Hebu mleteni hapa kabla ya kuwachia kuna maswali mawili matatu nataka kumuuliza.”
“Hakuna tatizo mkuu.”
John alitoka baada ya muda alirudi na yule msichana aliyekuwa mrembo kwenye macho ya mwanaume.
“Shikamoo,” yule msichana alimsalimia Mr Deus. “Marahaba, hujambo?”
”Sijambo mkuu.”
“Karibu ukae,” alimwambia huku akimuonesha sehemu ya kukaa.
“Asante,” Alijibu huku akikaa kwenye kiti. Baada ya ukimya mfupi Mr Deus alituliza macho kwa binti yule ambaye alikuwa ameinama chini. “Unaitwa nani?”
“Thereza Mayunga.”
“Ni Mtanzania?”
“Ni Mtanzania mwenye uraia wa Itaria.”
“Naomba Paspoti yako.” Teddy alifungua mkoba wake na kutoa paspoti na kumkabidhi Mr Deus, aliipokea na kuisoma kwa muda kisha alimrudishia.
“Okay, Wazazi wako wapo wapi?”
“Kwa kweli siwajui, ila niliambiwa niliibiwa nikiwa na umri wa miaka mitano na mwanamke mmoja aliyekuwa akikaa Itaria ambaye alinifanya mwanaye mpaka alipokaribia kufa ndipo aliponieleza kuwa wazazi wangu wapo Tanzania ila hakujua wapo wapi. Pamoja na kuniiba bado jina langu na la baba yangu hakulibadilisha.”
“Una shughulika na nini?”
“Ni mfanya biashara wa vitu mchanganyiko.”
“Hapa Dar unafikia wapi na kwa nani?”
“Nafikia Masaki kwa ndugu wa marehemu mume wangu.”
“Mumeo alikuwa Mtanzania?”
“Ndiyo.” “Okay, unaweza kwe...” Mr Deus kauli yake ilikatwa na mlio wa simu ulioingia kwenye simu yake. “Samahani,” alisema huku akipokea simu. “Bila samahani,” alijibu Teddy. Mr Deus alipokea simu na kuzungumza kwa sauti ya chini. “Eeh.”
“Mkuu simu ile ya Italia.”
“Okay, nipe nizungumze naye.”
“Haloo.”
“Haloo mkuu.” “Ndiyo.”
“Mmemuona?”
“Hebu subiri kidogo,” Mr Deus alisema huku akimuomba yule msichana amsubiri nje mara moja. “Hakuna tatizo,” alijibu yule binti huku akinyanyuka na kutoka nje. Baada ya kutoka Mr Deus alirudi hewani.
“Ehe! Msamalia mwema.”
“Nauliza mmemuona?”
“Ndiyo.”
”Mmepata hayo madawa?”
“Hatujayapata.”
“Nilijua hamuwezi kupata kitu.”
“Sasa kama ulijua hatupati kitu kwa nini umetusumbua?”Mr Deusi aliuliza kwa sauti hya ukali kidogo. “Siyo kuwasumbua, niligundua nilifanya kosa katika maelezo ya kuyapata hayo madawa, ndiyo maana nimepiga tena simu haraka.”
“Kwa hiyo tutakuwa basi tumechemsha.”
“Bado hamjachemsha.”
“Tusaidie jinsi ya kuyapata.”
“Mkoba wake mwekundu anao?”
"Ndiyo."

Itaendelea Ijumaa
 
SEHEMU: 15
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500
ILIPOISHIA:
“Siyo kuwasumbua, niligundua nilifanya kosa katika maelezo ya kuyapata hayo madawa, ndiyo maana nimepiga tena simu haraka.”
“Kwa hiyo tutakuwa basi tumechemsha.”
“Bado hamjachemsha.”
“Tusaidie jinsi ya kuyapata.”
“Mkoba wake mwekundu anao?”
“Ndiyo.”
SASA ENDELEA...
“Basi huo ndio wenye dawa hizo.”
“Mbona tumempekua hatujaona kitu?”
“Huyo dada ni muuzaji wa kimataifa wa dawa za kulevya, hata siku moja hamuwezi kumkamata kirahisi.”
“Tusaidie basi tujue ameficha wapi?”
“Huo mkoba wake umeshonwa maalumu kwa ajili ya kuvusha dawa za kulevya, una karatasi za lailoni ambazo haziwezi kuruhusu vipimo vyenu kuona ndani kuna kitu gani. Juu kuna manyoya hufanya mkoba huo mtu yeyote asiutilie wasiwasi. Kwa mtindo huo, umemfanya mwanamke huyu aendeleze biashara yake haramu ya dawa za kulevya bila kushikwa.”
“Kwa hiyo una maanisha mkoba alishonwa na dawa zake kabisa?”
“Ndiyo maana nikasema huyo dada ni muuzaji wa kimataifa, huzunguka sehemu zote bila kukamatwa na kumfanya aweze kujikusanyia fedha nyingi kila kukicha.”
“Una uhakika na unachokisema?”
“Kwa nini nimewapa picha jinsi alivyo na mmempata bila tatizo, kuna kitu nilichowaeleza akakataa?” “Mpaka sasa upo sahihi.”
“Basi pasueni mkoba wake mtanipa jibu, asante.”
Baada ya kusema vile alikata simu. Baada ya simu kukatwa, Deus alitumia dakika tano kutafakari maneno ya mtu aliyejiita msamalia mwema ili kutoa uamuzi ambayo kama utakwenda kinyume unaweza kumuhalibia sifa. Aliamuru yule mwanamke aingie, aliitwa na kuingia ndani na kukaa kwenye kiti. “Samahani,” alianza Mr Deus kumtaka radhi Teddy. “Bila samahani mkuu.”
“Naomba uniambie ukweli kuhusu sehemu ulipoficha dawa za kulevya.”
“Nimeeleza kila kitu, sasa mnataka nini? Sijui lolote juu ya dawa za kulevya nashangaa kunihusisha na biashara hatari kama hizo.”
“Naomba nifanye upekuzi kwenye mkoba wako.” “Huu hapa angalia,” Teddy alisema huku akiuweka mkoba wake juu ya meza.
“Kabla sijaupasua naomba uniambie ukweli juu ya kuficha dawa za kulevya.”
“Mkoba si huo hapo fanyeni muwezavyo utajua ukweli kuwa sihusiki japo kuwa watu wananipaka matope,” Teddy alisema kwa kujiamini. Mr Deus aliagiza kisu ili aupasue mkoba mbele yake, Kabla hajaupasua Teddy alimtaadhalisha.
“Kumbuka mkoba huu nimeununua pesa nyingi robo ya bajeti ya wizara moja kubwa katika serikali yako.” “Hiyo siyo juu yako.”
“Sema unataka shilingi ngapi ili usiharibu mkoba?”
“Sihitaji fedha yoyote zaidi ya kuupasua mkoba huu.” “Haya fanya uwezavyo lakini mwisho wa siku utaumbuka.”
Mr Deus hakumsikiliza alichukua kisu na kuanza kuupasua mkoba ili kupata uhakika kwa yale aliyoelekezwa na msamalia mwema. Alipoanza kuupasua mkoba Teddy aliomba asitishe zoezi. “Samahani mkuu.”
“Bila samahani,” Deus alijibu akiwa amesitisha zoezi la kuupasua mkoba.
“Naomba tuzungumze.” “Tutazungumza nikimaliza, fedha ya robo bajeti ya wizara hata mimi naweza kuilipa peke yangu wala usiwe na wasiwasi,” Mr Deus alijibu huku akinyanyua kisu kukididimiza kwenye mkoba.
“Naomba unisikilize kaka yangu,” Teddy alikuwa mpole ghafla.
“Juu ya nini?”
“Kuhusu huo mkoba.”
“Una nini?”
“Samahani kaka yangu naomba unisilize mdogo wako.”
Mr Deus aliacha kuuchana mkoba na kumgeukia Teddy aliyekuwa akitokwa na jasho japo ofisi ya Mr Deus ilikuwa na kiyoyozi kikali.
“Mhu! Unasemaje?”
“Najua nimepatikana, lakini naomba msaada wako?” “Umepatikana kivipi na unaomba msaada upi?”
“ Kila ulichoelezwa ni kweli?”
“Na nani?”
“Simjui, lakini inaonekana ananijua vizuri, sasa nifae kwa mvua nitakufaa kwa jua.” “Sijakuelewa,” Mr Deus alimshangaa Teddy.
“Ni kweli mfuko huu una dawa na kwa sasa nipo chini ya ulinzi na ukinifisha mahakamani nitafia gerezani, umri wangu bado mdogo. Nakuomba uniokoe kwa hili nipo radhi kukupa kiasi chochote ukitakacho hata ukiacha kazi unaweza kula miaka hamsini bila tatizo.”
“Lakini unajua dawa za kulevya ni haramu?” “Najua, na ndiyo maana nipo chini ya ulinzi.” “Sasa nikiwasikiliza wote tutamkamata nani?”
“Yaweza usione umuhimu wangu kwako leo, lakini kwangu mimi wewe ni mtu muhimu kama malaika mtoa roho aliyeahilisha kuchukua roho mama mzazi muda mfupi baada ya kujifungua.”
“Kwa ubinaadamu ni kweli nilitakiwa kukusaidia, lakini kwa vile ni dhamana niliyopewa na taifa sina budi kuwa na uso wa mbuzi.”
“Si kwamba nakulazimisha au nakufundisha kazi, hata hao wakubwa zako waliokutuma wanapokea mrungula. Amini usiamini kuna viongozi katika serikali yako hata viongozi wa dini mwenye heshima katika taifa hili wanaifanya biashara hii. Unaweza kunikamata na nikafungwa, lakini bado utakuwa umechota kikombe cha maji kwenye bahari hutapunguza kitu. “Nina imani msaada wako leo unaweza kukusaidia siku za mbele, mbegu ya wema siku zote haiozi.
Naomba unisaidie kwa leo nina imani nitakapotoka huwezi kujilaumu kwa msaada wako. Sema kiasi chochote ukitakacho hata kikipita fedha za mzigo huu nipo tayari kukupa tena muda huu.”
Kauli ile ilimfanya Deus alitulie kwa muda huku akiona sura ya yule binti ilivyoonesha kuomba msaada wake. Kila alilolizungumza alililona lina uzito kwake. Taratibu moyo ulilainika na kuona kuna umuhimu wa kumsikiliza yule msichana.
“Unajua binti unanipa wakati mgumu,” Deus alisema kwa sauti ya chini.
“Kivipi kaka yangu?”
“Unajua vijana wangu wakiona nakuachia wakati mimi ndiye kiongozi wao watanielewaje?”
“Sikiliza mkuu hakuna hata mmoja anayejua huku ndani kipi kinaendelea, wengi wanajua ni mazungumzo ya kawaida.”
“Mmh! Sasa kwa kesi nzito kama hii unanipa kiasi gani?”
“Chochote ukitakacho utakachokiona kinalingana na kosa hili.” “Kwa vile wewe ndiye uliyetangaza biashara kusema ili nione kama kinalingana na kosa lenyewe.”
“Lakini huu mzigo si utaniachia?”
“Itategemea na kiasi cha mzigo utakaotangaza.”
“Milioni 50.”
“Hailingani na kosa lako, kumbuka hapa nauza kazi naweza hata kufungwa maisha ikigundulika.”
“75.”
“Okay, nisikuumize sana nipe hizohizo.”
“Na mzigo wangu?”
“Utaondoka nao, nitapataje mzigo wangu?”
“Kama una kijana wako nimuagize aende sasa hivi akachukue mzigo mimi nikiwa hapa akipata utaniruhusu niondoke.”
“Itakuwaje?”
“Nampigia simu mtu ukisikia kisha unanipa mtu wako nimuelekeze akachukue.”
“Okay, fanya hivyo.”
Teddy alichukua simu yake iliyokuwa mezani na kubofya namba kisha alisema:
“Haloo Tonny.”
“Eeh, Teddy.”
“Andaa milioni 75 kuna mtu atakuja muda si mrefu.”
“Hakuna tatizo, nitamtambuaje?”
“Nitakujulisha.” Teddy alikata simu na kumgeukia Mr Deus aliyekuwa akishangazwa na uwezo wa kifedha aliokuwa nao binti yule.
Alikubaliana na kauli ya mtu aliyejiita msamalia mwema kuwa binti yule ni mfanya biashara mzoefu pia mwenye utajiri mkubwa.
“Basi mjulishe huyu mtu wako ili nimwelekeze akachukue mzigo.”
“Hakuna tatizo ngoja nimpigie ili nikupe umuelekeze,” Deus alisema huku akichukua simu na kumpigia rafiki yake Kinape afuatilie dili lile.
“Haloo Kinape upo wapi?”
“Ndiyo natoka kazini.”
“Hebu zungumza na dada huyu akuelekeze sehemu akakupe mzigo wangu.”
“Hakuna tatizo,” Deus alimpa simu Teddy ambaye alimuelekeza sehemu ya kukutana ampe mzigo huo. Baada ya maelekezo Teddy alimgeukia Deus na kumuuliza.
“Nina imani utaamini kwamba mimi si mtu wa kubabaisha.”
“Mpaka tutakapo maliza kazi.”
Mr Deus alinyanyua simu na kumwita secretary wake, baada ya muda alifika na kukakamaa kikakamavu mbele ya mkuu wake.
“Abee bosi.”
“Mletee mgeni kinywaji.”
“Sawa mkuu.” Aligeuka na kuondoka, baada ya muda alirudi na sahani iliyokuwa juisi ya paketi na glasi mbili. Aliweka juu ya meza na kuwawekea wote kisha aliwakaribisha.
“Karibuni Juisi dada.”
“Asante,” alijibu Teddy huku akichukua glasi ya juisi moyo wake ukiwa umeanza kutulia. “Lete stori,” Deus alivunja ukimya.
“Ninalo kaka yangu, nakuahidi si leo si kesho msaada wako hutaujutia.”
“Kwa nini mnakaa na fedha nyingi kiasi hicho ndani?”
“Kaka yangu kazi yenyewe bila ya kuwa na fedha za haraka unaozea gerezani.”
Wakati wa mazungumzo simu iliingia toka kwa secretary, alipokea na kuzugumza.
“Simu ya Italia mkuu.”
“Niachie.”
“Haloo.”
“Ndiyo msamalia mwema?”
“Vipi mzigo umeuona?” “Kazi umeisha tupa tuachie tuifanye,” Deus alijibu kwa jeuri kidogo.
“Mkuu sina maana ya kukufundisha kazi bali kufanikisha kukamatwa kwa huyo malaya.”
“Asante kazi inakwenda vizuri.” “Mmeziona?” “Hiyo si kazi yako.”
“Sawa mkubwa mara hii nimekuwa adui?” “Siyo adui tunashukuru kwa msaada wako mambo mengine ni siri ya ndani hatakiwi mtu mwingine kujua.”
“Nakutakia kazi njema.”
“Na wewe pia.”
Baada ya kukata simu Teddy aliyekuwa akifuatilia mazungumzo yale alijua mbaya wake bado alikuwa akimuandama kwa kufuatilia mpango wake.
“Samahani mkuu.”
“Bila samahani.” “Naomba nimjue huyo mtu.” “Hapana ni siri ya jeshi.”
“Kaka yangu nipo radhi kukuipa pesa ile mara mbili ili nimjue tu.” “Ukimjua?”
“Basi tu nitakaa naye mbali.”
“Kwa kweli amekataa kutaja jina lake zaidi ya kujiita msamalia mwema.”
“Anatokea wapi?”
“Italia.”
“Asante kwa msaada wako.”
Mara simu iliita, Teddy aliipokea na kusema: “Eeh! Tayari hebu mpe simu nizungumze naye,” Baada ya kupewa alizungumza:
“Eeh! Umefika?” “Ndiyo.” “Hebu zungumza na mkuu hapa,” alimpa simu azungumze na Kinape.
“Eeh! Kinape umefika?”
“Ndiyo.”
“Ni yeye,” Deus alimgeukia na kumwambia Teddy.
“Nipe simu.”
Baada ya kumpa alimwambia mtu wa upande wa pili.
“Tonny mpe mzigo mpe ulinzi mpaka atakapozifikisha salama.”
“Hakuna tatizo.” Teddy alikata simu na kumgeukia Mr Deus na kumuuliza:
“Utazipeleka wapi?”
“Nyumbani.”
“Naomba uzipeleke benki ni nyingi sana sitaki upoteze nguvu zako bure,” Teddy alimshauri Deusi.
“Sawa nitafanya hivyo.”
“Deus alipigia Kinape simu na kumweleza azipeleke benki katika akaunti ya Kinape yeye angezichukua baadaye.
Tonny alimsindikiza Kinape mpaka benki ambapo aliweka fedha yote aliyopewa kwenye akaunti yake. Baada ya kuweka alimpigia simu Deus kumjulisha.
“Mkubwa kazi imekwenda vizuri.”
“Amekupa zote?”
“Ndiyo.”
“Shilingi ngapi?”
“Milioni 75.”
“Ooh, vizuri umeshaziweka benki?”
“Ndiyo natoka sasa hivi.”
“Basi tutaonana baadaye nyumbani.” “Hakuna tatizo mkuu?” Deus baada ya kupata uhakika kwa Kinape alimgeukia Teddy aliyekuwa akiendelea kunywa juisi taratibu bila wasi kama hakuna kitu cha hatari kilikuwa mbele yake.
“Teddy,” alimwita.
“Abee.” “Nafikiri kila kitu kimekwenda vizuri.”
“Hakuna tatizo, naheshimu sana kazi yako pia muda wako.”
“Asante lakini kumbuka umeniweka katika wakati mgumu sana.”
“Kawaida tu kaka yangu, nakuapia ulichokifanya leo hutakijutia maishani kwako, huenda leo usione umuhimu wake lakini ipo siku utayakumbuka maneno yangu.”

Itaendelea Jumatatu
 
SEHEMU: 16
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500

ILIPOISHIA:
Deus baada ya kupata uhakika kwa Kinape alimgeukia Teddy aliyekuwa akiendelea kunywa juisi taratibu bila wasi kama hakuna kitu cha hatari kilikuwa mbele yake.
“Teddy,” alimwita.
“Abee.” “Nafikiri kila kitu kimekwenda vizuri.”
“Hakuna tatizo, naheshimu sana kazi yako pia muda wako.”
“Asante lakini kumbuka umeniweka katika wakati mgumu sana.”
“Kawaida tu kaka yangu, nakuapia ulichokifanya leo hutakijutia maishani kwako, huenda leo usione umuhimu wake lakini ipo siku utayakumbuka maneno yangu.”
SASA ENDELEA...
“Basi wacha nikutoe ili ukapumzike na safari.”
“Na kweli muda huu ningekuwa nimelala, hata chakula ningekula jioni baada ya kuamka.”
“Pole sana ni harakati za maisha.”
“Tunaweza kwenda,” Deus alisema huku akinyanyuka na kuweka vitu vyake sawa kwenye meza. Teddy alinyanyuka na kuchukua mkoba wake wenye dawa za kulevya na kuuweka begani kisha alitangulia kutoka, alipofika kwenye korido la kutokea nje alisimama kumsubiri Deus kuogopa maswali kwa baadhi ya watu ambao angekutana nao njiani.
Baada ya kuweka ofisi yake sawa Deus alitoka na kumpitia Teddy kwa kumshika mkono, kwa mtu angewaona kwa mara ya kwanza angeamini wale ni marafiki wanaojuana muda mrefu.
Lakini kumbe muda mfupi walikuwa chui na paka. Walikwenda kwenye gari na kuondoka kumrudisha sehemu aliyofikia, lakini Teddy aliomba aachwe sehemu ambako ataingia kwenye gari litakalomfuata na kwenda kwake. Wakiwa njiani Teddy alianzisha mazungumzo.
“Nashukuru kwa ukarimu wako.”
“Japo unanishukuru, lakini kumbuka nimenilazimisha nimeisaliti nchi yangu kwa damana waliyonipa ya kulinda nchi yangu.”
“Huenda leo huijui faida yake lakini narudia kukuapia msaada wako hautakwenda bure, ila nilikuwa na wazo moja.” “Wazo gani?”
“Najua kazi hii umepewa na taifa lakini kuna maisha badala ya kazi.”
“Hayo najua, ulikuwa na maana gani?”
“Hivi ukistaafu utalipwa kiasi gani?”
“Kiasi cha kawaida.”
“Nina imani hakitaweza kuyaendesha maisha yako?” “Ni kweli kabisa.”
“Sasa unaona unafanya kazi ya mamilioni lakini mwisho wa siku unakufa maskini.”
“Ni kweli, lakini kazi yetu inalenga kujitolea na si kujitajirisha.”
“Wewe unasema hivyo wakati wakubwa zako wanaokutisha usichukue rushwa, wao ndiyo wanaongoza kuwa na utajiri wa kutisha.”
“Sasa wewe ulikuwa unanishauri nini?” “Nataka kupitia kazi yako uweze kufaidika ili mwisho wa siku ulie kivulini.”
“Kwa hiyo unanishauri nile rushwa.”
“Kula rushwa siwezi kukushauri nina imani hii si rushwa ya kwanza inawezekana umeisha kula nyingi, inaonesha kabisa unakula za kawaida mimi nilitaka tufanye biashara kwa muda mwaka mmoja uwe trionea.”
“Kazi hii ukiifanyia tamaa huchelewi kushtukiwa na mwisho wa siku unapigwa chini au unategewa mtego na ukinasa unafia gerezani.”
“Biashara hiyo nataka tufanye sisi wawili.”
“Kumbuka biashara hii mwisho wake mbaya kwa mfano ungekutana na mtu aliyekunywa maji ya bendera ya taifa si ungepotelea gerezani?” “Kabla ya kupotelea gerezani yeye kabla ya jioni jina lake lingebakia historia midomoni mwa watu.”
“Una maana ungemuua?”
“Siku zote kazi na dawa.”
“Nani angemuua wakati wewe umo ndani?”
“Mtandao ni mkubwa, miongoni mwenu kuna mtu angemuua.”
“Kwa nini mnamuua?”
“Kifo chake ni kupoteza ushahidi ili wakubwa wako wapate nafasi ya kunitoa kwa urahisi.” “Kama kuna wakubwa wanaweza kukutoa kwa njia hiyo, kwa nini hukuitumia kuliko kutoa fedha nyingi kiasi hicho?”
“Hii ni biashara kati yako na mimi hivyo lazima tukubaliane tukishindani lazima nitumie ya upande wa pili ambayo huwa sipendi kuitumia kwa kuamini kila mwanadamu ni muelewa wote tunatafuta kwa njia ya halali na haramu.”
“Kwa nini usiokoe fedha nyingi kuliko kutoa bila sababu.”
“Njia ya pili ina faida na hasara zake, faida ni kutoka salama lakini hasara zake kwanza kutoa uhai wa mtu ambao kwa kupitia uwezo wangu wa kifedha huwa sipendi kuutumia.
“Pili mara nyingi unaweza kutoka salama lakini mzigo wako ukapotea mikononi mwa dola, mara nyingi ukikamatwa kwanza taarifa zako zinafika katika vyombo vya habari hata kama ukitoka unakuwa umechafuka. Na mzigo nao unakuwa katika stoo kabla ya kuteketezwa hivyo inakuwa vigumu kuupata. Kama nitatumia njia ya kutoa fedha nyingi lakini ukiuza unarudisha faida japo kidogo.”
“Inaonesha una fedha nyingi, kwa nini usiachane na kazi hatari kama hii?”
“Hakuna mwanadamu anayetosheka fedha kila kukicha matajiri wanabuni miradi kuongeza kipato.”
“Lakini si kwa kazi kama hii.”
“Basi kwa taarifa yako kuwa watu wana fedha kufuru kwa kazi hii, kutokana na uwezo wao wamekuwa wakiwatuliza wenye viherehere. Hebu tuachana na hayo naomba tufanye kazi niliyokueleza awali, kwa muda mfupi nimeamini wewe ni mtu muhimu sana kwangu.”
“Kazi gani?”
“Kwa vile upo kwenye kitengo hiki naomba utumie cheo chako kufanikisha biashara hii. Nakuahidi kila safari yangu ikivuka salama una milioni 250.”
“Una sema?” Deus aliuliza kama hakusikia. “Nitakapopita salama, nikifika nyumbani nakukabidhi milioni 250 hata kabla sijafanya biashara.”
“Kwa mwezi utakuja mara ngapi?”
“Itategemea mara moja au mara moja kwa miezi miwili.”
“Naomba unipe muda wa kufikiria jambo hili.”
“Kama ningekuwa mimi wala nisingesubiri kwani kijua ndicho hiki, ila napenda kukuonya kitu kimoja.”
“Kitu gani?”
“Kama utakubali kuufanya mpango huu ambao nakuhakikishia kwa mwezi kupitia mtandao wangu utatengeneza bilioni moja.”
“Bilioni moja?”
“Ndiyo, watu wanne wakiingia kwa mwezi mmoja utakuwa na kiasi gani?”
“Nimekuelewa na nini ulichotaka kunionya?”
“Nakuomba chonde chonde mpango hatari kama huu usimshirikishe mkeo.”
“Kwa nini?”
“Wanawake nawajua mvizuri si waficha siri kwenye wakati mgumu, kosa lolote litalotokea kwenye ndoa anaweza kutumia kukuangamiza.”
Kauli ile ilimshtua Deus kwani mipango yote ya awali aliyofanya, mkewe ndiye aliyekuwa msiri wake. Lakini alikuwa mstari wa mbele kumshauri mambo ya kimaendeleo hata baadhi ya fedha za rushwa aliziweka kwenye akaunti ya mkewe.
“Deus najua kabisa ulimshirikisha mkeo mambo yako ya nyuma, lakini kwa hili naomba iwe siri yako. Watu wengi wanaocheza michezo michafu kama hii huwaua hata wake zao pale wanapoona wamegundua kazi zao za hatari zinazoweza kuwapotezea maisha.
Lakini sikushauri umuue mkeo, ila nakuomba ili uweze kuwa tirionea kwa muda mfupi kwani mtando una watu zaidi ya kumi mwezi mmoja wote wakipitia katika mikono yako salama utajikuta ukitengeneza bilioni mbili na nusu kwa mwezi, unataka Mungu akupe nini?”
“Nimekuelewa nina imani ukiwa tayari nijulishe, tutaifanya kazi.”
“Nashukuru kuwa muelewa, huwezi kuamini wewe ni mtu wa kwanza kumueleza mpango huu wa hatari. Naomba usinigeuke unaweza kunishangaa pamoja na umbile langu dogo lakini nitakachokufanya hutasahau maisha yako yote.”
“Ondoa wasiwasi kazi itafanyika.”
“Niteremshe hapa watu wangu wamenifuata, mambo mengine tumia namba yangu hii ya simu ambayo ni watu muhimu tu wanayoijua.
” Deus alimteremsha Teddy ambaye aliingia kwenye gari lenye tinted na kutoweka kwa mwendo wa kasi na kumwacha Deus akilisindikiza kwa macho huku akiuona utajiri mbele yake.
Baada ya Teddy mwanamke hatari katika kuuza dawa za kulevya kuondoka, Deus alijikuta akipoteza ujasiri wa kulitumikia taifa na kujikuta akiota ndoto ya utajiri kwa kujiingiza kwenye biashara ya madawa ya kulevya. Aliamua kurudi ofisini kumalizia kazi zake ili jioni akakutane na Kinape akiamini kabisa rafiki yake hawezi kumweleza mtu yeyote siri ile kama livyomkataza.
*******
Wakati akiwaza yale rafiki yake Kinape alikuwa na furaha ya ajabu moyoni mwake, alipofika nyumbani Kilole alitaka kujua furaha yake inatokana na nini.
“Vipi mwenzangu leo mbona una furaha umeongezwa mshahara nini?”
“Sasa hivi mimi ni milionea.”
“Una maana gani kusema hivyo?” Kilole alihoji. Alimpa picha yote ilivyokwenda, Kilole baada ya kusikiliza taarifa ile alimweleza kitu Kinape. “Mungu mkubwa.”
“Una maana gani kusema hivyo?” “Sasa mpango wetu utakamilika.”
“Una maana gani?”
“Sasa hivi ni wakati muzuri wa kumpotezea mbali Deus.”
“Tusifanye hivyo.” “Shauri yako akigundua atakumaliza wewe.”
“Kwa hiyo unanishauri nini?”
“Kwa vile benki kuna milioni 75 zinatutosha kwangu nina milioni 24 huoni milioni 99 zitatusaidia kufanya mambo mazuri baada ya kumuua tutauza majumba yake mawili na magari kisha tutafungua mradi wowote wa kutuendeleza kimaisha na kuuhama mji huu.”
“Hapana tusimuue.”
“Lazima Deus afe, ikiwezekana kazi ifanyike leo usiku.”
“Hapana tusifanye pupa tunaweza kuozea gerezani au hata kunyongwa kama ikigundulika sisi ndiye tuliyehusika na kifo chake.”
“Sasa tufanye nini?” “Hebu nipe muda.”
“Muda gani Kinape, mchicha umeisha kolea nazi fedha za kutosha tunazo tunasubiri nini?”
“Japo lolote zuri halihitaji haraka,” Kinape alimtuliza Kilole aliyekuwa na pupa. “Mpaka lini?”
“Nipe siku mbili.”
“Na ziwe siku hizo mbili, ukizidisha utakuta mzoga wa mtu ndani.”
“Unataka kujiua?”
“Nani afe, nitamnyongelea mbali Deus.”
“Punguza pupa kila kitu kitakwenda vizuri.”
“Lazima nikueleze ukweli Kinape hakuna mwanaume chini ya jua ninaye mpenda kama wewe.”
“Hilo nalijua lakini yote uliyataka wewe.”
“Lakini kukubali kwangu kuolewa na Deus huoni faida leo hii akaunti yako kuna milioni 75 hukuwahi kuota kuingiza fedha kama hizi.”
“Mmh! Na kweli.”
***
Deus baada ya kazi alirudi nyumbani na kupokewa kwa furaha na mkewe huku Kilole akionesha mapenzi mazito kwa mumewe ili kumfumba macho kabla kumtendea unyama. Baada ya chakula cha usiku Deus alimtoa nje rafiki yake ili ampe taarifa za utajiri wa ajabu unaokuja mbele yake.
“Unataka kuniambia kwa mwezi utakuwa unaingiza milioni 1000?”
“Ndio maana yake, nataka baada ya muda nipabadilishe kijijini kwetu pawe kama peponi.”
“Mmh! Mshiko mzito kauli ya yule dada kwa miaka mitano dunia utaishika mkononi.”
“Yaani naona kama ndoto.”
“Ungekuwa mnoko ungeishia na virushwa vya milioni kumi.”
“Basi naomba siri hii isimpe mtu mwingine, nimekupa wewe mtu wa karibu hata mke wangu sitamwambia ni siri ya hatari sana.”
“Hii ni siri nzito siwezi kumwambia mtu.”
“Hujui dhamira yangu kwako, katika kila fedha itakayo ingia asilimia kumi nitachukua wewe.”
“Unataka kuniambia katika milioni 1000 zangu ngapi?”
“Milioni 100.”
“Wachaaa, usinitie uchizi kwa furaha.”
“Lazima nikujali nataka nawe kijiji upabadilishe wajue kweli watoto wao tumekuja kutafuta maisha.” “Kweli nimeamini wewe ni zaidi ya ndugu.”
“Nathamini urafiki wetu tumetoka mbali kumbuka ndoto zetu tulipanga kufanya nini?” Baada ya mazungumzo walirudi ndani, Kilole hakuwa na haraka ya kujua walichokuwa wakizungumza kwa kuamini yote angeyajua kupitia kwa Kinape. Usiku nao ulikuwa wa raha kwa Kilole kuendelea kuonesha kumjali mumewe kwa kumpa penzi tamu ambalo lilimpagawisha Deus na kujikuta akimuahidi mkewe gari la milioni 20.
Kilole alijisemea moyoni kuwa asali ile aliyomlambisha ni chambo cha kumuingiza kwenye mtego wamlipue hakuwa na mapenzi tena na mumewe na kumuona shetani wa roho yake aliyetamani afe wakati wowote ili afaidi penzi tamu la Kinape.

Itaendelea Jumatano
 
SEHEMU: 17
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500
ILIPOISHIA:
Kilole alijisemea moyoni kuwa asali ile aliyomlambisha ni chambo cha kumuingiza kwenye mtego wamlipue hakuwa na mapenzi tena na mumewe na kumuona shetani wa roho yake aliyetamani afe wakati wowote ili afaidi penzi tamu la Kinape.
SASA ENDELEA...
***
Siku ya pili Kinape alichelewa kutoka kwenda kazini kutokana na ishara aliyooneshwa na Kilole kuwa asiondoke ili wazungumze. Deusi aliondoka peke yake kuwahi kazini huku akijiona alichelewa kupata dili kubwa kama zile. Alipofika ofisini aliwasiliana moja kwa moja na Teddy mwanamke muuza unga. “Haloo Teddy.”
“Ooh! Brother za asubuhi?”
“Nzuri.”
“Nina imani una habari njema asubuhi hii?”
“Ni kweli, mimi nipo tayari kuifanya ile kazi.”
“Ooh! Vizuri sana, tena una bahati washirika wangu wote wapo hapa.”
“Kwa hiyo?”
“Basi jioni tukutane ili tuzungumze jinsi ya kufanya.”
“Hakuna tatizo.”
“Nakutakia kazi njema kaka yangu.”
Deus baada ya kukata simu alitabasamu kidogo kabla ya kuanza kazi. Wakati yeye anapanga mipango ya utajiri, nyumbani kwake pia kulikuwa na mipango ya kummaliza. Kinape baada ya kujiandaa kwenda kazini kabla ya kutoka chumbani Kilole alimfuata.
“Vipi mpenzi?”
“Safi.”
“Naona jana jamaa alikuita chemba alikuambia nini, au ndiyo anataka uwahi kumuoa Happy?”
“Walaa.”
“Alikuitia nini?”
“Jamaa anataka kututajirisha.”
“Kututajilisha una maana gani?” Kinape alimueleza yote aliyoelezwa na Deus pamoja na kukatazwa kuitoa siri ile nje. Pamoja na kusikia mpango ule wa mabiloni ya shilingi bado Kilole aliona wanamchelewesha.
“Kinape hiyo fedha itapatikana lini huoni kama tunachelewa, tuachane na mpango wake tummalize tufikiri mambo mengine.”
“Kilole zile ni fedha nyingi zitakazo tufanya tuishi kama peponi, tutakula mpaka tunakufa bila kufanya kazi.”
“Kwani huo mpango mwezi gani?”
“Wanamsubiri yeye tu watu waingine unga wakati wowote.”
“Mmh! Nitavumilia lakini kwa upande wangu naona zilizopo zinatutosha.”
“Ni kweli lakini tutafanya kosa kumbwa kuacha mabilioni ya fedha.”
“Mmh! Sawa.”

****
Wakati Kilole na Kinape wanapanga mipango ya kummaliza Deus, Jimmy mpiga picha naye alikuwa akipanga yake. Aliamini kupitia picha zile atajipatia fedha na penzi toka kwa Kilole mwanamke aliyempenda kupindukia. Aliamua kumtumia rafiki yake kumtisha ili wapate fedha. Kilole akiwa katika usafi wa kawaida wa nyumba simu yake iliita, namba ilikuwa ngeni kwake. Alibofya cha kupokelea na kusema:
“Haloo.”
“Haloo, nazungumza na Kilole.” “Ndiyo, nani mwenzangu?”
“Naitwa Simon, kumeokota picha zako ambazo zinaonesha unafanya uchafu kwa hiyo ili nisizisambaze nataka milioni tano.”
“Picha zangu?” Kilole alishtuka.
“Eeh, tena unafanya uchafu na ndugu wa mumeo, kabla picha hazijamfikia mumeo tunaomba huo mzigo.”
“Na..na..omba unipigie baada ya dakika tano,” Kilole alichanganyikiwa na kuona Jimmy amemgeuka. Kwa haraka alimpigia simu Jimmy kutaka kujua picha zake zimemfikiaje mtu mwingine. Alipopiga simu iliita kwa muda bila kupokelewa, hakukoma alirudia tena na kupokewa upande wa pili.
“Haloo Sister,” Jiimy alipokea upande wa pili. “Nazungumza na Jimmy?”
“Ndiyo Sister, lete stori.”
“Jimmy nilikueleza nini?”
“Kuhusu nini?”
“Kuhusu picha.”
“Kwani vipi?” “Kuna mtu kanipigia simu anasema ameokota picha zangu kwa hiyo anataka milioni tano la sivyo atazisambaza au kumpelekea mume wangu.”
“Ha!” Jimmy alijifanya kushtuka.
“Jimmy tulizungumza nini na umefanya nini?”
“Samahani Sister, wiki mbili zilizopita nilivamiwa ndani na kuibiwa vitu vingi, nina siku mbili tangu nitoke hospitali.”
“Taarifa ulifikisha polisi?”
“Niliogopa kwa vile kulikuwa na picha zako.” “Jimmy kwa nini umekaa na picha zangu, kama pesa yako nilikulipa yote?”
“Sister niliamini picha zile ulikuwa na umuhimu sana kwako hivyo ungeweza kuzipoteza ndiyo nikaamua kuzihifadhi nyingine kwangu.”
“Sasa umeona umenitia hasara?”
“Sikujua ingekuwa hivyo.”
“Sasa nitafanyaje, utawezaje kunisaidia?”
“Dada yangu kama fedha unayo ungempa kwa kweli picha zile siyo nzuri kuonwa na mumeo.” “Nampa lakini kumbuka umenifanyia kitu kibaya sana.”
“Najua lakini nia yangu ilikuwa nzuri tu.”
“Okay, imekwisha tokea sina jinsi, ila baadaye nitakupa kazi ya kunifanyia.”
“Hakuna tatizo dada yangu ila pole sana.”
“Bado sijapoa mpaka uifanye kazi yangu kwa asilimia mia.”
“Hakuna tatizo.”
“Basi baadaye.”
Kilole alikata simu na kumpigia aliyempa taarifa ya kuokotwa kwa picha zake. Baada ya kuita ilipokelewa upande wa pili.
“Ndiyo, sema.”
”Ulisema?” Kilole aliuliza.
“Kuhusu nini?”
“Si umesema una picha zangu?”
“Ndiyo.”
“Samahani kaka angu.”
“Samahani ya nini, fedha haipungui hata senti tano kama huna niifanye kazi yangu,” upande wa pili ulimtisha.
“Kaka yangu mbona unanifanyia ukatili kama huo, nimekukosea nini mpaka kushindwa kunisikiliza?” “Dada eeh, niambie utatoa mzigo au hutoi nijue moja sikuja kubembelezana.”
“Sio kwanza sitoi, nitatoa hata zaidi lakini nilitaka kujua hizo picha umeziokota wapi na zilikuwa kwenye nini?”
“Dada yangu eeh, sipo mahakamani kama mshiko upo nijulishe nina mambo mengi, hivi unafikiri nikimweleza mumeo kuwa nina picha hizo ningepata hata mara tatu ya fedha yako.”
“Basi naomba unielekeze nizilete wapi hizo fedha?”
“Unazo sasa hivi?”
“Hapana nakwenda kwenye mashine ya kutolea fedha.”
“Basi ukiisha kuwa nazo nijulishe nikuelekeze.”
“Nielekeze wala haichuki hata nusu saa.”
“Nitakujulisha baada ya dakika tano.” Jamaa baada ya kukata simu alimgeukia Jimmy aliyekuwa pembeni yake.
”Sasa mkuu fedha ndiyo hiyo atuletee wapi?”
“Mwambie Sea Green view hotel.”
“Poa.”
“Yule mwanamke anaonekana ana fedha za kuchezea lazima tumtumie kutengeneza maisha.” “Hakuna noma mkuu.”
Baada ya mazungumzo alimpigia simu Kilole. “Haloo Sister tukutane Sea Green view hotel.”
“Nje au ndani?”
“Aah! Jambo hili si la kitoto tunatakiwa tukabidhiane ndani.”
“Mmh! Sawa.”
“Mbona unaguna?”
”Si unajua mimi mke wa mtu naweza kuingia kwenye matatizo nikionekana katika mazingira ya kutatanisha.”
“Kuachika na kuonekana kipi kibaya?”
”Mmh! Sina jinsi kisu kimegusa mfupa.”
“Nikupe dakika ngapi?”
“Sidhani itachukua nusu saa, naomba basi nikukute kwani nina haraka.”
“Hakuna tatizo.”
Kilole alijikuta akiingia katika matatizo ambayo hakuyategemea, moyoni aliapa kumfanyia kitu kibaya Jimmy ambacho hatakisahau maishani mwake. Baada ya kutoka kwenye mashine ya kutolea fedha, alielekea Sea Green view hotel. Alipofika nje ya hoteli alimpigia simu mwenye picha zake.
“Haloo nimeisha fika upo wapi?”
“Njoo ndani ghorofa ya pili chumba namba 112.”
“Mmh! Mbona makabidhiano ndani ya chumba cha hotel?”
“Kwa vile wewe ni mke wa mtu.”
“Mmh! Sawa nakuja.
” Haikumpa shida kuingia ndani bila kujulikana kutokana na kujitanda kanga iliyomfunika kichwa na kujiziba na miwani nyeusi. Aliingia hadi ndani ya hoteli na kwenda moja kwa moja kwenye chumba namba 112, kabla ya kuingia alipumua kidogo na kugonga mlango.
“Pita mlango upo wazi,” sauti toka ndani ilimjibu.
Alizungusha kitasa na kusukuma mlango, mlango ulifunguka na kuingia ndani. Alimkuta kijana mmoja aliyekuwa amekaa kwenye sofa akinywa maji yaliyokuwa juu ya meza ndogo.
“Karibu,” alimkaribisha huku akitabasamu.
“Asante,” Kilole alijibu huku akikaa pembeni yake akiwa hajiamini. “Karibu soda.”
”Hapana nina haraka fedha hii hapa nipe picha zangu niondoke.” “Sikiliza dada yangu kufanya mambo yako kwa pupa utajikuta kila siku unarudia makosa.”
“Nimekuelewa kaka yangu ila naomba unipe kwanza hizo picha mambo mengine tutapanga siku nyingine.”
“Basi kunywa soda kidogo.”
“Hapana kaka yangu nina haraka.”
“Ina maana mimi ni mjinga kukununulia soda?” Jamaa alionesha kukasilishwa na kauli ya Kilole. “Basi wacha ninywe kidogo,“ Kilole alisema huku akichukua chupa ya soda iliyokuwa imekwisha funguliwa kabisa.
Alikunywa kidogo bila kujua alikuwa amepangiwa mchezo mwingine katika soda, aliona kama inamchelewesha alikunywa yote ili awahi kuondoka. Lakini hakufanya lolote baada ya kupatwa na kuzunguzungu na kujilaza kwenye kochi bila kujua. Joe alimpigia simu Jimmy aliyekuwa nje ya hoteli.

Itaendelea
 
SEHEMU: 18
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500

ILIPOISHIA:
Alikunywa kidogo bila kujua alikuwa amepangiwa mchezo mwingine katika soda, aliona kama inamchelewesha alikunywa yote ili awahi kuondoka. Lakini hakufanya lolote baada ya kupatwa na kuzunguzungu na kujilaza kwenye kochi bila kujua. Jamaa alimpigia simu Jimmy aliyekuwa nje ya hoteli.
SASA ENDELEA...
Jimmy aliingia ndani ya hoteli na kumkuta Kilole amejilaza kwenye kochi hakiwa hajitambui. “Ooh! Kazi nzuri sana,” alimpongeza mwenzake.
“Mmh! Nilikuwa kwenye wakati mgumu unajua kazi kama hujaifanya hata siku moja lazima utakuwa hujiamini, wasiwasi wangu anaweza kuja na polisi.”
“Aje na polisi hajitaki, vipi mzigo amekuja nao?”
“Huu hapo,” Joe alimpa bahasha lililokuwa na fedha. Kabla ya kufanya lolote walihesabu fedha na kukuta milioni tano taslimu, Jimmy alimkatia Joe milioni moja kama malipo ya kazi aliyompa.
“Mzee nafikiri zinakutosha.” “Asante mkuu, nini kinaendelea?”
“Bado sinema inaendelea, sasa hivi tutafanya naye mapenzi kwa zamu huku tukipiga picha ambazo naamini zitazidi kututengenezea fedha.”
“Hakuna tatizo.”
Walimbeba Kilole aliyekuwa hajitambui na kumlaza kitandani kisha walimvua nguo zate na kuanza kumbaka kwa zamu huku wakimpiga picha za aibu. Baada ya kumaliza zoezi la aibu waliondoka na kumwacha Kilole akiwa amelala hajitambui.
********
Majira ya mchana Teddy alimpigia simu Mr Deus kutaka kujua kama ana nafasi waonane kutokana na baadhi ya washirika wake jioni ya siku ile kuwa na safari kufuata mzigo. “Haloo brother za kazi?” “Nzuri, sijui zako.”
“Zangu ziko poa, samahani tunaweza kuonana mchana huu?”
“Hakuna tatizo.”
“Basi njoo mara moja nikukutanishe na jamaa zangu ili tuianze kazi mara moja.” “Hakuna tatizo, tutakutana wapi?”
”Njoo na gari mpaka sehemu uliyoniacha siku ile.”
“Hakuna tatizo ndani ya robo saa nitakuwa hapo.”
“Okay, baadaye.”
Deus alikata simu na kujiandaa kwenda kuonana na kundi la wauza madawa ya kulevya. Baada ya kupanga vitu katika hali nzuri alitoka na kumuaga msaidizi wake.
“Happy natoka kidogo.” “Hakuna tatizo bosi.” Mr Deus alielekea kwenye maegesho kuchukua gari lake na kuelekea kwenye wito, alipofika eneo aliloelezwa alilipaki gari pembeni ya barabara kusubiri maelekezo. Baada ya muda simu yake iliita, alipoitazama alikuta ni Teddy, alibofya cha kupokelea na kuweka sikioni.
“Haloo.” “Haloo nimekuona, teremka kwenye gari lako na kupanda kwenye gari litakalo simama mbele yako.”
“Na gari langu?” “Liache tu litakuwa katika usalama wa hali ya juu, kwa hilo usihofu.”
“Okay,” Mr Deus alikata simu na kuteremkana kulifunga gari lake na kufuata maelekezo. Kabla hajapiga hatua Range Rover Vogue nyeusi yenye vioo visivyoonesha ndani ilisimama mbele yake na kufunguliwa mlango.
Hakupoteza muda aliingia ndani ya gari na kufunga mlango na gari liliondoka. Ndani ya gari kulikuwa na watu watatu Teddy aliyekuwa akiendesha gari na wanaume wawili waliokuwa wamekaa siti za nyuma.
“Habari zenu?”
“Nzuri,” Walijibu kwa mkato.
“Samahani brother,” Teddy alisema huku akipaki gari pembeni. “Bila samahani.”
“Naomba ufuate utaratibu wetu kabla ya kufika kwetu.”
“Hakuna tatizo.” “Utafungwa kitambaa usoni mpaka tutakapofika.”
“Hakuna tatizo mnaweza kufanya.”
Baada ya kukubali alifungwa kitambaa cheusi usoni na safari iliendelea bila kujua anapelekwa wapi. Baada ya dakika tano gari lilisimama na kuombwa
Mr Deus aliteremke, alitii amri na kuteremka kisha alishikwa mkono na kuongozwa hadi sehemu na kufunguliwa kitambaa usoni.
Baada ya kufunguliwa alijikuta yupo mbele ya sebule lililokuwa na kila kitu cha thamani. Ndani ya sebule ile kulikuwa na watu zaidi ya nane ukijumlisha watatu aliokuja nao wakawa jumla watu kumi na mbili pamoja na yeye mwenyewe.
“Karibu Mr Deus jisikie huru, ila samahani kukuleta kama mateka.”
“Kawaida tu wala hakuna baya.”
“Karibu kwenye kochi.”
“Asante,” alijibu huku akikaa kwenye kochi, baada ya kuketi aliwasalimia aliowakuta.
“Habari zenu.”
“Nzuri,” Waliitikia kwa pamoja.
“Mr Deus hawa ndiyo washirika wangu, huyo hapo ni Mateez anayefuata Sopas, Natalie, Suzy, Moops, Sweet, Pako, Flog, JMS na Poona, nina imani mimi unanifahamu?”
Mr Deus alikubali kwa kutikisa kichwa. “Waungwana huyu ndiye mtu niliyewaeleza ana umuhimu mkubwa kwetu, nimeweza kumwelewesha na kanielewa. Kwa vile kazi hii haihitaji kupoteza muda nina imani kuanzia muda wowote biashara ifanyike.
“Mr Deus hawa ndiyo washirika wangu niliokueleza kwa bahati nzuri tumekutana sehemu kubwa ya kundi letu. Wengine watatu utawajua kwa vile wiki ijayo wanaingia nimezungumza nao ili wapitie katika mikono yako salama japo wawili wamesema wataanza baada ya sisi ila mmoja atakuja na mzigo ndogo kujaribu.”
“Hakuna tatizo kazi itafanyika vizuri kila mmoja ataifurahia,” alisema Mr Deus baada ya kumsikiliza Teddy.
“Kwa hiyo kazi rasmi inaanza mwezi ujao kwa mwezi una uhakika wa kutengeneza zaidi ya bilioni mbili.”
“Hakuna tatizo nina imani mtafurahia kufanya kazi pamoja japo ni ya hatari.”
“Baada ya makubaliano hayo, tunakuonya tena kosa lolote la kizembe litagharimu uhai wako,” Teddy alitoa onyo lingine.
“Najiamini kuliko mnavyonidhania,” Mr Deus aliwatoa wasi.
“Kumbuka nilikukataza usimwambie siri hii hata mkeo.”
“Siwezi kumwambia mtu.”
Baada ya mazungumzo Mr Deus aliagwa na kupewa asante wa kukubali kufanya kazi na kundi lile ya milioni 55 kwa kila mmoja kutoa milioni tano. Baada ya mazungumzo yale alifungwa tena kitambaa na kurudisha hadi kwenye gari lake na kumkabidhi huku wakimuacha Mr Deus akiwa hajui alikuwa wapi.
******
Kilole alishtuka na kujishangaa yupo wapi baada ya kushtushwa na mazingira aliyoyaona mbele yake. Alijiuliza pale amefikaje na anafanya nini, kingine kilichomshtua ni kujikuta kitandani akiwa mtupu na pembeni yake kulikuwa na kondomu zaidi ya nne zilizotumika.
Alishtuka na kujishika sehemu za siri na kukuta kweli amebakwa, pembeni yake kulikuwa na bahasha mbili zilizokuwa imeandikwa jina lake. Kabla ya kuichukua ile bahasha alitulia na kuvuta kumbukumbu ya kufika pale. Alikumbuka alipeleka milioni tano ili apewe picha alizipiga akifanya mapenzi na Kinape. Aliendelea kuvuta kumbukumbu na kukumbuka baada ya kuonana na yule kijana alikaribishwa soda lakini kilichoendelea hakujua mpaka aliposhtuka na kujikuta akiwa mtupu kitandani huku ikionesha amebakwa zaidi ya mara nne kutokana na mipira minne ya kiume iliyotumika.
Alijipa ujasiri na kunyanyuka hadi bafuni na kuoga kisha alirudi chumbani na kuvaa nguo zake kisha alichukua bahasha mbili zilizokuwa na jina lake na kuziweka katika mkoba wake na kutoka nje ya hoteli kurudi nyumbani kwake.
Alipofika nje ilionesha kiza kilikuwa kimeingia, alitoa simu yake kwenye mkoba na kuangalia saa ilimuonesha ni saa mbili usiku. Alijikuta akishtuka na kujiuliza utamueleza nini mume wake, katika simu yake kulionesha kuna simu zilizopigwa zaidi ya mara kumi za mume wake pamoja na Kinape.
Japo roho ilimuuma kwa kitendo cha kinyama alichofanyiwa na kuapa kulipa kisasi, lakini aliweka pembeni maumivu yale na kutafuta njia ya kukabiliana na mumewe nyumbani atakayetaka kujua alikuwa wapi. Lakini ilikuwa tofauti na alivyofikiria, alipofika nyumbani alishangaa kukuta mumewe hajarudi. Mfanyakazi wa ndani alipomuuliza alisema hajarudi, ile ilimpa nguvu na kumpigia simu mumewe. “Haloo sweet.”
“Ooh! Honey vipi mbona napiga simu hupokei mpenzi, kuna nini?”
“Nilikuwa nimelala kichwa kimeniuma ghafla.”
“Nilitaka kukujulisha kuwa nitachewa tuna kazi moja nzito.”
“Mmh! Mume wangu, siyo unanila kisogo,” Kilole alijifanya kulalamika.
“Mke wangu siwezi kutoka nje ya ndoa yangu nakupenda sana, hasa mwenetu ambaye ndiye mrithi wetu na yote nayafanya kwa ajili yenu.”
“Asante mume wangu, nashukuru kusikia hivyo.” “Nikimaliza tu narudi nyumbani.”
“Nakutakia kazi njema, nakusubiri kwa hamu,” Kilole alizidi kumtia ujinga mumewe. Baada ya kukata simu aliingia chumbani mwake na kuziangalia zile bahasha, bahasha ya kwanza ilikuwa na picha alizopiga akifanya mapenzi na Kinape. Bahasha ya pili kulikuwa na picha ambazo zilimmaliza nguvu lakini akijikaza na kuendelea kuzitazama.
Alijiona akibakwa na wanaume wawili, alishtuka na kukumbuka soda aliyokunywa ndiyo ilimfanya apoteze fahamu na kumfanya yule mwanaume na mwenzake wambake.
Roho ilimuuma kutoa milioni tano bado wamembaka na kumpiga picha chafu. Ndani ya bahasha kulikuwa na karatasi iliyokuwa na ujumbe usemao;
Kwa vile unapenda mchezo huo, baada ya kukupa picha zako na kutupa milioni tano, picha hizo zingine zinataka milioni kumi, la sivyo siri ilimfikia mumeo. Tutakupigia simu kujua utatupa lini na wapi?
Kilole jasho lilimtoka na kuona kama laana ya matendo yake ndiyo inayomtafuna, alijiuliza milioni kumi akiwapa lazima watatengeneza mpango mwingine. Wasiwasi wake huenda mpango ule Jimmy anaujua, lakini hakutaka kutumia pupa zaidi ya kutumia hata kishawishi cha fedha ili Jimmy amsaidie. Wazo lingine lilikuwa kumuwahi Deus kabla hajajua lolote kwa kumuua ili kuepusha aibu, lakini wazo la kuua bado hakulipa nafasi kutokana na Kinape kuweka pingamizi. Akiwa amechanganyikiwa simu yale iliita, aliipokea na kusema:
“Haloo.”
“Haloo, bahasha umeiona?”
”Wewe nani?” “Mdau wako, nina imani ujumbe umeuona nieleze hizo fedha nitapata lini?”
”Lakini kaka yangu nimekukosea nini mpaka kunifanyia unyama kama huo?” Kilole alilalamika huku akimwaga chozi. “Hujadhalilishwa na mtu, biashara umeianza wewe, sisi tunaiendeleza.”
“Kaka yangu milioni tano nimekupa leo, hizo kumi nitazipata vipi?”
“Kama huna pa kuzipata basi salamu utazikuta kwa mumeo,” sauti ya upande wa pili ilimtisha.
“Msifanye hivyo, nioneeni huruma.”
“Hukujionea huruma sisi tutakuonea vipi?”
“Basi nipunguzieni.”
“Tulikuwa tunataka milioni hamsini, lakini nimepunguza mpaka kumi bado huoni huruma yangu.”
“Basi nipeni muda wa muda ili nizikusanye.”
“Tutakupa siku mbili.”
“Mbona ndogo?”
“Kama ndogo utajuana na mumeo tena tuinampa na za mwanzo ulizopiga na shemeji yako.”
“Basi nitawapeni, nakuombeni msimpe mtu.”
“Hakuna tatizo timiza haja zetu.”
“Hakuna tatizo.”
“Kwa heri, usiku mwema.”
Baada ya kukata simu alijikuta akirudiwa na maneno ya mtu aliyetaka fedha kwa kusema alifanya mapenzi na shemeji yake ile ilionesha kabisa Jimmy huenda mpango mzima anaujua. Kilole pamoja na kutokewa na tukio zito la kumdhalilisha huku likizidi kumuingiza kwenye mazingira magumu. Lakini hakutaka kuyumba kwani aliamini vita ile ni yake na yeye ndiye anayetakiwa kupambana mpaka tone la mwisho.
Alizirudia zile picha na kuuona unyama aliofanyiwa ikiwa pamoja na kuingiliwa kinyume na maumbile. Moyo ulimuuma sana na kujikuta akidondokwa na machozi kutokana na udhalilishwaji kama ule. Aliapa kupigana nayo mpaka hatua ya mwisho hata kwa mtutu kwani alikuwa anajua kutumia vizuri chombo cha moto baada ya kufundishwa na mumewe na kujua kuitumia vizuri.
Alikumbuka visasi vingi ambavyo ameviona kwenye sinema hutendeka usiku kwa mtu kuingia sehemu na kufanya mauaji kisha kutokomea bila mtu kujua.
Wazo lake lilikuwa kwenda kumbana Jimmy ili amtaje mtu mwenye picha zake na alipanga kuhakikisha anamuua Jimmy na kijana anayemtumia kama mtaji. Wakati akiwaza vile alishtuka kusikia mlango ukigongwa, alificha picha kwenye kabati na kwenda kufungua mlango.
Alifuta machozi na kujirudisha katika hali ya kawaida kisha alipofungua akijua mumewe karudi, lakini kumbe alikuwa Kinape ambaye alionekana mwenye jambo zito kichwani mwake kutokana na mwonekano wake. Kilole alizidi kuchanganyikiwa na hali ile ambayo aliona huenda inafanana na yake.
“Kilole mbona hivyo?” alimuuliza kwa mshangao. “Kilole umeniweka katika wakati mgumu sana,” Kinape alisema huku akikuna kichwa.
“Mungu wangu! Amejua? Kwa nini tusimmalizie mbali?”
“Tummalizie mbali nani?”
“Si Deus.”
“Kwa kosa gani?”
“Si amejua.”
“Wala si hilo.”
“Picha ameziona?”
“Kilole hebu acha papala, yote unayouliza siyo.”
“Sasa nimekuweka kwenye wakati mgumu kivipi?”

Tukutane Jumatatu
 
SEHEMU: 19
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500

ILIPOISHIA:
“Mungu wangu! Amejua? Kwa nini tusimmalizie mbali?” “Tummalizie mbali nani?”
“Si Deus.”
“Kwa kosa gani?” “Si amejua.”
“Wala si hilo.”
“Picha ameziona?”
“Kilole hebu acha papala, yote unayouliza siyo.”
“Sasa nimekuweka kwenye wakati mgumu kivipi?”
SASA ENDELEA...

”Happy hanielewi kabisa, kila kukicha naitwa na familia yake naichenga, nikienda nitawaelezea nini wanielewe.”
“Kinape unakuwa kama siyo mwanaume, mwambie kuwa humtaki kwani mapenzi ni lazima.”
“Si rahisi kiasi hicho, kuvunjika kwa penzi kuna sababu huwezi kuzima chuma cha moto na maji baridi lazima kitapinda na Deus nitamwambia nini mtu niliyempeleka kwa wazazi wa Happy kumtambulisha kama kaka yangu?”
“Yote uliyataka wewe, kwa nini hukuniuliza kabla ya kwenda huko?”
”Kilole, wewe ni mke wa mtu na Happy ni mchumba wangu hivyo nilikuwa na haki ya kufanya vile.”
“Sasa Deus atakulazimishaje umpende Happy wakati humtaki?”
“Nitaanzia wapi ikiwa nilimweleza mengi juu ya mapenzi yangu ya dhati kwa Happy huku akiniahidi kusimamia harusi yangu. Kibaya zaidi Happy na wazazi wake watakuja hapa jioni ya leo ili kujua hatima ya ndoa.”
“Kwani wewe ulimjibu nini Happy?”
“Nilimueleza asubiri kidogo mzazi wangu mmoja alikuwa na matatizo.”
“Sasa yeye anataka nini na ulikwisha mweleza ukweli?”
“Anataka kwenda kumuona kwa vile anajua na yeye ni mzazi wake, pia muda wa kuwa naye umepungua si kama zamani. Kingine majibu yako ya mkato yamemshtua kitu ambacho kimemetia wasiwasi huenda tuna uhusiano wa kimapenzi.”
“Sasa akijua atafanya nini? Tena mweke wazi ili ajue hana chake.”
“Kilole acha kujisahau wewe ni mke wa mtu, kibaya kosa tunalifanya ndani ya kinywa cha simba. Hivi wakija hapa nitamwambia nini Deus na kwa vile huu ni mwisho wa wiki huenda akasema kesho tunakwenda kijijini. Siyo siri tabia ya Happy ilimvutia sana Deus na kusema atanipigania hata kwa fedha kuhakikisha namuoa, hivi niseme simtaki Happy nitaanzia wapi?”
“Kinape, Deus hawezi kukulazimisha kuoa mwanamke usiyempenda.”
“Unasema tu lakini kauli hiyo kwa mtu mwenye akili timamu hawezi kuitamka.”
“Kwa hiyo unamuogopa Deus?” “Ndiyo.”
“Kwa nini tusimpoteze?”
“Kilole acha papara nimekueleza tutajipanga.” “Nataka kukueleza kitu kimoja Deus ni kikwazo kwa nini mnamlea?”
“Tukifanya kwa pupa tutakosa mwana na maji ya moto.”
“Sasa tutafanyaje?”
“Nimekueleza niache niangalie tufanye nini?”
“Na kuhusu Happy najua ndiye anayeweza kuharibu kila kitu kama ataonekana kijijini?”
“Kwa kweli la Happy ndilo linalonichanganya nashindwa nifanye nini, nilipokutana naye leo nimechanganyikiwa jinsi alivyokonda kwa muda mfupi niliokuwa karibu yako na amenitishia nikimuacha lazima atajiua.” “Sasa akijiua wewe utapungukiwa nini, kwanza ndiyo itakuwa safi tunakuwa na nafasi ya kuishi wawili baada ya kumpoteza na Deus.”
“Siwezi kufanya hivyo, kama Happy atafariki basi nitakuwa na dhambi kubwa sana ambayo itakuwa kama tone la rangi nyekundu kwenye nguo nyeupe haitanitoka mpaka nitakapo ingia chini ya udongo.”
“Mmh! Sasa tutafanya nini?”
“Ndiyo maana nikasema umenipa mtihani mzito ambao sikuwahi kuusoma hata siku moja kwangu naona kiza. Kwa nini tusiachane na wazo kama hili?” ”Wazo gani?”
“Ukaniachana nioane na Happy na wewe unakie na Deus?”
“Kinape huwezi kunivisha kitanzi kisha uniweke juu ya donge la barafu likiyenyuka lazima nitakufa. Heri nife mimi kuliko kuendelea kuishi kwani naamini maisha yangu baada ya zile picha hayana thamani.
Kwa hiyo ulitaka kunidhalilisha ili ufurahi kwa vile nimeolewa na Deus kama kweli ulitaka niishi na Deus kwa nini ulinitendea unyama kama ule?”
“Happy..Ooh! Sorry Kilole mbona umekosa subira.”
“Nimekuelewa Kinape, tutazungumza kesho.”
Waliachana na Kilole alirudi chumbani akiwa amechanganyikiwa na kushindwa afanye nini juu ya picha mpya na habari za Happy.
Kilole baada ya kuachana na Kinape alirudi chumbani kwake na kujifungia kwa ndani, kila dakika iliyokuja mbele yake ilikuwa na maumivu makali yaliyomfanya akose jibu la haraka afanye nini. Kubakwa hakuona tatizo zaidi ya kusikia habari za Happy kupigania penzi lake ambalo ndilo lililomfikisha katika maumivu yale makali.
Alijiona mtu mmoja ambaye alikuwa akipigana na watu wengi bila msaada wa mtu mwingine, alijiuliza atawezaje kumdhibiti Happy kuhakikisha anampata Kinape mwanaume ambaye aliamini ndiye wa maisha yake.
Alichukua bahasha na kurudia kuangalia picha alizopigwa akibakwa na wanaume wawili kwa mpigo ambao hawakuonesha sura zao zaidi ya yeye peke yake.
Picha zile zilimchanganya sana na kuamini kama zitamfikia Kinape zitamweka katika mazingira magumu ambao utakuwa kama fimbo ya kumpigia ili kumuoa Happy.
Alipiga ngumi kwenye godoro kwa hasira baada ya kujiona yupo njia panda asijue aanze na kitu gani ili aweze kuyazima yote na mwisho wa siku awe na Kinape.
Akiwa katikati ya mawazo mlango uligongwa, alijua ni Kinape amekuja na wazo jipya, alikwenda hadi mlangoni na kufungua lakini alikuta ni mumewe ambaye alimchanulia tabasamu pana.
Kwa mshtuko aliufunga mlango haraka na kufunga na komeo, kwa haraka alichukua picha zake na kuzificha kisha alitoka hadi mlango ambako mumewe alikuwa bado amepigwa na butwaa.
“Ha! Kumbe ni mume wangu?” Alijifanya kushtuka.
“Unaniona sasa mwanzo ulifikiria nani?”
“Mmh! Hata sijui niseme nini, wakati unagonga mlango nilikuwa nimejinyoosha kitandani na kupitiwa na usingizi na kuota nimevamiwa na majambazi. Ulipogonga nilikuwa bado na usingizi nilipofungua na kukuona nilifikiri ni jambazi mpaka uliponiita na kuitambua sauti yako nisamehe mume wangu.”
“Kawaida, pole kwa ndoto mbaya.”
“Asante mume wangu.”
“Vipi mbona kama haupo sawa?”
“Mume wangu si nimekueleza naumwa, hata ndoto zangu zilikuwa za kutisha.” “Ooh! Pole sana.”
Kilole alijikuta akiangua kilio kilichomshtua mumewe.
“Vipi tena?” alimuuliza.
“Aah! Basi tu.”
“Basi tu nini! Au umezidiwa?”
“Walaa, hata sijiui nalia nini.”
”Niambie kama umezidiwa nikuwahishe hospitali, utalia bila kujua unalia nini?”
“Nimemeza dawa naomba kitu kimoja.”
“Kipi hicho mke wangu?”
“Uniache nipumzike nisiamshwe na mtu yeyote na mtoto alale kwa msichana wa kazi.”
“Hakuna tatizo mke wangu.” Deus hakutaka kumsumbua mkewe alifanya yote aliyoelekezwa, alitumia nafasi ile ya mkewe kutotaka usumbufu kuzungumza na rafiki yake juu ya mpango aliozungumza na Teddy na wauza unga wenzake.
Baada ya kuoga na kupata chakula cha usiku kilichopikwa na msichana wa kazi alikwenda chumba cha rafiki yake. Alimkuta amejipumzisha, alipomuona rafiki yake alimkaribisha kwa furaha.
“Ooh! Best karibu.”
“Naona umejipumzisha.” “Nifanye nini baada ya mihangaiko ya siku nzima.”
“Basi leo tulikuwa na kazi moja nzito ya kukamata gari lililokuwa na madawa kutokana na taarifa za watoa habari. Wenye gari waligoma kufungua mpaka walipokuja wakubwa zetu ambao waliliruhusu bila hata kuuliza. Lakini taarifa zilisema gari lile lina dawa za kulevya.”
“Basi hapo kuna rushwa imetembea kwa wakubwa.”
“Umeona eeh!”
“Ukweli ni huo unafikiri ndani ya gari kulikuwa na mzigo kiasi gani, ndiyo maana walikuwa wabishi kuwafungulia gari kwa vile kuna watu wanawategemea.” “Kitendo kile kimenivunja nguvu kweli, siwezi mkupote muda wangu kwa upuuzi kama ule.”
“Nawe kula sehemu yako.”
“Sasa kuna dili moja nimeingia leo si mchezo.”
“Mmh! Dili gani tena mzee?”
“Si nilikueleza yule mwanamke alisema atanikutanisha na wenzake?” “Eeh, ndiyo.”
”Basi leo mchana alinipigia simu na kunikutanisha nao.”
“Acha utani! Ehe ikawaje?”
“Tumekubaliana kuinza mwezi ujao kwa hiyo mpaka mwezi ukikatika nitakuwa nimetengeneza bilioni mbili.” “Acha utani!”
“Ukweli sasa hivi najiona nimekwisha uaga umasikini, kweli! Umefikia wapi mambo yako na Happy?”
Swali lilikuwa kama pigo zito moyoni mwa Kinape hakuwa na jibu la haraka, Deus hakujua rafiki yake anawaza nini baada ya kumuuliza na kukaa kimya. “Ni hivi nina fedha kidogo nitakupa ili kuhakikisha unakamilisha harusi yako.”
“Kiasi gani?”
“Milioni ishirini ambazo nitakupa sasa hivi ufanye maandalizi yako na shemeji, umekwisha mpeleka kwa wazazi kijijini?”
“Bado.”
“Unasubiri nini? Fanya hivi kesho kutwa hakikisha unakwenda na Happy kwa wazazi ili tupange nipango mingine. Utatumia gari langu sawa pia tafuta nyumba ya milioni hamsini ili nikununulie kwa siri ili shemeji yako asijue kitu.”
“Hakuna tatizo nimekuelewa mkuu.”
“Mbona kama upo mbali au umechoka?”
Deus alimuuliza Kinape aliyeonekana yupo mbali kimawazo. “Ni kweli leo nimefanya kazi kama mbwa, hapa nilipo natamani kulala tu si kitu kingine.”
“Basi pumzika tutaonana kesho.”
“Usiku mwema.”
“Na kwako pia.”
Deus alitoka na kwenda sebuleni kutafuta mkanda wa filamu ili kuvuta muda kabla ya kupanda kitandani huku akiwa anaisikia harufu ya utajiri. Alipiga mahesabu hata kama wataingiza mara moja kwa miezi miwili kwa mwaka aliziona bilioni kumi na mbili mbele yake.
Alijikuta akicheka peke yake huku akisema kwa sauti ya chini: “Kumbe utajiri hauna njia ndefu.”
Wakati akiwaza yale chumbani mkewe alikuwa akigaagaa kitandani kama nyoka aliyemwagiwa mafuta ya taa kutokana na kuwa na maswali yasiyo na majibu juu vitu vilivyopo mbele yake alijiuliza aanze na lipi la Jimmy au la Happy.
Alipanga usiku atoroke na kwenda kwa Jimmy kumbembeleza kwa njia yoyote ili tu amjue nani aliyemfanyia mchezo mchafu kama ule tena kujua picha za awali akifanya mapenzi na shemeji yake. Pamoja hakuwa na usingizi alitulia kitandani akisubiri mumewe akilala atumie nafasi hiyo kwenda kwa Jimmy.
Naye Kinape baada ya kutoka Deus alijikuta kwenye mtihani mzito wa kutoa uamuzi sahihi ambao hautaleta madhara kati ya Happy na Kilole. Lakini Happy kwake alikuwa muhimu kuliko Kilole ambaye tayari alikuwa mke wa mtu.
Swali ambalo kila kukicha lililokuwa likimla akili lilikuwa kuhusu picha alizopigwa akifanya mapenzi na Kilole nani aliyezipiga, alipata wazo la kumtafuta ili kupata ukweli wasiwasi wake huenda mtego ule ulipangwa na Deus.
Kingine kilichomkosesha raha kama picha zile zikivuja na kumfikia Deus angekuwa kwenye wakati gani. Wazo la kuua Deus au kumfanyia baya lolote alilipinga kwa nguvu zote japo hakuweza kumweleza ukweli Kilole. Taarifa za siku ya tatu kwenda kijijini kumtambulisha Happy zilizidi kumchanga kwa kujiuliza habari zile akimweleza Kilole atazipokea vipi.
Aliamua liwalo na lile lazima amweleze ukweli na hiyo kesho kutwa lazima ampeleke kijijini mengine yatakayotokea atakuwa tayari kukabiriana nayo. Alipuuza mkwara wa Kilole na kujilaza kuitafuta siku ya pili.
*****
Majira ya saa saba usiku baada ya kuona mumewe amelala na kukoroma, Kilole alijinyanyua kitandani na kumtazama mumewe aliyekuwa amepitiwa na usingizi hajitambui. Alinyanyuka taratibu kwa kunyata hadi pembeni ya kitanda na kuunyanyua mto aliokuwa amelalia mumewe taratibu na kutoa bastola ya mumewe.
Alikwenda hadi kwenye kabati na kuvaa kaptura na fulana, aliichomeka bastora kiunoni kisha alijifunga kanga zilizomziba mwili mzima na kutoka taratibu bila kumshtua mtu yeyote. Aliegesha mlango na kutoka kwa kunyata hadi nje ya geti na kuchepua mwendo kupitia barabara kubwa kuelekea kwa mpiga picha Jimmy ambako hapakuwa mbali sana na kwake.
Baada ya mwendo mfupi aliacha barabara ya rami na kuingia kwenye uchochoro ambao ungemfanya atokee nyuma ya nyumba anayoishi Jimmy pia ndipo palipokuwa na dirisha lake. Alishukuru Mungu muda wote hakupata kizuizi chochote alitembea kwa taadhari kubwa, shida yake kwenda kugonga dirisha la Jimmy ili azungumze naye na kutaka msaada wake. Alipokaribia alitembea kwa kunyata ili mtu wa ndani asijue nje ya nyumba kuna mtu anapita. Aliporikaribia dirisha la Jimmy alisikia sauti za watu wawili mwanaume na mwanamke.
Mwanaume alimtambua ni Jimmy lakini mwanamke hakujua ni nani, lakini alijua ni mwanamke wake japo Jimmy hakuwa ameoa. Alitulia akijifikiria amwite au afanyeje kwani wasiwasi wake huenda pakatokea tatizo kwa muda ule mwanamke wake akajua yeye ni hawala yake. Wakati akiwaza afanye nini, aliendelea kusikia mazungumzo yaliyokuwa yakizunguzwa ndani.
“Sasa mpenzi hiyo fedha utanipa lini?”
“Kuna dili moja litatiki muda si mrefu nitakupatia.”
“Kumbuka na mimi ninataka kuendesha gari.” “Nimekueleza nitakupatia hiyo fedha baada ya wiki kila kitu kitakuwa tayari.”
“Najua unanidanganya.”
“Mbona laki nane za kupangia nyumba nilikupa kisha laki nane zingine za kununulia sofa nimekupa nitashindwa vipi milioni nne?”
Kauli ile ilimshtua sana Kilole na kujiuliza Jimmy uwezo ya kutoa fedha kiasi kile ameutoa wapi, wakati maisha yake yalikuwa ya kubahatisha mpaka apige picha na muda mwingi alishinda kijiweni.
Wakati akijiuliza maswali yasiyo na majibu ndani mazungumzo yaliendelea.
“Ha..ha..lafu mpenzi siku hizi unafanya kazi gani maana fedha zimeibuka kama uyoga?”

Itaendelea Jumatano
 
Back
Top Bottom