mizambwa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2008
- 4,421
- 1,792
HADITHI: KIVULI CHEUSI
SEHEMU YA KWANZA
Panga boi lilikuwa linazunguka taratibu, bila kuleta dalili yoyote ya ubaridi. Sifahamu kama ilikuwa ni udogo wa chumba, ama ni hali ya hewa ya jiji la Dar es salaam? Lakini hiyo haikumsumbua mlalaji huyu mgeni, katika kitongoji duni cha keko magurumbasi.
Kitongoji kilichobeba vibaka wa simu, makahaba na zile biashara haramu; kama uuzwaji wa bangi na pombe aina ya gongo, zilipatikana kwa wingi. Karani wa nyumba ya kulala wageni, yeye alipokea bakshishi ndogo kutoka kwake. Jumamosi yake ikaelekea kuisha vizuri jioni ile ya saa kumi na mbili.
Mgeni huyo aliyehifadhiwa ndani ya kofia kuukuu, alitoa masharti ya kutomuelekeza mgeni yeyote chumbani kwake. Alidai kuwa, hakuna anayemfahamu; hivyo hakuna atakayekuja kumtafuta. Hiyo haikuwa tatizo, kuitikia kwa kichwa; haraka haraka tabasamu jepesi la kiushawishi likipita juu ya papi zake. Elfu arobaini alizisunda kibindoni. Nyongeza mara nane ya bei ya kawaida. Binafsi aliiona bahati ya ngekewa, iliyomdondokea zaidi ya nyota ya jaa. Akampatia ufunguo mgeni huyo asiyeeleweka. Macho yaliyo nyuma ya miwani mikubwa meusi na mwendo wake kama anayechechemea. Yeye aliuchukua ufunguo aliopewa na kuondoka.
Ufunguo wenyewe, ulininginizwa kwenye kibao kilichoandikwa namba ya chumba na kulifuata korido lililopanga vyumba kwa nambari zilizofuatana kimpangilio. Baada ya kuhesabu vyumba vyote, alisimama mbele ya chumba ambacho ufunguo wake alikuwa nao yeye. Aliufungua mlango na kujitoma ndani.
Hakutaka kuwasha taa, kwa sababu mwanga hafifu wa jua lililoashiria kudondokea magharibi, ulimtosha kukiona kitanda. Alilala vile vile kama alivyoingia. Kitanda kikamlaki kama kilivyowalaki wengine. Kunguni waliifurahia damu yake, viroboto nao wakamchoma choma. Hakujisumbua kukishusha Chandarua, hivyo mbu walicheza gombania goli katika sikio lake.
Mara akaamka ghafla. Hakuamka kwa sababu ya usumbufu wa chumba hicho duni. Ni mlio wa simu ulioita ghafla, saa tano ya usiku. Muda ulikuwa umeenda kasi sana. Ilikuwa ni namba ya Bertha, mpenzi wake. Alijiuliza ni nani atakuwa anaitumia namba hiyo. Baada ya kuipokea, aliifahamu sauti iliyoongea kwa sauti ya hamaniko. Aliongea kiutulivu na kumchota akili yule aliyewehuka upande wa pili. Baada ya maongezi aliyoyafanya katika simu hiyo iliyoingia punde, Alijinyanyua kitandani na kurudi maeneo ya kijitonyama sayansi nyuma ya kanisa. Eneo ambalo alikuwa akiishi mpenzi wake Bertha.
Baada ya kumaliza shughuli iliyompeleka. Saa saba ya usiku alirudi katika chumba chake, Keko magurumbasi. Alitumia taksi iliyompeleka. Ikamsubiri na kumrudisha mpaka Buguruni na yeye kuamua kuchukua taksi nyingine mpaka hapo. Sasa akawa anautafuta usingizi akiwa na bia nane kichwani. Bia alizozinywa katika ile klabu ya usiku maarufu kwa jina la kimboka by night. Hapo kulikuwako na madada poa waliouza miili yao kama ndafu ya shereheni.
Usingizi ukamkubali.
Licha ya usumbufu wa kunguni na mbu wa usiku alioupata, unadhani hata alijigusa? Lah! Aliyafurahia maficho yake. Japo usingizi ulimpaa jirani na alfajiri. Hali hiyo ilisababshwa na jinamizi la mawazo lililokuwa likimnyonga. Mwanga hafifu wa jua la alfajiri uliojipenyeza katika dirisha la chumba chake, ndio uliyomfanya aamke kivivu huku akitanguliza kitambi chake. Hatua zake zikiwa nzito kuubeba mwili mfupi kiasi uliobeba kifua kipana na kitambi cha bia na nyama choma; zote kwake zilikuwa kheri, mpaka alipokifikia kioo kilichopachikwa ukutani.
Akashituka.
Nadhani alianza hata kuisahau sura yake. Aliyasahau macho yaliyokosa nguvu ya kope za juu na kusababisha kuwa kama anayetaka kusinzia. Hata hivyo haikua sura ngeni aliyokuwa anatazamana nayo. Akakumbuka kuwa macho hayo yalikuwa ya kawaida. Macho yaliyomuwezesha kumpora Bertha kutoka kwa rafiki yake, Yesaya. Kidevu chake kikatawaliwa na msitu wa ndevu. Lakini hiyo haikuwa sababu ya kuisahau miaka ishirini na nne aliyoifukia kwa kula na kunywa kwa anasa. Aligeuza macho kukitazama kitanda alicholalia. Godoro jembamba kama ngozi ya tembo, likamdhihaki. Akajitusi mama yake mzazi kwa hasira. Kisha kicheko kisicho na ladha yoyote ya raha kikauharibu uso wake.
Akili yake ikaanza kutafakari yaliyotokea asubuhi ya siku ya jana, iliyomfanya apahame Osterbye na kuja kujificha huku vichochoroni, Keko Magurumbasi. Ghafla ulimi wake ukapata nguvu ya kuinua matamshi kadhaa Bertha aliita jina la msichana aliyefanya urafiki wake na Yesaya kuangamia.
Msichana waliyesoma wote chuo cha mlimani, kitivo cha sheria. Msichana aliyeiiba nafsi yake na kuiyumbisha yumbisha kama mawimbi ya bahari. Aliikumbuka siku ya kwanza Bertha alipowasili chuoni hapo akitokea Nyegezi Mwanza.
Anha! Kumbe na wewe ni msukuma? Mimi ni mwenzio bwana, naitwa Moses akalikumbuka Tabasamu lililoacha uchi kinywa chake na kuonesha meno yaliyojipanga na kufanya mpangilio sahihi katika kinywa cha Bertha. Kwa mara ya kwanza Moses alikiri kuushika mkono wa malaika laivu waliposalimiana kwa kushikana mikono.
Ila Bertha sasa si Bertha tena. Ingefaa utangulize jina jipya, kabla hujaamua kumuita Bertha. Bertha kwa sasa aliitwa marehemu. Maiti yake yalifichwa na Moses ndani ya chumba chake mwenyewe Bertha. Chini ya kitanda na kuhifadhiwa kwa kuviringishwa ndani ya mkeka.
Hakika aliuwawa kinyama. Moses alifanya unyama zaidi ya mnyama. Unyama aliomfanyia binadamu mwenzake. Shingo yake Bertha haikutenganishwa na kiwili wili wakati alipochinjwa kama kuku na kisu kilichopoteza makali kwa kukatiwa nyanya na vitunguu; mpaka Moses alipohakikisha kumlisha masoksi machafu mdomoni ili Bertha asitoe sauti. Japo si Bertha pekee aliyekuwa maiti ndani ya nyumba yake. Rafiki yake Pamela pia, alipoteza roho yake kwa kutaka kutoa ushahidi polisi.
Yeye aliuwawa kikawaida kwa sumu aliyoinywa ndani ya maji ya baridi. Ilikuwa ni sumu kali sana. Nyongo ya mamba waliovuliwa kutoka katika ziwa Tanganyika. Ilisagwa na kuwa unga baada ya kukaushwa sana. Pamela aliipoteza roho yake kwa kiu ya maji ndani ya dakika kumi tu.
Baada ya kufanya yote hayo, Moses alikumbuka kufanya jambo. Alikaa uelekeo ambao mwanga wa taa ulimpiga na kutumia kamera yake aina ya Kodak, kukipiga kivuli chake mwenyewe. Baada ya kuridhika na picha aliyoipata, akatumia mashine ndogo ya kusafishia picha hiyo, picha ikatoka vile alivyotaka.
Akatabsamu kwa kebehi, kisha nyuma ya picha hiyo akaandika maandishi haya KIVULI CHEUSI akaiweka picha hiyo pembeni ya kichwa cha Bertha, alichokiweka ndani ya friji.
ITAENDELEA...............
SEHEMU YA KWANZA
Panga boi lilikuwa linazunguka taratibu, bila kuleta dalili yoyote ya ubaridi. Sifahamu kama ilikuwa ni udogo wa chumba, ama ni hali ya hewa ya jiji la Dar es salaam? Lakini hiyo haikumsumbua mlalaji huyu mgeni, katika kitongoji duni cha keko magurumbasi.
Kitongoji kilichobeba vibaka wa simu, makahaba na zile biashara haramu; kama uuzwaji wa bangi na pombe aina ya gongo, zilipatikana kwa wingi. Karani wa nyumba ya kulala wageni, yeye alipokea bakshishi ndogo kutoka kwake. Jumamosi yake ikaelekea kuisha vizuri jioni ile ya saa kumi na mbili.
Mgeni huyo aliyehifadhiwa ndani ya kofia kuukuu, alitoa masharti ya kutomuelekeza mgeni yeyote chumbani kwake. Alidai kuwa, hakuna anayemfahamu; hivyo hakuna atakayekuja kumtafuta. Hiyo haikuwa tatizo, kuitikia kwa kichwa; haraka haraka tabasamu jepesi la kiushawishi likipita juu ya papi zake. Elfu arobaini alizisunda kibindoni. Nyongeza mara nane ya bei ya kawaida. Binafsi aliiona bahati ya ngekewa, iliyomdondokea zaidi ya nyota ya jaa. Akampatia ufunguo mgeni huyo asiyeeleweka. Macho yaliyo nyuma ya miwani mikubwa meusi na mwendo wake kama anayechechemea. Yeye aliuchukua ufunguo aliopewa na kuondoka.
Ufunguo wenyewe, ulininginizwa kwenye kibao kilichoandikwa namba ya chumba na kulifuata korido lililopanga vyumba kwa nambari zilizofuatana kimpangilio. Baada ya kuhesabu vyumba vyote, alisimama mbele ya chumba ambacho ufunguo wake alikuwa nao yeye. Aliufungua mlango na kujitoma ndani.
Hakutaka kuwasha taa, kwa sababu mwanga hafifu wa jua lililoashiria kudondokea magharibi, ulimtosha kukiona kitanda. Alilala vile vile kama alivyoingia. Kitanda kikamlaki kama kilivyowalaki wengine. Kunguni waliifurahia damu yake, viroboto nao wakamchoma choma. Hakujisumbua kukishusha Chandarua, hivyo mbu walicheza gombania goli katika sikio lake.
Mara akaamka ghafla. Hakuamka kwa sababu ya usumbufu wa chumba hicho duni. Ni mlio wa simu ulioita ghafla, saa tano ya usiku. Muda ulikuwa umeenda kasi sana. Ilikuwa ni namba ya Bertha, mpenzi wake. Alijiuliza ni nani atakuwa anaitumia namba hiyo. Baada ya kuipokea, aliifahamu sauti iliyoongea kwa sauti ya hamaniko. Aliongea kiutulivu na kumchota akili yule aliyewehuka upande wa pili. Baada ya maongezi aliyoyafanya katika simu hiyo iliyoingia punde, Alijinyanyua kitandani na kurudi maeneo ya kijitonyama sayansi nyuma ya kanisa. Eneo ambalo alikuwa akiishi mpenzi wake Bertha.
Baada ya kumaliza shughuli iliyompeleka. Saa saba ya usiku alirudi katika chumba chake, Keko magurumbasi. Alitumia taksi iliyompeleka. Ikamsubiri na kumrudisha mpaka Buguruni na yeye kuamua kuchukua taksi nyingine mpaka hapo. Sasa akawa anautafuta usingizi akiwa na bia nane kichwani. Bia alizozinywa katika ile klabu ya usiku maarufu kwa jina la kimboka by night. Hapo kulikuwako na madada poa waliouza miili yao kama ndafu ya shereheni.
Usingizi ukamkubali.
Licha ya usumbufu wa kunguni na mbu wa usiku alioupata, unadhani hata alijigusa? Lah! Aliyafurahia maficho yake. Japo usingizi ulimpaa jirani na alfajiri. Hali hiyo ilisababshwa na jinamizi la mawazo lililokuwa likimnyonga. Mwanga hafifu wa jua la alfajiri uliojipenyeza katika dirisha la chumba chake, ndio uliyomfanya aamke kivivu huku akitanguliza kitambi chake. Hatua zake zikiwa nzito kuubeba mwili mfupi kiasi uliobeba kifua kipana na kitambi cha bia na nyama choma; zote kwake zilikuwa kheri, mpaka alipokifikia kioo kilichopachikwa ukutani.
Akashituka.
Nadhani alianza hata kuisahau sura yake. Aliyasahau macho yaliyokosa nguvu ya kope za juu na kusababisha kuwa kama anayetaka kusinzia. Hata hivyo haikua sura ngeni aliyokuwa anatazamana nayo. Akakumbuka kuwa macho hayo yalikuwa ya kawaida. Macho yaliyomuwezesha kumpora Bertha kutoka kwa rafiki yake, Yesaya. Kidevu chake kikatawaliwa na msitu wa ndevu. Lakini hiyo haikuwa sababu ya kuisahau miaka ishirini na nne aliyoifukia kwa kula na kunywa kwa anasa. Aligeuza macho kukitazama kitanda alicholalia. Godoro jembamba kama ngozi ya tembo, likamdhihaki. Akajitusi mama yake mzazi kwa hasira. Kisha kicheko kisicho na ladha yoyote ya raha kikauharibu uso wake.
Akili yake ikaanza kutafakari yaliyotokea asubuhi ya siku ya jana, iliyomfanya apahame Osterbye na kuja kujificha huku vichochoroni, Keko Magurumbasi. Ghafla ulimi wake ukapata nguvu ya kuinua matamshi kadhaa Bertha aliita jina la msichana aliyefanya urafiki wake na Yesaya kuangamia.
Msichana waliyesoma wote chuo cha mlimani, kitivo cha sheria. Msichana aliyeiiba nafsi yake na kuiyumbisha yumbisha kama mawimbi ya bahari. Aliikumbuka siku ya kwanza Bertha alipowasili chuoni hapo akitokea Nyegezi Mwanza.
Anha! Kumbe na wewe ni msukuma? Mimi ni mwenzio bwana, naitwa Moses akalikumbuka Tabasamu lililoacha uchi kinywa chake na kuonesha meno yaliyojipanga na kufanya mpangilio sahihi katika kinywa cha Bertha. Kwa mara ya kwanza Moses alikiri kuushika mkono wa malaika laivu waliposalimiana kwa kushikana mikono.
Ila Bertha sasa si Bertha tena. Ingefaa utangulize jina jipya, kabla hujaamua kumuita Bertha. Bertha kwa sasa aliitwa marehemu. Maiti yake yalifichwa na Moses ndani ya chumba chake mwenyewe Bertha. Chini ya kitanda na kuhifadhiwa kwa kuviringishwa ndani ya mkeka.
Hakika aliuwawa kinyama. Moses alifanya unyama zaidi ya mnyama. Unyama aliomfanyia binadamu mwenzake. Shingo yake Bertha haikutenganishwa na kiwili wili wakati alipochinjwa kama kuku na kisu kilichopoteza makali kwa kukatiwa nyanya na vitunguu; mpaka Moses alipohakikisha kumlisha masoksi machafu mdomoni ili Bertha asitoe sauti. Japo si Bertha pekee aliyekuwa maiti ndani ya nyumba yake. Rafiki yake Pamela pia, alipoteza roho yake kwa kutaka kutoa ushahidi polisi.
Yeye aliuwawa kikawaida kwa sumu aliyoinywa ndani ya maji ya baridi. Ilikuwa ni sumu kali sana. Nyongo ya mamba waliovuliwa kutoka katika ziwa Tanganyika. Ilisagwa na kuwa unga baada ya kukaushwa sana. Pamela aliipoteza roho yake kwa kiu ya maji ndani ya dakika kumi tu.
Baada ya kufanya yote hayo, Moses alikumbuka kufanya jambo. Alikaa uelekeo ambao mwanga wa taa ulimpiga na kutumia kamera yake aina ya Kodak, kukipiga kivuli chake mwenyewe. Baada ya kuridhika na picha aliyoipata, akatumia mashine ndogo ya kusafishia picha hiyo, picha ikatoka vile alivyotaka.
Akatabsamu kwa kebehi, kisha nyuma ya picha hiyo akaandika maandishi haya KIVULI CHEUSI akaiweka picha hiyo pembeni ya kichwa cha Bertha, alichokiweka ndani ya friji.
ITAENDELEA...............