Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,638
- Thread starter
- #101
SEHEMU YA 68
Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam, machangudoa wengi wanaanza kuuawa katika mazingira ya kutatanisha. Hakuna anayemjua muuaji, kila changudoa anayenunuliwa na mwanaume aliyekuwa kwenye gari aina ya Volkswagen nyeusi, anauawa kikatili.
Kila mmoja anaogopa, machangudoa wengine wanaacha kujiuza, wanajifungia vyumbani mwao, ila kwa wengine ambao hawakuweza kuishi bila kufanya biashara hiyo, wanakwenda huko, bado wengine wanaendelea kuuawa.
Aliyekuwa akiwaua wanawake hao ni Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda ya Dar es Salaam, Dickson. Aliwaua kwa siri lakini baada ya kipindi fulani kupita, akagundulika na hivyo kuanza kutafutwa.
Aliamua kukimbia kupitia Mlandizi, huko, akapitia misukosuko mingi na mwisho wa siku akajikuta kwenye kijiji kimoja ambapo baada ya wanakijiji kumuona, wakaanza kujificha. Huku akijiuliza nini kinaendelea, akatokea kijana aliyekuwa na picha yake mkononi, Dickson akashtuka.
Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…
“Umefikia wapi?” ilisikika sauti ya kamanda IGP Mayala.
“Bado, ila nimefanikiwa kupita alipopita, naona hivi karibuni nitampata,” alisema Fredrick.
“Basi sawa. Hakikisha anapatikana, huku mambo yapo ovyo na wananchi wamecharuka sana,” alisikika IGP.
“Sawa mkuu!”
Mpelelezi Fredrick alikuwa akizungumza na IGP Mayala katika simu. Zilipita siku kadhaa hakuwa amemtafuta kumwambia ni kitu gani kilikuwa kimeendelea tangu alipoanza safari ya kumtafuta Dickson ambaye alikuwa akichanja mbuga kuelekea jijini Mwanza kwa kupitia pori kwa pori.
Kuna kipindi aliwaona wanyama wakali kama simba, ngiri na wanyama wengine, akapanda juu ya mti na kutulia na hali ilipokuwa shwari, akateremka na kusonga mbele. Alitembea mpaka alipofika katika mto mmoja, ulikuwa mkubwa na hakukuwa na sehemu ya kuvukia hivyo alichokifanya ni kusubiri kwanza. “Au nipige mbizi?” alijiuliza.
Alikuwa amesubiri hapo kwa zaidi ya dakika arobaini na tano, hakukuwa na mtu yeyote aliyetokea na mtumbwi na kitu alichokifikiria ni kuingia ndani ya mto huo na kupiga mbizi kuelekea upande wa pili. Alipotaka kufanya hivyo, moyo wake ulikuwa mzito mno, hakuelewa ni kwa sababu gani lakini aliutii sana moyo wake kuliko maamuzi yake, hivyo akataka kusubiri zaidi.
Hiyo ilikuwa ni saa mbili asubuhi lakini mpaka inafika saa nne, hakukuwa na mtu yeyote aliyejitokeza mahali hapo kitu kilichomfanya kuanza kujiandaa kuuvuka mto huo kwa kupiga mbizi mpaka upande wa pili.
“We kijana unafanya nini hapo?” ilisikika sauti kutoka kwa mwanaume mmoja aliyesimama nyuma yake, alipogeuka, macho yake yakatua kwa mzee mmoja aliyekuwa na ndevu nyingi, mkononi alishika panga.
“Nataka kwenda upande wa pili.”
“Kwa kuogelea?”
“Ndiyo!”
“Una hatari sana kijana, wewe ni mgeni mahali hapa? Hujui hatari juu ya huu mto? Hujaambiwa kwamba jana tu mamba wameua familia nzima huku mtoni?” aliuliza mzee huyo, Dickson akashtuka.
“Unasemaje?”
“Hebu sogea huku, hata hapo uliposimama, kuna hatari kubwa,” alisema mzee huyo, Dickson akamsogelea.
Hapo ndipo mzee yule akamwambia Jackson kuhusu mto huo, ulikuwa ni hatari sana, ulimaliza watu wengi kijijini hapo kutokana na mamba waliokuwa humo ndani. Jackson alipoambiwa hivyo, moyo wake ulisisimka, kijasho chembamba kikamtoka na hapo ndipo alipokumbuka kwamba moyo wake haukupenda kabisa kuvuka kwa kuogelea.
“Unakwenda wapi?” aliuliza mzee huyo.
“Nataka niende mbele zaidi, kuna sehemu nakwenda,” alijibu.
“Basi sawa. Kama unataka kuvuka, nitakusaidia, sina mtumbwi ila nitakupa dawa, utajipaka kisha kuvuka bila tatizo lolote,” alisema mzee huyo.
“Mmh!”
“Unaamini katika dawa za asili?”
“Siamini, ila kama unataka kuniaminisha, hakuna tatizo,” alijibu Dickson, hapohapo mzee huyo akamchukua na kuondoka naye kwenda nyumbani kwake, huko, akachukua dawa fulani na kumpaka mwili mzima na kumwambia aende akauvuke mto ule kwa kupiga mbizi.
Kwanza hakuamini, ila kwa sababu aliambiwa tena kwa kutolewa mifano ya watu waliowahi kuuvuka mto huo baada ya kujipaka dawa hiyo, hakuwa na jinsi, akakubaliana naye, alipofika mtoni, akaanza kuingia taratibu. Alipopiga macho pembeni, akagundua kulikuwa na mamba waliokuwa pembezoni mwa mto wakimtazama, alipoingia mtoni tu, nao mamba wakaingia pamoja naye.
* * *
Dickson alitulia, alijisogeza pembeni kidogo na kumwangalia mtu aliyekuwa amemnyooshea bunduki ile, alikuwa mzee wa makamo ambaye kwa kumtazama tu alionekana kuwa miongoni mwa watu wenye roho mbaya, mmoja wa watu waliopitia mafunzo ya kijeshi.
Dickson akamuomba mzee huyo asimpige risasi kwani hakuwa mtu mbaya, alifika hapo porini kwa sababu alikuwa na matatizo makubwa hivyo alihitaji msaada wake. Mzee yule akamwangalia vizuri Dickson, hakukubaliana na maneno yake, alivyomwangalia vizuri, jinsi sura yake ilivyokuwa mbaya, akapata uhakika kwamba mtu huyo hakuwa mtu mzuri hata kidogo, alikuwa miongoni mwa majambazi waliokuwa wakiitetemesha nchi kwa kuteka mabasi. Akamsogelea.
“Nyie ndiyo mliomuua mke wangu! Lazima nilipe kisasi na nitawatafuta wenzako wote,” alisema mzee yule, tayari alikigusa kitufe cha kuruhusu risasi itoke katika bunduki hiyo na kumuua Dickson ambaye jasho lilikuwa likimtoka tu.
“Mimi siyo mtu mbaya mzee wangu, naomba unisaidie, nimetoka kukimbizwa na Savimbi, walitaka kuniua pia,” alisema Dickson huku akitetemeka pale chini alipokuwa.
Mzee huyo aliposikia jina la Savimbi, akatulia kwanza, huyo ndiye mtu aliyekuwa akimtafuta kwa udi na uvumba na ndiye aliyemuua mke wake, akajikuta akishusha mkono uliokuwa na bunduki na kumkazia macho Dickson.
“Savimbi yupo wapi?” aliuliza huku akionekana kuwa na hasira.
“Yupo humuhumu porini, wamenikimbiza, walitaka kuniua,” alijibu Dickson.
Hiyo ndiyo ilikuwa salama yake. Mzee huyo akaiweka bunduki yake vizuri kisha kumuinua Dickson mahali pale na kuondoka naye. Huko, alimwambia wazi kile kilichokuwa kimetokea mpaka kuanza kumtafuta huyo Savimbi.
Alisema kwamba mkewe aliuawa na mtu huyo alipokuwa akitoka Mara kwenda Dakawa, mkoani Morogoro. Njiani basi lao lilitekwa na majambazi saba waliokuwa na silaha nzito waliowalazimisha abiria wafanye ngono wao kwa wao, waliokataa waliwamininia risasi na kuwaua kama wanyama bila huruma.
“Mke wangu alikataa, hivyo wakamuua,” alisema mzee huyo.
Wakati mzee huyo akizungumza, alionekana kuwa na hasira dhidi ya majambazi hayo.
“Pole sana…”
“Ahsante! Wewe ni nani na unakwenda wapi?” aliuliza mzee huyo.
“Naitwa Fabian, naelekea Mwanza kwa miguu!”
“Mwanza kwa miguu?”
“Ndiyo!” alijibu Dickson, mzee huyo akabaki akiwa na mshangao na kujiuliza kwa nini asitumie usafiri na kuamua kuhatarisha maisha yake kwa kupita porini kulikowa na hatari nyingi!
Je, Dickson atasalimika kutoka mikononi mwa mzee huyo?
Hali ya sintofahamu inazuka jijini Dar es Salaam, machangudoa wengi wanaanza kuuawa katika mazingira ya kutatanisha. Hakuna anayemjua muuaji, kila changudoa anayenunuliwa na mwanaume aliyekuwa kwenye gari aina ya Volkswagen nyeusi, anauawa kikatili.
Kila mmoja anaogopa, machangudoa wengine wanaacha kujiuza, wanajifungia vyumbani mwao, ila kwa wengine ambao hawakuweza kuishi bila kufanya biashara hiyo, wanakwenda huko, bado wengine wanaendelea kuuawa.
Aliyekuwa akiwaua wanawake hao ni Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda ya Dar es Salaam, Dickson. Aliwaua kwa siri lakini baada ya kipindi fulani kupita, akagundulika na hivyo kuanza kutafutwa.
Aliamua kukimbia kupitia Mlandizi, huko, akapitia misukosuko mingi na mwisho wa siku akajikuta kwenye kijiji kimoja ambapo baada ya wanakijiji kumuona, wakaanza kujificha. Huku akijiuliza nini kinaendelea, akatokea kijana aliyekuwa na picha yake mkononi, Dickson akashtuka.
Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…
“Umefikia wapi?” ilisikika sauti ya kamanda IGP Mayala.
“Bado, ila nimefanikiwa kupita alipopita, naona hivi karibuni nitampata,” alisema Fredrick.
“Basi sawa. Hakikisha anapatikana, huku mambo yapo ovyo na wananchi wamecharuka sana,” alisikika IGP.
“Sawa mkuu!”
Mpelelezi Fredrick alikuwa akizungumza na IGP Mayala katika simu. Zilipita siku kadhaa hakuwa amemtafuta kumwambia ni kitu gani kilikuwa kimeendelea tangu alipoanza safari ya kumtafuta Dickson ambaye alikuwa akichanja mbuga kuelekea jijini Mwanza kwa kupitia pori kwa pori.
Kuna kipindi aliwaona wanyama wakali kama simba, ngiri na wanyama wengine, akapanda juu ya mti na kutulia na hali ilipokuwa shwari, akateremka na kusonga mbele. Alitembea mpaka alipofika katika mto mmoja, ulikuwa mkubwa na hakukuwa na sehemu ya kuvukia hivyo alichokifanya ni kusubiri kwanza. “Au nipige mbizi?” alijiuliza.
Alikuwa amesubiri hapo kwa zaidi ya dakika arobaini na tano, hakukuwa na mtu yeyote aliyetokea na mtumbwi na kitu alichokifikiria ni kuingia ndani ya mto huo na kupiga mbizi kuelekea upande wa pili. Alipotaka kufanya hivyo, moyo wake ulikuwa mzito mno, hakuelewa ni kwa sababu gani lakini aliutii sana moyo wake kuliko maamuzi yake, hivyo akataka kusubiri zaidi.
Hiyo ilikuwa ni saa mbili asubuhi lakini mpaka inafika saa nne, hakukuwa na mtu yeyote aliyejitokeza mahali hapo kitu kilichomfanya kuanza kujiandaa kuuvuka mto huo kwa kupiga mbizi mpaka upande wa pili.
“We kijana unafanya nini hapo?” ilisikika sauti kutoka kwa mwanaume mmoja aliyesimama nyuma yake, alipogeuka, macho yake yakatua kwa mzee mmoja aliyekuwa na ndevu nyingi, mkononi alishika panga.
“Nataka kwenda upande wa pili.”
“Kwa kuogelea?”
“Ndiyo!”
“Una hatari sana kijana, wewe ni mgeni mahali hapa? Hujui hatari juu ya huu mto? Hujaambiwa kwamba jana tu mamba wameua familia nzima huku mtoni?” aliuliza mzee huyo, Dickson akashtuka.
“Unasemaje?”
“Hebu sogea huku, hata hapo uliposimama, kuna hatari kubwa,” alisema mzee huyo, Dickson akamsogelea.
Hapo ndipo mzee yule akamwambia Jackson kuhusu mto huo, ulikuwa ni hatari sana, ulimaliza watu wengi kijijini hapo kutokana na mamba waliokuwa humo ndani. Jackson alipoambiwa hivyo, moyo wake ulisisimka, kijasho chembamba kikamtoka na hapo ndipo alipokumbuka kwamba moyo wake haukupenda kabisa kuvuka kwa kuogelea.
“Unakwenda wapi?” aliuliza mzee huyo.
“Nataka niende mbele zaidi, kuna sehemu nakwenda,” alijibu.
“Basi sawa. Kama unataka kuvuka, nitakusaidia, sina mtumbwi ila nitakupa dawa, utajipaka kisha kuvuka bila tatizo lolote,” alisema mzee huyo.
“Mmh!”
“Unaamini katika dawa za asili?”
“Siamini, ila kama unataka kuniaminisha, hakuna tatizo,” alijibu Dickson, hapohapo mzee huyo akamchukua na kuondoka naye kwenda nyumbani kwake, huko, akachukua dawa fulani na kumpaka mwili mzima na kumwambia aende akauvuke mto ule kwa kupiga mbizi.
Kwanza hakuamini, ila kwa sababu aliambiwa tena kwa kutolewa mifano ya watu waliowahi kuuvuka mto huo baada ya kujipaka dawa hiyo, hakuwa na jinsi, akakubaliana naye, alipofika mtoni, akaanza kuingia taratibu. Alipopiga macho pembeni, akagundua kulikuwa na mamba waliokuwa pembezoni mwa mto wakimtazama, alipoingia mtoni tu, nao mamba wakaingia pamoja naye.
* * *
Dickson alitulia, alijisogeza pembeni kidogo na kumwangalia mtu aliyekuwa amemnyooshea bunduki ile, alikuwa mzee wa makamo ambaye kwa kumtazama tu alionekana kuwa miongoni mwa watu wenye roho mbaya, mmoja wa watu waliopitia mafunzo ya kijeshi.
Dickson akamuomba mzee huyo asimpige risasi kwani hakuwa mtu mbaya, alifika hapo porini kwa sababu alikuwa na matatizo makubwa hivyo alihitaji msaada wake. Mzee yule akamwangalia vizuri Dickson, hakukubaliana na maneno yake, alivyomwangalia vizuri, jinsi sura yake ilivyokuwa mbaya, akapata uhakika kwamba mtu huyo hakuwa mtu mzuri hata kidogo, alikuwa miongoni mwa majambazi waliokuwa wakiitetemesha nchi kwa kuteka mabasi. Akamsogelea.
“Nyie ndiyo mliomuua mke wangu! Lazima nilipe kisasi na nitawatafuta wenzako wote,” alisema mzee yule, tayari alikigusa kitufe cha kuruhusu risasi itoke katika bunduki hiyo na kumuua Dickson ambaye jasho lilikuwa likimtoka tu.
“Mimi siyo mtu mbaya mzee wangu, naomba unisaidie, nimetoka kukimbizwa na Savimbi, walitaka kuniua pia,” alisema Dickson huku akitetemeka pale chini alipokuwa.
Mzee huyo aliposikia jina la Savimbi, akatulia kwanza, huyo ndiye mtu aliyekuwa akimtafuta kwa udi na uvumba na ndiye aliyemuua mke wake, akajikuta akishusha mkono uliokuwa na bunduki na kumkazia macho Dickson.
“Savimbi yupo wapi?” aliuliza huku akionekana kuwa na hasira.
“Yupo humuhumu porini, wamenikimbiza, walitaka kuniua,” alijibu Dickson.
Hiyo ndiyo ilikuwa salama yake. Mzee huyo akaiweka bunduki yake vizuri kisha kumuinua Dickson mahali pale na kuondoka naye. Huko, alimwambia wazi kile kilichokuwa kimetokea mpaka kuanza kumtafuta huyo Savimbi.
Alisema kwamba mkewe aliuawa na mtu huyo alipokuwa akitoka Mara kwenda Dakawa, mkoani Morogoro. Njiani basi lao lilitekwa na majambazi saba waliokuwa na silaha nzito waliowalazimisha abiria wafanye ngono wao kwa wao, waliokataa waliwamininia risasi na kuwaua kama wanyama bila huruma.
“Mke wangu alikataa, hivyo wakamuua,” alisema mzee huyo.
Wakati mzee huyo akizungumza, alionekana kuwa na hasira dhidi ya majambazi hayo.
“Pole sana…”
“Ahsante! Wewe ni nani na unakwenda wapi?” aliuliza mzee huyo.
“Naitwa Fabian, naelekea Mwanza kwa miguu!”
“Mwanza kwa miguu?”
“Ndiyo!” alijibu Dickson, mzee huyo akabaki akiwa na mshangao na kujiuliza kwa nini asitumie usafiri na kuamua kuhatarisha maisha yake kwa kupita porini kulikowa na hatari nyingi!
Je, Dickson atasalimika kutoka mikononi mwa mzee huyo?