Mchungaji Gwajima ni Mtumishi wa Mungu wa kweli au? Asema Uongo. Adai yeye ni zaidi ya Rais

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,498
113,604
Wanabodi,

Manabii wa Uongo na Tutawatambuaje?
Kwa sisi waumini wa dini ya Kikristo, tunayemwamini Bwana wetu Yesu Kristo, kabla hajapaa mbinguni, alituhusia kuwa "kutajitokeza manabii wa uongo, ambao watahubiri neno na kutoa mapepo kwa jina langu lakini sii wangu". Wanafunzi wake wakamuuliza, "Jee tutawatambuaje?", Yesu akawajibu, "Mtawatambua kwa matendo yao".

Mchungaji Dr. Josephat Gwajima ni Nabii wa Kweli au Nabii wa Uongo?
Hii ni thread ya swali kumhusu Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo wa Uzima, Mchungaji, Dr. Josephat Gwajima, Jee ni Mtumishi wa Mungu wa Kweli?!, ni Nabii wa kweli au ndio wale manabii wa uongo aliowazungumza Bwana wetu Yesu Kristo?.

Akiwa katika mimbari, madhabahuni, mbele ya Mungu na wana kondoo wake, badala ya kuihubiri Injili na neno la Mungu lenye uzima na lenye kujenga upendo, amani na mshikamano miongoni mwa jamii, yeye anahubiri siasa kwenye nyumba ya ibada, tena mahubiri juu ya chuki dhidi ya binadamu mwingine hadi kumuita "huyu kiumbe"!.

Japo ni kweli Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda alimdhalilisha Mchungaji Gwajima kwa kumtaja kujihusisha na madawa ya kulevya, Makonda alipewa tuu list yenye majina na kazi yake ilikuwa ni kuwataja tuu, aliyemtaja Gwajima kuwa anajihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya, sio Mkuu wa Mkoa, Makonda, bali ni muumini wake mtiifu, ambaye nimemtaja hapa chini na alichokisema!, sasa kosa la Makonda ni lipi?!.

Jee namna ambayo Mchungaji Gwajima, anavyomzungumzia Mkuu wetu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa ubaya na kumsingizia uongo, ndivyo Bwana wetu Yesu Kristo alivyotufundisha namna ya kuwashughulikia wale walio tukosea?!. Yesu alifundisha mtu akikupiga kibao shavu la kushoto, mgeuzie na la kuume!. Yesu ametufundisha "adui mpende". Yesu ametufundisha "samehe hata saba mara sabini". Vipi kuhusu Baba Mchungaji Gwajima kumuishi Bwana Yesu kwa maneno na matendo?

Clip ya Mchungaji Gwajima Akihubiri Mambo ya Dunia Hii na Si Mambo ya Mungu
Baada ya Mashekhe wa Mkoa wa Dar es Salaam, kuridhishwa na kazi nzuri iliyofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, kuwaumbua kwa kuwataja wazi wazi, baadhi ya wabwia unga na wauza unga hadharani, hivyo wakaamua kumuombea dua maalum ya ulinzi, ili Mungu azidi kumlinda, Mkuu wetu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda, ndipo Mchungaji Gwajima, amemuonea vivu kuwa dua zile zitazidi kumnyooshea mambo yake Makonda, yazidi kuwa mazuri na kumyookea, hivyo Yeye Gwajima,(mwenye utajiri wa ajabu ikiwemo Hammer, Helcopter, na kanisa kubwa, waumini lukuki ambao ni masikini wa kutupwa!), akaamua kumbomoa, na kumponda, na kumsingizia Makonda vitu vya uongo!.

Mahubiri ya Gwajima Kumhusu Makonda
Katika mahubiri yake ya jana, kanisani kwake Ubungo Maji jijini Dar es Salaam, Mchungaji Gwajima, amemuelezea Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda kuwa ni mtu mhalifu wa makosa ya jinai ya kufanya fojari ya kuiba jina la mtu mwingine, na kosa la kughushi kwa vyeti vya mtu mwingine na kujipatia elimu kwa njia ya udanganyifu, na alikwenda mbali zaidi hadi kudai kuwa eti jina analotumia Paul Makonda, sii jina lake halisi, bali ni jina la wizi, jina la ku foji, na kueleza kuwa ni jina la mtu mwingine kabisa ambaye yupo!. Mchungaji Gwajima, alikwenda mbali zaidi kwa kulitaja jina halisi la Paul Makonda kuwa anaitwa Daudi Albert Bashite!

Swali ninalojiuliza mpaka sasa, Makonda ndie Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam mwenye mamlaka kuu kuhusu mkoa huu, ikiwemo kukamata mtu na kumtia kizuizini!, iweje huyu Mchungaji Gwajima, anawezaje kuusema uongo kama huu jijini Dar es Salaam, tena mbele ya kadamnasi ya watu ambao ni waumini wake, lakini hadi sasa bado hajakamatwa, wala hajachukuliwa hatua zozote za kisheria?!.

Je, ni Kweli Mkuu wetu wa Mkoa, Paul Makonda ni Mhalifu?
Mkuu wa Mkoa, ni mteule wa rais, mtu huwezi kuteuliwa na rais, kushika wadhifa wowote mkubwa kabla ya hufanyiwa vetting na vyombo husika, hadi kijijini kwake alikozaliwa, hivyo haiwezekani kabisa Mhe. Paul Christian Makonda, ambaye ndie Mkuu wetu wa Mkoa wa Dar es Salaam, akawa ni mhalifu aliyefoji vyeti, hadi yeye Gwajima akagundua na kutangaza kanisani kwake, wakati tuna vyombo vya uchunguzi na ulinzi na usalama ambavyo vilipaswa kulijua hili kabla. Gwajima anamaanisha ama rais Magufuli amedanganywa na kututeulia kilaza kuwa mkuu wetu wa mkoa wa Dar es Salaam, ama yeye Mchungaji Gwajima ndie atakuwa ni muongo!.

Kama ni kweli Paul Makonda ni majina bandia, na majina yake ya ukweli ni Daudi Bashite, na pia kama ni kweli Daudi Bashite amefoji vyeti vya Paul Christian, saa hizi, asingekuwa bado ni mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam!, bali angepaswa kuwepo pale mahali wahalifu wengine wote wanapaswa wawepo!, kitendo cha Paul Makonda kuwa bado ni Mkuu wa Mkoa wa DSM mpaka saa hii, hii inamaanisha Mchungaji Gwajima ndiye muongo!.

Kwa Magufuli ninayemfahamu mimi, kama hizi tuhuma kuhusu Makonda zingekuwa na ukweli wowote, saa hizi, zamani angeishatumbuliwa!. Kitendo cha Makonda anaendelea kudunda mpaka sasa, huu ni uthibitisho, tuhuma hizi ni uongo za kupikwa tuu na wabwia na wauza unga!, ila jambo la ajabu sana ambalo hata mimi linanishangaza ni kitendo cha Mchungaji Gwajima kuusema uwongo mkubwa hivi na hajachukuliwa hatua yoyote!. Kitendo cha Gwajima kumuita Makonda ni kilaza, na kuachwa hivi hivi, pia kunamdhalilisha rais wa JMT, kutuleulia vilaza. Kama wakati ikiteuliwa, mamlaka ya uteuzi haikumjua kuwa ni kilaza, lakini baada ya taarifa hizi za Gwajima, zingekuwa ni za kweli, mamlaka yake ya uteuzi ingeishatengua utauzi huu!.

Mchungaji Gwajima ni Zaidi ya Mbunge, Zaidi ya Waziri, Zaidi ya Rais?!
Kwa vile Bwana wetu Yesu Kristu, ametufundisha, namna ya kuwatambua manabii wa uongo, tutawatambua kwa matendo yao, jee Yesu aliwahi kujitapa kuwa yeye ni zaidi ya yeyote?. Alipopelekwa kwa Pilato kwa kosa la kutajwa "Yesu Mnazareti Mfalme wa Mayahudi", licha ya Yesu kuwa ni Mfalme kweli, alinyamaza kimya, na alivyosisitizwa, akasema "wewe wasema", sasa iweje Mtumishi wa Mungu, Mchungaji Gwajima, akajiinua kuwa yeye ni zaidi ya rais wa nchi?, na kuwa kugombea urais kwake ni demotion!. Hivi kwa mtumishi wa Mungu wa kweli, anaweza kusema maneno kama haya madhabahuni kwa Mungu, au Mchungaji huyu, ni wale Manabii wa Uongo, Bwana wetu Yesu Kristu aliotuhusia?.

Msikilize Mchungaji Dr. Josephat Gwajima. Sikiliza Kwa sikio la roho, na sio sikio la mwili.


Mimi nimeisikiliza hii clip hii ya Mchungaji Gwajima, akimzungumzia Daudi Albert Bashite, A.K.A Paul Christian Makonda, akidai kuwa kilichomponza yeye Mchungaji Gwajima hadi kusingiziwa madawa ya kulevya, ni dhana kuwa Gwajima anataka kugombea ubunge jimbo la Misungwi, kufuatia kutua kijijini Kolomije kwa Chopa, (Helcopter), hivyo Daudi Bashite, A.K.A Paul Makonda ambaye anajipanga kugombea jimbo hilo mwaka 2020! kumuona Gwajima kama ni tishio!. Mchungaji Gwajima akajitapa Ubunge, Uwaziri hadi Urais kwa Mtumishi wa Mungu aliye hai ni demotion!. "Mtumishi wa Mungu ni zaidi ya Rais wa nchi!". Jee hii ni kweli?.

Daudi Albert Bashite, A.K.A Paul Christian Makonda "Kiumbe Huyu"
Akielezea kuhusu Daudi Albert Bashite, na yeye Mchungaji Gwajima, ni watu wa kabila moja na wametokea kijiji kimoja cha Kolomije. Daudi Bashite alisoma Shule Msingi ya Kolomije hadi darasa la tano, akahamia Shule ya Msingi ya Nyanza hadi akamaliza Darasa la 7, hakuchaguliwa, lakini akajiunga na Shule ya Sekondari Pamba ambayo ni ya serikali kwa jina jingine, akiwa anakaa kwa mama Kamese (Gwajima ana simu yake) ambako alipata Divisheni 0, ndipo dada mmoja wa Kihaya kwa jina la Christina (Gwajima ana simu yake) akamuunganishia Daudi Albert Bashite, kwa mdogo wake, Paul Christian, hivyo Daudi Bashite akaanza kutumia cheti cha kaka yake Paul Christian ndipo akajiunga Nyegezi kusomea certificate ya uvuvi kwa jina la Paul Christian, kisha akajiunga Chuo cha Mbegani Bagamoyo kuchukua diploma ya uvuvi kwa kutumia jina la Paul Christian na kumalizia Chuo cha Ushirika Moshi kuchukua degree kwa majina ya kughushi ya Paul Christian. Huu jamani sio uongo huu?.

Katika kumuelezea Daudi Bashite, Mchungaji Gwajima amemuita "kiumbe huyu", hili sio neno zuri kwa kiongozi wa dini ya Mungu kweli, kumuita binadamu mwenzako kiumbe!.

Uongo wa Gwajima ni Kumiliki Vyeti vya Daudi Albert Bashite na Paul Christian Makonda Mezani Kwake!.
Ila pia Mchungaji Gwajima amedai, anavyo vyeti vyote ofisini kwake tangu cha Daudi Albert Bashite alichopata Divisheni 0, hadi cheti cha Paul Christian alichounganishiwa na Christina!, na kudai kuwa ana mshitaki Makonda kwa Ndalichako na kwa Magufuli, na asipochukuliwa hatua zozote, yeye atashangaa sana na atavitoa vyeti hivyo hadharani, umma uvione. Jee hii inaweza kuwa kweli?, huu sio uongo mwingine wa mchana kweupe?

Hili la Mchugaji Gwajima kudai anavyo vyeti vya Daudi Bashite na Paul Christian, kwa maoni yangu, huu ni uongo!, kwa sababu nijuavyo mimi, mtu ulikuwa ukipata Div. 0 hupewi cheti chochote na NECTA zaidi ya Leaving Certificate, Leaving huwa haionyeshi umepata nini, sasa hicho cheti cha Daudi Bashite alichonacho Mchungaji Gwajima, kinachoonyesha Daudi Bashite alizungusha, Gwajima amekitoa wapi?

Kwa vile Daudi Bashite alifeli darasa la saba Nyanza, hawezi tena huyo huyo Daudi Bashite akajiunga na Shule ya Sekondari ya Pamba ambayo ni ya serekali, bali Daudi Bashite baada ya kufeli darasa la 7, hapo ndio mwisho rasmi wa jina la Daudi Albert Bashite, hivyo mtu aliyejiunga na shule ya sekondari ya Pamba, sio Daudi Bashite, bali alitumia jina la mwanafunzi mwingine aliyefaulu, hivyo Mchungaji Gwajima, hawezi kuwa na vyeti vya Daudi Bashite vinavyoonyesha kuwa alizungusha. Kwa kifupi, hakuna Daudi Bashite yoyote aliyesoma sekondari, Daudi Bashite original, aliishia darasa la saba!, hivyo kama Mchungaji Gwajima, anadai, anavyo vyeti vya Daudi Bashite, vinavyoonyesha alipata Div 0, huu utakuwa ni uongo!, ila mtanisamehe sana, sisi wengine tuu miongoni mwa wale wenye imani haba kamaTomaso, hatuamini mpaka tuone!. Kwa hapa naendelea kumwita Mchungaji Gwajima ni muongo hadi pale atakapo vitoa vyeti vya Daudi Bashite hadharani tuvione ndipo nitaamini!.

Hoja 20 za Uongo Kumhusu Paul Makonda
1. Alizaliwa tar.15/02/1981 katika kijiji cha Koromije, wilaya ya Misungwi, mkoa wa Mwanza.

2. Majina yake halisi ni Daudi Albert Bashite

3. Alianza darasa la kwanza mwaka 1988 katika shule ya msingi Koromije akitumia majina ya Daudi Albert Bashite. Mwaka 1991 alifeli darasa la 4, akarudia.

4. Mwaka 1992 alifeli tena na hivyo akahamishiwa Mwanza mjini, ili aweze kusoma na kupata masomo ya jioni (tuition).

5. Mwaka 1996 alihitimu darasa la 7 lakini hakuchaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari katika shule ya serikali.

6. Mwaka 1997 akajiunga na kidato cha kwanza shule ya sekondari ya Pamba.

7. Mwaka 2000 akahitimu kidato cha 4 na kupata daraja sifuri (division zero).

8. Mwaka 2001 akatumia cheti cha Ndg.Paul Christian Muyenge (chenye div.3 ya points 25) kujiunga na chuo cha uvuvi Nyegezi (Nyegezi Fisheries Training Institute) kwa masomo ya Certificate akahitimu mwaka 2002.

9. Mwaka huohuo 2002 akitumia cheti cha Ndg. Paul Christian Muyenge, alijiunga na Chuo cha uvuvi Mbegani Bagamoyo kwa masomo ya Diploma ya uvuvi (ORDINARY DIPLOMA IN MASTER FISHERMAN, NTA LEV.6), na kuhitimu mwaka 2005.

10. Mwaka 2003 alikutana na Ndg. Benjamin Sitta (mtoto wa Marehemu Samwel Sitta, ambaye ni Meya wa Kinondoni kwa sasa). Wakawa marafiki.

11. Mwaka 2005 baada ya kuhitimu Stashahada yake ya uvuvi, aliombaadmission Chuo cha Kilimo Sokoine kusoma shahada lakini akakosa nafasi.

12. Baada ya kukosa nafasi alienda kuishi nyumbani kwa Marehemu Sitta akiwa kama rafiki wa Ben (mtoto wa Sitta). Kwakuwa alitoka familia duni, Sitta aliahidi kumsomesha elimu ya juu.

13. Mwaka 2006, alipata udahili Chuo cha ushirika na biashara Moshi (wakati huo kikiwa chuo kikuu kishiriki cha SUA), kwa kutumia vyeti vyake vya certificate (ya Nyegezi) na diploma (ya Mbegani).

14. Alidahiliwa kwa course ya BA in Cooperate Management & Accounting. Mwaka 2007 alimaliza first year lakini akashindwa kuendelea na 2nd year baada ya kupata Suplementary 6 kati ya Course 8 alizokuwa akisoma (akawa discontinued).

15. Mwaka huohuo 2007 akaomba Admission upya. Akamaliza first yearakiwa na carries 3 ambazo alienda nazo 2nd year. Mwaka 2008 akiwa 2nd year akapata supplementary 4 kati ya course 8 alizokua akisoma. Akawa na mzigo wacarry over na supplementary. Akaamua kuacha chuo.

16. Mwaka 2008 akaenda kujaribu kuomba udahili chuo kikuu SUA kwa mara nyingine lakini akakosa.

17. Mwaka 2009 akarudi tena MUCcoBS kwa udahili mpya. Akaachana na CMA akachagua Community & Economic Development (CED).

18. Mwaka 20012 akahitimu shahada ya kwanza ya Community & Economic Development kwa jina la Paul C Makondabadala ya majina yake halisi ya Daudi Albert Bashite

19. Jina Makonda analitumia baada ya kula kiapo mahakamani kubadili jina. Cheti cha Form four kinasomeka Paul C Muyenge lakini vyeti vya elimu ya juu vinasomeka Paul C Makonda baada ya kuapa mahakamani.

20. Ndugu Daudi Albert Bashite ameoa (tangu mwaka 2009) lakini hajabahatika kupata mtoto. Na ndiye Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa sasa.

Hoja Moja ya Kweli Kumhusu Paul Makonda
Paul Makonda ndilo jina la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam aliyeteuliwa na Rais wa JMT. Jina la Paul Christian Makonda ndilo jina lake na elimu yake ni Shahada ya Chao Kikuu.

Mengine Yote ni Uongo Mtupu. Ukweli ni hiki kilichopo Sasa kuwa Paul Makonda ndiye Mkuu wetu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Je, Maneno na Matendo ya Mchungaji Gwajima ni Kama Yesu, ni ya KiMungu?
Swali ni jee huu ndio utendaji wa watu wa Mungu, kuwatakia wenzao mabaya?, kuwazushia uongo mchana kweupe tena madhabahuni kwenye mimbari ya Mungu?!. Yesu alitufundisha, "tumpe Kaisari yaliyo ya Kaisari, na tumpe Mungu yaliyo ya KiMungu, kwanini Mchungaji Gwajima, analeta ya Kaisari mezani kwa Bwana?!. Jee huyu Mchungaji Gwajima, ni mchungaji wa Mungu au ni wa mungu?.

Mchungaji Gwajima kama mtu wa Mungu wa kweli, anaweza kweli kusema uwongo kama ule madhabahuni kwa Bwana?!. Jee huyu ni mchungaji wa kweli anayemtumikia Mungu wa kweli, au ndio wale wachungaji aliyewasema Bwana wetu Yesu Kristo kuwa "kutajitokeza manabii wa uongo, ambao watahubiri neno na kutoa mapepo kwa jina langu lakini sii wangu". Wanafunzi wake wakamuuliza, "Jee tutawatambuaje?", Bwana Yesu akawajibu, "Mtawatambua kwa matendo yao".
Jee kwa matendo kama haya, kuna kitu chochote cha kutambua?

Mchungaji Gwajima ni Nabii wa Mungu, au nabii wa mungu?.
Japo nimewahi kushiriki Ibada kwa Mchungaji Gwajima, naomba mimi nisiseme kitu bali msikilize mmoja wa waumini wake ambaye pia ni mwanachama mwenzetu hapa jf.

Mwisho nimalizie na wewe mchungaji, tulipokutana mara ya kwanza nilikuchukulia kama kaka na kama mlezi wetu wa kiroho!! Lakini umegeuka shetani mwenye pembe saba, umeparaganyisha familia yangu, umeleta maumivu makali kwenye ukoo!! Nakuonya tena kwa mara nyingine, muache mkewangu!! Huyo ni mkewangu, nilimtolea mahali mimi mwenyewe na wazazi wake waliniamini na kunikabidhi!!! Nasema niachie mkewangu!! Wewe ni nyoka, imefika time watanzania wakujue ukweli wako wewe mbwa mwitu mkali uliyevaa ngozi ya kondoo!!! Umedanganya watu vya kutosha na umefarakanisha ndoa nyingi sana kwa sababu ya kiburi cha pesa zako chafu za sembe!! Umeudhalilisha ulokole kiasi cha kutosha imefika time tuwaeleze watanzania ukweli na wakufahamu kuwa wewe ni nyoka!!

Sitakubali kuona ukiendelea kuitesa familia yangu, nitapambana na nitakushinda!!! Siogopi fedha zako wala connection ulizonazo, ni bora nife nikiwa nimesimama kuliko kuishi nimepiga magoti! Nitapambana na wewe mpaka mwisho ili historia isomeke vizuri ili hata wanangu wakiwa wakubwa wajue kuwa baba yao sikuwa lofa kiasi cha kupiga magoti na kuelekeza shingo kibla kuruhusu mdhalimu kama wewe uichinje familia yangu, bali licha ya umasikini wangu nilisimama kiume na kupigana kutetea familia yangu!!!

Narudia tena mchungaji, nitapambana na nitakushinda.."
- The bold
Kwa ushuhuda huu mtaona tuhuma unga kwa Mchungaji hazikutolewa na Makonda kwa wivu wa helicopter au vita vya Jimbo bali Makonda alipewa majina na akayaanika.

Jumatatu Njema.
Paskali

Update
Wanabodi, kwenye siasa, hakuna rafiki wa kudumu, wala adui wa kudumu, kuna just common interest.
Japo katika bandiko hili, nilitofautiana na Gwajima, lakini kufuatia kwa sasa na mimi ni kada, wa Chama Cha Mapinduzi na mgombea aliyepitishwa na chama changu kugombea ubunge wa jimbo la Kawe kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, ni Askofu Gwajima, then naomba kudeclare kuwa sasa namuunga mkono Askofu Gwajima 100% kwa 100% tukalikomboe jimbo la Kawe lilokuwa utumwani kwa kipindi cha miaka kumi, tulirejeshe CCM!.
Kwa Kawe ya Maendeleo, chagua CCM, Chagua Gwajima, na kwenye uRais ni Magufuli, Mbunge ni Gwajima na madiwani wa CCM.
Mimi na Gwaji Boy...dam dam!.
P
 
Binadamu ni kiumbe, tunaposema kiumbe hai hatujatenga kua digidigi na kicheche ndiyo wanastahili jina kiumbe.

Zamani hata mtu akifeli alipata cheti lakini hata result slip itaonesha matokeo pia, pengine ana result slip.

Imeandikwa kua 'Ukiishi kwa upanga utakufa kwa upanga' kama maisha yako unayaendesha kinafiki subiri ukutane na wanafiki wenzako.
 
Hajasema ana matokeo, amesema ana vyeti mezani kwake, hivi kweli kuna cheti cha divisheni 0 ya miaka hiyo?.

Paskali
Aisee kumbe wengine mmesoma kw kukariri,kwani akiwa na result slip si ni cheti pia? Nyinyi mnawajua watumishi wote wanaosali kwa gwajima je kama wamempelekea ushahidi huo wa kuprint hata kama ni document sio cheti?pascally wewe nina wasi wasi utakuwa ni mhanga kama daudi bashite.
 
Nchi hii ni ngumu sana. Nilikua najiuliza kwa nini Kagame anaseaze watu kumbe ni watu kama gwajima na halafu amemnanga Raisi kiujanja ujanja kua hatompiga rais lakini atampiga Makonda.
 
Back
Top Bottom