M-mbabe
JF-Expert Member
- Oct 29, 2009
- 13,203
- 23,020
Manara chizi, GSM machizi na leadership yote ya Yanga ni machizi tu!View attachment 1930225
View attachment 1930248
View attachment 1930250
View attachment 1930262
Ndio kuna biashara,ndio kuna pesa. Lakini kumbukeni kuna utu na heshima mbele za watu.Zaidi ya yote kuna Akhera.
GSM mnajua kabisa huyu mtu ana msongo mkubwa wa mawazo baada ya kufukuzwa Simba Sc. Tunatambua nyinyi mlikuwa marafiki zake wakubwa hata kipindi akiwa Simba. Sasa urafiki gani huu usiojali utu na ubinaadamu.
Mnamtumia huyu ndugu kama msukule bila kujali utu wake mbele ya jamii?
Haya yanayoendelea yanaweza kumletea madhara makubwa zaidi kisaikolojia zaidi ya mvuta bangi. Msaidieni kiungwana,mbona kuna wapenzi wa Simba kama Ommy Dimpoz tunaona anatangaza bidhaa zenu bila kujihusisha na mambo ya Yanga? Tunzeni utu wa huyu ndugu anaoza ndani kwa ndani