Green Guard ina tofauti na Interahamwe?

Green Guard ina tofauti na Interahamwe?

Msharika

JF-Expert Member
Joined
May 15, 2009
Posts
947
Reaction score
71
Ndugu wana JF, nimesikitishwa sana kusikia kuwa Chama Cha Mapinduzi kina jeshi.

Je hii ndio katiba ya nchi kuwa kila chama kiwe na jeshi lake? Mbona hapatatosha.

Ninasadiki kuwa Nyerere (RIP) aliona mbali kwa kuondoa kile kiitikio cha "zidumu fikra sahihi za mwenyekiti wa chama".

Nielewesheni jamani
 
Yawezakana hukupata bahati ya kusoma historia ya nchii hii, sasa historia inabaki kuwa historia tu hata kama haitakuvutia.

Wakati TANU ikianzishwa kulikuwa na vijana waliokuwa na majukumu ya kulinda chama na viongozi wake, kulinda mikutano ya TANU na kazi zingine ambazo vijana wangeweza kuzifanya kulingana na ujana wao kwa maslahi ya Chama. vijana hawa waliitwa TANU YOUTH BANTU na baadae TANU YOUTH LEAGUE (umoja wa vijana wa TANU)!

Baada ya kuanzishwa kwa CCM umoja huo uliendelea na kubadilika kuwa UVCCM(Umoja wa Vijana wa CCM) wenye sehemu ya chipukizi na green Guard, hawa green guard majukumu ni yao ni sawa na niliyokueleza hapo kwenye sehemu ya TANU YOUTH BANTU. swali jingine?
 
Leo wameripotiwa na chombo kimoja cha habari kama Janjaweed wa CCM baada ya kumchakaza mwanachama wa cha cha upinzania na kumvunja mbavu kule Busanda. Janjaweed kule Zanzibar ni maarufu kwa vurugu dhidi ya Wapinzani kama ilivyo kule Dafur Sudan.

Kwa ufupi ni wasaidizi wa Jeshi la Polisi na hutumika pale inapoonekana Polisi wanashindwa kutimiza maagizo na matazamio ya CCM katika chaguzi mbalimbali.
 
Nimekuwa nikifatilia hiki kikundi kinachoitwa green guard kwa muda hivi malengo yake nn?mbona kama baadhi ya vitendo vyake kama kupiga wapinzani vinashabihiana na vilivyofanywa na kile kikundi maalufu kilichotekeleza mauaji ya kimbari kule rwanda?mwenye kujua shughuli zake kwa undani atupashe,usipoziba ufa utajenga ukuta
 
Mahakama ya uharifu wa kivita inawasubiria,ukiwaangalia hali zao ni ngumu na wanakubali kuendelea kutumika,waache siku zao zinahesabika
 
Tofauti ya Simba na chui kwa ukatili haipo kwa hiyo ni walewale....ICT(R)T
 
Hata wakiwatumia hao Green Guards, ipo siku tu watashindwa na nguvu ya umma.
 
swali la msingi ni moja, kama tanzania ni nchi ya amani, na ccm ni chama chenye demokrasia safi, kuna haja gani ya jeshi lao jingine nje ya majeshi ya ulinzi na usalama? hakuna tofauti kati ya green guard na wahalifu
 
Green Guard wanaratibiwa kwa ufanisi zaidi kuliko Interahamwe....
 
Nimekuwa nikifatilia hiki kikundi kinachoitwa green guard kwa muda hivi malengo yake nn?mbona kama baadhi ya vitendo vyake kama kupiga wapinzani vinashabihiana na vilivyofanywa na kile kikundi maalufu kilichotekeleza mauaji ya kimbari kule rwanda?mwenye kujua shughuli zake kwa undani atupashe,usipoziba ufa utajenga ukuta


Swali zuri sana hilo. Kwanini CCM haiamini jeshi letu la polisi hadi kuamua kuwa na jeshi lao?
 
Hilo ni jeshi la CCM, watatwambia walipata kibali wapi cha kuanzisha jeshi. Halafu Mwema na Mwamunyange wako wapi mpaka chama kinaanzisha na kuimarisha jeshi lake?
 
sheria ya nchi inazuia kuanzishwa vikundi vyenye malengo kama ya green guard, sasa wao wako juu ya sheria au ndo mambo ya kibanzi na boriti ndani ya jicho?
Upinzani umeshindwa mara 3 uchaguzi mkuu lakini hawana hivi vikundi vyenye mrengo na sera za kiinterahamwe/ janjaweed. Sasa anayehatarisha amani ni ccm au wapinzani? madaraka matamu jamani! sheria zinapindishwa haswa (kukidhi matakwa ya ccm)
 
Nimekuwa nikifatilia hiki kikundi kinachoitwa green guard kwa muda hivi malengo yake nn?mbona kama baadhi ya vitendo vyake kama kupiga wapinzani vinashabihiana na vilivyofanywa na kile kikundi maalufu kilichotekeleza mauaji ya kimbari kule rwanda?mwenye kujua shughuli zake kwa undani atupashe,usipoziba ufa utajenga ukuta

"The military don't start wars. Politicians start wars."
 
Sasa anayetaka kuleta umwagaji damu nchini ni wale ambao hawana jeshi lao au wale wenye jeshi lao ambalo linafanywa siri? Hebu tuelezwe vizuri hapa nani hasa anayetaka kuleta umwagaji damu.
 
sheria ya nchi inazuia kuanzishwa vikundi vyenye malengo kama ya green guard, sasa wao wako juu ya sheria au ndo mambo ya kibanzi na boriti ndani ya jicho?
Upinzani umeshindwa mara 3 uchaguzi mkuu lakini hawana hivi vikundi vyenye mrengo na sera za kiinterahamwe/ janjaweed. Sasa anayehatarisha amani ni ccm au wapinzani? madaraka matamu jamani! sheria zinapindishwa haswa (kukidhi matakwa ya ccm)

blue guard je?!
 
Mwenyezi mungu awe nasi Wana wa Tanzania, nimesikia sauti ikinipa ujumbe kwamba ni muda muafaka sasa kwa viongozi wa dini wakasema neno juu ya green guard. Inavyoonekana hawajaanza kusema juu ya hilo wakati tayari limeshaanza kuleta madhara.Tunajua watasema maana wao si wanafiki siku zote na tumezoea kuwaona wakiwa hivyo.Zipo sauti za baadhi ya viongozi wa DINI ambao mara nyingi wakiongea huwa nchi inatikisika kwa watu wote pamoja na serikali hufungua masikio, lakini hadi sasa hawajaongea mimi naamini lazima wataongea kwani wao si wanafiki lakini wasiwasi wangu ni kwamba wanaweza waje kuongea muda umepita na madhara tayari yametokea na pengine hayadhibitiki tena.
Tunawasihi sasa waongee kabla hatujafika huko. Hawa wana karama hiyo si kwamba kuna upendeleo, hapana wamejariwa na mwenyezi mungu kuwa hivyo(sauti zao ni mamalaka kamili) .Naamini hata wewe unayesoma unakubaliana na mimi.Najua pia kwa sasa wako bussy wanasali kwa kufunga novena na hija mbalimbali kwa nia nzuri ya kuombea amani.Basi ni vema watoke mafichoni wasema MOJA KWA MOJA KWA KUKEMEA JESHI HARAMU LA CCM,nasi tutasikia hata serikali isiyo sikivu itasikia na itaweweseka kwa kuelewa ahaaa wenye AMANI, UPENDO NA MATUMAINI wamenena.
SEMENI BUS LILOBEBA AMANI YA TANZANIA KARIBU LINAOONDOKA HAMTALIPATA KWANI LINA MWENDO MKALI
Ni hayo tu
 
Hii ni hatari sana!sana mambo ya Rwanda ya 1994 yameshaanza kuandaliwa hapa!
 
KWELI TUMEFIKA HAPA??


DSC01454.jpg



DSC01451.jpg



Wakazi wa Musoma walivyokatana (Green Guard) mapanga hivi karibuni


Source: Mjengwa
 
Maggid anaona kwa wanamusoma kuuana siyo tatizo. hiyo amenukuu kwa bosi wake (JK) alipokuwa anaelezea vita vya kikabila musoma kwamba wakurya ni utamaduni wao kuuana wanapohitilafiana.

Sasa maggid aje huku kufafanua hiyo jadi ya wakurya. halafu fujo za CCM dhidi ya vyama vingine wa kulaumiwa ni polisi.
haya sisi yetu macho
 
Back
Top Bottom