Graduates, how do you survive?

Graduates, how do you survive?

mimi nilisoma mzumbe Bsc.applied statistics,huwa tukifika mwaka wa pili tunakuwa na likizo ndefu ya miezi sita,kipindikile cha likizo nilitafuta field halmashauri ya wilaya niliyozaliwa ili kuhakikisha nasave pesa yangu ya field nifanyie kitu cha maendeleo.Nilifanikiwa kuanzisha saloon yangu pale wilayani kwangu,saloon ile inanipa 10,000 kila siku ya mungu kwahiyo nilipomaliza chuo kwakweli machungu ya kutoajiriwa sikuyaona mimi,mpaka baada ya miaka miwili nilipopaka kazi nikaendelea na maisha.Tatizo watoto wa siku hizi wanachezea hela unamkuta na lisimu la 1mil mara ana IPAD mazaga zaga kibao afu akimaliza chuo hana kazi analalamika tu mtaani,tumieni fedha mnazopata vizuri jamani usingojee mpaka umalize chuo ndo uanze kuhangaika hii ni sawa na mtu kufanya kazi akajisahau akaja kushtuka wakati wa kustaafu NI HATARI,PUNGUZENI STAREHE PUNGUZENI KWENDA KUPOTEZA MUDA MLIMANI CITY,PUNGUZENI POMBE,PUNGUZENI NGONO HAKUNA AJIRA SIKU HIZI NDUGU ZANGU AJIRA YAKO NI UBONGO WAKO.

umeongea kitu kikubwa sana.. mimi nilimaliza 2010 na kubahatika kupata kazi nzuri tu kiasi chake ( kwa mshahara niliokuwa napata sio mbaya kakini nilikuwa siipendi hiyo kazi tu).. nikafanya kwa miaka minne na kusave kama m 10 hivi + nssf nilikuwa na salio kama m 13 hivi.. nikaacha hiyo kazi na kujiajiri kwenye shughuli zangu za ujanani..

sasa safari hii nikarudi kisasa sababu nilikuwa na mtaji.. nikawekeza kama m15 hivi kwenye vifaa vya kazi na kuanz Rasmi safari ya kujiajiri..

inakaribia mwaka sasa toka niache kazi na sijawai kujutia..

halafu cha kushangaza.. nowdays napata sana kazi.. wakati nipo busy kwenye ajira yangu mwenyewe
 
mkuu hata huko kuvolunteer hakupatikani kirahisi hivyo!!


Duh! Poleni sana aisee, miaka yetu ilikuwa ukisema ku-volunteer wanakukimbilia faster, lakini kazi zote za hiyo idara utafanya wewe, wenzio wapo busy na shughuli zao binafsi. Walikuwa wanatukimbilia ili tuwapunguzie u-busy ofisini kwao, basi kwasasa mambo yamebadilika.
 
Tatizo ya graduate wengi hawapendi kuvaa uhalisia MTU mda wote anapenda achomekee na wakati buku ya nauli kaomba kwa jama take. me nilimaliza pale st john miaka mitatu iliyopita Lakin baada yakuomba ajira sana niliamua kujiajiri na sasa namshukuru mungu kwani biashara yangu nishaisajili mambo yanaenda. Mtaji ndio wimbo WA kila MTU shida ni usubutu ukiwa na laki moja ni mtaji mkubwa sana Yule mmachinga pale Kariakoo anapata faida zaidi ya elf 20 KWA siku mtaji wake hauzid laki mbil sawa na simu yako ya smart phone

we ni mjinga wa mwisho, yaan umesoma hadi university alafu ukafanye umachinga? sasa kwa nini uliedna chuo kikuu badala ya kua machinga toka enzi izo?
 
we ni mjinga wa mwisho, yaan umesoma hadi university alafu ukafanye umachinga? sasa kwa nini uliedna chuo kikuu badala ya kua machinga toka enzi izo?
sasa we unaona ni bora aombe hela kwa watu sababu anadegree. Bakharesa na utajiri wote anauza chapati na maandazi
 
mimi nilisoma mzumbe Bsc.applied statistics,huwa tukifika mwaka wa pili tunakuwa na likizo ndefu ya miezi sita,kipindikile cha likizo nilitafuta field halmashauri ya wilaya niliyozaliwa ili kuhakikisha nasave pesa yangu ya field nifanyie kitu cha maendeleo.Nilifanikiwa kuanzisha saloon yangu pale wilayani kwangu,saloon ile inanipa 10,000 kila siku ya mungu kwahiyo nilipomaliza chuo kwakweli machungu ya kutoajiriwa sikuyaona mimi,mpaka baada ya miaka miwili nilipopaka kazi nikaendelea na maisha.Tatizo watoto wa siku hizi wanachezea hela unamkuta na lisimu la 1mil mara ana IPAD mazaga zaga kibao afu akimaliza chuo hana kazi analalamika tu mtaani,tumieni fedha mnazopata vizuri jamani usingojee mpaka umalize chuo ndo uanze kuhangaika hii ni sawa na mtu kufanya kazi akajisahau akaja kushtuka wakati wa kustaafu NI HATARI,PUNGUZENI STAREHE PUNGUZENI KWENDA KUPOTEZA MUDA MLIMANI CITY,PUNGUZENI POMBE,PUNGUZENI NGONO HAKUNA AJIRA SIKU HIZI NDUGU ZANGU AJIRA YAKO NI UBONGO WAKO.
Mkuu hapo kwenye red umepiga za chembe!!!

Vijana wa siku hizi hovyo kabisa wamebaki kulalamika tu kama mawaziri wa serikali ya Kikwethe! Unakuta kijana yuko home tu analala mpaka saa 4 akiamka anapiga chai ya home baadaye anaingia vijiweni tu bila kazi, muda wa lunch ukifika anajivuta kurudi home kupiga msosi!! Halafu unakuta eti naye anachagua kazi. Sasa hivi mbona fursa kibao? Shule za Yebo Yebo hazina walimu kwa nini usipige tempo pale wakati unasubiria ajira ya maana? Hapo hukosi ya maji, masomo ya sayansi hayana walimu kwa nini usifungue kijiwe cha tuition hapo mtaani kwenu? Hili hata kijijini linawezekana kabisa!! Vijana acheni kuchagua kazi, pigeni mzigo mtaishi tu!!

Nakumbuka miaka ile wakati serikali imesimamisha mambo ya ajira, tulivyomaliza chuo cha kati tuliaagwa kwenda mitaani bila uhakika wa ajira. Mtaani kulipokuwa kuchungu ilibidi tupige kazi ya kusogeza zege kwa mafundi, kujifunza ufundi uashi. Kila siku kulikuwa na uhakika wa 5,000/= (ya wakati huo). Maisha yalikuwa tambarare tu mpaka tulipokuja kupata ajira!
 
sasa we unaona ni bora aombe hela kwa watu sababu anadegree. Bakharesa na utajiri wote anauza chapati na maandazi

Uza chapati na maandazi basi tuone nawewe kama utakuwa bakhressa.
 
Tatizo ya graduate wengi hawapendi kuvaa uhalisia MTU mda wote anapenda achomekee na wakati buku ya nauli kaomba kwa jama take. me nilimaliza pale st john miaka mitatu iliyopita Lakin baada yakuomba ajira sana niliamua kujiajiri na sasa namshukuru mungu kwani biashara yangu nishaisajili mambo yanaenda. Mtaji ndio wimbo WA kila MTU shida ni usubutu ukiwa na laki moja ni mtaji mkubwa sana Yule mmachinga pale Kariakoo anapata faida zaidi ya elf 20 KWA siku mtaji wake hauzid laki mbil sawa na simu yako ya smart phone

Mkuu ukituambia ulijiajiri katika kazi gani au biashara gani na kwa mtaji kiasi gani utakuwa umetusaidia zaidi.
 
Kapige kazi za ku-volunteer kwenye profession yako, Angalau utakuwa unapata lunch free (kama ofisi hiyo sio makauzu) unapunguza machungu huku unaendelea kupata uzoefu.

Nshatafuta sana. Nimepata sehemu moja lakini hata lunch yenyewe haipo
 
We ni mkumbafu KWA kuwa umemaliza chuo kikuku ndio usiwe mmachinga utaishia na elimu yako ya chuo kikuku vijana wenye umri sawa na wewe washaanza maisha kitambo we we utazeeka na hiyo elimu yako yachuo kikuu unaish maisha ya nadharia unataka uwe na gari kal nyumba nzuri nawakati hata mia huna
 
Imenigusaaa hiii nenda kajitolee hata kupigaa Tempo Shule za kata utajikeep bize usionee ugum Wa maishaa
 
Unatakiwa kuielewa sentensi hiyo::: Maisha ni kupambana so there is either upambane na utoke au ugive up!! Giving up life u understand maana yake nini... So usifikiri ni utani bali ni njia ya kuconvey message kwako kwamba fight and utatoka... Sasa unafight nini... Do any work that is legal and win ur daily bread, make connections na watu waliopo kazini ili kupata wigo Zaidi wa discipline yako
Tatizo kubwa la Graduate wa siku hizi ukilogwa ukampa nafasi ya volunteer au maana nyingine tunaita Entership, umekwisha. WANAPIGA SI KAWAIDA. Sasa tabu ya nini, nikuajili alafu nikae kukuchunga husinipige mtaji. Kwa kweli mimi nikishasikia mtu ni graduate alafu kavaa Kata Kiuono. Mwogope sana.
Ndugu zangu mnachagua kazi, mnataka high life, wakati baadooo ndo kumekucha. Fungukeni pia tafuta nauri kama shida yako ni kuajiliwa nenda hapo Singapore kazi za mahotelini na viwandani zimejaa tu. DRC ni za kumwaka ukipiga miaka yako 2 au 3 una mtaji sasa ukajipige mwenyewe. Hapa Bongoland mmeshakuwa nuksi. Kila mahali, kila ofisi ilokuwa imemwajili mtu on intership basis inalia kwa kupigwa.
Kimsingi mmeshakuwa issue. JIFUNZENI UJASILIA MALI (ENTERPRENAURESHIP). ITAWASAIDIA. AMBAYE HAWEZI HAJE HAPA KWANGU
 
Mkuu ukituambia ulijiajiri katika kazi gani au biashara gani na kwa mtaji kiasi gani utakuwa umetusaidia zaidi.
Kijana wewe una tatizo kubwa sana. Mtaji mkubwa kwenye ajila ni WAZO. Ukiwa na wazo na ukalitathimini likwa feasible then umeshatokaaaaaaa. Mtaji utakuja tu. Uwezi kusema unataka shs ngapi wakati hujui la kufanya.
 
Back
Top Bottom