Graduates, how do you survive?

Graduates, how do you survive?

juakal

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2015
Posts
587
Reaction score
125
Salama wakuu?

Iko wazi kuwa sio vijana wote wanapata ajira baada ya kuhitimu masomo.
Naomba tubadilishane ujuzi jinsi ya kuyakabiri maisha baada ya kuhitimu. Mwenye mapenzi mema anaweza ku8tueleza ni shughuli gani amekuwa akizifanya ili kuingiza chochote mfukoni na aliwezaje kupata hiyo shughuli au kazi.

Kila atakayetoa mchango wake hapa atakuwa amewawezesha au kuwafungua vijana wengi ambao wako kama mimi niliyehitimu chuo yapata miaka mitatu iliyopita nikiwa na vyeti vizuri lakini maisha yanazidi kuwa magumu kila kukicha.

Nawakaribisheni sana.
 
Ndugu Mimi naona una uzoefu wa kutosha kabisa!! Miaka mitatu bila kazi na uliweza kusurvive! Hebu waambie graduates wafanye nini... Maisha ndo hayahya...
"Kama maisha magumu achana nayo fanya issue nyingine"
 
Sasa tunaishi vzuri kwani tunajifanya 4U movement hivyo posho tunapata kutoka kwa ndg yetu mtanzania mwenzetu Lowassa. Hali cjui itakuwaje akishindwa au akipata urais.
 
mimi nilisoma mzumbe Bsc.applied statistics,huwa tukifika mwaka wa pili tunakuwa na likizo ndefu ya miezi sita,kipindikile cha likizo nilitafuta field halmashauri ya wilaya niliyozaliwa ili kuhakikisha nasave pesa yangu ya field nifanyie kitu cha maendeleo.Nilifanikiwa kuanzisha saloon yangu pale wilayani kwangu,saloon ile inanipa 10,000 kila siku ya mungu kwahiyo nilipomaliza chuo kwakweli machungu ya kutoajiriwa sikuyaona mimi,mpaka baada ya miaka miwili nilipopaka kazi nikaendelea na maisha.Tatizo watoto wa siku hizi wanachezea hela unamkuta na lisimu la 1mil mara ana IPAD mazaga zaga kibao afu akimaliza chuo hana kazi analalamika tu mtaani,tumieni fedha mnazopata vizuri jamani usingojee mpaka umalize chuo ndo uanze kuhangaika hii ni sawa na mtu kufanya kazi akajisahau akaja kushtuka wakati wa kustaafu NI HATARI,PUNGUZENI STAREHE PUNGUZENI KWENDA KUPOTEZA MUDA MLIMANI CITY,PUNGUZENI POMBE,PUNGUZENI NGONO HAKUNA AJIRA SIKU HIZI NDUGU ZANGU AJIRA YAKO NI UBONGO WAKO.
 
Sasa tunaishi vzuri kwani tunajifanya 4U movement hivyo posho tunapata kutoka kwa ndg yetu mtanzania mwenzetu Lowassa. Hali cjui itakuwaje akishindwa au akipata urais.

Lakini bora mnaweza kuishi kwa sasa
 
Joking nyingi kwenye mambo ya serious tatizo..

Unatakiwa kuielewa sentensi hiyo::: Maisha ni kupambana so there is either upambane na utoke au ugive up!! Giving up life u understand maana yake nini... So usifikiri ni utani bali ni njia ya kuconvey message kwako kwamba fight and utatoka... Sasa unafight nini... Do any work that is legal and win ur daily bread, make connections na watu waliopo kazini ili kupata wigo Zaidi wa discipline yako
 
mimi nilisoma mzumbe Bsc.applied statistics,huwa tukifika mwaka wa pili tunakuwa na likizo ndefu ya miezi sita,kipindikile cha likizo nilitafuta field halmashauri ya wilaya niliyozaliwa ili kuhakikisha nasave pesa yangu ya field nifanyie kitu cha maendeleo.Nilifanikiwa kuanzisha saloon yangu pale wilayani kwangu,saloon ile inanipa 10,000 kila siku ya mungu kwahiyo nilipomaliza chuo kwakweli machungu ya kutoajiriwa sikuyaona mimi,mpaka baada ya miaka miwili nilipopaka kazi nikaendelea na maisha.Tatizo watoto wa siku hizi wanachezea hela unamkuta na lisimu la 1mil mara ana IPAD mazaga zaga kibao afu akimaliza chuo hana kazi analalamika tu mtaani,tumieni fedha mnazopata vizuri jamani usingojee mpaka umalize chuo ndo uanze kuhangaika hii ni sawa na mtu kufanya kazi akajisahau akaja kushtuka wakati wa kustaafu NI HATARI,PUNGUZENI STAREHE PUNGUZENI KWENDA KUPOTEZA MUDA MLIMANI CITY,PUNGUZENI POMBE,PUNGUZENI NGONO HAKUNA AJIRA SIKU HIZI NDUGU ZANGU AJIRA YAKO NI UBONGO WAKO.

Asante mkuu. Pia hongera kwa mafanikio hayo. Hata mimi naikumbuka sana ile pesa ya field, sikuifanyia lolote la maana.
Thanx once more…
 
Miaka mitatu!?? Pole sana, ila tuambie umewezaje kisurvive muda wote huo!!
 
Tatizo ya graduate wengi hawapendi kuvaa uhalisia MTU mda wote anapenda achomekee na wakati buku ya nauli kaomba kwa jama take. me nilimaliza pale st john miaka mitatu iliyopita Lakin baada yakuomba ajira sana niliamua kujiajiri na sasa namshukuru mungu kwani biashara yangu nishaisajili mambo yanaenda. Mtaji ndio wimbo WA kila MTU shida ni usubutu ukiwa na laki moja ni mtaji mkubwa sana Yule mmachinga pale Kariakoo anapata faida zaidi ya elf 20 KWA siku mtaji wake hauzid laki mbil sawa na simu yako ya smart phone
 
Kapige kazi za ku-volunteer kwenye profession yako, Angalau utakuwa unapata lunch free (kama ofisi hiyo sio makauzu) unapunguza machungu huku unaendelea kupata uzoefu.
 
Kapige kazi za ku-volunteer kwenye profession yako, Angalau utakuwa unapata lunch free (kama ofisi hiyo sio makauzu) unapunguza machungu huku unaendelea kupata uzoefu.

mkuu hata huko kuvolunteer hakupatikani kirahisi hivyo!!
 
Back
Top Bottom