TANZANIA PATRIOT
Member
- Jul 2, 2019
- 32
- 43
Roma Mkatoliki azua taharuki
Jumapili , 17 Nov , 2019
Mwandishi: Ismail Sarumbi
Rapa Roma Mkatoliki amewaacha njia panda mashabiki wake kwa kile alichokiimba katika wimbo wake mpya wa 'Naitwa Roma' ambapo watu wengi wameshindwa kutafsiri mashairi yalitumiwa humo huku wengine wakijiulza kwa nini ameamua kumkosoa Rais John Pombe Magufuli na kuikosoa serikali ya awamu ya tano katika wimbo huo ambao unaongoza kuangliwa zaidi katika mtandao wa YouTube.
Naitwa Roma: Umewakera sana viongozi wa Serikali kutokana na ujumbe mzito ambao unailenga serikali kama utekaji wa watu,watu kuuliwa, wakulima wa korosho kutokulipwa pesa zao,pia Roma ametaja kuwa viongozi wa awamu ya tano wanapenda sifa na hawapendi kukosolewa. Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo Dr. Harrison Mwakyembe ni kiongozi wa kwanza kuongelea hadharani wimbo huo na kusema kama Roma darasa la saba atamwambia nini yeye ana shahada nne na pia ni mwalimu mbobezi wa falsafa katika vyuo vingi. Akaendelea kusema kwamba kama Roma ataendelea kuikosoa Serikali hivo bora basi ananzishe chama chake cha siasa ili ijulikane ni mwanasiasa. Pia tuliona katika mtandao wa Twitter Msemaji wa Ikulu Msigwa aliposti akisema “Anaitwa JPM” muda mchache baada ya Roma kuwa ana-trend katika mitandao.
Katika wimbo huo Roma Mkatoliki amejaribu kuhusisha matukio mbalimbali ya kisiasa pamoja na lile la kwake kubwa la kutekwa ambapo hii ndiyo kazi yake ya kwanza kufunguka wazi tokea ule mkasa wake wa kutekwa kuisha na kusababisha maumivu mengine makali kutoka kwa mashabiki zake baada ya kuona 'video' yake mpya iliyojaa hisia kali za maumivu.
Hata hivyo, kuna tetesi kwamba wimbo huo mashairi pamoja na gharama za kuutengeneza na kuupeleka studio kuna kikundi cha wanaharakati Nchini ambao wamekuwa wakipigania haki pamoja na mabadiliko ya uwongozi wakina Maria Sarungi, Fatma Karume, ambao inaaminika kwamba wana vikundi vya vijana waliopo nje na ndani ya nchi kama vile Tito Magoti ambaye ni mfamyakazi katika kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Kigogo14 ambaye pia inaaminika anasapotiwa na viongozi wa upinzani Mh Zitto Kabwe ametajwa sana. Pia kuna watu wengine kama Mwanaharakati wa Haki za LGBT anayeitwa Goodluck Haule, pia View attachment 1264856kuna mtu anatumia jina la Mcomoro kwenye mtandao wa Twitter. Hawa wamekuwa mstari wa mbele kuusambaza na kuupigia kampeni wimbo huo ambao ndani ya masaa 24 ulifika namba moja ukizipita nyimbo kama “Baba Lao” ya Diamond na “Mshumaa” ya Ali Kiba.
Bashite ya wadau wa mziki nchini wametoa maoni yao jinsi walivyoupokea ujio mpya wa Roma na hizi ni baadhi tu ya zile zilizoandikwa na mashabiki wa Roma.
Pharergy Ramson: “#AnaitwaRoma ni harakati atazifanya nani zaidi ya Roma 'but' ngoma iko poa hujawahi kuniangusha ila umebadirika kidogo mzee. Nadhan kwenye hii ngoma umejibu maswali ya watu wengi sana kipindi unafanya 'show' pale 'Dar live' nilitamani urudie hii nyimbo 'but' sikuwa na uwezo ila umefanya vizur."
Blandina Bilau: "Simjui sana Roma wala kufuatilia nyimbo zake lakini huu wimbo umeniliza, 'message' imefika jipe moyo. Mtetezi wako Mungu aendelee kukutetea"
Arthur Oyaro: "Duuh 'so sad' na utu uzima huu machozi nimeshindwa kuyazuia,'thank' pia kwa kunifikirisha. Viva Roma viva''
Mdachi Classic: "Nimefatilia 'comment' nyingi sana ila sijaona hato komenti inayozungumzia vibaya hii ngoma zaidi ni za upendo na za kuumizwa tu. 'In short' hii imetugusa sana pole sana kaka yupo mungu hakimu wa yote".
Ibrahim Utenga: ''This song reflects the real prevailing situation, it's very sensitive song, congratulations to you brother, God save you "
Ndongo Nyambalya: "Nina wasiwasi wewe Mkatoliki hicho siyo kichwa ni semi-computer, kwenye Mungu wa John na Daud hapo nimefikiria hadi najikuta nurudiarudia kusikiza, U deserve bro! Gat u! 100".
Kwa upande mwingine, Roma Mkatoliki amemwagiwa sifa kedekede na mashabiki zake ambao walikuwa wamemisi kusikia na kuona kazi zake na kuweza kurudi katika uhalisia wake bila ya kuhofia jambo lolote litakaloweza mtokea tena mbele yake kwa ukali wa tungo zilizojaa za kufikirika.
Jumapili , 17 Nov , 2019
Mwandishi: Ismail Sarumbi
Rapa Roma Mkatoliki amewaacha njia panda mashabiki wake kwa kile alichokiimba katika wimbo wake mpya wa 'Naitwa Roma' ambapo watu wengi wameshindwa kutafsiri mashairi yalitumiwa humo huku wengine wakijiulza kwa nini ameamua kumkosoa Rais John Pombe Magufuli na kuikosoa serikali ya awamu ya tano katika wimbo huo ambao unaongoza kuangliwa zaidi katika mtandao wa YouTube.
Naitwa Roma: Umewakera sana viongozi wa Serikali kutokana na ujumbe mzito ambao unailenga serikali kama utekaji wa watu,watu kuuliwa, wakulima wa korosho kutokulipwa pesa zao,pia Roma ametaja kuwa viongozi wa awamu ya tano wanapenda sifa na hawapendi kukosolewa. Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo Dr. Harrison Mwakyembe ni kiongozi wa kwanza kuongelea hadharani wimbo huo na kusema kama Roma darasa la saba atamwambia nini yeye ana shahada nne na pia ni mwalimu mbobezi wa falsafa katika vyuo vingi. Akaendelea kusema kwamba kama Roma ataendelea kuikosoa Serikali hivo bora basi ananzishe chama chake cha siasa ili ijulikane ni mwanasiasa. Pia tuliona katika mtandao wa Twitter Msemaji wa Ikulu Msigwa aliposti akisema “Anaitwa JPM” muda mchache baada ya Roma kuwa ana-trend katika mitandao.
Katika wimbo huo Roma Mkatoliki amejaribu kuhusisha matukio mbalimbali ya kisiasa pamoja na lile la kwake kubwa la kutekwa ambapo hii ndiyo kazi yake ya kwanza kufunguka wazi tokea ule mkasa wake wa kutekwa kuisha na kusababisha maumivu mengine makali kutoka kwa mashabiki zake baada ya kuona 'video' yake mpya iliyojaa hisia kali za maumivu.
Hata hivyo, kuna tetesi kwamba wimbo huo mashairi pamoja na gharama za kuutengeneza na kuupeleka studio kuna kikundi cha wanaharakati Nchini ambao wamekuwa wakipigania haki pamoja na mabadiliko ya uwongozi wakina Maria Sarungi, Fatma Karume, ambao inaaminika kwamba wana vikundi vya vijana waliopo nje na ndani ya nchi kama vile Tito Magoti ambaye ni mfamyakazi katika kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Kigogo14 ambaye pia inaaminika anasapotiwa na viongozi wa upinzani Mh Zitto Kabwe ametajwa sana. Pia kuna watu wengine kama Mwanaharakati wa Haki za LGBT anayeitwa Goodluck Haule, pia View attachment 1264856kuna mtu anatumia jina la Mcomoro kwenye mtandao wa Twitter. Hawa wamekuwa mstari wa mbele kuusambaza na kuupigia kampeni wimbo huo ambao ndani ya masaa 24 ulifika namba moja ukizipita nyimbo kama “Baba Lao” ya Diamond na “Mshumaa” ya Ali Kiba.
Bashite ya wadau wa mziki nchini wametoa maoni yao jinsi walivyoupokea ujio mpya wa Roma na hizi ni baadhi tu ya zile zilizoandikwa na mashabiki wa Roma.
Pharergy Ramson: “#AnaitwaRoma ni harakati atazifanya nani zaidi ya Roma 'but' ngoma iko poa hujawahi kuniangusha ila umebadirika kidogo mzee. Nadhan kwenye hii ngoma umejibu maswali ya watu wengi sana kipindi unafanya 'show' pale 'Dar live' nilitamani urudie hii nyimbo 'but' sikuwa na uwezo ila umefanya vizur."
Blandina Bilau: "Simjui sana Roma wala kufuatilia nyimbo zake lakini huu wimbo umeniliza, 'message' imefika jipe moyo. Mtetezi wako Mungu aendelee kukutetea"
Arthur Oyaro: "Duuh 'so sad' na utu uzima huu machozi nimeshindwa kuyazuia,'thank' pia kwa kunifikirisha. Viva Roma viva''
Mdachi Classic: "Nimefatilia 'comment' nyingi sana ila sijaona hato komenti inayozungumzia vibaya hii ngoma zaidi ni za upendo na za kuumizwa tu. 'In short' hii imetugusa sana pole sana kaka yupo mungu hakimu wa yote".
Ibrahim Utenga: ''This song reflects the real prevailing situation, it's very sensitive song, congratulations to you brother, God save you "
Ndongo Nyambalya: "Nina wasiwasi wewe Mkatoliki hicho siyo kichwa ni semi-computer, kwenye Mungu wa John na Daud hapo nimefikiria hadi najikuta nurudiarudia kusikiza, U deserve bro! Gat u! 100".
Kwa upande mwingine, Roma Mkatoliki amemwagiwa sifa kedekede na mashabiki zake ambao walikuwa wamemisi kusikia na kuona kazi zake na kuweza kurudi katika uhalisia wake bila ya kuhofia jambo lolote litakaloweza mtokea tena mbele yake kwa ukali wa tungo zilizojaa za kufikirika.