Desprospero
JF-Expert Member
- Feb 1, 2023
- 887
- 2,201
Uhuru wa kujieleza haumaanishi kuvuka mipaka. Uhuru wako usivuke mipaka na kumkwaza mtu mwingine.
Nimesikia wimbo Mpya aliyouachia Msanii Roma Mkatoliki anayeishi ughaibuni akisema, "Roma tunakumisi rudi nyumbani". Sina hakika kama wapo wanaomkosa Roma.
Yote ni tisa. Kumi katika mistari ya Roma ambapo amevuka mstari mwekundu ni pale anaposema, "Mama (Samia) anaongoza yuko Ikulu lakini rimoti iko Msoga (Jakaya Kikwete).
Huku si tu Roma ametweza taasisi ya Rais lakini pia amemdharau na kumdhihaki Rais Samia Suluhu Hassan kwamba hawezi kuongoza hadi ashikiwe akili na Rais mstaafu Jakaya Kikwete jambo ambalo ni uzushi, uongo na upuuzi wa kisanii.
Roma haamini katika uwezo wa kiuongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan jambo ambalo limethibitishwa na jumuiya zote za Kimataifa kuwa anaweza na ameuthibiyishia Ulimwengu kuwa anaweza tena hata kuwapiku watangulizi wake.
Wimbo unatakiwa kupigwa ban kokote na popote, kuanzia mikusanyiko ya watu: baa, maafali, harusi, misinani, vyombo vya usafiri na hata watu binafsi nadhani TCRA wanaweza. Basata isilale huku Rais Samia Suluhu Hassan anadhalilishwa hadharani na msanii Roma.
Nani yuko nyuma ya Roma? Kiburi cha kumdhihaki Rais anapata wapi? Kwanini anachekewa? Kwani hafikiki? This is too much. Roma akamatwe na kuletwa hapa nchini tukutane Kisutu kwa Pilato. Ova.
Zaidi, soma: Nipeni maua yangu - Roma Mkatoliki
Nimesikia wimbo Mpya aliyouachia Msanii Roma Mkatoliki anayeishi ughaibuni akisema, "Roma tunakumisi rudi nyumbani". Sina hakika kama wapo wanaomkosa Roma.
Yote ni tisa. Kumi katika mistari ya Roma ambapo amevuka mstari mwekundu ni pale anaposema, "Mama (Samia) anaongoza yuko Ikulu lakini rimoti iko Msoga (Jakaya Kikwete).
Huku si tu Roma ametweza taasisi ya Rais lakini pia amemdharau na kumdhihaki Rais Samia Suluhu Hassan kwamba hawezi kuongoza hadi ashikiwe akili na Rais mstaafu Jakaya Kikwete jambo ambalo ni uzushi, uongo na upuuzi wa kisanii.
Roma haamini katika uwezo wa kiuongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan jambo ambalo limethibitishwa na jumuiya zote za Kimataifa kuwa anaweza na ameuthibiyishia Ulimwengu kuwa anaweza tena hata kuwapiku watangulizi wake.
Wimbo unatakiwa kupigwa ban kokote na popote, kuanzia mikusanyiko ya watu: baa, maafali, harusi, misinani, vyombo vya usafiri na hata watu binafsi nadhani TCRA wanaweza. Basata isilale huku Rais Samia Suluhu Hassan anadhalilishwa hadharani na msanii Roma.
Nani yuko nyuma ya Roma? Kiburi cha kumdhihaki Rais anapata wapi? Kwanini anachekewa? Kwani hafikiki? This is too much. Roma akamatwe na kuletwa hapa nchini tukutane Kisutu kwa Pilato. Ova.
Zaidi, soma: Nipeni maua yangu - Roma Mkatoliki