Nimezisoma hizo nyarakafeki, sijaona ukashfa wala chembe ya kuiua chadema!
Mods: kumekuwa na taswira flani ya uachaji wa mijadala ya kizushi inayotupotezea mda na kushusha hadhi ya jukwaa hili!
Uzushi kama huu haina haja ya kuuacha watu waendelee kuangalia!
Bila kamanda godbless lema tusingetwaa jimbo la arusha mjini..!
Saa nyingine chama kinasaidia lakini bila juhudi za mtu binafsi, chama hakiwezi kupata ushindi mnono..!
Mfano mzuri mbozi magharibi na kibaha mjini,chadema kilikuwa na nguvu kubwa ya kushinda lakini
kutokana na viongozi wadhaifu mtela mwampamba na habib mchange chama kikashindwa kunyakua hayo majimbo sasa wanatumikia ccm kuivuruga chadema kwa kumwaga matutsi hapa jamvini na kugombanisha viongozi wa juu wa chama..!
Nikija suala la arusha, niulize mama porojo umelipwa shs.ngapi kumchafua lema, kumbuka godbless lema ana nguvu ya umma na ana nguvu ya mungu ipo nyuma yake, hata ccm walimtaka kumchukua kwaajili ya uchaguzi ubunge 2010,
godbless lema hagombani na wenye uchungu na hii nchi,wapenda haki,wapambanaji wa ufisadi bali anagombana na wala rushwa,mafisadi,wezi,wazinifu,na wasiopenda haki na kudhulumu watu maskini..! Mfano mzuri ni ww mama porojo
godbless nusura afe kwaajili yha kugombania kiti cha umeya, baada ya polisi kutumia nguvu na kumpiga inanikumbusha hayati patric lumumba alivyouwawa na wabelgiji akipambania haki
godbless najua ameahidi mengi,lakini ubunge wake uliingiliwa na ccm, kuhusu ambulance,trekta,pesa za nmc is non of ur business, lema baba tutachangia paka mifuko itoboke, kwani matunda tunayaona.,hatuchangii bure
naona ccm mmekuja na mbinu mpya ya kuidhoofisha cdm, kwa kutumia vibaraka ndani ya chadema
ujumbe kwako kwa mama porojo,
godbless lema ni nguvu ya umma, maneno yako ya nguoni hayawezi kumteteresha ama kumpungizi ari,andika utakavyo barua, lakini lema atakujibu kwa maendeleo 2015,
mlianza na dk.slaa, sasa lema,baadaye mbowe, kisha sugu, n.n.
Usichotwe kirahisi na chuki za mtu mmoja kwa mwingine akitaka nawe umchukie bila hata wewe kujua source ya chuki yake kama ni personal au lah.
Huwezi kuniambia kuwa Lema Arusha ni maarufu kuliko CDM nikakuelewa, ni majuzi tu Lema akiwa amevuliwa ubunge wana Arusha wenyewe walikuwa wakitamka kuwa Hata likiwekwa jiwe Lenye nembo ya CDM na mgombea yeyote wa CCM watalichagua Jiwe....
Je hili halitoshi kutoa uwiano wa umaarufu wa CDM na Lema Arusha??
Mimi kama mkazi wa Arusha na mpenda mabadiliko ya kweli, tuhuma zilizotolewa juu ya Lema ni nzito sana na zimewakilishwa makao makuu ya Chadema. kwanza Lema anatakiwa ajitafakari na kuona kama zinaukweli wowote, na kama zinaukweli basi hana budi kujirekebisha kwa maslahi ya chama, ya wananchi na wapenzi wa Chadema Arusha.
Pili Chadema tusilewe sifa tukajisahau kwamba siku zote tutaendelea kukaa juu, pale mtu anapokosea sisi kama wadau tunatakiwa tumrekebishe (kama Mwenyekiti Taifa- Mhe Mbowe anakubali kurekebishwa kwanini Lema akatae!).
Mtoa mada ameleta barua iliyotumwa makao makuu kama ilivyo ila inashangaza wadau tunaanza kumshambulia kama yeye ndio mwandishi wa hiyo barua. Tulitakiwa tuchambue yaliyoandikwa kama yana ukweli wowote ndio tutoe hoja, kubisha bila misingi inaashiria hatujakomaa kifikra.
kama Great Thinkers lazima tujiulize hicho kiwanja kimeandikishwa kwa jina gani? Je Trekta lipo na nani alishasaidiwa kulima? ambulance ipo wapi na nani ameshawahi kuiona? ArDF imeshapokea kiasi gani cha fedha na watoto wangapi wameshasaidiwa?
Tulianza na Mungu,tutamaliza na Mungu.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Chadema.
Mkuu Munyangaa utashanga hautojiwa sana sana utaambulia matusi na kupachikwa majina ya ajabu ajabu mara msalia mara msaliti hapa bado hawajachukua nchi hawataki kujibu hoja bali viroja ha ha ha ha.
[1] Tunataka kujua kwanini kiwanja cha Hospitali kimeandikwa jina lake na mke wake ?
[2] Tunataka kujua michango ya M4C anayokusanya inafanyiwa audit mara kwa mara ,Tayari kuna fedha zimeshatafunwa ingawa zipo juhudi kubwa za kuficha huu wizi kwania ya kutowakatisha tamaa wachangiaji
[3] Tunakataa uhuni wa Lema kutumia jina la wajane kwaajili ya kujipatia trecta kwa faida zake.
[4] Tunataka wasomi wajitokeze kugombea nafasi katika ngazi mbali mbali badala ya kuwapiga vita kwa hoja hafifu kwamba ni wanausalama wa taifa.
[5] Tunataka michango kwaajili ya waanga wa mauaji ya Arusha ziwafikie walengwa bila kupungua hata ndururu.
Naomba kuwasilisha.
Porojo nyingi za nini? Kama unajua kweli kinachoendela jibu swali rahisi tu. Je, Dr. Slaa amepokea barua hii iliyoandikwa kamati kuu ya Chadema?
Lema ni Mwiba kwa Mamluki na CCM.Mlitegemea wangekaa kimya muda huu?Lengo ni kurusha tuhuma tu katika namna ya kujinusuru.uongo mtupu.Mlikua wapi siku zote?Hamtaweza kututoa kwenye ajenda yenu ya usaliti.hizi zinajibiwa au kupuuzwa na kisha tunaendelea na ajenda yenu ya vibaraka.nothing more,nothing Less....
Mkuu Ritz,nimeamini hiki chama kina wenyewe Lema anapiga watu jukwaani halafu uongozi,wakombozi na wanajiita makamanda ndio kwanza wanapiga makofi na vigelegele mkutanoni.Mods,
Msaada sisi wenye simu za mchina tuweze japo kusoma.
Wala usihangaike nae huyo baada ya kuomba radhi amepewa probation ndio maana anatetea kila upuuzi anatumika kama kingamuzi.Kamanda BEN acha mahaba mkuu, be objective....utachekwa na watu na utapoteza heshima yako...soma kwa makini hoja zilizoainishwa na wana wa arusha dhidi ya lema kabla hujarukia keybord na kupost.