Godbless Lema: Arusha inaharibiwa na uselamavi

Godbless Lema: Arusha inaharibiwa na uselamavi

Ukitaka kujua hembu fanya ziara ofisi za laki laki Kisongo kila Jmapili ujionee ushenzi vijana wanavo fanya mapiki piki. Wanafunga bara bara, wanakula mirungi na bangi, viongozi wamekaa kimya wanaona sifa sijui tutafika wapi. Serikali inaona inatengeneza ila italeta kizazi kibayaa sana
Kwa hiyo Mh Lema yupo sahihi ,?Arusha napitapita TU lakini maisha Yao kiundani siyajui
 
Arusha kila mtu ni mbabe ustaarabu upo kwa mbali sana yaani ngumi mkononi dakika yeyote na mtu yeyote awe Mwanamke au Mwanaume wanajiamini hao kama wanaweza vita jana kuna tukio limetokea huko Sanawari ya juu kwa Wameru Mwanamke kamchinja koromeo mume wake usiku hadi kufa..
Moja ya mikoa nayo iyonaga jau ni huu Arusha, Zaidi ya mara NNE nikienda nakutana na usela mavi
 
Kama tatizo ni mitandao ya kijamii, najiuliza kwanini mitandao ya kijamii ionekane kuharibu vijana wa Arusha zaidi kulinganisha na maeneo mengine?

Je, kweli hili tatizo ni kubwa kama linavyozungumzwa kwenye hizi forum?

Kwamba leo mtu yeyote akienda Arusha, basi lazima atakutana na hali isiyo ya kawaida machoni pake, ambayo hajawahi kuiona maeneo mengine hapa Tanzania?

Siwatetei hao vijana wa Arusha Mjini, lakini nijuavyo kila sehemu ina watu wake waliovurugwa.

Kama tatizo ni kuogopa mavazi, nadhani hao watoto wa kike wanaweza kuolewa na wale wanaopenda mavazi hayo, kwani wapo pia wanaovaa madera siku zote na bado hawajaolewa.

Hii dunia haijawahi kueleweka, ukijisumbua kuielewa utachanganyikiwa, mtengeneze kwa kwako nyumbani.
Umeandika kistaarabu lakini umeandika ujinga.
 
Eneo lolote likiwa hub ya ujambazi hutengeneza jamii ya watu wababe na wakorofi.
Arusha ilikuwa kitovu cha uhalifu wa kutumia silaha itachukua muda mrefu sana kuondoa hiyo culture.

Kama tatizo ni mitandao ya kijamii, najiuliza kwanini mitandao ya kijamii ionekane kuharibu vijana wa Arusha zaidi kulinganisha na maeneo mengine?

Je, kweli hili tatizo ni kubwa kama linavyozungumzwa kwenye hizi forum?

Kwamba leo mtu yeyote akienda Arusha, basi lazima atakutana na hali isiyo ya kawaida machoni pake, ambayo hajawahi kuiona maeneo mengine hapa Tanzania?

Siwatetei hao vijana wa Arusha Mjini, lakini nijuavyo kila sehemu ina watu wake waliovurugwa.

Kama tatizo ni kuogopa mavazi, nadhani hao watoto wa kike wanaweza kuolewa na wale wanaopenda mavazi hayo, kwani wapo pia wanaovaa madera siku zote na bado hawajaolewa.

Hii dunia haijawahi kueleweka, ukijisumbua kuielewa utachanganyikiwa, mtengeneze kwa kwako nyumbani.
 
Huyo ndiye mbunge , hapo ni kwao so anaumia sana , yule mwingine aligombea kigamboni akakosa , mara kageuka kuwa mkazi wa Arusha akagombea huko ...Yuko bussy na matamasha ila wananchi hana muda nao.
 
Watu wa Arusha mumepindukia kwa ujuaji yani hamna msichokijua kumbe ni washamba tu from my own experience
Nilifika huko , nikaona mashati ya draft yale na nguo za mtumba kama uniform zao , kuna yale mashati kama ya CHADEMA , yana kaki fulani hivi ya bahasha 😀 😀 kila kona ni hayo tena mtumba .
 
Nimeishi Arusha, ule usela mavi wao ni ushamba! Vijana wanavuta sana bange na ya kule Olkokola, ngaramtoni ya juu ni balaa mtu wa kawaida ukivuta ile inakutia uchizi. Kingine Arusha inapotezwa na machimbo ya Mererani, vijana hawataki kazi wanawaza kwenda machimboni. Ule mji ni shida, ukichanganya na uzao wa wasomali uliopo pale, ubabe ubabe utasema upo Mogadishu.
 
Sio mabinti tu, hata wanaume asilimia kubwa ni changamoto....uizi wameupa kipaumbele sana si maofisini Wala mitaani, hata madereva wa magari ni hivyo hivyo uizi, uongo uongo, kujifanya wao wanajua matusi na mambo mengine mabaya kuzidi watu wengine, uhuni ni kwa wote wakiume kwa wakike...sijui tamaduni zao ilikuwa ni uhuni na uizi, ukisikia napambana sana ujue ni kuiba sana🙆😎...tusameheane rafiki zangu wa Kanda hiyo
 
Hapana mkuu
Wadudu wa Arusha hawa hapa:-

Screenshot_20260731_144939_Google.jpg


Screenshot_20260731_145054_Google.jpg
 
Back
Top Bottom