Godbless Lema anashikiliwa na jeshi la Polisi Arusha

Godbless Lema anashikiliwa na jeshi la Polisi Arusha

tatizo viongozi wengi wa upinzani tz ni mataburalasa a.k.a vilaza wao ndio kila siku wanapiga kelele kuhusu tume huru ya uchaguzi alafu haohao wanaingilia kazi za tume mara ooh muda hautoshi, mara mashine mbovu sasa hapo tume kazi yake nini au wenyewe upinzani ndio wanajua kila kitu. huyo LEMA anaenda kupiga siasa kwenye kituo cha uchaguzi anatukana watu acha wamu arrest. maeneo mengi mashine za bvr zinafanya kazi vizuri labda zizingue arachuga inamaana ni kuna watu wengi

Kumbe ww makc hauko hata Arusha afu unapiga ramli
 
Elimu siyo issue Ccm mmehaza maprofesa kakini bado nchi imekuwa tambara. Tunahitaji mtu anae jitoa kwa ajili ya watu kwani Mzee Kawawa alikuwa na elimu gani? Mchango wake kwa hili taifa unaweza kuufananisha na hawa maprof, wachumia tumbo ndani ya Ccm?? Mzee Karume alikuwa na ekimu gani! Hebu nenda Zanzibar leo uone kumbukumbu alizo acha Mzee Karume walio mfuata hadi leo hamna aliye weza kuiga uthubutu wa Mzee wetu Karume. Inapofikia swala la Utaifa elimu haina msingi.


Wew nawe unakurupuka,

Nilim-qoute mtu alosema Elimu imeanzia kaskazini, Rudi nyuma kasome convers yote Ndo uje na argument yako
 
hii tume serikali na wadau wasipokuwa makini itatuletea ya kenya. watu wengi sana wameachwa na hawaandikishwi kote tume ilikopita..
 
tunawahitaji watu kama lema wengi katika nchi hii.ccm wana mbinu chafu sana za kuiharibu hii nchi na bila kupambana nao hawa wap.u.u.zi watatuachia mashimo tu.

huo ndo ukweli mkuu kinachofanyika na tume ni uhuni mtupu.
 
nimesoma mengi sana mpaka sasa hakuna sliyeeleza lema kakamatwa kwa kosa gani. zaidi ya uccm na uchadema, hakuna lingine la maana. kwa nini msilete taarifa iliyobalance?
 
Eleza kilichotekea acha kueleza kama mchimvi, kwa hali hii inayoendelea kwenye vituo vya bvr watu kama akina Lema lazima tuwaunge mkono. Kila siku tunaona kwenye Tv jinsi hili ziezi lilivyogeuzwa adhabu kwa wapiga kura. Inakuwaje watu walale vituoni na uhakika wa kuandikishwa kesho yake haupo!!? Hizi mashine zenye matatizo mengi hivyo ni za dunia hii ya technoligia ama. Achia huo uchache wake na siku za kujiandikisha. Mnabaki hapa kutetea ubovu na hila kwa kigezo cha ustaarabu wa kipuuzi. Nyinyi ndio mnaacha mfumo mbovu kubaki madarakani huku ukiwa hauwajibiki ipasavyo kwa umma, halafu serekali ikitenda kinyume na matakwa ya umma mnabaki kuongea mbele ya familia zenu lugha za kikondoo eti huwezi kushindana na serekali.

Acha jazba!
 
Lema ni jembe,tunahitaji akina Lema miamoja tu bungeni,mafisadi mtatia adabu
 
nimesoma mengi sana mpaka sasa hakuna sliyeeleza lema kakamatwa kwa kosa gani. zaidi ya uccm na uchadema, hakuna lingine la maana. kwa nini msilete taarifa iliyobalance?

Siri yetu wana Arusha, hatutaki kumuaibisha mbunge wetu tunayempenda! Tunaamini alitereza!!
 
toa sababu za kumwaga damu. Historia ya nchi yetu inatuffundishaje kuhusu harakati za kisiasa? Wao ccm walimwaga damu? ifanye akili yako ifikiri tofauti but positively. Chama chochote kitakachoshinda kitakabidhiwa nchi kwa amani na si vinginevyo. Ni imani yangu kuwa ccm watakuwa walijifunza kutoka Malawi, Zambia na Kenya ambapo mabadiliko ya vyama vingine kushinda chaguzi vyama vilivyokuwa vinatawala havikusababisha umwagaji damu bali waliwakabidhi nchi walioshinda kwa amani.Na vivyo hivyo hapa kwetu itakuwa the same.


Inawezekana wewe nawe umekaririshwa na ukameza kama kasuku ,hivi viongozi wa nchi hii toka chama tawala huwa wanazifuata hata sheria walizojitungia kweli !!!?

Tizama wizi umebarikiwa Serikalini

1 -Kagoda

2-Richmond

3-Dowans

4-Epa

na sasa ESCROW na wizi huu pesa zake zilichotwa bank kuu na wahusika wake walikuja kusafishwa na Ikulu mchana kweupe bila hata chembe ya uoga.
 
yangu macho,mbona hawataki kujifunza kwa gadafi au mkuruzinza
 
Nec inacho jaribu kufanya ni kuzuia mkondo wa maji wenye nguvu kwa mikono.Mabadoliko hayakwepeki ndugu yangu
 
Mbunge Lema anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kufanya vurugu kwenye vituo vya uandikishaji. Tunawaomba polisi wamshikilie mpaka uandikishaji utakapoisha.
Lema ni mpuuzi na mtumwa vurugu tu, watu kama hawa sio wa kuwapa uongozi hawafai wanaweza kuleta vita nchini kwetu
 
Inawezekana wewe nawe umekaririshwa na ukameza kama kasuku ,hivi viongozi wa nchi hii toka chama tawala huwa wanazifuata hata sheria walizojitungia kweli !!!?

Tizama wizi umebarikiwa Serikalini

1 -Kagoda

2-Richmond

3-Dowans

4-Epa

na sasa ESCROW na wizi huu pesa zake zilichotwa bank kuu na wahusika wake walikuja kusafishwa na Ikulu mchana kweupe bila hata chembe ya uoga.

Huyo jamaa kameza cd ya ccm
 
Lema anawajulia kweli watu wa arusha,
Anaamua kufanya siasa nyepesi ili apate huruma ya wananchi.

anajua kati ya vitu vingi alivyoahidi hajatekeleza hata nusu yake,
Vurugu ndiyo ahueni yake.
Vinginevyo bunge ataliangalia kwenye runinga,
Sipati picha anavyopenda posho.
 
Back
Top Bottom