....Godbles Lema akirudi bungeni nakunywa sumu

....Godbles Lema akirudi bungeni nakunywa sumu

Status
Not open for further replies.

sokoinei

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2012
Posts
1,832
Reaction score
566
Katika kauli ambazo kwa kweli ziliwahi kunichefua ni hii iliyokua ikitolewa na Matthias Manga ambaye ni Diwani wa Kata ya MLANGARINE,(CCM) ktk Jimbo la Arumeru Magaribi.

Kwa wale wanaomjua vema,huyu ni Miongoni mwa Watu wanaotumiwa na Mzee Mamvi Mkoani Arusha kuhujumu Harakati za CHADEMA, na pia alitumika ktk chaguzi za ndani za CCM, Mkoani Arusha mwaka jana 2012 kuhakikisha kua Nafasi zote za juu,kuanzia Mkoani na Wilayani,haswa Wilaya ya Arusha Mjini hachaguliwi mtu asiekua Mzaliwa wa Asili wa Mkoa wa Arusha. Na kauli mbiu yao ilikuwa Nyumbani kwanza.!!

Ikumbukwe kuwa, Magamba yalikua na uhakika 100% kwamba Lemma angeshindwa Rufaa na Kupelekea, Uchaguzi kurudiwa.! Matthias Manga,na Phelemon Mollel Mkurugenzi,BANDIA wa Monaban kwa kutumiwa walianzisha Mikutano iliyojulikana,kama MAA!! yaani Harakati za Wamasai(Waarusha)kushika Nyadhifa zote za Kisiasa na Kiuongozi Mkoani Arusha.! Haswa Ubunge na Udiwani, ndipo Kikao cha Kwanza kilikaa Mwezi wa 8,maeneo ya Nanenane Njiro, kikao cha pili kilifanyika Maeneo ya Kaloleni mwezi wa 10,na cha Tatu kilifanyika mwezi wa 12,maeneo ya Ngaramtoni TPRI ukumbi wa Wakorea! Mikutano yote iliratibiwa na MATHIAS MANGA wakishirikiana,na PHELEMON MOLLEL.

Mwenyekiti wa Mikutano alilikuwa ni Phelemon Mollel (Ushahidi upo)..pale ndipo maneno ya Kusema Lemma akirudi Bungeni nakunywa sumu! yalikuwa yakitamkwa..Lakini baada ya Mahakama Kuu ya Rufani chini ya Majaji watatu,Kufutilia mbali Hukumu ile,na Kumrudishia Mrufani(Lemma) Ubunge, Vile Vikao vya MAA (Vya Ubaguzi wa Kikabila) vilikufa,! Na bwana Matthias Manga Diwani wa Mlangarin,kwa Aibu ya Ahadi aloyoitoa ya Kunywa Sumu japo hakufanya hivyo baada ya Lemma kurudishiwa Ubunge! Aliwanunua Vijana Usiku wa tar 31-12 2012,na kwenda kuzivunja na kuziharibu baadhi ya Ofisi na Matawi ya CHADEMA! ktk Kata anayoiongoza.

Huyu Ndie Matthias Manga, Diwani wa Mlangarine aliyeapa kwamba Jembe Lema akirudi Bungeni Anakunywa Sumu.
 
Yangu macho. Mathias na Lema wote mabest wangu..!!
Hii vita mie simo
 
....mwambie 2015 ni tarakimu nne....magharibi... inatamkwa ....fooo namaanisha four kiswahili ni ....nne
 
Kwa kawaida Watanzania hasa viongozi wetu hawana tabia ya kufakari maneno yanayowatoka midomono mwao na hii ni kwa sababu hawamaanishi wanachokisema bali wanataka kuwafurahisha waliowatuma. Kwa vile na wao wana njaa basi hujisemea tu neno lolote linaloweza kutoka kwenye kinywa. Leo hii akihijiwa juu ya kauli yake hiyo ataruka vibaya sana kuwa hakusema, na inawezekana kweli hakumbuki kwa kuwa hakumaanisha na haikuota kwenye dhamira yake. Haya ndiyo matokeo ya siasa za njaa.
 
hana haja ya kunywa sumu aendelee kuishi kwa matumaini hadi 2015 aone ukombozi wa pili ila anayo nafasi ya kutubu na kujiunga na ukombozi sasa!!
 
Do ni jamaa yangu ye ndo mwenye mahakama nashangaa kweli kutoa kauli za ajabu namna hio mwenyewe siamini "Anakunywa sumu" kweli ni ntafanya juu chini nitamuuliza tu kajidhalilisha hata kwa familia FIKIRIA KWA NDUGU KABLA HUJANENA
 
Kwa wasio mfahamu matias manga,huyu ni mmoja ya watanzania wanaomiliki mgodi pale mererani,hela ni kweli anayo ya kutosha.
Ila hizi tuhuma zinamchafua mazima.
 
Asubiri Aanze kuwashiwa moto kuhusu lile ghorofa lake alilolijenga mtoni kinyume cha sheria za nchi!
 
Afanye haraka kunywa hiyo sumu maana hata hicho kiti alichokalia yeye sio chake. Mbona hakuwasaidia wakina Hapiness kulipa gharama za Kesi ya Lema kama ana hela huyo.

Huo utajiri mnaomsifia nao mbona ndo kwanza nasikia jina lake?au ni tajiri kwenye Kata yake (shame), what is the definition of utajiri? Mwambie ukituuliza tajiri wa mawe sisi tunamjua Askofu hata kama kafilisika lakini angalau aliuza sura kwenye media za kibongo atuondokee na fedha zake za mawazo hapa
 
Hayo ndio madhara ya kupenda sifa za kijinga unajikuta umeropoka neno lolote ili kumfurahisha anayekusifia bila kujua madhara gani utayapata.Huo mkakati wa waarusha kushika nyazifa zote hautafanikiwa wao wenyewe wanadhauliana kati ya boma au koo na koo nyingine.
 
Manga Digital.. Asee Tanzanite ina kiburi duh.
 
I talk what i mean and i mean what i talk lakini kwa viongozi wetu hii ni tofauti kidogo kwani wao wanakiongea wasichokimaanisha na wanakimaanisha wasichokiongea
 
wajinga kama huyo ni wengi, kumbuka Tambwe hiza
 
We mwenyewe nahisi una element ya ugamba,kichwa cha habari chenyewe kimekaa kimshituo we unajua umewashitua wangapi leo?halafu haitwi lemma.ni jembe lema.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom