Mara nyingi ukiona mtu anatoa story kama hizi ujue na yeye kuna dili alikuwa amelilenga la kumpa ulaji kwenye hiyo ziara likampita pembeni, kama siyo yeye basi anatumiwa na mtu aliyelenga kunufaika na yeye kapigwa chini. Na inaonekana kuna watu walikuwa wanagombania ulaji kwenye hiyo ziara wakazidiana kete sasa waliokosa wanaamua kuharibu.
Hebu, tusaidie pia ndugu yangu Yericko, lengo la hiyo ziara ilikuwa ni nini? Alilenga kwenda/ alienda wapi na wapi? ni yapi matokeo ya hiyo ziara (matokeo yaliyopatikana au yanayotarajiwa) kwa maendeleo ya taifa letu?
Sheikh Yahya upo kazini unztabiri! Mshukuru mtoa taarifa kwa taarifa aliyokujulisha na siyo kumtaka akafanye kazi ya kufuatilia hayo maswali yako! Kama unataka iamini taarifa yake, kama hutaki baki hivyo hivyo! Na ukitaka taarifa zaidi idai serikali yako sikivu ikupe wakwambie lengo na mrejesho wa hiyo ziara ya propesa muongo dalali