Gharama kubwa ya kuoa

Gharama kubwa ya kuoa

Magnificient

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2013
Posts
1,177
Reaction score
733
Kwanza nawasalimu wadau wote wa jf! Juzi juzi hapa kuna mshkaji wangu wa muda mrefu kaniambia dhamira yake ya kuoa, nikafurahi na kuahidi kumpa sapoti kadiri nitakavyoweza. Jamaa kaenda kuchumbia ukweni ndipo kizaazaa kikaanzia hapo. Barua haikuwa na shida, elfu ishirini tu ilitosha. Kilichoendelea ni kwamba jamaa akaambiwa mpenzi wake kataka mahari ya laki nne tu, ila wanaukoo nao wanataka jasho la malezi ya yule binti! Watu na mahitaji yao kwenye mabano ndo kama ifuatavyo:
Baba (boda boda 1 tu) mama (jiko la gesi) mjomba (kiroba cha mbolea) babu (simu yenye redio) bibi (kanga, vitenge na ndoo ya mafuta ya alizeti) na kaka ndo kataka afunguliwe biashara ya tigo pesa! So akaambiwa ajiandae andae tarehe 14.2.2014 aende kupeleka hivyo vitu na wao wamfanyie mipango ili tar 26.2.2014 ndoa ifungwe. Kwa ufupi rafiki yangu hana uwezo kiviile, ila kama laki 3 angemudu na wadau tungeongeza hata 3 nyingine; ila hayo makorokoro ndo pasua kichwa. Sasa hapa rafiki afanyaje? Nakabidhi kwenu wadau.
 
Ukiangalia kwa haraka haraka ni gharama ya kawaida yeye alitaka apewe mke bure? Waulize wenzetu wasukuma na idadi ya ng'ombe. Pia mazungumzo yapo ajaribu kuwaomba.
 
Hahahahaha makubwa haya....mila nyengine bhana mtu unaoa mwanamke tu tena uwape vitu sijui bibi babuu hata kama ungekua unao wote basi...aaaagh

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Kama hawezi kulipa mahari ataweza kutunza mke kweli? Halafu muache uongo, bodaboda inakuwa mahari?! Oa na wewe, uache kushabikia mahari za wenzio
 
Kama hawezi kulipa mahari ataweza kutunza mke kweli? Halafu muache uongo, bodaboda inakuwa mahari?! Oa na wewe, uache kushabikia mahari za wenzio

Mahari sio bodaboda, iko peke yake nayo ni laki 4. Kimsingi iko standard, ila hivyo vitu vingine
 
Ahsanteni kwa hilo wazo jipya la kujaribu kunegotiate nao na kuwaomba. Nadhani sasa tutaanzia hapo, thanks jf!
 
Duh! Hapo bado gharama za Harusi yenyewe! Tutaoa ndoa za mkeka tu aisee duh!
 
Dawa ni kupiga mimba halafu unakua kama staki nataka ,watakupa hata bure.
 
Ahsanteni kwa hilo wazo jipya la kujaribu kunegotiate nao na kuwaomba. Nadhani sasa tutaanzia hapo, thanks jf!

kama ni hivyo basi mwambie alipe mahari pekee. hivyo vingine atoe vilivyo ndani ya uwezo wake...
 
Duuh! Kweli dunia ina mambo. Ina maana ndipo wanataka kumalizia umasikini wao?
 
It aint right kwa kweli. Mi nampenda mtu I wont even let my parents do that to him. Ni kukomoana au?
 
Back
Top Bottom