Ghalama za power tiler toka nje

Ghalama za power tiler toka nje

Mi pia nahitaji hiyo power tiller wadau hats ikiwa na jembe tu
 
Wakuuu,nimejaribu kupitia nyuzi mbalimbali zinazohusu power tiler lakini nyingi ni 2012 kurudi nyuma. Pia watu wengi wameshamaliza mizigo hiyo. Sio kwamba hazipo mtaani,zipo ila bei si rafiki sana,nimejaribu kuangalia mitandaoni nimeona kuna uafadhari iwapo itaagizwa moja kwa moja.

Kupitia alibaba bei zina range US$80-150 kwa used, na 500-1200 kwa mpya kwa seti moja. Kilichofanya nije hapa ni kubadilishana mawazo juu ya njia bora ya kununua hizi mashine.
Mtaani bei ni Tsh 3.5mil-11mil,ukiangalia hizi bei ni km Mara tatu ya zile za mtandaoni.TUSAIDIANE KATIKA

GHALAMA NA TARATIBU ZA USAFIRISHAJI

Watu wanaoagiza magari anaweza kuagiza moja na akaletewa,je kwa upande wangu naweza kuagiza seti moja tu! Na nikaletewa?. Pia nimeangalia mizigo mikubwa huwa kwenye makontena,lakini powertiler set moja ni box moja tu la mbao,je kunauwezekano wa kusafirishwa katika hali hiyo?

Pia ghalama za bandalini zipoje kwa upande wa powertiler au hupigwa hesabu kwa kontena zima?
Tusaidiane maana isije kuwa ghalama ni kubwa kuliko za mitaani au nikalizwa tu mitandaoni

af7a4b04d56768de5cc6e462e563258e.jpg



UPDATES: NIMEPATA POWER TILLER MPYA

Nawashukuru wadau wote kwa michango ya mawazo na wengine mliokuja PM kunipa muongozo n.k. nilipoona mipango imeyumba niliipeleka hela kwenye kilimo. Mwaka huu nimepata 8mil na katika pita pita mtaani nikapata taarifa juu ya power tiller zinazoizwa na mbunge wa mbarali kwa bei ya 2 mil ikiwa full kila kitu eg disc plough, Rotavator, iron/Cage wheels+trailer.

Mwezi may 27 2018 Nimechukua hiyo na mpaka sasa inapiga kazi za kusomba mchanga,tofari na mazao nimerudisha kwa hiyohiyo.

Nimenunua Amec 18 HP

Nawashukuruni sana kwa michango yenu ya mawazo , kama nawe utahitaji nitakusaidia uipate

Picha zinagoma kupanda
Nahitaji power tiller Kubota ya kulimia kwenye mpunga ntajie bei ni shilling ngapi. Tafadhali nusaidieni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kubota full ni 12 - 15 mill, bila tela 9- 12 mill kwasasa, used 8 - 10 mill full. Ila kuna mashine muundo wa kubota kuna Toyo, Swami na Boa ni 7mill full na 5 mill bila tela.
Nahitaji power tiller Kubota ya kulimia kwenye mpunga ntajie bei ni shilling ngapi. Tafadhali nusaidieni

Sent using Jamii Forums mobile app

Barafu la moto
 
Kubota full ni 12 - 15 mill, bila tela 9- 12 mill kwasasa, used 8 - 10 mill full. Ila kuna mashine muundo wa kubota kuna Toyo, Swami na Boa ni 7mill full na 5 mill bila tela.

Barafu la moto
Nahitaji hii power tiller yenye nguvu inayoweza kulima sehemu ngumu ngumu. Nafikiri iyo ya 12 Mpaka 15milliom itanifaa. Iyo ya 12 Mpaka 15 million . Sjajua ni za uwezo wake upoje. Sjajua wanaangalia cc au horse power

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kubota full ni 12 - 15 mill, bila tela 9- 12 mill kwasasa, used 8 - 10 mill full. Ila kuna mashine muundo wa kubota kuna Toyo, Swami na Boa ni 7mill full na 5 mill bila tela.

Barafu la moto
Kwa huzi Kubota za 12 Mpaka 15 million huwa zina HP ngapi. Mi sio mzoefu Sana Ila nmeona zikifanya kazi mashambani.unaweza ukanisaidia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nahitaji hii power tiller yenye nguvu inayoweza kulima sehemu ngumu ngumu. Nafikiri iyo ya 12 Mpaka 15milliom itanifaa. Iyo ya 12 Mpaka 15 million . Sjajua ni za uwezo wake upoje. Sjajua wanaangalia cc au horse power

Sent using Jamii Forums mobile app
Zote zina HP 14 hizo bei ni ikiwa pekee ni 12 pamoja na tela ni 15. Zina lima vizuri sana na zinafaa kwa mazingira ya namna zote.

Barafu la moto
 
Sasa ki power tiller kimoja ukiagize kutoka nje ya nchi wakati hapa vimejaa tena bei poa, kama si upunguani huo ni nini?

Huo niliompa ni muongozo tosha kabisa na msaada mkubwa kwa wenye kufikiri.

Wewe unamuongoza aagize nje, siyo?
Watu wanaagiza hata chupi sembuse powetiller

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wanaagiza hata chupi sembuse powetiller

Sent using Jamii Forums mobile app

Hao siwashangai kwani Wauza nguo wanaokwenda nje kurudi nazo kwenye manegi ni wengi sana.

Lakini power tiller? Ni kitu ambacho hakina ushuru na hapa zipo tena mpya kabisa kwa bei nzuri tu. Sioni sababu ya kuiagiza nje.

Lakini aah, mtumwa hajifichi.
 
Zote zina HP 14 hizo bei ni ikiwa pekee ni 12 pamoja na tela ni 15. Zina lima vizuri sana na zinafaa kwa mazingira ya namna zote.

Barafu la moto
Kubota nzuri zaidi na ambayo inaweza ikadumu kwa muda mrefu ni ya aina gani?.
 
Kubota nzuri zaidi na ambayo inaweza ikadumu kwa muda mrefu ni ya aina gani?.
Zote zinadumu ingawa zile za mikono mifupi sio heavy-duty kwasababu hutumika kuvurugia tu, lakini zile za mikono mirefu ndio nzuri zaidi na zinapiga kazi zote kwa usahihi na uharaka na huchukua mpaka miaka 3 bila kugusa injini wala gia box kama operator ni mzuri.

Barafu la moto
 
Zote zinadumu ingawa zile za mikono mifupi sio heavy-duty kwasababu hutumika kuvurugia tu, lakini zile za mikono mirefu ndio nzuri zaidi na zinapiga kazi zote kwa usahihi na uharaka na huchukua mpaka miaka 3 bila kugusa injini wala gia box kama operator ni mzuri.

Barafu la moto
asante, je baada ya kulima unaweza kuzitumia kupandia na kupalilia?.
 
Back
Top Bottom