Gereza la Hazwa

FEBIANI BABUYA

JF-Expert Member
Mar 5, 2022
1,059
2,018
NOTE
HADITHI ZANGU ZOTE NI ZA KUBUNI TU HAZIHUSIANI NA MTU YEYOTE, TAASISI YOYOTE WALA MAMLAKA YOYOTE ILE WALA HAZILENGI KUMCHAFUA MTU, TAASISI AU MAMLAKA YOYOTE.
HADITHI: GEREZA LA HAZWA

UTANGULIZI....................
Mvua ilikuwa ni Kali sana majira haya ya usiku ikiambatana na upepo mkali ambao uliweza kuilaza chini miti yenye mizizi dhaifu, radi za kutisha ziliupamba masitu huo na kuufanya kuwa na mwanga kwa mbali majira hayo ya usiku wa manane. Ni ndani ya msitu Elnino upatikanao kusini mashariki mwa nchi ya Libya, ni msitu unao tisha sana hata ikiwa ni mchana una historia ya kupotezesha watu waliokuwa wanaingia humo hali iliyo pelekea watu kuanza kuogopa kuingia kwenye huo msitu, miti minene na iliyo shonana ilifanya giza muda wote hata muda wa mchana ndani ya msitu huo na ndiyo sababu ulimiliki viumbe vya kutisha sana kwa usalama wa maisha ya watu.

Majira haya ya usiku wa manane palitulia sana mvua na mjongeo wa maji ndicho kilichokuwa kinasikika sana na upepo mkali pamoja na radi zisizoisha zilizalisha mwanga ndani ya msitu huo, ndani ya tope zito mwanaume mmoja ambaye usoni kwake kulichafuka nywele za kutisha na ndevu zilizofanya hata sura yake isionekane alionekana akiwa anakimbia mno kuweza kuyaokoa maisha yake, hakuwa na namna angeweza kusimama alikuwa anakufa na hakuwa tayari hilo litokee, nyuma yake walikuwa wanakuja kwa kasi sana wanaume sita ambao wanne walivaa nguo za kininja hao walikuwa wanapotea na kurudi huku wawili wakiwa wamevaa magwanda ya jeshi ni wazi walikuwa ni makomando japo kwa lile giza ilikuwa ni ngumu kujua magwanda yao ni ya nchi gani.

Kisu kilikuwa kinakuja huku kikiwa kinajizungusha kilimkosa kichwa kikapita na nywele zake alihema kwa nguvu kisha hakuonekana tena, watu hao walifika hapo mmoja alijaribu kuvuta hisia kujua mtu huyo ameingia wapi lakini upepo ulikuwa unayapotezea utulivu masikio yake. Walipeana ishara ya kutawanyika wote wakionyesha alama ya kuua kwenye shingo kama wakimpata, baada ya kutawanyika hatua kumi na tano mbele yule komando mmoja ambaye alikuwa kwenye gwanda lake alihisi kuna tone limemdondokea lakini lilikuwa na harufu akajua wazi hilo ni jasho mkono wake ulikuwa kiunoni taratibu, ni kweli kuna mtu alitoka juu ya mti akishuka kwa kasi mithili ya paka kwenye kila kiganja kidole cha katikati kilikuwa na kitu kama pete ila haikuwa Pete kwa ajili ya mapenzi na mapambo bali Pete hizo zilikuwa na nyembe Kali sana tatu tatu kila upande na kufanya kuwa sita.

Komando aliikoki bastola yake mwa kisigino cha mguu wake aliirusha juu akiwa ameiachia kwa nguvu sana ikiwa inaelekea juu ya mti mrefu sana ambao ni wazi kwa juu kulikuwa na mtu anashuka kwa nguvu, bastola hiyo ilikuwa inajifyatua risasi yenyewe wakati huo komando alikuwa anapanda kwenye mti huo kama anatumia uchawi lengo alikuwa anamfuata mtu ambaye naye alikuwa anakuja aliko, bastola ilitoka risasi zote sita hakuna iliyo mgusa mtu huyo ikapigwa teke kwa nguvu wanaume walikuwa wamekutana Kati kati ya mti ilipigwa mikono kwa dakika moja kila mtu akiwa ameshikilia mti kwa miguu yake. Nywele za mtu huyo ambaye alionekana kuwa mchafu sana zilicheza upande wa jicho la kulia alijirusha kama anataka kupanda juu mpaka mti ulibonyea kwa nguvu alizotumia komando yule wakati anataka kumfuata alishangaa haoni chochote mbele yake alihisi mtu yupo nyuma yake wakati anageuka alikuwa amechelewa shingo yake ilikuwa inatoka damu nyembe zaidi ya sita ziliiharibu shingo yake, alijaribu kuchomoa bastola nyingine shingo yake ilikuwa tayari imevunjwa.

Baada ya kufanya hayo mauaji aligeuka nyuma mtu huyo mwenye nywele nyingi baada ya kutua chini kisu kilikuwa kimezama kwenye mgongo wake kilimlegeza sana lakini hakutaka kufia kwenye mikono ya hao watu wa kutisha ambao ni wazi aliwaogopa mno huenda alikuwa akiwajua namna walivyo, alianza kukimbia kwa nguvu wote watano waliobaki walikuwa wapo nyuma yake wanakuja kwa kasi ya ajabu, alisimama ghafla mbele yake kulikuwa na maporomoko makubwa na ya kutisha ambayo hayakuonekana hata yameishia wapi, alitoa damu mdomoni zaidi ya visu vidogo vitatu vingine vilikuwa vimezichana mbavu zake, hatua kumi kutoka hapo alipo kwa nyuma yake walisimama maninja wanne na mwanaume mwenye gwanda mmoja baada ya kujua hakuwa na sehemu ya kwenda, hakuhangaika hata kuwaangalia alijirusha huko chini ambako alikuwa anabeti maisha yake.

"He is not a human, he's completely a devil"
"But no survive, he is no more there"
"Let's go and take Donald's body"

Baada ya kumaliza mazungumzo yao kwa lugha ya kiingereza waliondoka hapo wakiwa kwenye tope zito ila kwao halikuwa na uzito wowote ule. Huyu mwanaume aliyekuwa anakimbizwa inasemekana alikuwa na miaka 10 ndani ya GEREZA na hakuwahi kutamka neno lolote lile mpaka siku anatoka ilikuwa ni lazima auawe kwa kufanya kosa la kutoroka kwenye gereza ambalo lilidumu kwa miaka 200 na hakuwahi kutoroka mwanadamu yeyote yule kwa aina ya ulinzi uliokuwepo na hakuna mfungwa hata mmoja ambaye alikuwa anajua wapi gereza hilo lipo, kuna binadamu leo yeye alikuwa nje ya GEREZA hili........what happens???? Nisikumalizie uhondo wako muda utaamua

Ni nini kilimpeleka gerezani? Hilo gereza liko wapi? Ni nani huyu binadamu hasa mpaka watu wamuandame sana kiasi hiki usiku wa manane na aliwezake kutoka huko? Je kwenye hayo maporomoko kuna kutoka kweli????????.......

GEREZA LA HAZWA.....na kalamu ya Bux the story teller
FB_IMG_1660464491079.jpg
 
NOTE
HADITHI ZANGU ZOTE NI ZA KUBUNI TU HAZIHUSIANI NA MTU YEYOTE, TAASISI YOYOTE WALA MAMLAKA YOYOTE ILE WALA HAZILENGI KUMCHAFUA MTU, TAASISI AU MAMLAKA YOYOTE.
HADITHI: GEREZA LA HAZWA

UTANGULIZI....................
Mvua ilikuwa ni Kali sana majira haya ya usiku ikiambatana na upepo mkali ambao uliweza kuilaza chini miti yenye mizizi dhaifu, radi za kutisha ziliupamba masitu huo na kuufanya kuwa na mwanga kwa mbali majira hayo ya usiku wa manane. Ni ndani ya msitu Elnino upatikanao kusini mashariki mwa nchi ya Libya, ni msitu unao tisha sana hata ikiwa ni mchana una historia ya kupotezesha watu waliokuwa wanaingia humo hali iliyo pelekea watu kuanza kuogopa kuingia kwenye huo msitu, miti minene na iliyo shonana ilifanya giza muda wote hata muda wa mchana ndani ya msitu huo na ndiyo sababu ulimiliki viumbe vya kutisha sana kwa usalama wa maisha ya watu.

Majira haya ya usiku wa manane palitulia sana mvua na mjongeo wa maji ndicho kilichokuwa kinasikika sana na upepo mkali pamoja na radi zisizoisha zilizalisha mwanga ndani ya msitu huo, ndani ya tope zito mwanaume mmoja ambaye usoni kwake kulichafuka nywele za kutisha na ndevu zilizofanya hata sura yake isionekane alionekana akiwa anakimbia mno kuweza kuyaokoa maisha yake, hakuwa na namna angeweza kusimama alikuwa anakufa na hakuwa tayari hilo litokee, nyuma yake walikuwa wanakuja kwa kasi sana wanaume sita ambao wanne walivaa nguo za kininja hao walikuwa wanapotea na kurudi huku wawili wakiwa wamevaa magwanda ya jeshi ni wazi walikuwa ni makomando japo kwa lile giza ilikuwa ni ngumu kujua magwanda yao ni ya nchi gani.
Kisu kilikuwa kinakuja huku kikiwa kinajizungusha kilimkosa kichwa kikapita na nywele zake alihema kwa nguvu kisha hakuonekana tena, watu hao walifika hapo mmoja alijaribu kuvuta hisia kujua mtu huyo ameingia wapi lakini upepo ulikuwa unayapotezea utulivu masikio yake. Walipeana ishara ya kutawanyika wote wakionyesha alama ya kuua kwenye shingo kama wakimpata, baada ya kutawanyika hatua kumi na tano mbele yule komando mmoja ambaye alikuwa kwenye gwanda lake alihisi kuna tone limemdondokea lakini lilikuwa na harufu akajua wazi hilo ni jasho mkono wake ulikuwa kiunoni taratibu, ni kweli kuna mtu alitoka juu ya mti akishuka kwa kasi mithili ya paka kwenye kila kiganja kidole cha katikati kilikuwa na kitu kama pete ila haikuwa Pete kwa ajili ya mapenzi na mapambo bali Pete hizo zilikuwa na nyembe Kali sana tatu tatu kila upande na kufanya kuwa sita.

Komando aliikoki bastola yake mwa kisigino cha mguu wake aliirusha juu akiwa ameiachia kwa nguvu sana ikiwa inaelekea juu ya mti mrefu sana ambao ni wazi kwa juu kulikuwa na mtu anashuka kwa nguvu, bastola hiyo ilikuwa inajifyatua risasi yenyewe wakati huo komando alikuwa anapanda kwenye mti huo kama anatumia uchawi lengo alikuwa anamfuata mtu ambaye naye alikuwa anakuja aliko, bastola ilitoka risasi zote sita hakuna iliyo mgusa mtu huyo ikapigwa teke kwa nguvu wanaume walikuwa wamekutana Kati kati ya mti ilipigwa mikono kwa dakika moja kila mtu akiwa ameshikilia mti kwa miguu yake. Nywele za mtu huyo ambaye alionekana kuwa mchafu sana zilicheza upande wa jicho la kulia alijirusha kama anataka kupanda juu mpaka mti ulibonyea kwa nguvu alizotumia komando yule wakati anataka kumfuata alishangaa haoni chochote mbele yake alihisi mtu yupo nyuma yake wakati anageuka alikuwa amechelewa shingo yake ilikuwa inatoka damu nyembe zaidi ya sita ziliiharibu shingo yake, alijaribu kuchomoa bastola nyingine shingo yake ilikuwa tayari imevunjwa.

Baada ya kufanya hayo mauaji aligeuka nyuma mtu huyo mwenye nywele nyingi baada ya kutua chini kisu kilikuwa kimezama kwenye mgongo wake kilimlegeza sana lakini hakutaka kufia kwenye mikono ya hao watu wa kutisha ambao ni wazi aliwaogopa mno huenda alikuwa akiwajua namna walivyo, alianza kukimbia kwa nguvu wote watano waliobaki walikuwa wapo nyuma yake wanakuja kwa kasi ya ajabu, alisimama ghafla mbele yake kulikuwa na maporomoko makubwa na ya kutisha ambayo hayakuonekana hata yameishia wapi, alitoa damu mdomoni zaidi ya visu vidogo vitatu vingine vilikuwa vimezichana mbavu zake, hatua kumi kutoka hapo alipo kwa nyuma yake walisimama maninja wanne na mwanaume mwenye gwanda mmoja baada ya kujua hakuwa na sehemu ya kwenda, hakuhangaika hata kuwaangalia alijirusha huko chini ambako alikuwa anabeti maisha yake.
"He is not a human, he's completely a devil"
"But no survive, he is no more there"
"Let's go and take Donald's body"

Baada ya kumaliza mazungumzo yao kwa lugha ya kiingereza waliondoka hapo wakiwa kwenye tope zito ila kwao halikuwa na uzito wowote ule. Huyu mwanaume aliyekuwa anakimbizwa inasemekana alikuwa na miaka 10 ndani ya GEREZA na hakuwahi kutamka neno lolote lile mpaka siku anatoka ilikuwa ni lazima auawe kwa kufanya kosa la kutoroka kwenye gereza ambalo lilidumu kwa miaka 200 na hakuwahi kutoroka mwanadamu yeyote yule kwa aina ya ulinzi uliokuwepo na hakuna mfungwa hata mmoja ambaye alikuwa anajua wapi gereza hilo lipo, kuna binadamu leo yeye alikuwa nje ya GEREZA hili........what happens???? Nisikumalizie uhondo wako muda utaamua

Ni nini kilimpeleka gerezani? Hilo gereza liko wapi? Ni nani huyu binadamu hasa mpaka watu wamuandame sana kiasi hiki usiku wa manane na aliwezake kutoka huko? Je kwenye hayo maporomoko kuna kutoka kweli????????.......

GEREZA LA HAZWA.....na kalamu ya Bux the story tellerView attachment 2323516
Tupo pamoja shusha mambo
 
NOTE: Hadithi zangu zote ni za kubuni tu hazihusiani na mtu yeyote, taasisi yoyote wala mamlaka yoyote ile wala hazilengi kumchafua mtu, taasisi au mamlaka yoyote.

HADITHI: GEREZA LA HAZWA

UTANGULIZI....................
Mvua ilikuwa ni Kali sana majira haya ya usiku ikiambatana na upepo mkali ambao uliweza kuilaza chini miti yenye mizizi dhaifu, radi za kutisha ziliupamba masitu huo na kuufanya kuwa na mwanga kwa mbali majira hayo ya usiku wa manane. Ni ndani ya msitu Elnino upatikanao kusini mashariki mwa nchi ya Libya, ni msitu unao tisha sana hata ikiwa ni mchana una historia ya kupotezesha watu waliokuwa wanaingia humo hali iliyo pelekea watu kuanza kuogopa kuingia kwenye huo msitu, miti minene na iliyo shonana ilifanya giza muda wote hata muda wa mchana ndani ya msitu huo na ndiyo sababu ulimiliki viumbe vya kutisha sana kwa usalama wa maisha ya watu.

Majira haya ya usiku wa manane palitulia sana mvua na mjongeo wa maji ndicho kilichokuwa kinasikika sana na upepo mkali pamoja na radi zisizoisha zilizalisha mwanga ndani ya msitu huo, ndani ya tope zito mwanaume mmoja ambaye usoni kwake kulichafuka nywele za kutisha na ndevu zilizofanya hata sura yake isionekane alionekana akiwa anakimbia mno kuweza kuyaokoa maisha yake, hakuwa na namna angeweza kusimama alikuwa anakufa na hakuwa tayari hilo litokee, nyuma yake walikuwa wanakuja kwa kasi sana wanaume sita ambao wanne walivaa nguo za kininja hao walikuwa wanapotea na kurudi huku wawili wakiwa wamevaa magwanda ya jeshi ni wazi walikuwa ni makomando japo kwa lile giza ilikuwa ni ngumu kujua magwanda yao ni ya nchi gani.
Kisu kilikuwa kinakuja huku kikiwa kinajizungusha kilimkosa kichwa kikapita na nywele zake alihema kwa nguvu kisha hakuonekana tena, watu hao walifika hapo mmoja alijaribu kuvuta hisia kujua mtu huyo ameingia wapi lakini upepo ulikuwa unayapotezea utulivu masikio yake. Walipeana ishara ya kutawanyika wote wakionyesha alama ya kuua kwenye shingo kama wakimpata, baada ya kutawanyika hatua kumi na tano mbele yule komando mmoja ambaye alikuwa kwenye gwanda lake alihisi kuna tone limemdondokea lakini lilikuwa na harufu akajua wazi hilo ni jasho mkono wake ulikuwa kiunoni taratibu, ni kweli kuna mtu alitoka juu ya mti akishuka kwa kasi mithili ya paka kwenye kila kiganja kidole cha katikati kilikuwa na kitu kama pete ila haikuwa Pete kwa ajili ya mapenzi na mapambo bali Pete hizo zilikuwa na nyembe Kali sana tatu tatu kila upande na kufanya kuwa sita.

Komando aliikoki bastola yake mwa kisigino cha mguu wake aliirusha juu akiwa ameiachia kwa nguvu sana ikiwa inaelekea juu ya mti mrefu sana ambao ni wazi kwa juu kulikuwa na mtu anashuka kwa nguvu, bastola hiyo ilikuwa inajifyatua risasi yenyewe wakati huo komando alikuwa anapanda kwenye mti huo kama anatumia uchawi lengo alikuwa anamfuata mtu ambaye naye alikuwa anakuja aliko, bastola ilitoka risasi zote sita hakuna iliyo mgusa mtu huyo ikapigwa teke kwa nguvu wanaume walikuwa wamekutana Kati kati ya mti ilipigwa mikono kwa dakika moja kila mtu akiwa ameshikilia mti kwa miguu yake. Nywele za mtu huyo ambaye alionekana kuwa mchafu sana zilicheza upande wa jicho la kulia alijirusha kama anataka kupanda juu mpaka mti ulibonyea kwa nguvu alizotumia komando yule wakati anataka kumfuata alishangaa haoni chochote mbele yake alihisi mtu yupo nyuma yake wakati anageuka alikuwa amechelewa shingo yake ilikuwa inatoka damu nyembe zaidi ya sita ziliiharibu shingo yake, alijaribu kuchomoa bastola nyingine shingo yake ilikuwa tayari imevunjwa.

Baada ya kufanya hayo mauaji aligeuka nyuma mtu huyo mwenye nywele nyingi baada ya kutua chini kisu kilikuwa kimezama kwenye mgongo wake kilimlegeza sana lakini hakutaka kufia kwenye mikono ya hao watu wa kutisha ambao ni wazi aliwaogopa mno huenda alikuwa akiwajua namna walivyo, alianza kukimbia kwa nguvu wote watano waliobaki walikuwa wapo nyuma yake wanakuja kwa kasi ya ajabu, alisimama ghafla mbele yake kulikuwa na maporomoko makubwa na ya kutisha ambayo hayakuonekana hata yameishia wapi, alitoa damu mdomoni zaidi ya visu vidogo vitatu vingine vilikuwa vimezichana mbavu zake, hatua kumi kutoka hapo alipo kwa nyuma yake walisimama maninja wanne na mwanaume mwenye gwanda mmoja baada ya kujua hakuwa na sehemu ya kwenda, hakuhangaika hata kuwaangalia alijirusha huko chini ambako alikuwa anabeti maisha yake.
"He is not a human, he's completely a devil"
"But no survive, he is no more there"
"Let's go and take Donald's body"

Baada ya kumaliza mazungumzo yao kwa lugha ya kiingereza waliondoka hapo wakiwa kwenye tope zito ila kwao halikuwa na uzito wowote ule. Huyu mwanaume aliyekuwa anakimbizwa inasemekana alikuwa na miaka 10 ndani ya GEREZA na hakuwahi kutamka neno lolote lile mpaka siku anatoka ilikuwa ni lazima auawe kwa kufanya kosa la kutoroka kwenye gereza ambalo lilidumu kwa miaka 200 na hakuwahi kutoroka mwanadamu yeyote yule kwa aina ya ulinzi uliokuwepo na hakuna mfungwa hata mmoja ambaye alikuwa anajua wapi gereza hilo lipo, kuna binadamu leo yeye alikuwa nje ya GEREZA hili........what happens???? Nisikumalizie uhondo wako muda utaamua

Ni nini kilimpeleka gerezani? Hilo gereza liko wapi? Ni nani huyu binadamu hasa mpaka watu wamuandame sana kiasi hiki usiku wa manane na aliwezake kutoka huko? Je kwenye hayo maporomoko kuna kutoka kweli????????.......

GEREZA LA HAZWA.....na kalamu ya Bux the story teller
FB_IMG_1660464491079.jpg


Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
Lete maneno....bila shaka hii ya Leo itaisha maana ya kwanza uliitelekeza hivi hivi
Ipi niliyo itelekeza? Au ww ndo haunifuatilii?? Hakuna hadithi hata Moja ambayo nimeitelekeza napost hadithi 3 Kila siku brother hiyo ni ya 4 ambayo inaenda kuanza hivi karibuni

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
Lete maneno....bila shaka hii ya Leo itaisha maana ya kwanza uliitelekeza hivi hivi
And ngoja nikupe sababu kwanini hadithi nyingi huwa zinapelea njiani...iko hivi uandishi ni Kama kazi ambayo inawaweka watu mjini na mtu anategemea imsaidie kwa namna Moja ama nyingine ila bahati mbaya wasomaji huwa hawalioni kabisa hili na huangalia upande wao tu pekee.....

Hizi hadithi za kijasusi zinahitaji akili na muda sana kuziandaa mpaka inaisha, Sasa imagine msomaji hata kukuchangia shilingi 3000 tu kwa kununua hadithi zako hawezi na unatakiwa ushinde ndani kuandika, je unakula Nini? Pesa ya matumizi unatoa wapi? Kwahiyo mtu anaamua tu kutafuta kazi ya kufanya ili apate chochote......ila Kama wasomaji wanakusupport kwa mchango trust me hadithi zingekuwa zinaletwa Kila siku kutoka kwa waandishi wengi...ila changamoto unashinda ndani hauingizi hata mia utaandika na kuacha kutafuta kazi ambayo itakuinguzia chochote????

Bahati mbaya sana wasomaji huwa wanalaumu Sana ila ukiomba support ya kununua hadithi zako ili upate angalau pesa kidogo ya kukufanya huwa wanapotea.....hilo ndilo tatizo kubwa ndugu yangu kipato hamna so unajikita kwenye majukumu mengine mwisho wa siku unakosa muda wa kuandika.

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
Ipi niliyo itelekeza? Au ww ndo haunifuatilii?? Hakuna hadithi hata Moja ambayo nimeitelekeza napost hadithi 3 Kila siku brother hiyo ni ya 4 ambayo inaenda kuanza hivi karibuni

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
Hii hii ya Gereza la Hazwa, uliwahi kuianzisha ukaishia episode moja hadi Leo yani😔

 
Hii hii ya Gereza la Hazwa, uliwahi kuianzisha ukaishia episode moja hadi Leo yani

Hadithi hii nilitoaga ukurasa mmoja kwa kutoa intro kwamba inaenda kuanza Sio muda wakati huo nilikuwa namalizia I WANT TO DIE JUDGE episode ya 100......so kivipi unasema nimeitelekeza?.....4 days ago nimeandaa ukurasa wa pili ndo ilitaka iweze kuanza kuruka rasmi nikafiwa na mdogo wangu....so how nimeitelekeza? Daah anyway sawa

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
Nadhani mimi ni mgeni huko Kama utakuwa una uelewa juu ya hilo utanisaidia ndugu yangu

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
Mimi huwa mfuatiliaji mzuri huko ingawa sijui wanafanyaje ila Kama unaweza pata Hawa watu Yeriko Nyerere na Kuna mtu anaitwa Emanuel S.S.Livanga Hawa naona kazi zao Amazon.Tena huyo Emanuel na kazi za juzi tu Mwezi Julai na Agosti Tena Vitabu viwili vya Kiswahili kabisa.Unaweza wapata humu au akawatafuta kwa namna nyingine kwenye mitandao ya kijamii.Wanaweza kukusaidia namna ya kuuza hata kitabu huko na namna wanavyopokea malipo.Nimekupa mwanga kidogo.Na Mimi nafuatilia nikifahamu nitakuja humu kutiririka.Hiyo ya short story inaitwa Kindle vela.
 
Mimi huwa mfuatiliaji mzuri huko ingawa sijui wanafanyaje ila Kama unaweza pata Hawa watu Yeriko Nyerere na Kuna mtu anaitwa Emanuel S.S.Livanga Hawa naona kazi zao Amazon.Tena huyo Emanuel na kazi za juzi tu Mwezi Julai na Agosti Tena Vitabu viwili vya Kiswahili kabisa.Unaweza wapata humu au akawatafuta kwa namna nyingine kwenye mitandao ya kijamii.Wanaweza kukusaidia namna ya kuuza hata kitabu huko na namna wanavyopokea malipo.Nimekupa mwanga kidogo.Na Mimi nafuatilia nikifahamu nitakuja humu kutiririka.Hiyo ya short story inaitwa Kindle vela.
Shukrani sana ndugu yangu

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
Hadithi hii nilitoaga ukurasa mmoja kwa kutoa intro kwamba inaenda kuanza Sio muda wakati huo nilikuwa namalizia I WANT TO DIE JUDGE episode ya 100......so kivipi unasema nimeitelekeza?.....4 days ago nimeandaa ukurasa wa pili ndo ilitaka iweze kuanza kuruka rasmi nikafiwa na mdogo wangu....so how nimeitelekeza? Daah anyway sawa

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
Pole Febiani ila sio lazima kila comment ujibu,vingine unajiumiza tu na wakati hata hatukulipi chochote
 
NOTE
HADITHI ZANGU ZOTE NI ZA KUBUNI TU HAZIHUSIANI NA MTU YEYOTE, TAASISI YOYOTE WALA MAMLAKA YOYOTE ILE WALA HAZILENGI KUMCHAFUA MTU, TAASISI AU MAMLAKA YOYOTE.
HADITHI: GEREZA LA HAZWA

UTANGULIZI....................
Mvua ilikuwa ni Kali sana majira haya ya usiku ikiambatana na upepo mkali ambao uliweza kuilaza chini miti yenye mizizi dhaifu, radi za kutisha ziliupamba masitu huo na kuufanya kuwa na mwanga kwa mbali majira hayo ya usiku wa manane. Ni ndani ya msitu Elnino upatikanao kusini mashariki mwa nchi ya Libya, ni msitu unao tisha sana hata ikiwa ni mchana una historia ya kupotezesha watu waliokuwa wanaingia humo hali iliyo pelekea watu kuanza kuogopa kuingia kwenye huo msitu, miti minene na iliyo shonana ilifanya giza muda wote hata muda wa mchana ndani ya msitu huo na ndiyo sababu ulimiliki viumbe vya kutisha sana kwa usalama wa maisha ya watu.

Majira haya ya usiku wa manane palitulia sana mvua na mjongeo wa maji ndicho kilichokuwa kinasikika sana na upepo mkali pamoja na radi zisizoisha zilizalisha mwanga ndani ya msitu huo, ndani ya tope zito mwanaume mmoja ambaye usoni kwake kulichafuka nywele za kutisha na ndevu zilizofanya hata sura yake isionekane alionekana akiwa anakimbia mno kuweza kuyaokoa maisha yake, hakuwa na namna angeweza kusimama alikuwa anakufa na hakuwa tayari hilo litokee, nyuma yake walikuwa wanakuja kwa kasi sana wanaume sita ambao wanne walivaa nguo za kininja hao walikuwa wanapotea na kurudi huku wawili wakiwa wamevaa magwanda ya jeshi ni wazi walikuwa ni makomando japo kwa lile giza ilikuwa ni ngumu kujua magwanda yao ni ya nchi gani.
Kisu kilikuwa kinakuja huku kikiwa kinajizungusha kilimkosa kichwa kikapita na nywele zake alihema kwa nguvu kisha hakuonekana tena, watu hao walifika hapo mmoja alijaribu kuvuta hisia kujua mtu huyo ameingia wapi lakini upepo ulikuwa unayapotezea utulivu masikio yake. Walipeana ishara ya kutawanyika wote wakionyesha alama ya kuua kwenye shingo kama wakimpata, baada ya kutawanyika hatua kumi na tano mbele yule komando mmoja ambaye alikuwa kwenye gwanda lake alihisi kuna tone limemdondokea lakini lilikuwa na harufu akajua wazi hilo ni jasho mkono wake ulikuwa kiunoni taratibu, ni kweli kuna mtu alitoka juu ya mti akishuka kwa kasi mithili ya paka kwenye kila kiganja kidole cha katikati kilikuwa na kitu kama pete ila haikuwa Pete kwa ajili ya mapenzi na mapambo bali Pete hizo zilikuwa na nyembe Kali sana tatu tatu kila upande na kufanya kuwa sita.

Komando aliikoki bastola yake mwa kisigino cha mguu wake aliirusha juu akiwa ameiachia kwa nguvu sana ikiwa inaelekea juu ya mti mrefu sana ambao ni wazi kwa juu kulikuwa na mtu anashuka kwa nguvu, bastola hiyo ilikuwa inajifyatua risasi yenyewe wakati huo komando alikuwa anapanda kwenye mti huo kama anatumia uchawi lengo alikuwa anamfuata mtu ambaye naye alikuwa anakuja aliko, bastola ilitoka risasi zote sita hakuna iliyo mgusa mtu huyo ikapigwa teke kwa nguvu wanaume walikuwa wamekutana Kati kati ya mti ilipigwa mikono kwa dakika moja kila mtu akiwa ameshikilia mti kwa miguu yake. Nywele za mtu huyo ambaye alionekana kuwa mchafu sana zilicheza upande wa jicho la kulia alijirusha kama anataka kupanda juu mpaka mti ulibonyea kwa nguvu alizotumia komando yule wakati anataka kumfuata alishangaa haoni chochote mbele yake alihisi mtu yupo nyuma yake wakati anageuka alikuwa amechelewa shingo yake ilikuwa inatoka damu nyembe zaidi ya sita ziliiharibu shingo yake, alijaribu kuchomoa bastola nyingine shingo yake ilikuwa tayari imevunjwa.

Baada ya kufanya hayo mauaji aligeuka nyuma mtu huyo mwenye nywele nyingi baada ya kutua chini kisu kilikuwa kimezama kwenye mgongo wake kilimlegeza sana lakini hakutaka kufia kwenye mikono ya hao watu wa kutisha ambao ni wazi aliwaogopa mno huenda alikuwa akiwajua namna walivyo, alianza kukimbia kwa nguvu wote watano waliobaki walikuwa wapo nyuma yake wanakuja kwa kasi ya ajabu, alisimama ghafla mbele yake kulikuwa na maporomoko makubwa na ya kutisha ambayo hayakuonekana hata yameishia wapi, alitoa damu mdomoni zaidi ya visu vidogo vitatu vingine vilikuwa vimezichana mbavu zake, hatua kumi kutoka hapo alipo kwa nyuma yake walisimama maninja wanne na mwanaume mwenye gwanda mmoja baada ya kujua hakuwa na sehemu ya kwenda, hakuhangaika hata kuwaangalia alijirusha huko chini ambako alikuwa anabeti maisha yake.
"He is not a human, he's completely a devil"
"But no survive, he is no more there"
"Let's go and take Donald's body"

Baada ya kumaliza mazungumzo yao kwa lugha ya kiingereza waliondoka hapo wakiwa kwenye tope zito ila kwao halikuwa na uzito wowote ule. Huyu mwanaume aliyekuwa anakimbizwa inasemekana alikuwa na miaka 10 ndani ya GEREZA na hakuwahi kutamka neno lolote lile mpaka siku anatoka ilikuwa ni lazima auawe kwa kufanya kosa la kutoroka kwenye gereza ambalo lilidumu kwa miaka 200 na hakuwahi kutoroka mwanadamu yeyote yule kwa aina ya ulinzi uliokuwepo na hakuna mfungwa hata mmoja ambaye alikuwa anajua wapi gereza hilo lipo, kuna binadamu leo yeye alikuwa nje ya GEREZA hili........what happens???? Nisikumalizie uhondo wako muda utaamua

Ni nini kilimpeleka gerezani? Hilo gereza liko wapi? Ni nani huyu binadamu hasa mpaka watu wamuandame sana kiasi hiki usiku wa manane na aliwezake kutoka huko? Je kwenye hayo maporomoko kuna kutoka kweli????????.......

GEREZA LA HAZWA.....na kalamu ya Bux the story tellerView attachment 2344274

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
Nitatoa ratiba yake ya kuanza kuisoma hapa
IMG-20220904-WA0014.jpg


Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
Nitatoa ratiba yake ya kuanza kuisoma hapaView attachment 2345422

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
NOTE:
HADITHI HII NI YA KUTUNGA TU HAIHUSIANI NA MAISHA YA MTU YEYOTE, MAMLAKA WALA SEHEMU YOYOTE ILE NA HAILENGI KABISA KUMCHAFUA MTU YEYOTE YULE, KILA KILICHOPO HUMU NDANI NI CHA KUTUNGA TU NA KUFIKIRIKA.

STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller

UKURASA WA KWANZA

ANZA NAYO..............

Wakati nyie mnalala sana mkiwa mnausaka usingizi wa pono watu wenye ndoto zao ambao wanaiogopa njaa kuliko kitu chochote kile wapo macho kuzitafuta na kuzisaka ndoto zao kuhakikisha mwana haramu ambaye anaitwa tumbo anaridhika kwa namna yoyote ile hata kwa kumlazimisha. Ni wanadamu ambao wanaamini mikono yao ndiyo msaada wao wa pekee wa kuweza kuendelea kuwa hai na kupunguza mateso pamoja na dhihaka za kuchekwa na wanadamu wasiokuwa na uoga wowote mbele ya dunia ya Muumba, hao ndio watu ambao wanaweza kuiishi hii dunia yenye kila aina ya vioja vya ajabu na vya kutisha pia, kwao hawaamini katika bahati juhudi kwanza ndizo zinazo wapa imani ya kujikwamua kwenye maisha magumu sana ambayo wanayapitia wakiamini hakuna kitu kirahisi kukipata kwenye ulimwengu ni lazima ulipie ndipo ukipate unacho kitaka.

Wanalipaje na hawana pesa? Basi jasho lao ndilo malipo ambayo wanatakiwa kulilipa ili tu wafanikishe moja ya ndoto zao za kuwa na maisha angalau kupata hata milo miwili mpaka mitatu kwa siku “the bright future is only for the brave people” ni kauli ambayo inawapa muongozo wa nini wanatakiwa kukifanya kwenye maisha yao kama tu watahitaji kuipata ahueni ya maisha wakiamini ujasiri wao na ushujaa wao ndicho kitawapa kesho iliyo njema, hawana mashamba ya kusema wajifariji kwamba kama wakitaka mali basi wataipata shambani, yes, hayo ndiyo maisha halisi kwao.

ARUSHA, TANZANIA

Ndani ya machimbo ya moja ya madini adimu zaidi ulimwenguni na yanapatikana ndani ya nchi moja tu ulimwengu mzima ambayo ni Tanzania pekee kuna wanaume wapo ndani kabisa sehemu ambayo ilikuwa na kiza cha kutosha, tochi zilizofungwa kwenye vichwa vyao zilikuwa ni sehemu ya kuwasaidia kuona vitu ambavyo vipo mbele yao. Sio kwamba walikuwa sehemu ambayo haina umeme kiasi kwamba watashindwa kuona nini kilichopo huko hapana bali ni moja ya njia za kuweza kuzisaka na kuzifikia ndoto zao, wapo mgodini ndani kabisa ambako hata mwanga wa jua huwa ni ndoto kuonekana, mtu anakuwa kama yupo dunia ya peke yake tofauti kabisa na hii dunia ya kawaida ambayo kila mwanadamu anaiishi. Kama mtu angeshtuka kutoka usingizini akajikuta hiyo sehemu basi angehisi moja kwa moja kwamba ulikuwa usiku wa manane sana kulingana na aina ya kiza kizito ambacho kilitanda ila ni muda ambao usingeamini kwamba ilikuwa ni jioni ya kawaida kwenye dunia ya huku nje ambayo watu walikuwa wanaendelea na shughuli zao za kila siku hasa kwa wale wasaka tonge na wengine wale ambao kwao kazi ni mwiba uwachomao sana hawakuacha kuendelea kupiga majungu na jingi kwenye vijiwe mbali mbali na kuendelea kuijutia zamani zao badala ya kuiwaza na kuijenga kesho yao iliyo bora.

Ndani ya mgodi ambao unajulikana kwa kuwa na madini ya Tanzanite ndimo wanamo onekana wanaume wa kazi wakiwa hawaongei sana ila vitendo vyao vinajionyesha majembe mazito, uma, nyundo na machepeo ndivyo vitu vinavyo ongea zaidi huko, wanaume hawalali kuhakikisha maisha bora yanakuja kupitia imani zao za ufanyaji kazi kwa bidi. Vijana zaidi ya watano kila mmoja akiwa upande wake wanapambania kombe chini ya ardhi ambako kama ikitokea namna yoyote kukajifunika basi hadithi zao zinakuwa zimeishia huko huko chini ila hakuna namna wanaweza kuyafanya maisha yakawa malaini kwao kwa mlo wao wa siku moja kwa siku zaidi ya kujitoa mhanga. Ni zaidi ya masaa matano wakiwa wanafanya kazi kwa bidii sana.

“Hey Alen una tatizo gani man” ni sauti ya mmoja wa wale vijana watano ambao walikuwa ndani ya mgodi baada ya kusikia mwenzake yupo kimya sio nyundo wala chepeo ambayo ilikuwa inasikika upande aliokuwa.

“Ni kichwa tu kidogo Kani usijali hakuna tatizo” alimjibu mtu wake huyo ambaye ni wazi walikuwa wanajuana kama sio kuwa marafiki kabisa.

“Oya kama uko vibaya pandisha juu huko chapu gusa kamba pale usije kutupatia kesi mwanangu nadhani unayajua maisha yetu yalivyo hata mia mbovu tu kuipata mpaka tujitoe maisha yetu humu ndani” alionekana kumjali mwenzake kama sio kumtaka atoke asije akaleta ugumu wa kazi kama akizidiwa huko chini yakawa mambo mengine.

“Napumzika dakika moja tu kisha naendelea man usiogope” alimaliza kwa kuongea huku akipigiza nyundo moja kwenye jiwe kama sio chuma maana mlio ulio sikia ni dhahiri lilikuwa ni jiwe limepitiwa na nyundo, baada ya kufanya hivyo aligeuza macho yake huku akiivua tochi kwa kuwaangalia wenzake ambao walitawanyika kidogo ilikuwa inaonekana miale ya mwanga tu kutokana na kiza kizito kilicho kuwepo. Alipoona kila mtu anaendelea na majukumu yake aliinama chini na kuokota vipande vidogo vidogo vya kutosha ambavyo alivitawanyisha kwa nyundo yake, alitoa nailoni ndogo kwenye nguo yake ya ndani akawa anaichana kidogo anakikunja kipande kimoja kimoja kisha anakimeza mpaka alipo kamilisha vinne. Akatulia kidogo kisha akachukua vipande vilivyokuwa vimebakia akavua suruali yake na kuvifunga sehemu zake za siri kwenye hicho kinailoni ambacho aliviweka ndani vipande hivyo kisha akajivalisha kwenye uume wake na kuvifunga kwa kikamba kidogo ambacho alikuwa amekihifadhi kwenye mfuko wake.

Ni wazi alipata maumivu makali alikuwa akiikunja sura yake kila anavyoikaza kamba ili iwe sawa na uume wake ila hakuwa na namna hiyo ndiyo ilikuwa njia ya pekee kwake, mkono wake ulilowa alijua ni damu inatoka baada ya sehemu zake za siri kupata majeraja kutokana na kubanwa sana na vipande hivyo vya mawe na kamba iliyokazwa sana kwenye uume wake hata hivyo hakujali sana alikuwa akiuma meno yake tu huku anaendelea na zoezi lake vizuri mpaka alipohakikisha amekamilisha baada yah apo akajifuta damu mkononi kwenye mchanga uliokuwa chini. Alikuwa na wasiwasi sana kiasi kwamba jasho lilikuwa linamtoka mno kwenye mwili wake wote aliivaa tochi yake tena kwenye kichwa chake akaendelea kupiga kazi machozi yakiwa yanamtoka alikuwa na mawe manne kwenye tumbo lake hiyo haikutosha kweye sehemu yake ya thamani zaidi kwenye mwili alikuwa amejifunga mawe ambayo yalikuwa yakimletea maumivu makali lakini alichagua kuichagua hiyo njia ya kuumia kwani alikuwa anaamini hakuna njia rahisi kabisa kwenye utafutaji.

“Kichwa changu mimi nakufaa nakufaaa jamani msaada” yule mwanaume ambaye jina lake alifahamika kama Alen alisikika akipiga makelele ya kuomba msaada kwa kudai kwamba kichwa chake kinamuuma sana na alikuwa akilia kwa sauti kali, ni hali iliyo washtua wenzake wa mle ndani lakini aliyekuwa na muda naye ni mmoja tu wengine waligeuka tu mara moja kisha wakaendelea na kazi zao za utafutaji walifunzwa kwenye utafutaji kuwa na roho ngumu zaidi ndiyo siri pekee ya mafanikio huruma zingewachelewesha kufika kwenye safari zao ndefu za maisha ndiyo sababu hawakuwa na huruma na mtafutaji mwenzao waliamini huyo kama anakufa atajua yeye na hata akiishi hakuna kitu atawasaidia. Kani kama jina lake lilivyo itwa na Alen alimkimbilia msaka tonge mwenzake akamkuta chini akiwa na joto sana kwenye mwili wake huku akiwa anatoa machozi kuonyesha wazi hali yake ni mbaya hata mwili wake ulikuwa umechemka mno baada ya kumgusa kwenye kichwa chake.

Akamkokota mwenzake kwa mwanga wa tochi anafanikiwa kufika mpaka sehemu ya kuingilia humo ndani ambapo kwa mbali aliuona mwanga wa nje, kuna kamba ya kutolea ishara aliigusa na kuivuta kwa nguvu kisha akakaa pembeni ya mwanaume mwenzake kwa dakika kama mbili mpaka ngazi iliposhuka alijua wakati wa kutoka sasa umefika. Mwanaume alimshika bega mtafutaji mwenzake na kupandisha naye juu ambako huko waliumizwa na mwanga wa kawaida wa dunia yetu ya kila siku baada ya kukaa huko chini kwa muda mrefu ila hawakuwa na namna ni aina ya utafutaji waliyo ichagua.

Kani alipiga kelele kwamba mtu huyo amezidiwa sana akicheleweshwa hapo lazima atakufa hivyo wafanye haraka kumpa msaada, ililetwa gari ndogo ya hapo machimboni ili kumuwahisha mtu huyo hospitali, kwa namna alivyo lala na hali yake ilivyo onekana hakuna mtu ambaye alipata ujasiri wa kuweza kumkagua mwili wake kwa maana alivaa nguo chache sana hivyo alipandishwa kwenye gari moja kwa moja na kuwahishwa hospitali ili kupewa matibabu ya haraka kuweza kuiponya nafsi yake.

Kani kama alivyo julikana alijitahidi sana kuomba amsindikize mtu huyo hospitali ili awe kama mwangalizi wake lakini hakuipata hiyo nafasi walimwambia yeye aendelee na kazi yake huyu wagemshughulikia mwenyewe basi kishingo upande alirudi ndani ya shimo akiwa anasikitika juu ya hali ya mwenzake ambayo ilibadilika ghafla tu.

HOSPITAL
Yes, mwili wa mgonjwa ulifikishwa salama akiwa anaonekana kuzidiwa na kuhema kwa shida sana, madaktari walimpokea na moja kwa moja alipokelewa na kupelekwa moja kwa moja kwenye chumba cha wagonjwa mahututi ambacho kinajulikana kama ICU (an Intensive Care Unit). Uongozi wa machimboni haukuwa na namna zaidi ya kuweza kusubiri vipimo vya madaktari ili wapate majibu mgonjwa wao ana shida gani kwa sababu kama kuna chochote kingetokea wao ndio watu ambao walitakiwa kujibu kuhusu hiyo kesi, ndani ya nusu saa tu daktari ambaye alikuwa amewapokea na ndiye ambaye alikuwa akishughuika na masuala yote ya ICU aliwapa taarifa kwamba mgonjwa wao hana tatizo lolote isipokuwa anaonekana kufanya kazi kwa muda mrefu sana bila kupumzika hivyo hali ya mwili ilibadilika na kufikia kwenye hiyo hali ambayo alikuwa nayo sasa hivyo atalala hapo ila kesho asubuhi waje kumchukua mtu wao atakuwa sawa kabisa akiwa kwenye afya nzuri pia daktari aliahidi kwamba mtu huyo akizinduka tu atarudi kwenye hali yake ya kawaida na atabadilishiwa wodi.

Asubuhi na mapema wale watu walikuwa wamefika hapo kwa sababu huyo mwanaume kama yupo sawa alihitajika kurudi maeneo ya kazi akajumuike na wenzake kama ilivyo siku zote ila cha ajabu daktari waliye mkuta jana aliwapa taarifa ambazo zilimshtua kila mmoja wao, waliambiwa kwamba mtu huyo tangu jana daktari alipoweza kutoka kwenye ile wodi alivyorudi hakumkuta huyo mgonjwa kabisa na hakujulikana ameelekea wapi, alidai kwamba walipitia mfumo wa kamera za ulinzi kwenye hiyo hospitali zote lakini cha ajabu zote zilizima kabisa hakuna hata moja ambayo ilikuwa imewaka kwa muda huo kwahiyo kwa lugha raisi tu ni kwamba mgonjwa alikuwa amepotea kwenye mazingira ya kutatanisha mpaka muda huo hospitali haikuwa na taarifa yoyote ambayo alikuwa ameandikisha sababu kubwa ni kwamba alikuja akiwa amezimia hivyo walisubiri aamke ndipo waweze kuziandika na kuzirekodi taarifa zake kwa usahihi.

Uliwahi kusikia wapi mgonjwa ambaye amezimia anatoroka?....... ni nani yeye hasa mpaka apotee kwenye mazingira kama haya? ...., unavyohisi atakuwa amepotelea wapi mwanaume huyu……….

Ndo kwanza tunaufungua ukurasa wa kwanza kabisa kwenye kigongo hiki ambacho kinaitwa GEREZA LA HAZWA……lina nini hili gereza? wanafungwa akina nani humo ndani? linahusikaje na hadithi hii? Na ni kiumbe gani kinakuja kuwa kiumbe cha hatari mno mpaka wanahitaji kukifunga kwenye hilo gereza?.......majibu utayapata humu ndani ungana na kalamu yangu tena mwanzo mpaka mwisho.

Wananiita

Bux the story teller

chao
IMG-20220904-WA0013.jpg


Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
NOTE:
HADITHI HII NI YA KUTUNGA TU HAIHUSIANI NA MAISHA YA MTU YEYOTE, MAMLAKA WALA SEHEMU YOYOTE ILE NA HAILENGI KABISA KUMCHAFUA MTU YEYOTE YULE, KILA KILICHOPO HUMU NDANI NI CHA KUTUNGA TU NA KUFIKIRIKA.

STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller

UKURASA WA KWANZA

ANZA NAYO..............

Wakati nyie mnalala sana mkiwa mnausaka usingizi wa pono watu wenye ndoto zao ambao wanaiogopa njaa kuliko kitu chochote kile wapo macho kuzitafuta na kuzisaka ndoto zao kuhakikisha mwana haramu ambaye anaitwa tumbo anaridhika kwa namna yoyote ile hata kwa kumlazimisha. Ni wanadamu ambao wanaamini mikono yao ndiyo msaada wao wa pekee wa kuweza kuendelea kuwa hai na kupunguza mateso pamoja na dhihaka za kuchekwa na wanadamu wasiokuwa na uoga wowote mbele ya dunia ya Muumba, hao ndio watu ambao wanaweza kuiishi hii dunia yenye kila aina ya vioja vya ajabu na vya kutisha pia, kwao hawaamini katika bahati juhudi kwanza ndizo zinazo wapa imani ya kujikwamua kwenye maisha magumu sana ambayo wanayapitia wakiamini hakuna kitu kirahisi kukipata kwenye ulimwengu ni lazima ulipie ndipo ukipate unacho kitaka.

Wanalipaje na hawana pesa? Basi jasho lao ndilo malipo ambayo wanatakiwa kulilipa ili tu wafanikishe moja ya ndoto zao za kuwa na maisha angalau kupata hata milo miwili mpaka mitatu kwa siku “the bright future is only for the brave people” ni kauli ambayo inawapa muongozo wa nini wanatakiwa kukifanya kwenye maisha yao kama tu watahitaji kuipata ahueni ya maisha wakiamini ujasiri wao na ushujaa wao ndicho kitawapa kesho iliyo njema, hawana mashamba ya kusema wajifariji kwamba kama wakitaka mali basi wataipata shambani, yes, hayo ndiyo maisha halisi kwao.

ARUSHA, TANZANIA

Ndani ya machimbo ya moja ya madini adimu zaidi ulimwenguni na yanapatikana ndani ya nchi moja tu ulimwengu mzima ambayo ni Tanzania pekee kuna wanaume wapo ndani kabisa sehemu ambayo ilikuwa na kiza cha kutosha, tochi zilizofungwa kwenye vichwa vyao zilikuwa ni sehemu ya kuwasaidia kuona vitu ambavyo vipo mbele yao. Sio kwamba walikuwa sehemu ambayo haina umeme kiasi kwamba watashindwa kuona nini kilichopo huko hapana bali ni moja ya njia za kuweza kuzisaka na kuzifikia ndoto zao, wapo mgodini ndani kabisa ambako hata mwanga wa jua huwa ni ndoto kuonekana, mtu anakuwa kama yupo dunia ya peke yake tofauti kabisa na hii dunia ya kawaida ambayo kila mwanadamu anaiishi. Kama mtu angeshtuka kutoka usingizini akajikuta hiyo sehemu basi angehisi moja kwa moja kwamba ulikuwa usiku wa manane sana kulingana na aina ya kiza kizito ambacho kilitanda ila ni muda ambao usingeamini kwamba ilikuwa ni jioni ya kawaida kwenye dunia ya huku nje ambayo watu walikuwa wanaendelea na shughuli zao za kila siku hasa kwa wale wasaka tonge na wengine wale ambao kwao kazi ni mwiba uwachomao sana hawakuacha kuendelea kupiga majungu na jingi kwenye vijiwe mbali mbali na kuendelea kuijutia zamani zao badala ya kuiwaza na kuijenga kesho yao iliyo bora.

Ndani ya mgodi ambao unajulikana kwa kuwa na madini ya Tanzanite ndimo wanamo onekana wanaume wa kazi wakiwa hawaongei sana ila vitendo vyao vinajionyesha majembe mazito, uma, nyundo na machepeo ndivyo vitu vinavyo ongea zaidi huko, wanaume hawalali kuhakikisha maisha bora yanakuja kupitia imani zao za ufanyaji kazi kwa bidi. Vijana zaidi ya watano kila mmoja akiwa upande wake wanapambania kombe chini ya ardhi ambako kama ikitokea namna yoyote kukajifunika basi hadithi zao zinakuwa zimeishia huko huko chini ila hakuna namna wanaweza kuyafanya maisha yakawa malaini kwao kwa mlo wao wa siku moja kwa siku zaidi ya kujitoa mhanga. Ni zaidi ya masaa matano wakiwa wanafanya kazi kwa bidii sana.

“Hey Alen una tatizo gani man” ni sauti ya mmoja wa wale vijana watano ambao walikuwa ndani ya mgodi baada ya kusikia mwenzake yupo kimya sio nyundo wala chepeo ambayo ilikuwa inasikika upande aliokuwa.

“Ni kichwa tu kidogo Kani usijali hakuna tatizo” alimjibu mtu wake huyo ambaye ni wazi walikuwa wanajuana kama sio kuwa marafiki kabisa.

“Oya kama uko vibaya pandisha juu huko chapu gusa kamba pale usije kutupatia kesi mwanangu nadhani unayajua maisha yetu yalivyo hata mia mbovu tu kuipata mpaka tujitoe maisha yetu humu ndani” alionekana kumjali mwenzake kama sio kumtaka atoke asije akaleta ugumu wa kazi kama akizidiwa huko chini yakawa mambo mengine.

“Napumzika dakika moja tu kisha naendelea man usiogope” alimaliza kwa kuongea huku akipigiza nyundo moja kwenye jiwe kama sio chuma maana mlio ulio sikia ni dhahiri lilikuwa ni jiwe limepitiwa na nyundo, baada ya kufanya hivyo aligeuza macho yake huku akiivua tochi kwa kuwaangalia wenzake ambao walitawanyika kidogo ilikuwa inaonekana miale ya mwanga tu kutokana na kiza kizito kilicho kuwepo. Alipoona kila mtu anaendelea na majukumu yake aliinama chini na kuokota vipande vidogo vidogo vya kutosha ambavyo alivitawanyisha kwa nyundo yake, alitoa nailoni ndogo kwenye nguo yake ya ndani akawa anaichana kidogo anakikunja kipande kimoja kimoja kisha anakimeza mpaka alipo kamilisha vinne. Akatulia kidogo kisha akachukua vipande vilivyokuwa vimebakia akavua suruali yake na kuvifunga sehemu zake za siri kwenye hicho kinailoni ambacho aliviweka ndani vipande hivyo kisha akajivalisha kwenye uume wake na kuvifunga kwa kikamba kidogo ambacho alikuwa amekihifadhi kwenye mfuko wake.

Ni wazi alipata maumivu makali alikuwa akiikunja sura yake kila anavyoikaza kamba ili iwe sawa na uume wake ila hakuwa na namna hiyo ndiyo ilikuwa njia ya pekee kwake, mkono wake ulilowa alijua ni damu inatoka baada ya sehemu zake za siri kupata majeraja kutokana na kubanwa sana na vipande hivyo vya mawe na kamba iliyokazwa sana kwenye uume wake hata hivyo hakujali sana alikuwa akiuma meno yake tu huku anaendelea na zoezi lake vizuri mpaka alipohakikisha amekamilisha baada yah apo akajifuta damu mkononi kwenye mchanga uliokuwa chini. Alikuwa na wasiwasi sana kiasi kwamba jasho lilikuwa linamtoka mno kwenye mwili wake wote aliivaa tochi yake tena kwenye kichwa chake akaendelea kupiga kazi machozi yakiwa yanamtoka alikuwa na mawe manne kwenye tumbo lake hiyo haikutosha kweye sehemu yake ya thamani zaidi kwenye mwili alikuwa amejifunga mawe ambayo yalikuwa yakimletea maumivu makali lakini alichagua kuichagua hiyo njia ya kuumia kwani alikuwa anaamini hakuna njia rahisi kabisa kwenye utafutaji.

“Kichwa changu mimi nakufaa nakufaaa jamani msaada” yule mwanaume ambaye jina lake alifahamika kama Alen alisikika akipiga makelele ya kuomba msaada kwa kudai kwamba kichwa chake kinamuuma sana na alikuwa akilia kwa sauti kali, ni hali iliyo washtua wenzake wa mle ndani lakini aliyekuwa na muda naye ni mmoja tu wengine waligeuka tu mara moja kisha wakaendelea na kazi zao za utafutaji walifunzwa kwenye utafutaji kuwa na roho ngumu zaidi ndiyo siri pekee ya mafanikio huruma zingewachelewesha kufika kwenye safari zao ndefu za maisha ndiyo sababu hawakuwa na huruma na mtafutaji mwenzao waliamini huyo kama anakufa atajua yeye na hata akiishi hakuna kitu atawasaidia. Kani kama jina lake lilivyo itwa na Alen alimkimbilia msaka tonge mwenzake akamkuta chini akiwa na joto sana kwenye mwili wake huku akiwa anatoa machozi kuonyesha wazi hali yake ni mbaya hata mwili wake ulikuwa umechemka mno baada ya kumgusa kwenye kichwa chake.

Akamkokota mwenzake kwa mwanga wa tochi anafanikiwa kufika mpaka sehemu ya kuingilia humo ndani ambapo kwa mbali aliuona mwanga wa nje, kuna kamba ya kutolea ishara aliigusa na kuivuta kwa nguvu kisha akakaa pembeni ya mwanaume mwenzake kwa dakika kama mbili mpaka ngazi iliposhuka alijua wakati wa kutoka sasa umefika. Mwanaume alimshika bega mtafutaji mwenzake na kupandisha naye juu ambako huko waliumizwa na mwanga wa kawaida wa dunia yetu ya kila siku baada ya kukaa huko chini kwa muda mrefu ila hawakuwa na namna ni aina ya utafutaji waliyo ichagua.

Kani alipiga kelele kwamba mtu huyo amezidiwa sana akicheleweshwa hapo lazima atakufa hivyo wafanye haraka kumpa msaada, ililetwa gari ndogo ya hapo machimboni ili kumuwahisha mtu huyo hospitali, kwa namna alivyo lala na hali yake ilivyo onekana hakuna mtu ambaye alipata ujasiri wa kuweza kumkagua mwili wake kwa maana alivaa nguo chache sana hivyo alipandishwa kwenye gari moja kwa moja na kuwahishwa hospitali ili kupewa matibabu ya haraka kuweza kuiponya nafsi yake.

Kani kama alivyo julikana alijitahidi sana kuomba amsindikize mtu huyo hospitali ili awe kama mwangalizi wake lakini hakuipata hiyo nafasi walimwambia yeye aendelee na kazi yake huyu wagemshughulikia mwenyewe basi kishingo upande alirudi ndani ya shimo akiwa anasikitika juu ya hali ya mwenzake ambayo ilibadilika ghafla tu.

HOSPITAL
Yes, mwili wa mgonjwa ulifikishwa salama akiwa anaonekana kuzidiwa na kuhema kwa shida sana, madaktari walimpokea na moja kwa moja alipokelewa na kupelekwa moja kwa moja kwenye chumba cha wagonjwa mahututi ambacho kinajulikana kama ICU (an Intensive Care Unit). Uongozi wa machimboni haukuwa na namna zaidi ya kuweza kusubiri vipimo vya madaktari ili wapate majibu mgonjwa wao ana shida gani kwa sababu kama kuna chochote kingetokea wao ndio watu ambao walitakiwa kujibu kuhusu hiyo kesi, ndani ya nusu saa tu daktari ambaye alikuwa amewapokea na ndiye ambaye alikuwa akishughuika na masuala yote ya ICU aliwapa taarifa kwamba mgonjwa wao hana tatizo lolote isipokuwa anaonekana kufanya kazi kwa muda mrefu sana bila kupumzika hivyo hali ya mwili ilibadilika na kufikia kwenye hiyo hali ambayo alikuwa nayo sasa hivyo atalala hapo ila kesho asubuhi waje kumchukua mtu wao atakuwa sawa kabisa akiwa kwenye afya nzuri pia daktari aliahidi kwamba mtu huyo akizinduka tu atarudi kwenye hali yake ya kawaida na atabadilishiwa wodi.

Asubuhi na mapema wale watu walikuwa wamefika hapo kwa sababu huyo mwanaume kama yupo sawa alihitajika kurudi maeneo ya kazi akajumuike na wenzake kama ilivyo siku zote ila cha ajabu daktari waliye mkuta jana aliwapa taarifa ambazo zilimshtua kila mmoja wao, waliambiwa kwamba mtu huyo tangu jana daktari alipoweza kutoka kwenye ile wodi alivyorudi hakumkuta huyo mgonjwa kabisa na hakujulikana ameelekea wapi, alidai kwamba walipitia mfumo wa kamera za ulinzi kwenye hiyo hospitali zote lakini cha ajabu zote zilizima kabisa hakuna hata moja ambayo ilikuwa imewaka kwa muda huo kwahiyo kwa lugha raisi tu ni kwamba mgonjwa alikuwa amepotea kwenye mazingira ya kutatanisha mpaka muda huo hospitali haikuwa na taarifa yoyote ambayo alikuwa ameandikisha sababu kubwa ni kwamba alikuja akiwa amezimia hivyo walisubiri aamke ndipo waweze kuziandika na kuzirekodi taarifa zake kwa usahihi.

Uliwahi kusikia wapi mgonjwa ambaye amezimia anatoroka?....... ni nani yeye hasa mpaka apotee kwenye mazingira kama haya? ...., unavyohisi atakuwa amepotelea wapi mwanaume huyu……….

Ndo kwanza tunaufungua ukurasa wa kwanza kabisa kwenye kigongo hiki ambacho kinaitwa GEREZA LA HAZWA……lina nini hili gereza? wanafungwa akina nani humo ndani? linahusikaje na hadithi hii? Na ni kiumbe gani kinakuja kuwa kiumbe cha hatari mno mpaka wanahitaji kukifunga kwenye hilo gereza?.......majibu utayapata humu ndani ungana na kalamu yangu tena mwanzo mpaka mwisho.

Wananiita

Bux the story teller

chaoView attachment 2346949

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
Wewe ni monster kwenye kazi hizi
 
NOTE:
HADITHI HII NI YA KUTUNGA TU HAIHUSIANI NA MAISHA YA MTU YEYOTE, MAMLAKA WALA SEHEMU YOYOTE ILE NA HAILENGI KABISA KUMCHAFUA MTU YEYOTE YULE, KILA KILICHOPO HUMU NDANI NI CHA KUTUNGA TU NA KUFIKIRIKA.

STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller

UKURASA WA KWANZA

ANZA NAYO..............

Wakati nyie mnalala sana mkiwa mnausaka usingizi wa pono watu wenye ndoto zao ambao wanaiogopa njaa kuliko kitu chochote kile wapo macho kuzitafuta na kuzisaka ndoto zao kuhakikisha mwana haramu ambaye anaitwa tumbo anaridhika kwa namna yoyote ile hata kwa kumlazimisha. Ni wanadamu ambao wanaamini mikono yao ndiyo msaada wao wa pekee wa kuweza kuendelea kuwa hai na kupunguza mateso pamoja na dhihaka za kuchekwa na wanadamu wasiokuwa na uoga wowote mbele ya dunia ya Muumba, hao ndio watu ambao wanaweza kuiishi hii dunia yenye kila aina ya vioja vya ajabu na vya kutisha pia, kwao hawaamini katika bahati juhudi kwanza ndizo zinazo wapa imani ya kujikwamua kwenye maisha magumu sana ambayo wanayapitia wakiamini hakuna kitu kirahisi kukipata kwenye ulimwengu ni lazima ulipie ndipo ukipate unacho kitaka.

Wanalipaje na hawana pesa? Basi jasho lao ndilo malipo ambayo wanatakiwa kulilipa ili tu wafanikishe moja ya ndoto zao za kuwa na maisha angalau kupata hata milo miwili mpaka mitatu kwa siku “the bright future is only for the brave people” ni kauli ambayo inawapa muongozo wa nini wanatakiwa kukifanya kwenye maisha yao kama tu watahitaji kuipata ahueni ya maisha wakiamini ujasiri wao na ushujaa wao ndicho kitawapa kesho iliyo njema, hawana mashamba ya kusema wajifariji kwamba kama wakitaka mali basi wataipata shambani, yes, hayo ndiyo maisha halisi kwao.

ARUSHA, TANZANIA

Ndani ya machimbo ya moja ya madini adimu zaidi ulimwenguni na yanapatikana ndani ya nchi moja tu ulimwengu mzima ambayo ni Tanzania pekee kuna wanaume wapo ndani kabisa sehemu ambayo ilikuwa na kiza cha kutosha, tochi zilizofungwa kwenye vichwa vyao zilikuwa ni sehemu ya kuwasaidia kuona vitu ambavyo vipo mbele yao. Sio kwamba walikuwa sehemu ambayo haina umeme kiasi kwamba watashindwa kuona nini kilichopo huko hapana bali ni moja ya njia za kuweza kuzisaka na kuzifikia ndoto zao, wapo mgodini ndani kabisa ambako hata mwanga wa jua huwa ni ndoto kuonekana, mtu anakuwa kama yupo dunia ya peke yake tofauti kabisa na hii dunia ya kawaida ambayo kila mwanadamu anaiishi. Kama mtu angeshtuka kutoka usingizini akajikuta hiyo sehemu basi angehisi moja kwa moja kwamba ulikuwa usiku wa manane sana kulingana na aina ya kiza kizito ambacho kilitanda ila ni muda ambao usingeamini kwamba ilikuwa ni jioni ya kawaida kwenye dunia ya huku nje ambayo watu walikuwa wanaendelea na shughuli zao za kila siku hasa kwa wale wasaka tonge na wengine wale ambao kwao kazi ni mwiba uwachomao sana hawakuacha kuendelea kupiga majungu na jingi kwenye vijiwe mbali mbali na kuendelea kuijutia zamani zao badala ya kuiwaza na kuijenga kesho yao iliyo bora.

Ndani ya mgodi ambao unajulikana kwa kuwa na madini ya Tanzanite ndimo wanamo onekana wanaume wa kazi wakiwa hawaongei sana ila vitendo vyao vinajionyesha majembe mazito, uma, nyundo na machepeo ndivyo vitu vinavyo ongea zaidi huko, wanaume hawalali kuhakikisha maisha bora yanakuja kupitia imani zao za ufanyaji kazi kwa bidi. Vijana zaidi ya watano kila mmoja akiwa upande wake wanapambania kombe chini ya ardhi ambako kama ikitokea namna yoyote kukajifunika basi hadithi zao zinakuwa zimeishia huko huko chini ila hakuna namna wanaweza kuyafanya maisha yakawa malaini kwao kwa mlo wao wa siku moja kwa siku zaidi ya kujitoa mhanga. Ni zaidi ya masaa matano wakiwa wanafanya kazi kwa bidii sana.

“Hey Alen una tatizo gani man” ni sauti ya mmoja wa wale vijana watano ambao walikuwa ndani ya mgodi baada ya kusikia mwenzake yupo kimya sio nyundo wala chepeo ambayo ilikuwa inasikika upande aliokuwa.

“Ni kichwa tu kidogo Kani usijali hakuna tatizo” alimjibu mtu wake huyo ambaye ni wazi walikuwa wanajuana kama sio kuwa marafiki kabisa.

“Oya kama uko vibaya pandisha juu huko chapu gusa kamba pale usije kutupatia kesi mwanangu nadhani unayajua maisha yetu yalivyo hata mia mbovu tu kuipata mpaka tujitoe maisha yetu humu ndani” alionekana kumjali mwenzake kama sio kumtaka atoke asije akaleta ugumu wa kazi kama akizidiwa huko chini yakawa mambo mengine.

“Napumzika dakika moja tu kisha naendelea man usiogope” alimaliza kwa kuongea huku akipigiza nyundo moja kwenye jiwe kama sio chuma maana mlio ulio sikia ni dhahiri lilikuwa ni jiwe limepitiwa na nyundo, baada ya kufanya hivyo aligeuza macho yake huku akiivua tochi kwa kuwaangalia wenzake ambao walitawanyika kidogo ilikuwa inaonekana miale ya mwanga tu kutokana na kiza kizito kilicho kuwepo. Alipoona kila mtu anaendelea na majukumu yake aliinama chini na kuokota vipande vidogo vidogo vya kutosha ambavyo alivitawanyisha kwa nyundo yake, alitoa nailoni ndogo kwenye nguo yake ya ndani akawa anaichana kidogo anakikunja kipande kimoja kimoja kisha anakimeza mpaka alipo kamilisha vinne. Akatulia kidogo kisha akachukua vipande vilivyokuwa vimebakia akavua suruali yake na kuvifunga sehemu zake za siri kwenye hicho kinailoni ambacho aliviweka ndani vipande hivyo kisha akajivalisha kwenye uume wake na kuvifunga kwa kikamba kidogo ambacho alikuwa amekihifadhi kwenye mfuko wake.

Ni wazi alipata maumivu makali alikuwa akiikunja sura yake kila anavyoikaza kamba ili iwe sawa na uume wake ila hakuwa na namna hiyo ndiyo ilikuwa njia ya pekee kwake, mkono wake ulilowa alijua ni damu inatoka baada ya sehemu zake za siri kupata majeraja kutokana na kubanwa sana na vipande hivyo vya mawe na kamba iliyokazwa sana kwenye uume wake hata hivyo hakujali sana alikuwa akiuma meno yake tu huku anaendelea na zoezi lake vizuri mpaka alipohakikisha amekamilisha baada yah apo akajifuta damu mkononi kwenye mchanga uliokuwa chini. Alikuwa na wasiwasi sana kiasi kwamba jasho lilikuwa linamtoka mno kwenye mwili wake wote aliivaa tochi yake tena kwenye kichwa chake akaendelea kupiga kazi machozi yakiwa yanamtoka alikuwa na mawe manne kwenye tumbo lake hiyo haikutosha kweye sehemu yake ya thamani zaidi kwenye mwili alikuwa amejifunga mawe ambayo yalikuwa yakimletea maumivu makali lakini alichagua kuichagua hiyo njia ya kuumia kwani alikuwa anaamini hakuna njia rahisi kabisa kwenye utafutaji.

“Kichwa changu mimi nakufaa nakufaaa jamani msaada” yule mwanaume ambaye jina lake alifahamika kama Alen alisikika akipiga makelele ya kuomba msaada kwa kudai kwamba kichwa chake kinamuuma sana na alikuwa akilia kwa sauti kali, ni hali iliyo washtua wenzake wa mle ndani lakini aliyekuwa na muda naye ni mmoja tu wengine waligeuka tu mara moja kisha wakaendelea na kazi zao za utafutaji walifunzwa kwenye utafutaji kuwa na roho ngumu zaidi ndiyo siri pekee ya mafanikio huruma zingewachelewesha kufika kwenye safari zao ndefu za maisha ndiyo sababu hawakuwa na huruma na mtafutaji mwenzao waliamini huyo kama anakufa atajua yeye na hata akiishi hakuna kitu atawasaidia. Kani kama jina lake lilivyo itwa na Alen alimkimbilia msaka tonge mwenzake akamkuta chini akiwa na joto sana kwenye mwili wake huku akiwa anatoa machozi kuonyesha wazi hali yake ni mbaya hata mwili wake ulikuwa umechemka mno baada ya kumgusa kwenye kichwa chake.

Akamkokota mwenzake kwa mwanga wa tochi anafanikiwa kufika mpaka sehemu ya kuingilia humo ndani ambapo kwa mbali aliuona mwanga wa nje, kuna kamba ya kutolea ishara aliigusa na kuivuta kwa nguvu kisha akakaa pembeni ya mwanaume mwenzake kwa dakika kama mbili mpaka ngazi iliposhuka alijua wakati wa kutoka sasa umefika. Mwanaume alimshika bega mtafutaji mwenzake na kupandisha naye juu ambako huko waliumizwa na mwanga wa kawaida wa dunia yetu ya kila siku baada ya kukaa huko chini kwa muda mrefu ila hawakuwa na namna ni aina ya utafutaji waliyo ichagua.

Kani alipiga kelele kwamba mtu huyo amezidiwa sana akicheleweshwa hapo lazima atakufa hivyo wafanye haraka kumpa msaada, ililetwa gari ndogo ya hapo machimboni ili kumuwahisha mtu huyo hospitali, kwa namna alivyo lala na hali yake ilivyo onekana hakuna mtu ambaye alipata ujasiri wa kuweza kumkagua mwili wake kwa maana alivaa nguo chache sana hivyo alipandishwa kwenye gari moja kwa moja na kuwahishwa hospitali ili kupewa matibabu ya haraka kuweza kuiponya nafsi yake.

Kani kama alivyo julikana alijitahidi sana kuomba amsindikize mtu huyo hospitali ili awe kama mwangalizi wake lakini hakuipata hiyo nafasi walimwambia yeye aendelee na kazi yake huyu wagemshughulikia mwenyewe basi kishingo upande alirudi ndani ya shimo akiwa anasikitika juu ya hali ya mwenzake ambayo ilibadilika ghafla tu.

HOSPITAL
Yes, mwili wa mgonjwa ulifikishwa salama akiwa anaonekana kuzidiwa na kuhema kwa shida sana, madaktari walimpokea na moja kwa moja alipokelewa na kupelekwa moja kwa moja kwenye chumba cha wagonjwa mahututi ambacho kinajulikana kama ICU (an Intensive Care Unit). Uongozi wa machimboni haukuwa na namna zaidi ya kuweza kusubiri vipimo vya madaktari ili wapate majibu mgonjwa wao ana shida gani kwa sababu kama kuna chochote kingetokea wao ndio watu ambao walitakiwa kujibu kuhusu hiyo kesi, ndani ya nusu saa tu daktari ambaye alikuwa amewapokea na ndiye ambaye alikuwa akishughuika na masuala yote ya ICU aliwapa taarifa kwamba mgonjwa wao hana tatizo lolote isipokuwa anaonekana kufanya kazi kwa muda mrefu sana bila kupumzika hivyo hali ya mwili ilibadilika na kufikia kwenye hiyo hali ambayo alikuwa nayo sasa hivyo atalala hapo ila kesho asubuhi waje kumchukua mtu wao atakuwa sawa kabisa akiwa kwenye afya nzuri pia daktari aliahidi kwamba mtu huyo akizinduka tu atarudi kwenye hali yake ya kawaida na atabadilishiwa wodi.

Asubuhi na mapema wale watu walikuwa wamefika hapo kwa sababu huyo mwanaume kama yupo sawa alihitajika kurudi maeneo ya kazi akajumuike na wenzake kama ilivyo siku zote ila cha ajabu daktari waliye mkuta jana aliwapa taarifa ambazo zilimshtua kila mmoja wao, waliambiwa kwamba mtu huyo tangu jana daktari alipoweza kutoka kwenye ile wodi alivyorudi hakumkuta huyo mgonjwa kabisa na hakujulikana ameelekea wapi, alidai kwamba walipitia mfumo wa kamera za ulinzi kwenye hiyo hospitali zote lakini cha ajabu zote zilizima kabisa hakuna hata moja ambayo ilikuwa imewaka kwa muda huo kwahiyo kwa lugha raisi tu ni kwamba mgonjwa alikuwa amepotea kwenye mazingira ya kutatanisha mpaka muda huo hospitali haikuwa na taarifa yoyote ambayo alikuwa ameandikisha sababu kubwa ni kwamba alikuja akiwa amezimia hivyo walisubiri aamke ndipo waweze kuziandika na kuzirekodi taarifa zake kwa usahihi.

Uliwahi kusikia wapi mgonjwa ambaye amezimia anatoroka?....... ni nani yeye hasa mpaka apotee kwenye mazingira kama haya? ...., unavyohisi atakuwa amepotelea wapi mwanaume huyu……….

Ndo kwanza tunaufungua ukurasa wa kwanza kabisa kwenye kigongo hiki ambacho kinaitwa GEREZA LA HAZWA……lina nini hili gereza? wanafungwa akina nani humo ndani? linahusikaje na hadithi hii? Na ni kiumbe gani kinakuja kuwa kiumbe cha hatari mno mpaka wanahitaji kukifunga kwenye hilo gereza?.......majibu utayapata humu ndani ungana na kalamu yangu tena mwanzo mpaka mwisho.

Wananiita

Bux the story teller

chaoView attachment 2346949

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller

UKURASA WA PILI

TULIPO ISHIA UKURASA WA KWANZA


Asubuhi na mapema wale watu walikuwa wamefika hapo kwa sababu huyo mwanaume kama yupo sawa alihitajika kurudi maeneo ya kazi akajumuike na wenzake kama ilivyo siku zote ila cha ajabu daktari waliye mkuta jana aliwapa taarifa ambazo zilimshtua kila mmoja wao, waliambiwa kwamba mtu huyo tangu jana daktari alipoweza kutoka kwenye ile wodi alivyorudi hakumkuta huyo mgonjwa kabisa na hakujulikana ameelekea wapi, alidai kwamba walipitia mfumo wa kamera za ulinzi kwenye hiyo hospitali zote lakini cha ajabu zote zilizima kabisa hakuna hata moja ambayo ilikuwa imewaka kwa muda huo kwahiyo kwa lugha raisi tu ni kwamba mgonjwa alikuwa amepotea kwenye mazingira ya kutatanisha mpaka muda huo hospitali haikuwa na taarifa yoyote ambayo alikuwa ameandikisha sababu kubwa ni kwamba alikuja akiwa amezimia hivyo walisubiri aamke ndipo waweze kuziandika na kuzirekodi taarifa zake kwa usahihi.


SONGA NAYO.................

Baada ya mgonjwa kuweza kutoweka kwenye moja ya hospitali huko ndani ya jiji la Arusha ambako alikuwa amepelekwa ili kuweza kupata matibabu hatukuweza kujua kwamba alikuwa ameelekea wapi na hali yake ilikuwaje kwa sababu kwa mara ya mwisho alionekana kabisa akiwa amezimia na hali yake ilikuwa mbaya sana kiasi kwamba alikuwa amepoteza fahamu.

Moja ya basi bora kabisa ambalo lilitoka Arusha majira ya asubuhi na mapema sana na sasa majira ya saa mbili za usiku lilikuwa linaingia ndani ya jiji pendwa zaidi nchini jiji la Dar es salaam, lilifika stendi walianza kushuka abiria mbali mbali ambapo kuna mwanaume mmoja ambaye alikuwa na begi lake mgongoni pamoja na kofia ambayo ilikuwa imeuziba uso wake vizuri alikuwa amekaa konani kabisa kwenye siti ya mwisho alibaki amekaa humo ndani mpaka pale alipo hakikisha kwamba watu wote wametoka ndipo naye alipo amua kutoka huku akiwa anaificha sana sura yake ni wazi hakuhitaji mtu yeyote yule aweze kumuona sura yake na alikuwa makini sana kwa kila hatua yake moja ambayo alikuwa anaipiga.

Alishuka kwenye gari na kuchukua usafiri wa bajaji akiwa makini sana kuulinda uso wake kwa kofia ambayo alikuwa ameivaa usoni kwake, bajaji hiyo ilimfiksha mpaka maeneo ya usalama ambapo aliomba usafiri huo uweze kumuacha huko mbele angeendelea mwenyewe na safari yake, mwanaume alishuka na kuanza kuikata mitaa ya jiji majira ya usiku wa mapema huo lakini alihisi kama kuna watu walikuwa wakimfuatilia kwa muda kidogo tangu pale alipoweza kushuka kwenye ile bajaji, aliigusa kofia yake kidogo na kutabasamu kisha akawa anaendelea na safari yake kama ilivyokuwa kawaida yake. Hatua kama saba alizozipiga alipotea kwenye hilo eneo ambalo alikuwa anaonekana yupo haukupita muda sana wakatokezea wanaume watatu waliangaza huku na huko walishangaa kutomuona mtu yeyote yule ilikuwa ni ghafla sio muda sana waliona kabisa kuna mtu hilo eneo.

“Kama ikitokea siku ukiwa karibu na huyo mtu ni kiumbe cha ajabu sana kinapokuwa kwenye uhalisia wake unapaswa kujihadhari kwa namna yoyote ile ambayo unaweza ili kuhakikisha maisha yako yanakuwa salama kama ukichezea hata sekunde moja tu ukafanya uzembe wowote basi jiandae kubadilishiwa jina lako halisi na kuitwa marehemu” ni kauli ambayo mmoja wa hao wanaume aliikumbuka vizuri siku moja wakati anapewa onyo na kiongozi wake na alionekana kuwa mkuu wa msafara huo wa watu watatu ambao walikuwa hapo usiku huo jiji likiwa limetulia mubashara.

“Jiangalieni na muwe makini hayupo mbali na hapa” aliongea ikiwa ni kuwatahadhalisha wenzake alionekana kumjua huyo mtu kwa uchache wake, bahati mbaya ni kama taarifa hiyo alichelewa sana kuitoa mmoja kati yao alikuwa anaenda chini akiwa amelainika kama tambi zilizopikwa, walimkimbilia na kumgusa walipigwa na butwaa uti wa mgongo wa mwenzao ulikuwa umevunjwa hauwezi hata kufanya kazi tena alikuwa ameshaanza kuwa wa baridi maana yake dunia hayakuwa makao yake tena.

“Vipi mnanitafuta mimi” mshtuko walioupata kwa kusikia sauti la kutisha ni kama walikuwa ndotoni, ni sauti iliyoshiba ambayo ilisikika kutoka kwa mtu ambaye alikuwa yupo nyuma yao.

“Mpige risasi kwenye mbavu haraka” aliyekuwa anapewa maagizo ya kupiga risasi huyo binadamu mwenzao utoaji wa risasi kwenye bastola yake ulikuwa mdogo sana kiasi kwamba ilimpelekea yeye kupiga magoti akiwa amejishika eneo la shingoni, yule mwanaume ambaye ndiye aliyekuwa anatafutwa alionekana kuwa na pete kwenye mkono wake iliyotumika kufanyia hayo mauaji japo haikueleweka pete imeweza vipi kuichana chana shingo ya mtu mpaka akadondoka na kupoteza maisha kwa sekunde kadhaa tu.

“Nenda kamwambie huyo aliyewatuma kwangu aje anitafute yeye mwenyewe”ni kauli moja tu ambayo aliweza kuitamka kwa mwanaume mmoja tu ambaye alikuwa amesalia na kuachwa hai kati ya hao watatu ambao walikuwa wapo hilo eneo, alibaki akitetemeka mno aliyo yashuhudia kwa wenzake kwa hizo sekunde chache kwenye mwili wake yalimfanya kuelewa nini maana ya hofu. Alimshuhudia mwanaume huyo akiondoka na kupotelea ambako alikujua yeye mwenyewe na hakuwa na cha kuweza kumfanya chochote kile, alijipapasa kwenye mwili wake baada ya kujigundua kwamba alikuwa ni mzima wa afya aliitupa bastola yake chini na kuanza kukimbia kwa nguvu sana hakuweza kuamini kama kweli aliweza kuachwa akiwa hai na mzima wa afya ya kutosha alishukuru MUNGU kwa hilo hakujua aina ya mtu ambaye alikuwa anamhangaikia usiku huo ni bora angebaki hata kuuza miguu ya kuku na kashata huko Tandika hii michezo ya wanaume alikuwa haiwezi.


Siku zilikatika, wiki ziliishaa, miezi ilienda na miaka ilikuwa inakimbia kwa kasi kubwa kama ilivyo kawaida kwa muda haujawahi kusimama hata siku moja kila siku huwa unakimbia kwa kasi, miaka mitano ilikuwa imepita tangu matukio yote hayo yaweze kutokea ndani ya Arusha na Dar es salaam. Kwenye moja ya Apartment kubwa ya kifahari alionekana bwana mmoja akiwa amesimama eneo la dirishani akiwa anaangalia nje kupitia kioo kikubwa kilichokuwa hapo akiwa anashuhudia kwa namna mji ulivyokuwa unavutia majira hayo ya usiku ulio tulia. Alionekana kuwa mtu ambaye mawazo yake yalikuwa yanakumbuka mbali sana, aligeuka na kuangalia upande wa pili ambako kulikuwa na mlimbwende kama sio mrembo kwa lugha ambayo ni rahisi zaidi, mwanamke ambaye tungesema ni sumaku kwa namna muumba alivyo tulia na kuvigawa viungo ambavyo viliufanya mwili wake kuwa sehemu ya kiburudisho cha macho kwa kila ambaye alikuwa ana uwezo wa kuona basi asingeweza kupita akakosa kuisaliti nafsi yake kwa kugeuza shingo yake na kumshuhudia huyo mwanamke jinsi alivyokuwa mzuri wa haja na alipendelewa uzuri wa kipekee ambao kwa hadithi ya neno moja moja ilitakiwa ramani nzima ya Afrika kuweza kumaliza kilomita za kumuelezea namna alivyokuwa ni mwanamke mzuri sana, sifa kubwa zilienda kwa MUNGU kwa uumbaji wake kiufupi ni kwamba MUNGU fundi sana.

Mwanamke huyo alikuwa kwenye tabasamu zito lililo mfanya meno yake ambayo yalikuwa ni meupe kwa asilimia mia moja na nukta zake yaonekane vizuri sana lakini hilo halikuwa tu la kumfanya atabasamu sana hivyo lahasha bali kiumbe kilichokuwa karibu yake ndipo lilipokuwa tabasamu lake kubwa, alikuwa akicheza na binti mdogo wa kike ambaye usingesita kusema alikuwa ana miaka miwili mpaka mitatu pale unapo muona, kama yeye alivyokuwa amependelewa kuwa mzuri basi hata yeye alimshukuru MUNGU kumpendelea mtoto mzuri kama huyo aliye mpata, aliye mfanya mpaka yeye mwenyewe asadiki kwamba hii dunia kuna watu wanabarikiwa kuwa wazuri akijisahau kwamba yeye ndiye mama wa huyo mtoto (hahahahha binadamu hawaridhiki kabisa bwana). Ilionekana kuwa moja ya familia iliyokuwa na furaha kubwa mno, hao wawili ndio ulikuwa moyo wa huyo mwanaume ambaye alikuwa pembezoni kabisa mwa dirisha kubwa la vioo akiwa anamuangalia mkewe na mwanae wa pekee wakiwa kwenye furaha kubwa mno na hilo ndilo lengo la kila baba bora kwa familia yake ni bora yeye alale njaa lakini sio kuona familia yake inalia au kutoa chozi (he was a good father indeed).

Hapo alipokuwa amesimama alikuwa anaongea na nafsi yake mwenyewe akiwa anajikumbushia namna alivyo mpata huyo mwanamke na aliweza vipi kukutana naye mpaka ikafikia hatua akawa mke wake kabisa wa ndoa. “Ilikuwa ni siku moja nikiwa nimetoka kwenye mishe mishe zangu za kila siku, kuvaa na kupendeza kila siku ilikuwa sehemu ya maisha yangu, nilibahatika kuwa miongoni mwa wale vijana waenda gym basi hata mwili wangu ulikaa vyema sana sikuwa na tatizo la kimwonekano. Ni usiku mmoja nilikuwa nimeenda na gari yangu kwenye hoteli moja japo nilikuwa makini sana kuulinda uso wangu usije ukapatikana kwenye kamera hata moja na mara nyingi nilikuwa ninatembea na barakoa pale ambapo naingia sehemu ambayo inaweza kuwa tatizo kwangu kuonyesha sura yangu.

Nilijibanza kwenye kona moja ambapo nilipata kinywaji changu ila kwa bahati mbaya sana nilijikuta sina waleti yangu ambayo ilikuwa na pesa nilihisi nimeibiwa ila nikakumbuka nitakuwa nimeidondoshea kwenye gari yangu, mhudumu alinijia juu na kusema kwamba mimi nilikuw atapeli na nisingeweza kutoka kwenda kwenye gari bila kulipia vinginevyo ilitakiwa nikamatwe kama ningeshindwa kulipa kitu ambacho kingenifanya nijulikane haraka na sikutaka hilo lifanyike lakini kwa bahati iliyokuwa njema pembeni yangu alikaa mwanamke mmoja mzuri sana tena sana ambaye nisingeweza kumuelezea nikamaliza nilishangaa ananilipia na kutabasamu hahhhaaa kilicho fuata ilibaki kuwa historia” alitabasamu sana baada ya hisia zake kumkumbusha namna alivyoweza kukutana na mwanamke huyo japo hakutaka hisia zake ziweze kuendelea kwa muda huo ili kuweza kujua kwamba ilikuaje mpaka akafikia hatua kabisa ya kumuweka ndani, alimshukuru sana MUNGU kumpendelea familia yenye furaha sana.

“MUNGU ni mkubwa sana sasa hivi hata mimi naishi maisha ya kawaida kama binadamu wengine” alitabasamu baada ya kuweza kuyatamka hayo maneno yake kisha akazamisha mkono wake mfukoni na kuitoa simu akaanza kuhangaika kuitafuta namba moja ambayo kwa muda huo ilionekana kuwa ya mhimu, baada ya kuipata alipiga ikaite kwa sekunde kadhaa tu kisha ikapokelewa.

“Halo”ni sauti kutoka upande wa pili uliokuwa umepokea simu bila shaka ilitoka kwa moja ya watu waliokuwa na njaa kali sana ndiyo sababu alikuwa tayari kuipokea simu kwa wepesi akihisi huenda ni ya chochote kitu cha kuliweka tumbo lake sawa.

“Kani uko wapi saivi?”

“Nani wewe?” sauti ya upande wa pili iliuliza kwa msisitizo mzito

“Alen”

“Whaaaaaaat?”

“Yes, uko wapi?”

“Mimi bado nipo Arusha ndugu yangu umeniharibia maisha yangu yote kwa ajili yako nilifungwa jela na kufukuzwa ka……”

“Kesho nahitaji uwepo Dar es salaam”

“Kufanya nini?”

“Acha jeuri kama umeyapatia maisha mjinga wewe wakati una shida kibao” upande wa pili mtu huyo alimeza mate kwani alikuwa ameambiwa ukweli kabisa wa maisha yake.

“Daaaah kaka sema sina nauli”

“Nakutumia, utanitafuta ukifika stendi” Baada ya simu kukatwa iliingia meseji ambayo huwa inabeba zaidi ya asilimia 99 ya furaha ya binadamu mwenye shida, shilingi laki tano ilikuwa imethibitishwa kwenye laini yake hiyo, hakuamini hicho kitu ndani ya chumba chake kidogo ambacho alikuwa ametandika godoro chini akiwa hajatia chochote tumboni alimshukuru MUNGU kwa hilo alinyanyuka na kukimbilia kwa wakala kabla mwenye pesa hajairudisha kwake, alienda kutoa pesa yote akiwa anacheka cheka njia nzima. Alienda kwenye moja ya migahawa bora sana akaagiza chakula cha bei kubwa akiwa anafidia siku alizo teseka, alikula akashiba vizuri baada ya hapo alienda club na kuchukua mwanamke mmoja mrembo sana akawa anakunywa pombe baadae aliingia naye chumbani kupunguza uzito aliokuwa nao ikiwa ni kama kulipiza kwa namna wanawake wazuri walivyokuwa wanamkataa kwa sababu hakuwa na pesa kwenye maisha yake yote basi alijisikia fahari sana siku hiyo. Asubuhi na mapema sana alikuwa ndani ya gari akiwa anaelekea zake kwenye moja ya jiji ambalo kwake ilikuwa ni ndoto kwenda kuliishi.


Huyu mwanadamu ambaye alionekana kuwa kiumbe cha hatari sana ni nani hasa?, kipi kimemfanya atafutwe sana namna hiyo? Tuna mengi sana ya kuyajua na kuyaelewa humu ndani kikubwa twende taratibu tutaelewana tu……. sehemu ya pili haina cha kukuongezea kwa sasa mpaka wakati ujao.

Bux the story teller

Chao
IMG-20220904-WA0014.jpg


Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller

UKURASA WA PILI

TULIPO ISHIA UKURASA WA KWANZA


Asubuhi na mapema wale watu walikuwa wamefika hapo kwa sababu huyo mwanaume kama yupo sawa alihitajika kurudi maeneo ya kazi akajumuike na wenzake kama ilivyo siku zote ila cha ajabu daktari waliye mkuta jana aliwapa taarifa ambazo zilimshtua kila mmoja wao, waliambiwa kwamba mtu huyo tangu jana daktari alipoweza kutoka kwenye ile wodi alivyorudi hakumkuta huyo mgonjwa kabisa na hakujulikana ameelekea wapi, alidai kwamba walipitia mfumo wa kamera za ulinzi kwenye hiyo hospitali zote lakini cha ajabu zote zilizima kabisa hakuna hata moja ambayo ilikuwa imewaka kwa muda huo kwahiyo kwa lugha raisi tu ni kwamba mgonjwa alikuwa amepotea kwenye mazingira ya kutatanisha mpaka muda huo hospitali haikuwa na taarifa yoyote ambayo alikuwa ameandikisha sababu kubwa ni kwamba alikuja akiwa amezimia hivyo walisubiri aamke ndipo waweze kuziandika na kuzirekodi taarifa zake kwa usahihi.


SONGA NAYO.................

Baada ya mgonjwa kuweza kutoweka kwenye moja ya hospitali huko ndani ya jiji la Arusha ambako alikuwa amepelekwa ili kuweza kupata matibabu hatukuweza kujua kwamba alikuwa ameelekea wapi na hali yake ilikuwaje kwa sababu kwa mara ya mwisho alionekana kabisa akiwa amezimia na hali yake ilikuwa mbaya sana kiasi kwamba alikuwa amepoteza fahamu.

Moja ya basi bora kabisa ambalo lilitoka Arusha majira ya asubuhi na mapema sana na sasa majira ya saa mbili za usiku lilikuwa linaingia ndani ya jiji pendwa zaidi nchini jiji la Dar es salaam, lilifika stendi walianza kushuka abiria mbali mbali ambapo kuna mwanaume mmoja ambaye alikuwa na begi lake mgongoni pamoja na kofia ambayo ilikuwa imeuziba uso wake vizuri alikuwa amekaa konani kabisa kwenye siti ya mwisho alibaki amekaa humo ndani mpaka pale alipo hakikisha kwamba watu wote wametoka ndipo naye alipo amua kutoka huku akiwa anaificha sana sura yake ni wazi hakuhitaji mtu yeyote yule aweze kumuona sura yake na alikuwa makini sana kwa kila hatua yake moja ambayo alikuwa anaipiga.

Alishuka kwenye gari na kuchukua usafiri wa bajaji akiwa makini sana kuulinda uso wake kwa kofia ambayo alikuwa ameivaa usoni kwake, bajaji hiyo ilimfiksha mpaka maeneo ya usalama ambapo aliomba usafiri huo uweze kumuacha huko mbele angeendelea mwenyewe na safari yake, mwanaume alishuka na kuanza kuikata mitaa ya jiji majira ya usiku wa mapema huo lakini alihisi kama kuna watu walikuwa wakimfuatilia kwa muda kidogo tangu pale alipoweza kushuka kwenye ile bajaji, aliigusa kofia yake kidogo na kutabasamu kisha akawa anaendelea na safari yake kama ilivyokuwa kawaida yake. Hatua kama saba alizozipiga alipotea kwenye hilo eneo ambalo alikuwa anaonekana yupo haukupita muda sana wakatokezea wanaume watatu waliangaza huku na huko walishangaa kutomuona mtu yeyote yule ilikuwa ni ghafla sio muda sana waliona kabisa kuna mtu hilo eneo.

“Kama ikitokea siku ukiwa karibu na huyo mtu ni kiumbe cha ajabu sana kinapokuwa kwenye uhalisia wake unapaswa kujihadhari kwa namna yoyote ile ambayo unaweza ili kuhakikisha maisha yako yanakuwa salama kama ukichezea hata sekunde moja tu ukafanya uzembe wowote basi jiandae kubadilishiwa jina lako halisi na kuitwa marehemu” ni kauli ambayo mmoja wa hao wanaume aliikumbuka vizuri siku moja wakati anapewa onyo na kiongozi wake na alionekana kuwa mkuu wa msafara huo wa watu watatu ambao walikuwa hapo usiku huo jiji likiwa limetulia mubashara.

“Jiangalieni na muwe makini hayupo mbali na hapa” aliongea ikiwa ni kuwatahadhalisha wenzake alionekana kumjua huyo mtu kwa uchache wake, bahati mbaya ni kama taarifa hiyo alichelewa sana kuitoa mmoja kati yao alikuwa anaenda chini akiwa amelainika kama tambi zilizopikwa, walimkimbilia na kumgusa walipigwa na butwaa uti wa mgongo wa mwenzao ulikuwa umevunjwa hauwezi hata kufanya kazi tena alikuwa ameshaanza kuwa wa baridi maana yake dunia hayakuwa makao yake tena.

“Vipi mnanitafuta mimi” mshtuko walioupata kwa kusikia sauti la kutisha ni kama walikuwa ndotoni, ni sauti iliyoshiba ambayo ilisikika kutoka kwa mtu ambaye alikuwa yupo nyuma yao.

“Mpige risasi kwenye mbavu haraka” aliyekuwa anapewa maagizo ya kupiga risasi huyo binadamu mwenzao utoaji wa risasi kwenye bastola yake ulikuwa mdogo sana kiasi kwamba ilimpelekea yeye kupiga magoti akiwa amejishika eneo la shingoni, yule mwanaume ambaye ndiye aliyekuwa anatafutwa alionekana kuwa na pete kwenye mkono wake iliyotumika kufanyia hayo mauaji japo haikueleweka pete imeweza vipi kuichana chana shingo ya mtu mpaka akadondoka na kupoteza maisha kwa sekunde kadhaa tu.

“Nenda kamwambie huyo aliyewatuma kwangu aje anitafute yeye mwenyewe”ni kauli moja tu ambayo aliweza kuitamka kwa mwanaume mmoja tu ambaye alikuwa amesalia na kuachwa hai kati ya hao watatu ambao walikuwa wapo hilo eneo, alibaki akitetemeka mno aliyo yashuhudia kwa wenzake kwa hizo sekunde chache kwenye mwili wake yalimfanya kuelewa nini maana ya hofu. Alimshuhudia mwanaume huyo akiondoka na kupotelea ambako alikujua yeye mwenyewe na hakuwa na cha kuweza kumfanya chochote kile, alijipapasa kwenye mwili wake baada ya kujigundua kwamba alikuwa ni mzima wa afya aliitupa bastola yake chini na kuanza kukimbia kwa nguvu sana hakuweza kuamini kama kweli aliweza kuachwa akiwa hai na mzima wa afya ya kutosha alishukuru MUNGU kwa hilo hakujua aina ya mtu ambaye alikuwa anamhangaikia usiku huo ni bora angebaki hata kuuza miguu ya kuku na kashata huko Tandika hii michezo ya wanaume alikuwa haiwezi.


Siku zilikatika, wiki ziliishaa, miezi ilienda na miaka ilikuwa inakimbia kwa kasi kubwa kama ilivyo kawaida kwa muda haujawahi kusimama hata siku moja kila siku huwa unakimbia kwa kasi, miaka mitano ilikuwa imepita tangu matukio yote hayo yaweze kutokea ndani ya Arusha na Dar es salaam. Kwenye moja ya Apartment kubwa ya kifahari alionekana bwana mmoja akiwa amesimama eneo la dirishani akiwa anaangalia nje kupitia kioo kikubwa kilichokuwa hapo akiwa anashuhudia kwa namna mji ulivyokuwa unavutia majira hayo ya usiku ulio tulia. Alionekana kuwa mtu ambaye mawazo yake yalikuwa yanakumbuka mbali sana, aligeuka na kuangalia upande wa pili ambako kulikuwa na mlimbwende kama sio mrembo kwa lugha ambayo ni rahisi zaidi, mwanamke ambaye tungesema ni sumaku kwa namna muumba alivyo tulia na kuvigawa viungo ambavyo viliufanya mwili wake kuwa sehemu ya kiburudisho cha macho kwa kila ambaye alikuwa ana uwezo wa kuona basi asingeweza kupita akakosa kuisaliti nafsi yake kwa kugeuza shingo yake na kumshuhudia huyo mwanamke jinsi alivyokuwa mzuri wa haja na alipendelewa uzuri wa kipekee ambao kwa hadithi ya neno moja moja ilitakiwa ramani nzima ya Afrika kuweza kumaliza kilomita za kumuelezea namna alivyokuwa ni mwanamke mzuri sana, sifa kubwa zilienda kwa MUNGU kwa uumbaji wake kiufupi ni kwamba MUNGU fundi sana.

Mwanamke huyo alikuwa kwenye tabasamu zito lililo mfanya meno yake ambayo yalikuwa ni meupe kwa asilimia mia moja na nukta zake yaonekane vizuri sana lakini hilo halikuwa tu la kumfanya atabasamu sana hivyo lahasha bali kiumbe kilichokuwa karibu yake ndipo lilipokuwa tabasamu lake kubwa, alikuwa akicheza na binti mdogo wa kike ambaye usingesita kusema alikuwa ana miaka miwili mpaka mitatu pale unapo muona, kama yeye alivyokuwa amependelewa kuwa mzuri basi hata yeye alimshukuru MUNGU kumpendelea mtoto mzuri kama huyo aliye mpata, aliye mfanya mpaka yeye mwenyewe asadiki kwamba hii dunia kuna watu wanabarikiwa kuwa wazuri akijisahau kwamba yeye ndiye mama wa huyo mtoto (hahahahha binadamu hawaridhiki kabisa bwana). Ilionekana kuwa moja ya familia iliyokuwa na furaha kubwa mno, hao wawili ndio ulikuwa moyo wa huyo mwanaume ambaye alikuwa pembezoni kabisa mwa dirisha kubwa la vioo akiwa anamuangalia mkewe na mwanae wa pekee wakiwa kwenye furaha kubwa mno na hilo ndilo lengo la kila baba bora kwa familia yake ni bora yeye alale njaa lakini sio kuona familia yake inalia au kutoa chozi (he was a good father indeed).

Hapo alipokuwa amesimama alikuwa anaongea na nafsi yake mwenyewe akiwa anajikumbushia namna alivyo mpata huyo mwanamke na aliweza vipi kukutana naye mpaka ikafikia hatua akawa mke wake kabisa wa ndoa. “Ilikuwa ni siku moja nikiwa nimetoka kwenye mishe mishe zangu za kila siku, kuvaa na kupendeza kila siku ilikuwa sehemu ya maisha yangu, nilibahatika kuwa miongoni mwa wale vijana waenda gym basi hata mwili wangu ulikaa vyema sana sikuwa na tatizo la kimwonekano. Ni usiku mmoja nilikuwa nimeenda na gari yangu kwenye hoteli moja japo nilikuwa makini sana kuulinda uso wangu usije ukapatikana kwenye kamera hata moja na mara nyingi nilikuwa ninatembea na barakoa pale ambapo naingia sehemu ambayo inaweza kuwa tatizo kwangu kuonyesha sura yangu.

Nilijibanza kwenye kona moja ambapo nilipata kinywaji changu ila kwa bahati mbaya sana nilijikuta sina waleti yangu ambayo ilikuwa na pesa nilihisi nimeibiwa ila nikakumbuka nitakuwa nimeidondoshea kwenye gari yangu, mhudumu alinijia juu na kusema kwamba mimi nilikuw atapeli na nisingeweza kutoka kwenda kwenye gari bila kulipia vinginevyo ilitakiwa nikamatwe kama ningeshindwa kulipa kitu ambacho kingenifanya nijulikane haraka na sikutaka hilo lifanyike lakini kwa bahati iliyokuwa njema pembeni yangu alikaa mwanamke mmoja mzuri sana tena sana ambaye nisingeweza kumuelezea nikamaliza nilishangaa ananilipia na kutabasamu hahhhaaa kilicho fuata ilibaki kuwa historia” alitabasamu sana baada ya hisia zake kumkumbusha namna alivyoweza kukutana na mwanamke huyo japo hakutaka hisia zake ziweze kuendelea kwa muda huo ili kuweza kujua kwamba ilikuaje mpaka akafikia hatua kabisa ya kumuweka ndani, alimshukuru sana MUNGU kumpendelea familia yenye furaha sana.

“MUNGU ni mkubwa sana sasa hivi hata mimi naishi maisha ya kawaida kama binadamu wengine” alitabasamu baada ya kuweza kuyatamka hayo maneno yake kisha akazamisha mkono wake mfukoni na kuitoa simu akaanza kuhangaika kuitafuta namba moja ambayo kwa muda huo ilionekana kuwa ya mhimu, baada ya kuipata alipiga ikaite kwa sekunde kadhaa tu kisha ikapokelewa.

“Halo”ni sauti kutoka upande wa pili uliokuwa umepokea simu bila shaka ilitoka kwa moja ya watu waliokuwa na njaa kali sana ndiyo sababu alikuwa tayari kuipokea simu kwa wepesi akihisi huenda ni ya chochote kitu cha kuliweka tumbo lake sawa.

“Kani uko wapi saivi?”

“Nani wewe?” sauti ya upande wa pili iliuliza kwa msisitizo mzito

“Alen”

“Whaaaaaaat?”

“Yes, uko wapi?”

“Mimi bado nipo Arusha ndugu yangu umeniharibia maisha yangu yote kwa ajili yako nilifungwa jela na kufukuzwa ka……”

“Kesho nahitaji uwepo Dar es salaam”

“Kufanya nini?”

“Acha jeuri kama umeyapatia maisha mjinga wewe wakati una shida kibao” upande wa pili mtu huyo alimeza mate kwani alikuwa ameambiwa ukweli kabisa wa maisha yake.

“Daaaah kaka sema sina nauli”

“Nakutumia, utanitafuta ukifika stendi” Baada ya simu kukatwa iliingia meseji ambayo huwa inabeba zaidi ya asilimia 99 ya furaha ya binadamu mwenye shida, shilingi laki tano ilikuwa imethibitishwa kwenye laini yake hiyo, hakuamini hicho kitu ndani ya chumba chake kidogo ambacho alikuwa ametandika godoro chini akiwa hajatia chochote tumboni alimshukuru MUNGU kwa hilo alinyanyuka na kukimbilia kwa wakala kabla mwenye pesa hajairudisha kwake, alienda kutoa pesa yote akiwa anacheka cheka njia nzima. Alienda kwenye moja ya migahawa bora sana akaagiza chakula cha bei kubwa akiwa anafidia siku alizo teseka, alikula akashiba vizuri baada ya hapo alienda club na kuchukua mwanamke mmoja mrembo sana akawa anakunywa pombe baadae aliingia naye chumbani kupunguza uzito aliokuwa nao ikiwa ni kama kulipiza kwa namna wanawake wazuri walivyokuwa wanamkataa kwa sababu hakuwa na pesa kwenye maisha yake yote basi alijisikia fahari sana siku hiyo. Asubuhi na mapema sana alikuwa ndani ya gari akiwa anaelekea zake kwenye moja ya jiji ambalo kwake ilikuwa ni ndoto kwenda kuliishi.


Huyu mwanadamu ambaye alionekana kuwa kiumbe cha hatari sana ni nani hasa?, kipi kimemfanya atafutwe sana namna hiyo? Tuna mengi sana ya kuyajua na kuyaelewa humu ndani kikubwa twende taratibu tutaelewana tu……. sehemu ya pili haina cha kukuongezea kwa sasa mpaka wakati ujao.

Bux the story teller

ChaoView attachment 2348569

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller

UKURASA WA TATU

TULIPO ISHIA UKURASA WA PILI

Alienda kwenye moja ya migahawa bora sana akaagiza chakula cha bei kubwa akiwa anafidia siku alizo teseka, alikula akashiba vizuri baada ya hapo alienda club na kuchukua mwanamke mmoja mrembo sana akawa anakunywa pombe baadae aliingia naye chumbani kupunguza uzito aliokuwa nao ikiwa ni kama kulipiza kwa namna wanawake wazuri walivyokuwa wanamkataa kwa sababu hakuwa na pesa kwenye maisha yake yote basi alijisikia fahari sana siku hiyo. Asubuhi na mapema sana alikuwa ndani ya gari akiwa anaelekea zake kwenye moja ya jiji ambalo kwake ilikuwa ni ndoto kwenda kuliishi.

ENDELEA..................................

Kani kwa mara ya kwanza alikuwa anashuka ndani ya jiji la Dar es salaam ambalo kwake lilikuwa ni geni mno hakuwahi kufika zaidi ya kusikia tu watu wakiwa wanalinakshi kwa uzuri wake wa kuvutia na umaridadi wa maisha ambayo watu waliomo ndani yake huwa wanayaishi kila siku, majira ya jioni wakati kiza kinaanza kuingia taratibu ndio muda ambao alikuwa anashuka stendi. Namba alikuwa nayo kwenye simu yake aliitoa kwenye mfuko wake kwa umakini sana na kuweza kuipiga iliita kwa mara ya kwanza na kukata, ikaitwa kwa mara ya pili kwa muda mrefu ndipo ilipoweza kupokelewa.

“Vuka hiyo lami kwa mbele utaona kuna gari nyeusi ingia humo” maelekezo aliyo yapata ilionekana mtu ambaye alikuwa akimuelekeza alikuwa anamuona moja kwa moja bila wasiwasi wowote ule basi alivuka na kweli hatua kama hamsini kutoka sehemu aliyokuwepo aliona kuna gari moja zuri sana la kifahari mno alisita kwenda ila aliamua kuufuata moyo wake na maamuzi yake, hatua mbili kabla hajafika mlango ulifunguliwa kana kwamba alikuwa akisubiriwa kwa muda mrefu kisha akaingia ndani ya gari. Ndani ya hiyo gari alikuwa amekaa mwanaume mmoja mwenye ndevu ambazo bila shaka zilichongoka na kukaa kwa usahihi kwa matunzo ambayo yalionekana kufanyika kwenye hizo ndevu, mustachi uliipamba sana sehemu ya juu kidogo ya mdomo wake na kuonekana kama alikuwa mhindi flani hivi, Kani ilimchukua kama dakika mbili kuweza kumtambua vizuri mtu ambaye alikuwa mbele yake alikuwa amebadilika mno na wala hakutegemea kama ndiye yule rafiki yake wa miaka mitano huko nyuma ilihitaji umakini wa hali ya juu na kwa mtu ambaye anamjua kiundani sana kuweza kumtambua kwamba ndiye alikuwa yeye mwenyewe.

Alen ndiye mwanaume aliyekuwa ndani ya gari hiyo ya kifahari walikumbatiana kwa furaha sana huku Kani machozi yakiwa yanamtoka kwa miaka mitano ambayo ilikuwa imepita alipitia mambo magumu sana ambayo yalimpelekea mpaka kuipoteza kazi yake.

“Ulikuwa wapi miaka yote hiyo ndugu yangu” Kani aliuliza akiwa anashangaa namna gari hiyo ilivyokuwa ya kifahari mno na hakuwahi hata siku moja kupanda wala kufikiria kama atakuja siku moja kuwa sehemu ya maisha hayo ya kifahari na kuyaishi kwenye uhalisia wake.

“Namba zinasoma kwa kasi kubwa sana ndugu yangu na miaka inazidi kukatika tu lakini wanadamu bado tupo, hilo ni swali ambalo nitakujibu siku nikipata muda ila kwa sasa nilihitaji kukusaidia ujitoe kwenye hiyo hali ya maisha ambayo ulikuwa nayo kwa muda mrefu sana nina imani umepitia shida za kutosha kwa sababu yangu mimi na hilo ndilo limenisukuma sana kuweza kulipa fadhila kwa wema wako ambao siwezi kuusahau kwa namna ulivyo nisaidia wakatii ule hakukuwa na mtu yeyote yule ambaye angeweza kusimama na kunikumbuka, kwa sasa twende sehemu ambayo ndiyo utafikia na utakuwa unakaa halafu kesho nitakupeleka sehemu ukafanye manunuzi ya nguo kidogo uanze kuendana na kasi ya mji” maneno hayo ya Alen Kani hata hakuwa anayasikia vizuri mawazo yake yalikuwa yapo mbali sana kushangaa namna mtu ambaye alikuwa naye kwenye machimbo ya madini miaka kadhaa nyuma leo alikuwa anaongea akiwa siriasi sana maisha yalikuwa yamebadilika mno kwa kiasi kikubwa.


“Ahhhh…. sawa” alijibu kwa kigugumizi, Alen alitabasamu tu kuona hiyo hali alimjua mwenzake huyo kwa ushamba hususani anapofika sehemu ambayo anakuwa haijui kabisa au ni ngeni kwenye maisha yake, alinyanyua gia na kuanza kutoka kwenye hilo eneo kwa spidi ya kawaida ikionekana wazi hakuhitaji kumuumiza mgeni wake.

“Hivi kaka wewe wazazi wako na asili yako kabisa huwa ni wapi?” ni swali ambalo lilionekana kumshtua sana Alen baada ya kuulizwa na Kani walionekana kuwa watu ambao walikutana na kusaidiana tu ila walikuwa hawajuani kiundani sana.

“Sikumbuki sana nilikuwa mdogo mno ila ninacho kijua mimi wakati naanza kujitambua nilijikuta naishi kwenye kituo cha watoto yatima mpaka pale nilipo ona kwamba nina uwezo wa kujitegemea nikaamua kuondoka hiyo sehemu nadhani hata siku ya kwanza niliwahi kukwambia hivyo” Alen alijibu lakini ni wazi hakupendezwa kabisa na hilo swali ilimbidi kufungua muziki taratibu kwenye gari akiwasha skrini ndogo ambayo iliuchukua umakini wa Kani wote na maswali yakawa yameishia hapo. Nusu saa ilipita waliingia Sinza kwenye mjengo ambao haukuwa mkubwa saana ila ulikamilika kwa mtu kuweza kujiita ana maisha mazuri ya kuvutia, mlango ulifunguliwa wakaingiza gari ndani kisha wakafunga geti, muda wote Kani macho hayakubanduka kwenye skrini ambayo ilikuwa ipo mbele ya gari mpaka pale alipokuja kushtuliwa na Alen kwamba walikuwa wamefika mwisho wa safari yao ndipo alipoweza kushuka ndani ya gari wakaongozana mpaka ndani ya nyumba.

“Kani kuanzia leo hapa ni kwako na ndipo utakapokuwa unaishi kwa sasa, yale magari mawili ambayo umeyaona pale nje ni yako yote ila kuhusu wafanyakazi utaamua wewe kama utawaleta au la itakuwa ni juu yako mwenyewe” Kani aligeuka kutoka kwenye mshangao aliokuwa nao wa kushangaa vitu vya thamani vilivyokuwepo ndani ya sebule hiyo na kumwangalia Alen kwa taharuki, hakuwa anaamini kwamba hivyo vitu humo ndani vilikuwa ni mali yake yeye na alikuwa anaruhusiwa kuvitumia kadri atakavyo, alijikuta analegea na kupiga magoti chini akiwa anatoa machozi huyo mwanaume mbele yake hakuwa ndugu, kaka wa kuzaliwa wala hawakutoka sehemu moja ya kuzaliwa ila leo ndiye aliyekuwa kama ndugu yake ndani ya jiji hili, ni binadamu wachache sana huwa wana moyo wa aina hiyo. Alen alimfuata rafiki yake huyo wa machimbo akamnyanyua na kumkumbatia.

“Kama ningekuwa na uwezo ningeurudisha muda nyuma uzaliwe wakwanza kwenye familia yetu kisha nifuate mimi nikuite kaka wa damu kabisa tumbo moja nadhani ningekuwa mwanadamu ambaye ningekuwa nina bahati kuliko binadamu yeyote yule hapa duniani, asante sana kaka” Kani aliongea kwa kumaanisha macho yake yalitoa ishara za msisitizo kuhusu hilo jambo wakati huo alikuwa amekumbatia sofa moja maridadi sana ambalo lilipita kwenye mkono bora wa fundi seremala.

“Hahahahahah Kani bado hujaachaga masiara yako, hivi ni vitu vidogo tu usijali, wewe ndiye binadamu pekee uliuona umuhimu wangu wakati ule mimi ni kapuku sina hata mia mbovu, ukanipeleka mpaka kazini kwako na kunisaidia sana sehemu ya kulala kwahiyo haya ninayo yafanya wewe ndiye unastahili pongezi kwani huenda kama sio wewe mimi leo nisingekuwa hapa” Alen aliongea kwa kumaanisha mashavu ya Kani yalituna kwa cheko kisha akakaa chini akiwa ana furaha sana, kilicho fuata alionyeshwa mazingira yote ya nyumba na namna ya kutumia vitu mbali mbali humo ndani, vyakula vilikuwa vipo vya kutosha kwenye friji alikula sana baada ya Alen kuondoka na kuahidi kwamba angekuja kesho yake kumchukua akabadilike kuanzia mavazi mpaka muonekano.

Sauti za kengele ndizo zilizo weza kumshtua kutoka kwenye usingizi mkali na mnono ambao alikuwa amelala, hakuwahi kwenye maisha yake kulala sehemu nzuri na bora kama hiyo leo ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kabisa hakuhitaji kuukosa usingizi huo hata kwa sekunde moja, alimlaani sana mtu ambaye alikuwa amehusika na kuikatisha safari yake ya usingizi, alitoka taratibu sebuleni na kwenda kuufungua mlango, alitabasamu baada ya kumuona Alen akiwa kwenye moja ya suti nzito mno hakuhitaji maelezo mengi alimhitaji watoke sasa akatengenezwe. Walipanda kwenye gari haraka sana wakaitafuta moja ya saloon kubwa Kani alienda kutengenezwa kuanzia uso wake na kufanyiwa masaji na watoto wakike ambao walinona mno, mate yalikuwa hayamkauki mdomoni na aliapia angerudi kuwatafuta, baada ya kumaliza safari yao ilienda kuishia ndani ya Mlimani City ambako walipanga kwenda kununua nguo za kutosha kwa ajili yake. Walifika na kushuka kwenye gari walianza taratibu kutembea kuelekea ndani Alen akiwa ametangulia mbele wakati anayakaribia malango ya kuingilia alijifanya kama anaishika kofia yake vizuri akaikutanisha mikono yake miwili na kuibonyeza kidogo tu saa ambayo ilikuwa kwenye mkono wake ghafla umeme kwenye sehemu zote ambazo zilikuwa karibu na hapo walipokuwa ulikata kwa dakika moja na kurudi haraka sana halikuwa jambo la kawaida liliwashangaza watu wote ambao walikuwa wapo karibu kutokana na sehemu hiyo kuto katika umeme hata kama umeme wa tanesco ungekata basi huwa kuna jenereta za kutosha ambazo huwa zinafanya sehemu hiyo kuwa yenye umeme muda wote.


Baada ya kumalizana na shoping yao ndani ya Mliman City siku ile maisha yaliendelea kama kawaida Kani akijitahidi sana kuwa mwenyeji wa jiji hili na kwa msaada wa rafiki yake Alen haikuwa kazi ngumu sana ilifika sehemu akawa ni mwenyeji kila sehemu japo alikuwa ana maswali mengi sana juu ya maisha ya rafiki yake kwanza alikuwa haelewi Alen alipoteaje ndani ya Arusha na kuja kuwa mtu tajiri kiasi hiki? Alijaribu kujijibu mwenyewe kwamba huenda mwanaume huyu alibahatika kuyapata madini lakini alilipinga hilo kwa sababu ilikuwa sio rahisi mtu kutoka na madini ndani ya yale machimbo na hata siku ambayo rafiki yake huyo aliondoka alikuwa kwenye hali mbaya mno kiasi kwamba asingekuwa na uwezo wa kufanya hicho kitu, swali la pili lilikuwa ni maisha ya mtu huyo kiujumla muda wote ambao alikuwa amekuja ndani ya jiji la Dar hakuwahi kabisa kuijua sehemu ambayo alikuwa akishi Alen lakini swali la tatu hakuelewa kwanini rafiki yake huyo alikuwa anakwepa sana kupiga picha kwenye uso wake na alikuwa makini sana kuweza kulikwepa hilo jambo hata hivyo aliamua kuuachia muda uamue kwa sababu hakuhitaji kulazimisha mambo wakati mhusika yeye mwenyewe hakuwa tayari kabisa kumwambia japo alitamani sana kuyajua majibu ya maswali yake.

“Kani nina imani utakuwa na maswali mengi sana juu yangu kwamba nimeyapataje haya maisha, kwanini sijawahi kukupeleka nyumbani? Muda ukifika utajua kila kitu ila kwa leo nataka kwa mara ya kwanza ukaione familia yangu ili hata siku nikipata tatizo wapate mtu wa kuwafariji” ni maneno ambayo yalimuacha Kani mdomo wazi alitetemeka kidogo hicho ndicho kitu ambacho alikuwa anakiwaza muda sio mrefu kwenye akili yake sasa alijiuliza huyo mtu kwanini amwambie hayo mambo muda huo kwamba alikuwa ameshajua anacho kiwaza? Hakupata jibu.

“Itakuwa ni vizuri sana ndugu yangu maana sijui hata familia ya rafiki yangu mpaka najisikia aibu muda mwingine” alijibu tu kama kujifariji ila kiuhalisia hata alicho kijibu alikuwa hajakijua, Alen alimwangalia kwa umakini sana Kani kiasi kwamba alikuwa ni mtu ambaye alikuwa anayapima macho yake kisha akatabasamu, waliingia kwenye gari na kuondoka kwa mwendo wa taratibu kabisa. Maeneo ya posta pembezoni kabisa mwa bahari ndipo gari ilipo enda kusimama nje ya mjengo mmoja ambao bila shaka mmiliki hakuwa mtu wa kuhesabu pesa kwa mkono lazima mashine ndizo zilikuwa zinafanya hiyo kazi ya kuhesabu ndipo walipoweza kufika, ilikuwa ni miongoni mwa majumba ya kifahari sana ndani ya eneo hilo Kani aliutazama huo mjengo bila kuumaliza alijikuta anameza mate na kikiri moyoni kwamba ukiachana nayeye kudumu hapa duniani ila dunia hii hii ina watu ambao walikuwa wanaishi kweli.

Baada ya kuingia ndani walikaribishwa na tabasamu la mwanamke mmoja mzuri mno ambaye alienda kumkumbatia Alen na kumpiga busu zito kwenye paji lake la uso.

“Welcome back my husband” ni sauti tamu ambayo ilipenya kwenye ngoma za masikio ya Kani na kujikuta akitabasamu akiwa haamini yule rafiki yake kapuku wa machimboni leo alikuwa anapokelewa na sauti nzuri laini kama hiyo mbele yake maisha yalikuwa yanakimbia mno, naye hakunyimwa haki ya kuisikia sauti hiyo baada ya kugutuliwa na sauti

“Karibu nyumbani shemeji” alijikuta anababaika hata kujibu huku akipokea mkono wa mwanamke huyo kabla hajakaa sawa ilisikika sauti yenye kicheko cha kitoto iliyokuwa na furaha sana ikiwa inakuja upande wao.

“Daddy” mtoto wa Alen alikuja na kumkumbatia baba yake kipenzi, ni kitendo kilicho muacha Kani mdomo wazi hakuweza kuamini kama rafiki yake alikuwa amefikia hatua mpaka ya kuwa na mtoto kabisa, alijikuta anainama chini kwa mshangao, kwake dunia ilikuwa ina siri kali ila wanadamu ndio walikuwa wenye siri zaidi ya mifuko iwekwayo ndani ya nguo ya mtu.

Ni mwanzo kabisa ndani ya GEREZA LA HAZWA ukurasa wa tatu tunaweka nukta tupumzike kidogo.

Bux the story teller.
IMG_20220904_175626_901.jpg


Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom