George bush akiwa mapumzikoni uingereza!!!!!!!!!!!

Kamaka

JF-Expert Member
Jun 7, 2010
563
33
George Bush alikwenda mapumzikoni Uingereza na akapata nafasi yakukutana na malkia Elizabeth..Malkia akataka kupima akili ya Bush akamuuliza hivi;Mtoto aliyezaliwa na Baba na Mama yako lakini si kaka wala dada yako anaitwa nani? Bush akawaza we akakosa jibu.Basi Malkia akamuita Prince Charles akamuuliza vile vile. Prince charles akajibu “Ni mimi”.Malkia akaridhika na jibu hilo sahihi, Basi Bush akarudi Amerika akamuuliza Mstaafu mwenzake Dick Cheney: Mtoto aliyezaliwa na Baba na Mama yako lakini si kaka wala dada yako anaitwa nani? Cheney akawaza we akakosa jibu, Ikabidi Bush amuagize Cheney aende kumuuliza Obama!Cheney akafika ikulu akamuuliza Obama : Mtoto aliyezaliwa na Baba na Mama yako lakini si kaka wala dada yako anaitwa nani? Obama akajibu; “Ni mimi”. Dick Cheney akaridhishwa na jibu na akarudi mbio kwa George Bush akamwambia nimepata jibu sahihi NI OBAMA!!!!! Bush akamwambia ACHA UPUMBAVU NI PRINCE CHARLES!!!!!!
 
Back
Top Bottom