Geita (gold exploration in Tanzania) hazina iliyofichika.

Taifa_Kwanza

JF-Expert Member
Sep 3, 2010
443
86
Miaka kama kumi na moja iliyopita, nilikutana na jamaa fulani maeneo ya Mwanza
kwenye counter ya Bar moja tukipata moja moto moja baridi.

Ghafla, tulizoena na kuanza kuongea mambo meeeengi sana, Mojawapo ni experience
yake ya kufanya Kazi kwenye Mgodi wa Geita Gold Mining akiwa ni mmoja kati ya watanzania
wa kwanza kabisa kuajiriwa katika Mgodi huo.

Yeye aliajiriwa kama Driver, elimu yake ikiwa ni form four, aliniambia alikuwa ni mmoja wa watanzania
wa kwanza kabisa kuendesha mamitambo ya kuchimba ardhi kuzamia Dhahabu chini ya Ardhi.

Katika mengi aliyonieleza leo naomba kupata uhakika wa hili kwa wenye details husika, Kwamba,
mji wa Geita maana yake ni Gold Exploration in Tanzania, Ulipewa jina hili na watafiti wa madini wa
Kizungu miaka mingi iliyopita kama sio nyakati za vita vya kwanza vya dunia.

Alinieleza kwamba, habari hizi alipewa na Kijana wa kizuru ambaye ndio alikuwa trainer wao
kwenye shughuli za uchimbaji wa madini, na kwamba hiyo ilikuwa ni siri kubwa sana miongoni
mwa jamii za kizungu, Kwamba ufahamu aliokuwa nao ni kwamba, Geita ni eneo lenye utajiri
wa Dhahabu kuliko eneo lolote lile duniani, na kwamba eneo hilo liko Marekani na wamarekani
hawakuwa tayari kuchimba dhahabu hiyo mpaka pale dhahabu itakapopongua maeneo
mengine duniani hasa South Africa, Ghana n.k, kwamba hakuwahi kufikiria geita
inaweza kuwa sehemu yoyote katika Ardhi ya Africa kutokana na msimamo ambao uliishapitishwa
wa kutochimba dhahabu eneo hilo.

Mzuru huyo, kwa namna iliyokuwa ikiashiria kwamba anatoa siri kubwa sana moyoni, mwake
alimueleza rafiki yule kwamba, yeye Binafsi machozi yalimtoka alipokuja kukuta kwamba Geita
ni sehemu ya ardhi ya Africa, tena Wakazi wa eneo hilo wakionyesha kwamba hawakuwahi
kujua kabisa kwamba chini ya ardhi hiyo kulikuwa na ADHINA ILIYOFICHIKA KWA MIAKA
MINGI SANA KWENYE MIOYO YA WAZUNGU.

Ninaandika maelezo haya, huku roho ikiniuma sana, Hasa nikikumbuka majuzi John Mnyika
aliuliza bungeni kama Madini yenu yana laana.

Mwenye taarifa zaidi naomba anisaidie. Ninakusanya hasira.
 
Hata ukiwa na hasira zaidi ya watu wa nyamongo wanaopigwa risasi na kuambiwa ni majambazi haisaidii.nchi hii ni tajili sana ila kumbuka usemi huu nakama unauamini utakupoza 'penye miti mingi hapana wajenzi'.pole ndugu.
 
Hata ukiwa na hasira zaidi ya watu wa nyamongo wanaopigwa risasi na kuambiwa ni majambazi haisaidii.nchi hii ni tajili sana ila kumbuka usemi huu nakama unauamini utakupoza 'penye miti mingi hapana wajenzi'.pole ndugu.
pole sana mapujds hali hiyo naona sasa ndo inaenda ukingoni so keep on waiting for a bit change is coming..
 
Unachosema ni kweli, mji wa Geita wote umejengwa juu ya dhahabu. Lilishawahi kutolewa pendekezo kwamba mji wa Geita uhamishwe, lakini tatizo ni kwamba wapi pa kuuhamishia, na pia fidia kubwa sana inayohitajika kulipwa kuwahamisha watu.
 
Geita has been associated with minerals particularly gold long time ago

Geita is a town in Tanzania of approximately 40,000 people, located 90 kilometers west of Mwanza. Geita first came into prominence as the site of a German colonial gold mine. A German gold prospector discovered the mineral in the early 1900s in the hills surrounding modern-day Geita town. This and other discoveries triggered a gold rush in the surrounding area, attracting German and native prospectors alike. The colonial government established a mine to exploit 'Bismarck Reef'. Mining activities significantly declined, however, when Germany ceded control of its colonies to the British after their defeat in World War I.
Geita regained prominence in the mid to late 1990s when the Tanzanian government opened the mineral sector to foreign investment. A number of medium to large-scale mining houses, including Ashanti and Anglo-American, conducted extensive exploration activities in the surrounding areas. The most significant outcome of those activities was the construction of the Geita Gold Mine, now owned by AngloGold Ashanti. The Geita Gold Mine is Tanzania's largest gold producer.
Gold rushes continue to occur in areas surrounding Geita, mainly in and around Rwamagasa and Matabe. These gold rushes have attracted tens of thousands of prospectors from all around the country. Being subsistence miners, their activities are highly unregulated, resulting in dangerous mining practices and considerable environmental destruction, not the least of which are increased mercury pollution and extensive deforestation.

Map of Mwanza's Districts


Geita became a region, and the regional seat of the new Geita Region, on January 1, 2011.
 
Ulipokosea ni pale tu ulipoweka Tanzania badala ya Tanganyika, it makes sense or mere coincidence!
 
Wabongo bana hii tabia ya conspiracy theories sijui itaisha lini? Anyways asili ya jina Geita ni geti lililokuwepo hapo enzi za mkoloni katika barabara ya Biharamulo-Mwanza, geti lilikuwa likiitwa Get A ambayo kwa ndugu zangu wasukuma wakawa wanaitamka Geeeta. Sasa huyo aliyekuambia kwamba sijui ni Gold Exploration Tanzania simply alikudanganya. Sehemu ambayo kuna proven gold reserve nyingi na ndiyo panapochimbwa kwa sasa ni Nyankanga. Sasa hiyo ya Geita mjini sijui exploration ilifanyika lini na nani? Ikumbukwe pia wakati makampuni kama Samax na Sutton resources yalipokuwa yanafanya explorations miaka ile ya tisini geita town ilikuwa na population ya watu kama 2000 tu, na hicho unachosema kama kingekuwa kweli mji ungehamishwa tu. Ila so far hiyo ni habari ya kijiweni na inaishushia hadhi JF

Geita ni eneo lenye utajiri
wa Dhahabu kuliko eneo lolote lile duniani, na kwamba eneo hilo liko Marekani na wamarekani
hawakuwa tayari kuchimba dhahabu hiyo mpaka pale dhahabu itakapopongua maeneo
mengine duniani hasa South Africa, Ghana n.k, kwamba hakuwahi kufikiria geita
inaweza kuwa sehemu yoyote katika Ardhi ya Africa kutokana na msimamo ambao uliishapitishwa
wa kutochimba dhahabu eneo hilo
.

Yaani huu ni uongo ambao tulikuwa tunaelezwa enzi za kikomunist mara ooh Tanzania inaongoza duniani kwa upelelezi, mara pale Dar Airport kuna madini ya kumwaga, mwanza airport pia. Nashangaa to this date tunasema tuko kwenye information age lakini bado uongo uongo kama huu unakuwa entertained. Yaani Geita ina dhahabu kuliko South Africa, kuliko Kalgoorlie, Mali???????????? Duh!!! cry my beloved country. And just for a fact and your information nilikuwepo Geita toka mwaka 1992 mpaka 2001. Hakujawahi kuwa na trainer wala mfanyakazi mzulu. There was only a zulu guy with Stanley Drilling company and he was just a driller not a trainer. Na such info is usually not understood or known by drillers but geologists. Let's move on....
 
Back
Top Bottom