Sasa bila huyo mfanyabiashara ku brainstorm na kufanya biashara inayomuingizia pesa unahisi Atakusanyaje kodi kwa niaba ya serikali?
Ama unahisi Biashara tu ni uteuzi unamaliza chuo unawekwa pale unakuwa mfanyabiashara, kulishwa mnalishwa ila hata shukran tu hamna?
Nimekupa tu mfano Wafanyabiashara walipogoma kuuza Korosho nje nini kilitokea? korosho hazikudoda?
-wa fanya biashara wakubwa ambao mauzo yao ya zaidi Bilioni 20 wana contribute Trilioni 11 sawa na asilimia 40 na kitu idadi yao wapo 158 tu.
So kuna Watu 158 wana contribute karibia nusu ya Makusanyo ya Nchi, Lami unayotembelea, Mshahara unaolipwa, Taa ya barabarani inayokumulika, Fly over unayoisifia, Treni unayopanda, Ukiona V8 linapita, Ukiskia Kina Musukuma wa naongea Bungeni, Ukiona sijui Maghorofa ya Serikali, Pikipiki za ma Afisa kilimo hadi zile chaki za shule za Serikali ujue kuna Watu 158 hawa wame contribute karibia nusu.
Source
Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2023/24 ni Sh44.39 trilioni huku TRA ikitarajiwa kukusanya mapato ya kodi ya Sh26.7 trilioni, kati ya hizo Sh11.98 trilioni sawa na asilimia 43 ya makusanyo...
www.mwananchi.co.tz
-Hapo bado huja weka Wafanyabiashara wa kati ambao ndio wengi zaidi wenye Milioni Mia kadhaa hadi bilioni 19.
Hivyo mkuu Zunguka unavyotaka kuna watu wachache wanaendesha hii nchi, wengi wetu humu tupo tupo tu tunamaliza soli za Viatu.