GDP inamaanisha kiasi Cha pesa tulichonacho katika taifa zima?

ndege JOHN

JF-Expert Member
Aug 5, 2015
19,565
44,756
Nimeona katika data za bank ya dunia kwenye Google kwamba GDP ya Tanzania kwa 2020 Ni dollar 62.41 billion..sikuzingatia Sana shuleni mambo ya accountant na finance au pengine nimesahau maana kiukweli sijui GDP Inatafutwaje ila swali langu la msingi kabisa Ni nataka kujua Kama GDP ndio jumla ya fedha ambayo Kama taifa tunayo yaani mikoa yote ukijumlisha pesa ambayo iko bank,hazina na kwa wananchi wote.Na je ile fedha ambayo husomwa Kama BAJETI ya serikali kwa mwaka husika ni Kama ASILIMIA ngapi ya fedha yote nchini.yaani nataka kujua wanaposema kwa mwaka BAJETI itakuwa trillion 36 je hio ndio fedha ambayo Ni jumla kuu ya hela zote zilizo mifukoni kwetu na zilizo kwenye mifumo yao??na swali langu la mwisho Ni je wanawezaje kujua net amount ya fedha tulizonazo wakati kuna hela zinapotelea let's say kuungua moto hazitakuja kuwepo Tena kwenye mzunguko japo wao watajua Bado zipo mifukoni mwetu.
 
Sio pesa iliyopo kwenye mzunguko.
Mfano tukizalisha sana tukauza njee pato linaongezeka.
Ukichukua pato lote la mwaka husika ukagawia idadi ya watanzania wote ikija zaidi ya usd 1006 hapo inamaana tuko uchumi wa kati.
 
Hilo ni pato la ndani kwa huo mwaka
UNAMAANISHA kwa mfano nimefanya export nikalipwa dollar so nikiingia nayo tu nchini ndo tayari itakuwa katika GDP?na je BAJETI ikiwa labda trillion 36 kwa mwaka je inamaanisha hio hesabu inapigiwa mpaka pesa ambayo sisi wananchi tunayo yaani mifukoni kwetu na kwenye account au hio trillion 36 watakaokusanya kufanyia matumizi na maendeleo ndo jumla yote...so kwa haraka haraka nambie hata kwa makisio tu tuna Kama shingapi yaani trillion 100-200?200-300? Au 36-100?
 
Kuhusu bajeti hiyo ni mipango na sio matumizi. Kumbuka wewe hapo unaweza panga huu mwaka utanunua boda boda lakini ukashindwa kununua kutokana na kukosa pesa.
Hivyo hivyo kwa serikali inaweza kukadiria bajeti trillions 36 lakini ikija kukusanya mapato, mikopo na misaada isifanikiwe kufikisha hiyo trillions 36
Soo unakuta inafeli kutekeleza mipango kwa asilimia 100
 
Kuna vitu viwili hapo vya kutofautisha yaan National income ( Pato la Taifa ) na public finance ( fedha za umma humu Kuna Kodi etc) .kwa lugha rahisi unaweza sema Pato la Taifa ndio hiyo GDP yaan wamaanisha Ni thamani ya jumla ya bidhaa na huduma zilitotolewa na kuzalishwa kwa mwaka husika.mfano final product ya mahindi Ni unga ,so inachukuliwa THAMANI ya unga inakwenda kujumuisha na mazao mengine na bidhaa zingine na huduma zote ndio tunapata total GDP. Hilo ndio Pato la nchi linavopatikana

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Serikali haingalii pesa watu walionayo mfukoni inapopanga pajeti.
Lazima ujue kila serikali inavipaumbele vyake inapopanga bajeti maji, elimu, umeme etc
Na ili bajeti itekelezeke serikali inahitaji pesa so gvnt inavyanzo vyake vya mapato
Kodi(TRA ushuru, faini), mikopo, misaada, govnt bond etc
Lazima ujue pia wakati inapanga bajeti unakuta bado haijaanza kukusanya hayo ni makadirio so kwa hivyo vyanzo unaweza kuta ilipanga trillions 36 lakini ikaambulia trillions 30 so kunavitu unakuta inashindwa kutekeleza kulingana na hali halisi
 
Nimeona katika data za bank ya dunia kwenye Google kwamba GDP ya Tanzania kwa 2020 Ni dollar 62.41 billion..sikuzingatia Sana shuleni mambo ya accountant na finance au pengine nimesahau maana kiukweli sijui GDP Inatafutwaje ila swali langu la msingi kabisa Ni nataka kujua Kama GDP ndio jumla ya fedha ambayo Kama taifa tunayo yaani mikoa yote ukijumlisha pesa ambayo iko bank,hazina na kwa wananchi wote.Na je ile fedha ambayo husomwa Kama BAJETI ya serikali kwa mwaka husika ni Kama ASILIMIA ngapi ya fedha yote nchini.yaani nataka kujua wanaposema kwa mwaka BAJETI itakuwa trillion 36 je hio ndio fedha ambayo Ni jumla kuu ya hela zote zilizo mifukoni kwetu na zilizo kwenye mifumo yao??na swali langu la mwisho Ni je wanawezaje kujua net amount ya fedha tulizonazo wakati kuna hela zinapotelea let's say kuungua moto hazitakuja kuwepo Tena kwenye mzunguko japo wao watajua Bado zipo mifukoni mwetu.
Thamani ya huduma na bidhaa zilizozalishwa nchini kwa kipindi cha mwaka mzima. Maana inahusisha bidhaa zote hata zitakazouzwa nje thamani yake huwa ni sehemu ya GDP, lakini pia thamani ya huduma zote zilizotolewa nchini kwa kipindi cha mwaka mzima.
GDP ya Tanzania huonekana ni ndogo kwa sababu bidhaa nyingi haziingizwi kwenye mfumo rasmi malipo unaoweza kusomeka. Mfano nauli za bodaboda, nauli za daladala, bidhaa za wajasiriamali, mazao ya wakulima hasa ambayo huuzwa kwenye masomo katika mfumo usiyo rasmi.
Hali kadhalika si sahihi kukubali kwamba watanzani zaidi ya nusu wanaishi chini ya dola moja kwa siku wakati huo watanzania walioko vijijini hakuna anayeshinda njaa, hula mihogo, viazi asubuhi, hula ugali na wali mchana au usiku ambavyo vyote hivyo hawanunui bali na mazao yao waliolima. Kwa kijijini familia ya watu sita inaweza kutumia elfu 5000 kwa wiki kwa mahitaji wakati huo imekula milo yote pasipo kukosa hata mlo mmoja. Ajabu sana wakati huo kuna watu wanakuja na Takwimu uchwara wanasema watanzania wanaishi chini ya dola moja kwa siku.
 
Kimsingi Tanzania kuna huduma na bidhaa nyingi sana zinazozalishwa nchi haziko kwenye mfumo rasmi wa malipo.
 
Thamani ya huduma na bidhaa zilizozalishwa nchini kwa kipindi cha mwaka mzima. Maana inahusisha bidhaa zote hata zitakazouzwa nje thamani yake huwa ni sehemu ya GDP, lakini pia thamani ya huduma zote zilizotolewa nchini kwa kipindi cha mwaka mzima.
GDP ya Tanzania huonekana ni ndogo kwa sababu bidhaa nyingi haziingizwi kwenye mfumo rasmi malipo unaoweza kusomeka. Mfano nauli za bodaboda, nauli za daladala, bidhaa za wajasiriamali, mazao ya wakulima hasa ambayo huuzwa kwenye masomo katika mfumo usiyo rasmi.
Hali kadhalika si sahihi kukubali kwamba watanzani zaidi ya nusu wanaishi chini ya dola moja kwa siku wakati huo watanzania walioko vijijini hakuna anayeshinda njaa, hula mihogo, viazi asubuhi, hula ugali na wali mchana au usiku ambavyo vyote hivyo hawanunui bali na mazao yao waliolima. Kwa kijijini familia ya watu sita inaweza kutumia elfu 5000 kwa wiki kwa mahitaji wakati huo imekula milo yote pasipo kukosa hata mlo mmoja. Ajabu sana wakati huo kuna watu wanakuja na Takwimu uchwara wanasema watanzania wanaishi chini ya dola moja kwa siku.
Umeiweka vizuri..
 
Back
Top Bottom