Hivi karibuni hili gazeti limekuwa na Tabia ya kutunga habari sijui kwa maslahi ya nani.
mtakumbuka wiki iliyopita iliandika habari na ikidai kumnukuu waziri wa nishati na madini mh.Sospeter Muhongo kuwa serikali ina mpango wa kuuza hisa zake kwa 49%, Mara serikali ikakanusha habari hizo tena ikaenda mbali zaidi kwa kukana hata waziri kuzungumza na mwandishi yeyote wa gazeti hilo.
Kama hiyo haitoshi juzi tena wamekuja na habari ya serikali eti imesitisha ujenzi wa bandari mpya ya bagamoyo lakini muda si mrefu nimemuona waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano mh.Makame Mbarawa kwenye taarifa ya habari ya TBC1 akikanusha habari hiyo ya gazeti la citizen.
na kueleza kuwa mchakato unaendelea kama kawaida ikiwa ni pamoja na ulipaji fidia kwa watakaopisha mradi huo pia wataalam wetu na wa nchi tunazoshirikiana nazo katika mradi huo kutoka nchi za China na Oman wanaendelea na kazi ili kufanikisha ujenzi huo,sasa sijui hili gazeti lina mkakati gani juu ya nchi yetu.
Natoa wito kwa serikali kulifuatilia ikiwezekana walifutilie mbali maana naona wana lao jambo.