Gazeti la mwana halisi linastahili pongezi!

:A S thumbs_down:Kwakweli nawakubali Mwanahalisi-Bravo Mwanahalisi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!:clap2:
 
huku kijijini kwangu halijafika halafu website yao sijui kama iko hai au la.........

lakini huwa nawasifu sana
 
Mambo mengine hayana ubishi. Raia Mwema, wanahalisi , mwananchi wanastahili pongezi tu kwisha. Huyo anyesema wamefanya kazi yao hawastahili pongezi ana problem upstairs, ila sishangai maana wanasociolojia wanasema criminals are born. Mtu anapingana na mawazo ya watu wengine wooote, huyu yeye ni tatizo, hana matatizo bali yeye mwenyewe ni tatizo. hongera sana Mwanahalisi
 
NNasubiri wakianza kuichambua CHADEMA kama karanga waanze kuitwa hawa hawa kuwa si mashujaa


maana ushujaa kwa baadhi ya watu ni kusifia Chadema na viongozi wake na kuitusi serikali na waandamizi wake
 
NNasubiri wakianza kuichambua CHADEMA kama karanga waanze kuitwa hawa hawa kuwa si mashujaa


maana ushujaa kwa baadhi ya watu ni kusifia Chadema na viongozi wake na kuitusi serikali na waandamizi wake

ivi wewe unaumwa nin?ujioni kama una matatizo unafikiri humu nisehemu ya kutafuta mabwana
 
mkuu kuna habari gani mkuu, huku mikoani bado halijafika, nitupie headline
Naomba tafadhari mwenye Gazeti la Mwana halisi ambaye ana uwezo wa kuscan ukurasa wa kwanza na wa pili, hasa ile Document ya Rex Attorneys abandike hapa jamaa zetu wa mikoani wahabarike.Mbarikiwe!!!!!!!
 
Mtu anapofanya vizuri ni ungwana kumpongeza, Mwanahalisi wanastahili pongezi za dhati. Pamoja nao wapo Raia Mwema na Mwananchi bila kusahau the East Africa ambao ndio walioiweka vizuri article kuhusu Dowans na Rostam Azizi katika toleo lao la Jumatatu hii.

Hiyo habari ipo wazi kwenye hukumu ya ICC inayotutaka tumlipe huyo ponjoli hiyo 94bn/=, lakini magazeti mengine yamekazania personalities za kina Sitta, Mwakyembe vs Lowasa na Rostam badala ya kuzama kwenye hukumu kisha mtu aje na article iliyoenda shule kama hiyo ya East Afrika Jumatatu na Mwanahalisi leo. Raia Mwema ya leo bado sijaiona.

Article ya East Africa na Mwanahalisi katika matoleo yao ya wiki hii kuhusu Rostam na Dowans ni ujumbe tosha kwa magazeti mengine nchini, hususani Tanzania Daima ambalo hivi sasa limejibainisha kuwa kundi moja na kina habari leo, uhuru, mtanzania na raia. WAANDISHI WA HABARI BADILIKENI, jifunzeni kwa wenzenu Mwanahalisi, Raia Mwema, Mwananchi na East Africa
Magazeti mengine hawawezi maana wanafuata sera za Maboss. Wewe ulitegemea RAI litazimika kwenye ulingo wa harakati?? Tusiwalaumu maana wanaangalia mkate wa watoto. Waropoke waone kazi itakuwa basi. Kama wanakereketwa wajitoe wajoin media house zingine mbona nyingi siku hizi.Wapeni pole!!!!!!!!!
 
wanatumia sehemu kubwa ya Bongo zao kufikiri na si kuripoti kama yale mengine, watanzania wengi tukiongozwa na Kikwete hatutumii hat theluthi ya BONGO zetu kutafakari na kuyaona mambo zaidi ya vile yalivyo, TUBADILIKE! TUSIMUIGE KIKWETE &Co. tutapotea. PONGEZI BWANA KUBENEA:clap2::clap2:
 
SAFI SANA TIMU YA MWANAHALISI HASA KIJANA EZEKIEL KAMWAGA ANATISHA MNO KWA HABARI ZAKE ZA KIUCHUNGUZI !!!!!:clap2:
 
Gazeti la mwanahalisi pamoja na Raia Mwema kama ukiyasoma haya magazeti kwa umakini mzuri kweli unaweza kwenda pale Ikulu na ukafanya fujo kwa kuzingati tu madudu wanayoyafanya viongozi waliochaguliwa na walala hoi wa nchi hii! KEEP IT UP JENERALI TWAHA ULIMWENGU /SAED KUBENEA!:clap2:
 
wamefanya kazi yao,pongezi ya nini.Watanzania tunapotea kwa kukosa maarifa kidogo,hiyo ndio kazi ya gazeti magazeti yanatakiwa yaige hapo sasa ukisema pongezi tena maana yake unaondoa uhalisia wa kazi za gazeti.HIYO NI KAZI YAO NA HAWAHITAJI PONGEZI YOYOTE

Ni kweli kazi yao ila wanapohatarisha maisha yao kwa mafuaa ya taifa wanabidi kupongezwa! Au unataka kusema kazi yao ni kumwagiwa tindikali??? Hiyo siyo kazi yao, ila mazingira ya ujasiri wao unawafikisha hapo! Wangapi wanaujasiri huo? Mtu yeyote anapongezwa akifanya jambo zuri, hata humu kwenye JF unapewa Thanks ukiandika thread nzuri! Lucy Mallya amepongezwa kwa kufaulu na kushika No. 1 kwenye matokeo ya Form IV, ila ni kazi ya mwanafunzi kufaulu. Huo ndiyo utamaduni wetu sisi watanzania.
 
Ndugu zangu wana JF mtu akifanya kazi nzuri anastahili pongezi. Tena ikiwa kazi ya utaalam anapewa award. Hili gazeti la mwana halisi linafanya kazi nzuri kabisa,hata kama ni biashara, maana linafanya watu in certain quarters hawalali.

Hiyo inaitwa investigative journalism ya Bwn Kubenea and company.

Hivyo nawaomba wana JF Hawa vijana tuwatie moyo kwa kazi hii ya kujituma na risk. Kumbuka yeye na Ndg yangu Ndimara waliwahi kumwagiwa tindi kali!!!!!!! Huo sio utani maana yake ilikuwa nia ya wahujumu ni kuwapofusha macho ili wasione waache kuandika. Lakini wanazidi kufukua uozo zaidi na hawana woga wa kutaja mafisadi wahusika moja kwa moja.

Isiwe wanapigana vita ya peke yao kumbe tutafaidi Watanzania wote tukishinda, bila kujali dini kabila wala chama cha siasa. Tuwapongeze tafadhari tubuni mbinu ya kuwatia moyo!!!!!!!!!!!!!!!! (Soma; Mwana Halisi Na.227 Juma Tano Feb 2-8, 2011)
tuambie ukaribu uliopitiliza kati ya mfanyabiashara-FREEMA MBOWE na mhariri- KUBENEA una maslahi gani kwa jamii yetu.
ukinipa jibu la uhakika utaniondolea utata unanikabili.
jiulize huyu mtu ana ugomvi gani na KABWE ZITO..............
 
Limeandika.....ANAYEDAI PESA ZA DOWANS NI ROSTAM!!!!!!!!
 
tuambie ukaribu uliopitiliza kati ya mfanyabiashara-FREEMA MBOWE na mhariri- KUBENEA una maslahi gani kwa jamii yetu.
ukinipa jibu la uhakika utaniondolea utata unanikabili.
jiulize huyu mtu ana ugomvi gani na KABWE ZITO..............

Nadhani hapa point ni kinachoandikwa kina manufaa kwa jamii ? au kina ukweli ?, hayo mengine ya behind the scenes sidhani kama yana maana sana...., after all siku hizi watu tuna akili zetu za kusoma kitu na kuchanganua.., sio kusoma kama Bible
 
Back
Top Bottom