Nasikitika sana kwa kushidwa kazi aliyopewa gavana wetu wa bank kuu Florens Luoga. Huyu gavana ni chaguo baya sana ambalo limewahi kutokea. Tujue tu kwamba huyu professor ni mwanasheria na sio mwana uchumi au mhasibu. Nashauri apewe Prof Mussa Assad kwa muda wa mpito.
Sababu moja ni kwamba bank kuu imepunguza riba za t-bills mpaka 7% kwa lengo la kupunguza mikopo ya bank za biashara ili ziwe 10%. Mara nyingi bank zina weka 2%-3% zaidi ya rate za bank kuu. Cha ajabu bank karibu zote zinatangaza riba za mikopo kuanzia 16% na utoaji wa mikopo ni riba za 21% kwa wenye hati za nyumba na mikopo mingine inaenda hadi 24%. Tusishangae banks zinaonyesha zinapata faida za ajabu wakati wakopaji wamepungua kutoka 24% mpaka chini ya 10%. Je hii ina maana gani
1. Ameshidwa kuongoza hizi bank au hajui kuziongoza. Hizi bank zime hakikisha zina marafiki serikalini na wakurugenzi wamekuwa na nguvu kuliko gavana wa bank kuu. Raisi alienda uingereza na mkurugenzi wa CRDB na sio gavana wa bank kuu. Hivyo imekuwa kama vile Professor hawezi hata kusimamia hizi bank .
2. Kuna miradi ya serikali wanachukuwa mikopo bank na ni wizi wa ajabu kama mradi wa serikali unachukuwa mkopo wa zaidi ya 10% kwa mwaka
Nitoe tu mfano nchi nyingine bank wanafanyaje US mfano bank kuu yao ina riba ya 2% na bank za biashara zinatoa mikopo kwa sasa ya 3%-5% yaani wanaongeza si zaidi ya 3% lakini tanzania bank ya biashara inaongeza kutoka 7% mpaka 21% ambayo ni ongezeko la 14%!!!. Hii maana yake ni kwamba biashara zisikotumia mikopo pesa nyingi ambazo zingetumia kuajiri wafanyakazi wapya, ununuzi na upanuaji wa biashara unasimama au unachukuwa muda mrefu. Hii inapunguza pesa kwenye mzunguko, inapunguza ajira na inakuwa vigumu kampuni zetu kushindana bila kuwa na pesa za mitaji.
Nchi zinazoendelea zina vitu vitatu vikubwa (1) Watu wanaojua kufanya kazi (2) Teknologia inayowezesha uzalishaji wa viwango na ufanisi (3) Upatikanaji wa mikopo nafuu. USA wasingekuwa na uchumi mkubwa kama mikopo ingekuwa 16%, 21% na 24%. Uchumi wa nchi hizi ungekuwa matatani sana sana. Sasa cha ajabu bank zinatoa mikopo ya 16%, 21% na 24% wa gavana kanyamaza tu!, waziri naye kanyamaza, Raisi naye kanyamaza!. Lakini vilevile Makamu wa Raisi Mpango anajua hili naye kanyamaza. Kwenye vitu muhimu kama hizi Rais, waziri na gavana waweke siasa na urafiki pembeni. Ni wafanya biashara wachache sana wanaweza kwenda kukopa nchi nyingine. Mo mfano ilibidi aende mpaka south Africa kukopa lakini wafanyabiashara wadogowadogo hawataweza kukuza biashara zao kwa riba hizi.
Lakini hata tukiacha yote hayo kwa kitendo cha Gavana wa bank kuu kushidwa kupunguza mikopo mpaka 10% kwa wafanyabiashara inatosha sana kumfukuza kazi. Waziri naye akishidwa kuongelea hili inabidi naye apishe wengine. Mwigulu ni mwana Ilboru mwenzangu lakini kama hili swala la riba halitapata ufumbuzi mapema inabidi aondolewe.
Zitto , Mwigulu Nchemba
Sababu moja ni kwamba bank kuu imepunguza riba za t-bills mpaka 7% kwa lengo la kupunguza mikopo ya bank za biashara ili ziwe 10%. Mara nyingi bank zina weka 2%-3% zaidi ya rate za bank kuu. Cha ajabu bank karibu zote zinatangaza riba za mikopo kuanzia 16% na utoaji wa mikopo ni riba za 21% kwa wenye hati za nyumba na mikopo mingine inaenda hadi 24%. Tusishangae banks zinaonyesha zinapata faida za ajabu wakati wakopaji wamepungua kutoka 24% mpaka chini ya 10%. Je hii ina maana gani
1. Ameshidwa kuongoza hizi bank au hajui kuziongoza. Hizi bank zime hakikisha zina marafiki serikalini na wakurugenzi wamekuwa na nguvu kuliko gavana wa bank kuu. Raisi alienda uingereza na mkurugenzi wa CRDB na sio gavana wa bank kuu. Hivyo imekuwa kama vile Professor hawezi hata kusimamia hizi bank .
2. Kuna miradi ya serikali wanachukuwa mikopo bank na ni wizi wa ajabu kama mradi wa serikali unachukuwa mkopo wa zaidi ya 10% kwa mwaka
Nitoe tu mfano nchi nyingine bank wanafanyaje US mfano bank kuu yao ina riba ya 2% na bank za biashara zinatoa mikopo kwa sasa ya 3%-5% yaani wanaongeza si zaidi ya 3% lakini tanzania bank ya biashara inaongeza kutoka 7% mpaka 21% ambayo ni ongezeko la 14%!!!. Hii maana yake ni kwamba biashara zisikotumia mikopo pesa nyingi ambazo zingetumia kuajiri wafanyakazi wapya, ununuzi na upanuaji wa biashara unasimama au unachukuwa muda mrefu. Hii inapunguza pesa kwenye mzunguko, inapunguza ajira na inakuwa vigumu kampuni zetu kushindana bila kuwa na pesa za mitaji.
Nchi zinazoendelea zina vitu vitatu vikubwa (1) Watu wanaojua kufanya kazi (2) Teknologia inayowezesha uzalishaji wa viwango na ufanisi (3) Upatikanaji wa mikopo nafuu. USA wasingekuwa na uchumi mkubwa kama mikopo ingekuwa 16%, 21% na 24%. Uchumi wa nchi hizi ungekuwa matatani sana sana. Sasa cha ajabu bank zinatoa mikopo ya 16%, 21% na 24% wa gavana kanyamaza tu!, waziri naye kanyamaza, Raisi naye kanyamaza!. Lakini vilevile Makamu wa Raisi Mpango anajua hili naye kanyamaza. Kwenye vitu muhimu kama hizi Rais, waziri na gavana waweke siasa na urafiki pembeni. Ni wafanya biashara wachache sana wanaweza kwenda kukopa nchi nyingine. Mo mfano ilibidi aende mpaka south Africa kukopa lakini wafanyabiashara wadogowadogo hawataweza kukuza biashara zao kwa riba hizi.
Lakini hata tukiacha yote hayo kwa kitendo cha Gavana wa bank kuu kushidwa kupunguza mikopo mpaka 10% kwa wafanyabiashara inatosha sana kumfukuza kazi. Waziri naye akishidwa kuongelea hili inabidi naye apishe wengine. Mwigulu ni mwana Ilboru mwenzangu lakini kama hili swala la riba halitapata ufumbuzi mapema inabidi aondolewe.
Zitto , Mwigulu Nchemba