Mkaa Mweupe
JF-Expert Member
- Jun 29, 2007
- 654
- 183
Kuna hali inayoendelea hivi sasa katika baadhi ya vituo vya kujazia mafuta kwenda sambamba na huduma za ki-Imani.
Katika uchunguzi binafsi, imebainika kuwa katika vituo vingi vinavyomilikiwa na Oilcom vimeambatanishwa na Misikiti kama sehemu ya kituo. Hii inajidhihirisha katika orodha hii:
1. Oilcom Ubungo: Msikiti upo kwenye hatua za mwisho.
2. Oilcom Mandela Rd: Msikiti umekamilika na unatumika.
3. Oilcom TAZARA Vetenary: Msikiti upo na unatumika.
Vilevile katika kituo cha Victoria, Ali Hassan Mwinyi Rd., kimeambatanishwa na Kanisa ambapo kwa siku za J'pili hupati huduma mpaka baada ya saa saba mchana.
Hii ni biashara Huria, lakini napenda kutoa angalizo. Tunakoelekea ni katika kubaguana ki-huduma kama tutaendelea kuendekeza uvunjifu wa mipango miji.
Sidhani kama ni sahihi kuambatanisha mambo ya Imani na Biashara. Kwani ni hatari sana endapo pale kituo kitashika moto na watu kwa makumi au mamia wapo pale kusikiliza neno la Mungu. Tuzingatie Usalama Kwanza.
Wapi EWURA, Wizara ya Ardhi, Manispaa, NEMC na Wananchi katika kutokomeza uoza huu ulioanza kwa kasi?
LETS BE SERIOUS japo kwa hili tusingojee mpaka tuambiwe "KWA HISANI YA WATU WA MAREKANI"
Katika uchunguzi binafsi, imebainika kuwa katika vituo vingi vinavyomilikiwa na Oilcom vimeambatanishwa na Misikiti kama sehemu ya kituo. Hii inajidhihirisha katika orodha hii:
1. Oilcom Ubungo: Msikiti upo kwenye hatua za mwisho.
2. Oilcom Mandela Rd: Msikiti umekamilika na unatumika.
3. Oilcom TAZARA Vetenary: Msikiti upo na unatumika.
Vilevile katika kituo cha Victoria, Ali Hassan Mwinyi Rd., kimeambatanishwa na Kanisa ambapo kwa siku za J'pili hupati huduma mpaka baada ya saa saba mchana.
Hii ni biashara Huria, lakini napenda kutoa angalizo. Tunakoelekea ni katika kubaguana ki-huduma kama tutaendelea kuendekeza uvunjifu wa mipango miji.
Sidhani kama ni sahihi kuambatanisha mambo ya Imani na Biashara. Kwani ni hatari sana endapo pale kituo kitashika moto na watu kwa makumi au mamia wapo pale kusikiliza neno la Mungu. Tuzingatie Usalama Kwanza.
Wapi EWURA, Wizara ya Ardhi, Manispaa, NEMC na Wananchi katika kutokomeza uoza huu ulioanza kwa kasi?
LETS BE SERIOUS japo kwa hili tusingojee mpaka tuambiwe "KWA HISANI YA WATU WA MAREKANI"