Gari za taka kumwaga taka viwanja vya jangwani na kupatikana viwanja vya Trillion 2

Hivi inamaana huko manispaa ya Ilala hakuna mtu aliyewahi kuwaza hili hata siku moja?, magari ya taka husafiri takriban kilomita 70 toka katikati ya jiji hadi dampo la pugu, sasa ni kwanini hayo magari yasiombwe kuliinua lile bonde la jangwani kuja level ya juu ambayo haitafikiwa na maji huku wakiacha njia katikati (njia ya mto) kwa ajili ya kupitisha maji kwenda baharini. Kisha wapime viwanja vinavyopatikana kwa ajili ya matumizi ya Open space, City garden, City park, Car parking, small scale market place, sports center na mengine mengi. Sidhani kama watendaji wa manispaa wana elimu ya kutosha, seriously..
Mkuu wazo lako ni zuri sana, lakini naona pale jangwani ni kama mapumulio ya maji ya nayotoka huku salenda yakiwa mengi sasa wakiubana yanaweza leta madhara mengine,ila hilo ni wazo langu tu najua hakuna linaloshindikana penye nia.
 
Huwezi fanya land filling/ reclamation kwa kujaza na taka. Hiyo itakuwa special Ilala tu
 
Taka na sumu zote zitaenda baharini wakati wa mafuriko trust me
Taka ziko za aina mbili 1.).Inorganic kama Plastic, Chuma, nylon. 2.) Organic kama majani na miti, mabaki ya vyakula na vingine vinavyooza. Pia hivi vimegawanyika katika makundi mawili 1.) Harzadous ambazo zina madhara mfano taka za sumu 2.).Non - hazodous ambazo hazina madhara kama taka za sumu. Magari ya taka huruhusiwa kubebe Non- hazodous waste na kuzitupa kwenye landfills, na hii hufanyika baada ya kusalvage all inorganic recyclable waste kama plastic na vyuma. Hivyo hakuna sumu itakayojazwa hapo.
 
Halafu water displaced yaende wapi?
Ukifanya landfill kuna mlipuko wa methane gas toka huko ulipofukia takataka, have account about this? Au unaongea tu pasipo kuwa na utaalam?
 
Itazuia MAJI kuingia baharini italeta mafuriko,pia taka ni sumu,km zilizochafua bonde La msimbazi,technology nzuri ni ya kuzirecycle ziwe malighafi kuzalisha mboleà,umeme, gas,diseal nk
Nimeshajibu haya kwenye post zangu namba 11, 18 na 23, zisome. Pia keep in mind, hojanyangu si jinsi gani ya ku-best manage solid waste, la hasha, hoja yangu ni jinsi gani tunaweza ku-reclaim viwanja vya Trillion 2+
 
Mkuu wazo lako ni zuri sana, lakini naona pale jangwani ni kama mapumulio ya maji ya nayotoka huku salenda yakiwa mengi sasa wakiubana yanaweza leta madhara mengine,ila hilo ni wazo langu tu najua hakuna linaloshindikana penye nia.
Mapumulio ya maji yote popote pale duniani ni bahari au ziwa, ukiona kingine hapo kati ni matokeo ya mmomonyoko tu, hivyo land reclamation inahitajika ili kurudisha land that was lost to erosion over a period of thousands of years.
 
Halafu water displaced yaende wapi?
Ukifanya landfill kuna mlipuko wa methane gas toka huko ulipofukia takataka, have account about this? Au unaongea tu pasipo kuwa na utaalam?
1.) Water displaced yaende wapi? Kwani maji ya mto huenda wapi? Na pia pale maji hujaa wakati wa mvua tu kutokana taka kuziba njia ya maji hasa kwenye daraja, otherwise yote yanapaswa kufuata mkondo wa mto hadi baharini.
2.) Methane gas ni advantage nyingine ya miradi kama hii, coz unaua ndege watatu kwa jiwe moja, kunakuwa na a small scale methane plant hapo hapo kwenye landfill kwa ajili ya kuvuna hiyo gesi kwa matumizi mbali mbali, yaan its a win win situation.
 
Maji hayazibiwi njia hahaha Dar nzima itakuwa mto msimbazi. chezea maji wewe
Nimeshaandika hapo kwamba patengenezwe njia pana ya mto kwa ajili ya kupitisha maji na pembezoni painuiliwe juu vya kutosha, sasa sijui hoja yako ni ipi
 
Nimeshaandika hapo kwamba patengenezwe njia pana ya mto kwa ajili ya kupitisha maji na pembezoni painuiliwe juu vya kutosha, sasa sijui hoja yako ni ipi
Hayo yamefanyika sana huko ulaya but siku ya maji ikotokea ni maafaa. Bonde lote lipanuliwe liachwe wazi kwa ajili ya mafuriko yakija
 
Hivi inamaana huko manispaa ya Ilala hakuna mtu aliyewahi kuwaza hili hata siku moja?, magari ya taka husafiri takriban kilomita 70 toka katikati ya jiji hadi dampo la pugu, sasa ni kwanini hayo magari yasiombwe kuliinua lile bonde la jangwani kuja level ya juu ambayo haitafikiwa na maji huku wakiacha njia katikati (njia ya mto) kwa ajili ya kupitisha maji kwenda baharini. Kisha wapime viwanja vinavyopatikana kwa ajili ya matumizi ya Open space, City garden, City park, Car parking, small scale market place, sports center na mengine mengi. Sidhani kama watendaji wa manispaa wana elimu ya kutosha, seriously..
Unatoa mawazo ambayo utekelezaji wake unahitaji knowledge ya uhandisi ambao wewe huna. Kuongea ni rahisi sana. Ungeanza kwa kuwauliza wahandisi posibility ya hicho kitu na cost yake ipoje, nadhani mjadala ungekuwa mzuri sana. Sasa umekurupuka kutoa suggestion ya nini kifanyike wakati wewe si mhandisi.
 
Wazo zuri na naamini lilishawahi toka ... tatizo can we manage to control environmental impacts zoezi hilo likianza kama tu vitu vidogo kabisa vinatushinda?

Inahitaji watu na serikali makini kwa Sasa wacha liendelee kuwa Wazo hatuwezi hii kitu
 
Hayo yamefanyika sana huko ulaya but siku ya maji ikotokea ni maafaa. Bonde lote lipanuliwe liachwe wazi kwa ajili ya mafuriko yakija
Kwahiyo huko ulaya yalifanyika ili siku maji yakija yatokee maafa? Au sijakuelewa; na bonde lote lipanuliwe kwenda wapi? Kwenye yale maghorofa ya Kariakoo? Au sijakulewa
 
Unatoa mawazo ambayo utekelezaji wake unahitaji knowledge ya uhandisi ambao wewe huna. Kuongea ni rahisi sana. Ungeanza kwa kuwauliza wahandisi posibility ya hicho kitu na cost yake ipoje, nadhani mjadala ungekuwa mzuri sana. Sasa umekurupuka kutoa suggestion ya nini kifanyike wakati wewe si mhandisi.
Wapi nimesema mimi si mhandisi, au nini unahisi nimeandika ambacho kinahitaji mhandisi aandike; unajua hizo ni hoja, na hoja hujibiwa kwa hoja; mimi kuwa mhandisi au laa hiyo si hoja. Hoja ziko mezani, jibu hoja ujibiwe kwa hoja, thanks.
 
Back
Top Bottom