Shadow7
JF-Expert Member
- Sep 28, 2020
- 13,796
- 20,205
Unamtafta Mayalla ugomviFuraha Dominic ambaye ni mpwa wa hayati Magufuli aliyegombea ubunge jimbo la Kawe na kushika nafasi ya kwanza huku Pascal Mayalla akiwa wa 162 amesema siku atakayokutana na Rais Samia atampa orodha ya Wafitini wote waliomzunguka.
Furaha anadai CCM kumejaa siasa chafu za kupakana matope, kufitinishana, kuchongeana na kusingiziana huku KUPE wa chama wakimnyonya damu Rais.
Furaha amesema ameshuhudia mengi sana katika utawala wa mjomba wake (Magufuli) ikiwemo yeye mwenyewe kudhibitiwa na kikundi cha Wasiojulikana ili asigombee ubunge
Furaha alikuwa akihojiwa na Aloyce Nyanda katika kipindi cha The Big Agenda, Star tv.
Mjadala ulikuwa mkali na Furaha alionekana akifuta machozi mara kwa mara huku mtangazaji Mtozi akimfariji.
Mahijiano yataendelea tena Ijumaa kwani jana hayakukamilika.
Mungu wa mbinguni awabariki sana!
Kama Furaha analizwa na CCM wewe ni nani hadi Uchekelee?