Funguka: Maisha yamekufunza nini?

Funguka: Maisha yamekufunza nini?

nimejifunza kuwa wanawake wawe waangalifu maana wanaume wengi wa sasa ni waoga wa maisha hivyo pendo la ndoa ni pamoja na kipato cha mke.

hapo Kweli kuna funzo...
 
Nimejifunza kuwa huweI kuwa njuu siku zote, ndio maana prof jay anasema wangapi walikuwa nazo na sasa hawana na wangapi walikuwa hawana na sasa wanazo concept ninayosema ni hii ni ivi utakuwa juu siku zote na utakuwa chini siku zote maisha mazuri ni kwa kila mtu ata ww masikin leo utaweza kuwa tajiri kesho
 
Nilichojifunza ni kuwa life is how you make it. Ukifikiri negative maisha yanakua magumu. Na ukifikiri positive na kutenda positive maisha yanakua murua.
 
nmejifunza1. kuwa mtumishi serikalini ni hamna stress kuliko kuwa kwenye private institutes 2.leo haifanani na kesho wala kesho kutwa au jana.3,ukiona uko na wakati mgumu sana jua mambo mazuri yatabisha hodi soon 4.hata iweje mke wako ni rafiki tu sio ndugu yako 5.vijana wengi hawapendi kazi ngumu yaani hawajitumi.

Serikalini ndio watu wanajifunza hivyo? Mhhh
 
Nimejifunza kuamini Mungu yupo ila Dini hazipo kabisa zimeletwa na wazungu na waarabu,nimejifunza kua mkarimu kwa yeyote pia kumshukuru Mungu napopitia magumu, pia kusamehe wanafiki na wachawi wa mitaan japo hua ni ngumu kwangu
Pia nimejifunza kumpenda anaenipenda na kupotezea anaenipotezeaa
Pia hakuna rafiki wa kweli duniani maana kikulacho kinguoni mwako
 
Maisha yamenifunza kutambua hakuna binadamu aliye mwema kwa mwingine 100%
 
Haya ndiyo niliyojifunza;
  1. Furaha katika maisha inajengwa na mtu binafsi, usitegemee binaadam mwenzio akusababishie furaha
  2. Ninaishi na binaadamu na sio malaika, at the same time na mimi ni binaadam sio malaika. Sishangai nikikosewa kwa sababu hata mimi nawakosea binaadam wenzangu. Kikubwa ni kuwa tayari kusamehe
  3. Kujishusha na kuomba msamaha ni sadaka kubwa sana, na ukifanikiwa katika hili hakika utaishi kwa amani
  4. Never say never!Dawa ni kuomba neema ya Mungu kila iwapo leo
 
Nimejifunza kutokata tamaa na kuwa risk taker...

Nilianza maisha from zero point na kila aliyenifahamu miaka 10 iliyopita hawezi kuamini hatua niliyopiga mpaka sasa kwa usimamizi wangu pekeyangu. Nimepita katika vizingiti kana kwamba mpaka mama yangu mzazi akanambia "mwanangu acha hiko ufanyacho kimeshindikana" lakini niligangamara kwa lazima mpaka kikanitoa. Na hiki sio kingine bali ni shule... Jamani elimu inalipa aisee.... "Kama elimu ni ghali, jaribu ujinga"

Cha muhimu ni kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kumuomba kwa sana hakika hatakutupa. Hii ni kwa wanaoamini uwepo wake...

Well said, Hata Mimi ckukata tamaa mazoezi mpaka kile kitambi kimeisha chote aisee
 
Maisha yamenifunza haya;
1.Hauwezi kumridhisha kila mtu
2.Si kila wakiaminio watu wengi ni sahihi.
3.Mpende adui yako...kuwa mwangalifu na rafiki zako
4.Kushindwa ndiyo mwanzo wa kuweza..
5.Mambo yakiwa magumu...hesabu baraka zako na uwe na moyo wa shukrani
 
Nimejifunza
1.kumtegemea Mungu katika kila jambo,
2.kuwa na upendo kwa Mungu wangu na kwa wanadamu wenzangu,
3.kuishi kwa kuwaheshimu watu wote maana huwezi jua nani atakufaa kwa lipi na kwa wakati upi,
4.kutokukata tamaa,
5.kujipa furaha kwanza maana furaha ya kweli hawezi nipa mtu mwingine ila mimi
5.kuwa na kiasi
 
Back
Top Bottom