Husninyo
Platinum Member
- Oct 24, 2010
- 24,167
- 10,226
msalato?
mpwapwa.
msalato?
uzalishaji wa mjini sio mkubwa sana lakini unasaidi matumiz ya hapa na pale. Pili lazima tukubali maeneo ya kilimo kidogo kidogo yapo mengi tu ila watu hawajatia akilini kwamba yawezekana kufanya hivyo. msukumo wa kuzalisha mwenyewe lendo sio kujitosheleza tu, ni kuweza kupata chakula fresh unachojua kimekuajekuaje, pili hewa safi, tatu ni kijishughuli tu cha kukufanya uwe buzi. Yawezekana kabisa kajisehemu hako huwezi kuzalisha vyote unavyohitaji, lakini unaweza kuzalisha japo asilimia tano!
Maji ya kumwagilia sio mengi sana. Ila maeneo mengine ya mjini kwenye baadhi ya majengo ni marufuku kulima ama kufuga!
Ndugu,
Nakumbuka katika kipingi cha awamu ya tatu (Mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe) fungu la mchicha hapa kwetu Ubungo (Riverside) lilikuwa linauzwa sh. 150/= na sukali kipindi hicho ilikuwa 600/= leo hii vitu hivyo havishikiki! Mchicha ni sh. 500/= na sukali kilo moja ni sh. 2400/=
Ongezeko hili haliendani kabisa na ongezeko la vipato kwa watanzania, mishahara iko pale pale lakini hata kama ikipaga haiwezi kuongeza tija kwasababu kuna ongezeko kumbwa la bidhaa. Serikali inabidi isimamie haraka mfumuko wa bei vinginevyo fungu la mchicha litauzwa sh. 10,000/= wakati huo huo serikali italaimika kutengeneza noti ya 100,000/=
unayoyasema yanawezekana mkuu.
Ila kwa sytem ya kibepari ya Working 9 to 5, utapeana huduma kwa kijishamba chako muda gani, kumbuka kuna kupanda, kupalilia, kuweka samadi n.k n.k...
Hebu niambie?
Tuliambiwa uchumi unapaa, na sasa mfumuko wa bei ni 20%, jamaa yangu mpenda dagaa ananiambia dagaa wa kigoma tsh.14,000/= kilo moja si gunia!
baleke bajobeke pambwani panyafu!
Tuseme upo dar es salaam umeamka saa kumi na moja kwa watu wa mazoezi au wakaa mbali. Kazini wengi wetu tunatakiwa tufike ama tumejiwekea utaratibu wa kufika kuanzia saa 1:30. Hushindwi kumwagilia kwa dakika 15 kama wewe sio mpika chai ama unatayarisha watoto kwa shule. Kama uko single ndio rahisi kabisa - unajenga kautamaduni tu. Ukirudi jioni kitu ni kile kile, kawaida kunakuwa na muda kati ya saa 1 hadi saa mbili kabla ya taarifa ya habari - utamwagia tena kama wewe sio mpishi. Kama ni mpishi unamwagia usiku baada ya taarifa ya habari. Kupalili weekend
Ndio.
Hiyo ndio hali halisi, hii ndio bei mpya ya mchicha kutoka viunga vya pale O'bay, adjacent na kota za polisi Oysterbay. Fungu hilo lilikuwa likiuzwa ShT. 500/= katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita, hivyo bei mpya ni sawa na ongezeko la 100%, pamoja na kwamba pale ndio sehemu ya kwanza ya uzalishaji, yaani hakuna gharama za kusafirisha wala faida ya mchuuzi wa rejareja.
Tafakari,
CHUKUA HATUA!
Lazima wafidie kwenye ongezeko la umeme. Si mmeamua kumlipa RA na JK (Dowans syndicate)
Ndio.
Hiyo ndio hali halisi, hii ndio bei mpya ya mchicha kutoka viunga vya pale O'bay, adjacent na kota za polisi Oysterbay. Fungu hilo lilikuwa likiuzwa ShT. 500/= katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita, hivyo bei mpya ni sawa na ongezeko la 100%, pamoja na kwamba pale ndio sehemu ya kwanza ya uzalishaji, yaani hakuna gharama za kusafirisha wala faida ya mchuuzi wa rejareja.
Tafakari,
CHUKUA HATUA!
unajua kulalamika na kulaumu serikali hakusaidii chochote....ndo ishatokea sasa na haitabadilika na bei zinazidi kupanda kila kukicha. Mi nafkiri cha maana ni mbinu na jinsi ya kujikimu katika mfumuko wa bei wa vitu....nini kama kijana ufanye kukabiliana na hii hali. kwangu hilo ndo la maana !!!!
Unaishi kwa mazoea eh?
Nioneshe mahala nilipoilaumu serikali. Kulalamika kunahusika kaka, hata Mungu kuna mahali alilalamika!
Mada ndo nimeileta humu ili tujadili cha kufanya, wewe waona tufanyaje?
jamii forums naitumia as a source of ideas nachanganya na zangu then napata a solution to a problem....so far sijapata idea from ur thread...ningechangia iwapo ulitoa idea !!!
sawa.
Lakini hudhani kama kung'amua tatizo ni sehemu ya kwanza ya kushughulika nalo?
Viongozi wetu wa kisiasa wamekuwa wakishindwa kukabili matatizo kwa kufeli katika kuyatambua, ambayo ni hatua ya kwanza.
Utakuta kwenye kampeni mtu anasema nitajenga barabara za ghorofa, nitaifanya hii iwe Dubai, nitajenga Machinga Complex tano, n.k n.k, bila kujua kuwa tatizo ni nini,
mfano hapo kwenye barabara za ghorofa, unakuta tatizo sio barabara, ila tatizo ni foleni inayotokana na msongamano,
ila mtu ashafika kwenye suluhisho kabla ya kung'amua tatizo, kisha kulichunguza.
Tuendelee...