Hizo ARV unatoa wewe? Na zile barabara kama ile ya Tunduma- Sumbawanga-Katavi, hela walitoa ukoo wako? Na ule umeme uliounganishwa zaidi ya vijiji 5,000 hela walitoa mizimu ya kwenu? Na hizo hela mnazopewa na kukopa WB, huko WB waliweka familia yako? Wasingeweka hao mabeberu mngekopa nini? Hata huko African Bank unajua hela nyingi ni ya nani? Au unadhani ni ya nchi za Africa? Kweli aheri ulemavu wa viungo kuliko kukosa uelewa.
Hakuna nchi hata moja iliyowahi kufanikiwa kwa kugombana na hao wakubwa ikafanikiwa. Wachina walirukaruka, wakaishia kuvaa nguo zenye viraka matakoni na magotini lakini hakuna kilichoeleweka. Wakasalimu amri, mabeberu wakaenda kuwekeza China, ukuaji wa uchumi wa China ukawa unaongoza Duniani. Mpaka leo, makampuni makubwa kabisa 10 nchini China, kampuni ya China ni moja tu. Mengine yote ya mabeberu. Na sahizi Trump anaitesa China, mpaka ukuaji wa uchumi wa China umeshuka. Na baadhi ya makampuni yameridhia kupunguza uwekezaji wake nchini China.
Kuna wakati mbwa anaweza kubweka na hata kumwuma anayemtunza. Lakini anayemtunza anaweza kummaliza wakati wowote akitaka.
Simu hiyo huwezi hata kuitumia Marekani asipotaka. Hata kagari kako huwezi hata kuwa nako, kama mabeberu wangesema tusiuziwe. Dhahabu yako na almasi vinaweza kuwa kokoto na mchanga usio na maana kama hayo mataifa makubwa yakisema hairuhusiwi kununua madini ya Tanzania.
Tanzania haiwezi kuwepo bila ya mataifa makubwa lakini mataifa makubwa yataendelea kuwepo hata bila ya uwepo wa Tanzania. Somalia leo hakuna Taifa. Nchi gani kubwa imeathirika?