Greatest Of All Time
JF-Expert Member
- Jan 1, 2017
- 20,714
- 45,103
Majira ya Saa 2:00 Usiku kwa Masaa ya Afrika ya Mashariki, Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itashuka dimbani Benjamin Mkapa kuwaalika Uganda (The Cranes) katika mchezo wa nne wa kundi F kuelekea kufuzu Afcon mwaka 2023..
Taifa Stars yenye point 4 iliyopo nafasi ya pili nyuma ya vinara Algeria ambao washafuzu itashuka dimbani ikiwa na kumbukumbu yakuibuka na ushindi wa 1-0 siku chache zilizopita.
Taifa Stars ikishinda itafikisha alama 7 na kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa mashindano hayo makubwa na adhimu kwa bara la Afrika kwa mara ya 3 katika historia ya mashindano hayo.
Tujitokeze kwa wingi tushangilie timu yetu ya Taifa, hatuna timu nyingine jamani.
Mechi itakuwa mubashara AzamtV, Dstv kupitia chaneli 225 ya kifurushi cha POA.
Kila la heri Taifa Stars!
Kila la heri Tanzania!!!
Taifa Stars yenye point 4 iliyopo nafasi ya pili nyuma ya vinara Algeria ambao washafuzu itashuka dimbani ikiwa na kumbukumbu yakuibuka na ushindi wa 1-0 siku chache zilizopita.
Taifa Stars ikishinda itafikisha alama 7 na kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu kwa mashindano hayo makubwa na adhimu kwa bara la Afrika kwa mara ya 3 katika historia ya mashindano hayo.
Tujitokeze kwa wingi tushangilie timu yetu ya Taifa, hatuna timu nyingine jamani.
Mechi itakuwa mubashara AzamtV, Dstv kupitia chaneli 225 ya kifurushi cha POA.
Kila la heri Taifa Stars!
Kila la heri Tanzania!!!